Ilikuwa ni Jumapili tulivu , kwa wale wakristo waliokuwa wakienda kanisani walikuwa wakienda na kwa wale ambao walikuwa ni wa dini nyingine walikuwa na pilipilika za mambo mengine za Maisha yao.
Roma kama kawaida yake aliamka asubuhi asubuhi na kwenda kufanya mazoezi ya hapa na pale ili kuweka mwili wake katika hali nzuri , kwa upande wa Bi wema alikuwa bize na kuandaa kifungua kinywa kwa siku hio na kwa upande wa Edna alikuwa bize na kusoma kama ilivyokuwa kawaida yake , aliamini matatizo yake yote yanaweza kutatuliwa na kusoma na ndio maana aliamini katika kusoma sana.
Alijitahidi kusoma kwa muda , lakini akili yake haikuwa ni yenye kutulia , alionekana kuna jambo lilikuwa likimuumiza kichwa kwani alikosa utulivu , baada ya kuona haelewi kile alichokuwa anakisoma alisogelea tarakishi yake ya mapakato na kuingia kwenye mtandao wa Google na kuanza kutafuta taarifa zinazohusiana na macho ya mtu kubadilika Rangi , lakini kila majibu yaliokuwa yamekuja yalionekana kutokumridhisha kabisa na kukosa jibu alilokuwa analitaka.
“Au nimuulize mimi mwenywe kwanini macho yake yanabadilika Rangi?” Aliwaza mrembo huyu huku akiwa amevalia kigauni chake kilichoufanya mwili wake mnene kiasi kupendeza.
“Ila naamini siku moja ataniambia mwenyewe kwanini yuko vile , sitakiwi kumuuliza”Alijiibu mwanamke huyu huku akiona hayupo kwenye nafasi ya kumuuliza mume wake Roma kwanini macho yake yanabadilika rangi anapokuwa na hasira kali.
Saa mbili kamili za asubuhi Edna alishuka chini kwa ajili ya kupata kifungua kinywa baada ya kuitwa na Bi Wema , Roma alikuwa tayari yupo mezani , na alikuwa anamsubiria mke wake waanze , baada ya Edna kuketi wanafamilia hawa watatu ndani ya jumba hili kubwa la kifahari walianza kupata kifungua kinywa chao ambacho kwa familia za Maisha ya chini wangedhania moja kwa moja aina hio ya chukula ni kwa ajili ya sherehe.
“Miss unaonaje ukienda na Mr Roma leo kituoni?”Aliongea Bi Wema na kupendekeza .
“Bi Wema kituo gani?”Aliuliza Roma
“Kuna kituo cha kulelea yatima kipo Mkoa wa pwani Bagamoyo Kiwangwa, Ni kituo ambacho kampuni inakifadhili na imekuwa utamaduni kila jumapili Miss Edna kwenda huko kuwatembelea Watoto hao na kuwapelekea baadhi ya mahitaji muhimu”Roma alishangaa.
Edna alimwangalia Roma , hakuwa akipinga swala hilo la kwenda nae , kwanza kabisa mrembo huyu alipanga kujiweka kidogo karibu na Roma ili kuweza kujua ni kwanini macho yake yanabadilika Rangi , aliamini kama watakuwa marafiki Roma anaweza kumfungukia.
“Bi Wema kama mke wangu anapenda kuongozana na mimi nipo tayari , isitoshe leo sina pakwenda na sijazoea kukaa ndani”Aliongea Roma.
“Roma itakuwa vizuri kama tutaenda wote , unisaidie kwenye kubeba mizigo ya kwenda nayo”Aliongea Edna na Roma aliitikia kwa kichwa.
Baada ya nusu saa Roma alikuwa ashajiandaa kwa ajili ya kuianza safari ya kuelekea Bagamoyo , alikuwa sebuleni akimsubiria Edna ambaye kama ilivyokuwa tabia ya wanawake kujiandaa muda mrefu Edna alichukua lisaa mpaka kuonekana akiwa anashuka.
Roma siku zote alikuwa akijivunia hata kuitwa mume wa Edna , kwani mwanamke huyu hata avae nini , alikuwa akipendeza sana na kuvutia,Edna alikuwa amevaa leo Suruali ya jeans rangi ya Bluu iliomfanya umbo lake kuonekana vyema, na kishati flani kitambaa mtelezo mikono mirefu , na akakikunJa hadi kwenye kiwiko cha mikono , chini akiwa amevalia viatu vyeupe kama Raba Rangi ya pink.
Edna alimpa Roma ufunguo na Roma alitangulia mpaka sehemu ya kuegeshea magari na kubonyeza Rimoti na Pickup aina ya Cadillac Escalade EX ili Tweak na kuwasha taa ,Roma alitabasamu na ufahari wa hii gari , aliitoa na kuleta mpaka katikati na Edna aliingia.
Bi Wema aliekuwa juu ya Gorofa alikuwa akitabasamu kwa furaha baada ya kuona Edna na Roma wakitoka , alijiambia ni mwenye akili sana kushauri waende pamoja.
“Kuanzia sasa misheni yangu ni kuhakikisha wanafanya mambo kwa pamoja , hii itawaongezea kuwa karibu” Aliwaza Bi Wema huku akijiona jasusi mbobezi likija swala la mapenzi.
Safari ya wanandoa hawa iliishia Mliman City , Watu waliokuwa ndani ya eneo hili waliwaangalia kwa macho ya tofauti kabisa huku kila mtu akiwa na mawazo yake ,Edna alikuwa amevalia miwani ambayo ilimfanya apendeze lakini yeye hakuvaa kwa ajili ya kupendeza , alikuwa amevaa kwa ajili ya kufanya watu wasimtambue.
Roma alievalia jeans lake Rangi nyeusi na koti la Ugolo alijongea upande upande na mke wake , huku akijisikia fahari namna ambavyo wanaume wa eneo hili walivyokuwa wanamwangalia kwa macho ya wivu.
Walinunua mahitaji mengi ndani maduka ya vyakula , baadhi ya nguo , taulo za kike na makolo koloo mengi sana ambayo yalikwa ni sehemu ya mahitaji ya Watoto , walichukua na baadhi ya zawadi kwa Watoto hao ikiwemo biskuti pipi na vitu vingine.
Baada ya kumaliza kufanya manunuzi , Roma kusaidiana na baadhi wafanya kazi walipakia huku Edna akiwa bize kulipia.
Wakati Roma akiwa bize kupandisha vitu , mara alisikia sauti iliokuwa ikimuita nyuma yake , sauti ya kike ambayo alikuwa akifahamu vyema, alikuwa ni mrembo Doris ambaye alikuwa akiegesha gari yake , akiwa yupo peke yake aliependeza kama kawaida.
“Doris !”Aliongea Roma kwa kushangaa baada ya kumuona mrembo huyu mbele yake.. wakati Doris anamwangalia Roma kwa mshangao mara alikuja Edna na kwenda kusimama karibu na Roma.
“Edna!”Macho yalimtoka Doris , hakuelewa ni kwanini wawili hao wako pamoja .
“Vipi Doris umekuja kufanya Shopping?”Aliuliza Edna wa kwanza baada ya kuona Dorisi yupo kwenye mshangao pasipo kuongea neno.
“Ndio Edna , lakini kwanini upo na Roma?”
“Nisamehe Dorisi rafiki yangu , nadhani unakumbuka nilikuambia nina mume?”
“Usiniambie Edna huyu ndio mumeo na siku zote huniambii?”.
“Ndio Dorisi huyu ni mke wangu,Tunaelekea Bagamoyo na muda unaenda tutaongea Zaidi”Aliongea Roma akikata mazungumzo hayo , hakutaka waendeleee kusimama ndani ya eneo hilo la maegeisho ya magari
“Nitakupigia simu Doris , tutaongea”Aliongea Edna na Roma alimshika bega Edna na kumsukumizia ndani na kufunga mlango na kisha akazunguka upande wa dereva na kuingia ndani na kuliwasha huku wakimwangalia Doris aliekuwa amesimama akiangalia gari yao ikitokomea.
“F**ck you Roma , siku zote unanichora tu kumbe mkeo ni Edna , halafu kwanini Edna hajaniambia”Alijiongelesha mwenyewe na kusahau kuwa baadhi ya watu walikuwa wakimshangaa , alifuta machozi kwa mkono ambayo yalikuwa yashaanza kujitengeneza ndani ya mboni za macho yake na kufungua mlango wa gari na kuingia na kisha akatoa gari ndani ya eneo hilo , alionekana kughairi , alichokuwa amefata hapo.
“Doris atakuwa amekasirika”Alianzisha maongezi Edna wakati wakipita Lugalo.
“Kwanini unasema hivyo?”
“Doris ni Rafiki yangu wa muda mrefu na niseme ni Zaidi ya Rafiki yangu , tumekuwa pamoja kwa muda mrefu kidogo , nilimwambia nimeolewa na kumuhaidi nitakutambulisha kwake lakini sikufanya hivyo na leo ametuona pamoja , kama marafiki atakasirika na kujisikia vibaya”.
“Mke wangu usiwe ni mwenye wasiwasi , Doris ni Rafiki yako na wewe ulikuwa pia na sababu za kutonitambulisha kwake mapema , hivyo atakuelewa , isitoshe hatuna muda mrefu tokea tumesajili ndoa yetu”.Edna aliitikia kwa kichwa.
“Kila jumapili unakujaga huku kutembelea kituo?”Aliuliza Roma kwa makusudi a ya kubadilisha stori.
“Ndio , imekuwa utamaduni , kila jumapili lazima nitembelee , napenda Watoto na najisikia faraja ninapokuwa nao karibu”.
“Mke wangu nilijua wewe ni kauzu kila sekta , kumbe una upande wako mwingine ambao sikuwa nikiufahamu”.
“Mimi sio kauzu ila napenda kuwa siriasi kwenye maeneo yanayonitaka kuwa hivyo , sipo kama wewe kila eneo haupo siriasi”.
“Kwa hio mke wangu wewe unataka niwe vipi?”Edna hakujibu aliendelea kukaza macho barabarani na Roma hakutaka kuongea Zaidi.
Ni masaa machache tu walikuwa washafika ndani ya kituo hiki , kilikuwa ni kituo kikubwa sana, kilikuwa na majengo makubwa kama chuo , jambo ambalo lilimshangaza Roma.
“Mke wangu hiki kituo ni kikubwa ni shirika gani limejenga hiki kituo?”
“Sio shirika ni mke wa raisi wa Kenya ndio amejenga hapa Tanzania”Roma alishangaa ,yaani mke wa raisi atoke Kenya kwao ambako kuna Watoto wengi waliozagaa mtaani aje ajenge Tanzania , alishangazwa na jambo hilo.
“Kwanini ajenge Tanzania sio Kwao Kenya?”
“Hata Kenya kajenga vituo vingi tu na sio Kenya wala Tanzania ,Uganda , Rwanda na Kongo kajenga vituo vinavyofanana hivi hivi, ni mwanamke ambaye ana moyo mzuri sana na anasifika sana ndani ya Afrika kwa kuisadia jamii.
Roma alitingisha kichwa baada ya kupewa jibu hilo na mke wake , aliona huyo mwanamama anapaswa kupewa tuzo kwa msaada mkubwa ambao anaufanya kwa jamii zenye uhitaji.
Kitendo cha kumaliza kuegesha Gari Tu ni kama Watoto waliokuwa ndani ya hili eneo walikuwa wakimsubiria Edna kwani kundi lote lilimkimbilia na kumzingira huku wakionyesha furaha yake na Edna na yeye hakuwa nyuma , alionekana kufurahi kweli uwepo wa Watoto na kwa mara ya kwanza Roma anamshuhudia Edna akiwa na furaha sana.
“Sikujua mke wangu kumbe mzuri hivi akicheka , halafu anaonekana kuwa na moyo mzuri sana , kanaigiza tu kuwa siriasi”Aliwaza Roma huku Watoto hao wakiwa hawana habari nae.
“Edna karibu” Aliongea mwanamama mmoja hivi mnene mwili wa kibonge mwenye umri si chini ya hamsini hivi alikuwa wa maji ya kunde.
“Asante Mama Issa ”Alijibu Edna aliekuwa akiwaangalia Watoto hawa , lakini kwa upande wa yule mama alimwangalia Roma na hapa ndipo Edna aliekuwa amemshau Roma akainuka.
“Mama Issa Watoto wamenifanya nisahau kukutambulisha , huyu ni mume wangu anaitwa Roma Ramoni” Mama huyu macho yalimtoka kwa mshangao huku Roma akiwa ni mwenye kutabasamu , alijiuliza huyu mwanaume ana nini mpaka kupata nafasi katika maisha ya Edna.
“Sikujua.. kumbe umepata mume Edna .. jamanii.. karibu baba mimi naitwa Tabea Singano ni mkuu wa hiki kituo”Aliongea mama huyu huku akionyesha furaha yake waziwazi , alionekana pia ni mtu ambaye alitamani siku moja Edna kumtambulisha mume wake kwake.
“Nashukuru sana kukufahamu Mama”.
“Karibu sana , unabahati sana kumpata Edna katika Maisha yako , umchunge sana”Aliongea mwanamama huyu huku Edna hata hakuwa akiwasikia , kwani alikuwa bize na Watoto aliokuwa akiwabeba mmoja mmoja juu.
Walishusha mizigo kwa kusaidiana na wafanya kazi wa hapa ndani , na Roma pia alisaidia katika kazi hio na baada ya zoezi hilo dogo kuisha Edna na Roma walichukua zawaidi walizokuwa wamekuja nazo na kuanza kuzigawa kwa Watoto hao .
Roma alimkubali sana aliejenga hiki kituo kutokana na wingi wa Watoto hao , kilikuwa mpaka na shule kubwa ya msingi mpaka sekondari , ni kituo ambacho kilionesha kujitosheleza sana kwa kila kitu.
Mama Issa alimchukua Roma na kuanza kumtembeza ndani ya kituo hichi , kwa kumuonesha baadhi ya huduma ambazo wanatoa kwa Watoto hawa ya kimalezi , mama huyu alionekana kuwa mkarimu sana.
“Edna ni msichana wa kipekee sana ,nimemuona akikua kwanzia alivyokuwa mdogo”Roma alishanga
“Mlikuwa maishi majirani?”.aliuliza Roma na mwanamama huyu alitabasamu.
“Hapana , wakati wa utoto wake alikuwa akija na bibi yake hapa mara kwa mara kucheza na Watoto na naweza kusema Muda wake wa utoto mwingi alicheza na Watoto ambao walikuwa kwenye hiki kituo”Aliongea mama huyu na kumfanya Roma ashangae , na wakati huu walikuwa wakiingia ndani ya mejengo ya ofisi hizi za kituo hiki kilichokuwa kinafahamika kwa jina la Son and Daughter Orphanage(SDO)..
Roma baada ya kuingia ndani ya hii ofisi kubwa ya mama Issa alijikuta akishangaa picha iliokuwa juu ya ukuta ,ilikuwa ni picha ya mwanamama mmoja maji ya kunde aliekuwa kwenye pozi la kutabasamu, kichwa chake kilianza kuuma na kupiga kama Radi na picha picha za matukio zikianza kupita .. macho yake yalianza kubadilika palepale na kuwa ya kijani.
Comments