Roma alishindwa kuvumilia , alikuwa akishindana na hali iliokuwa ikiendelea kwenye mwili wake , alifumba macho yake haraka sana , ili Mama Issa asimuone akibadilika na kisha akageuka, Uzuri ni kwamba mwanamama huyu alikuwa amempa mgongo Roma na hakuwa akijua kilichokuwa kikiendelea kwenye kichwa chake.
Roma alikimbilia nje , lakini ile anatoka kwenye ofisi alijikuta akikumbana na Edna ambaye aliona hali yake ya macho Alitaka kumwepa lakini Edna hakufanya hivyo , alimshika mkono.
“Roma Calm Down”Aliongea Edna na Roma ni kama ameshituka kwani macho yake yaligeuka na kurudi katika hali yake ya kawaida na kumwangalia Edna.
“Am Sorry Edna”.
“Sorry ya nini?”
“Sijui …”Kabla Roma hajaibu walishitushwa na sauti ya Bi Tabea.
“Nilishangaa umeenda wapi kumbe umemfata mkeo”Aliongea Bi Tabea na Edna alitabasamu.
“Edna niseme tu hongera sana kwa kupata mume , Roma anaonekana kuwa kijana mzuri naamini mama yako na bibi yako watakuwa na furaha na wanaweza kupumzika kwa amani maana wewe..”
“Mama Issa Maana nini…”aliongea huku akicheka.
“Umekuwa mgumu sana , nakumbuka yule nani yule .. ee Elvice alikuwa akitoka jeshini lazima aje hapa kulalamika..”Mama huyu alijikuta akiishia njiani kuongea na kujiona ameropoka ila kwa Roma alikuwa amesikia kila kitu na akajiuliza kuna historia gani kati ya Elvice na Edna ambayo hakuwa akiijua , ila hakutaka kuuliza.
Saa moja kamili za jioni ndio muda ambao wawili hawa walitoka ndani ya kituo hiki kurudi nyumbani , Edna alionekana kuchoka kweli kutokana na kucheza na Watoto , kwa upande wa Roma yeye hakuwa amechoka , kwanza hakucheza kabisa na Watoto kwani sio mtu wakupenda sana kama ilivyokuwa kwa Edna.
Alimwangalia mke wake aliekuwa amesinzia pembeni na kujikuta moyo wake ukiwa wa moto , alitamani Maisha yake yawe kama hivyo kila siku ,awe anapendana na mke wake , watembee hapa na pale kurefresh mind, alitamani kufurahi na kuendeleza Maisha ya ukawaida , lakini Roma Maisha ya aina hio yalikuwa kwake ni ndoto.
“Hapana lazima nifanye juu chini nina kamilisha yote yalionileta Tanzania , nikishachimba swala hili kwa undani na kujua kwanini nilikuwa kwenye kile kisiwa cha mateso mimi na Seventeen na kuifahamu familia yangu nadhani nitatulia na mke wangu, Edna licha ya kwamba hatujaoana kimapenzi , lakini sidhani kama itakuja siku nitakuacha hata pale mkataba utakapoisha”Roma aliwaza mawazo hayo mchanganyiko huku akizidi kukanyaga pedeli kuelekea jijini Dar es salaam.
Wakati akiendelea kuendesha gari alikumbuka kauli ya Bi Issa kumuuliza hali ya kimaendeleao ya Nasra , alijiuliza kwanini mwanamama yule kauliza juu ya maendeleo ya Nasra ila alikosa majibu kwa wakati mmoja , alijiambia kuwa atafahamu kadri atakavyokuwa karibu na Nasra.
****
Doris alijikuta ni mwenye hasira sana , baada ya kujua kuwa Edna na Roma ni mume na mke , alikasirika sana , lakini na kuumizwa kwa wakati mmoja.
Alianza kukumbuka tukio ambalo Roma alimuomba hela ya nauli wakati akiwa anarudi nyumbani na kumpatia , alikumbuka usiku wao waliotumia na kufanya mapenzi na mwanadada huyu alizidi kutokwa na machozi ,alihisi moyo wake ulikuwa ukimuuma sana kiasi cha kwamba mwenyewe alishindwa kuelewa kwamba moyo wake ulikuwa ukimuuma kutokana na kwamba Edna na Roma walimficha na kumuona mjinga siku zote , au ni kwasababu alijua kuwa Roma mke wake ni Edna mwanamke mrembo na kilichokuwa kikimliza ni wivu wa kimapenzi.
Alisimama kukodolea maji ya baharini muda huu wa jioni huku machozi yakiwa yanamtoka , lakini kila alipokuwa akiangalia baadhi ya wapenzi waliokwa ndani ya fukwe hii ya Coco walivyokuwa wakifurahi na kuonyesheana mapenzi , aliijikuta akizidi kutoa machozi.
“Ninaonekana kutokuwa na bahati katika Maisha yangu , Edna nifanye nini mimi nahisi kumpenda sana mumeo , najiona kabisa siwezi kumuacha hata kidogo , kwanini iwe wewe rafiki yangu”Aliwaza mwanadada huyu na kuwazua huku akionekana ni mwenye kukosa jibu , alionekana alikuwa akishindana na hisia zake.
Doris licha ya kwamba alikuwa sio mwenye kuonyesha waziwazi mapenzi yake kwa Roma alikuwa ashampenda tokea siku ya kwanza wanaonana ,Roma alivyomuomba kiasi cha pesa , tokea siku ile alikuwa alikuwa ni mwenye kumkumbuka Roma , hakujua ni kwanini alikuwa akimkiumbuka mwanaume huyo , lakini picha yake haikuwa ni yenye kutoka kwenye kichwa chake.
Siku ambayo anamuona Roma kwa mara nyingine ndani ya kampuni yake , akija kufanya usaili , alijiambia kabisa ni Mungu ndie aliekuwa amewakutanisha kwa mara nyingine na hivyo hapaswi kuzarau kile Mungu alichompatia na ndio maana siku ile ile aliona atumie nafasi ile kumtambulisha Roma kwa mwanaume mzee aliekuwa akimsumbua , mwanaume aliekuwa akimfahamu kama Mr Kijembe .
Hakujali kabisa katika moyo wake kwamba Roma ameoa , alichokuwa akiamini ni Kwamba Roma alikuwa amepangiwa kuwa nae katika Maisha yao yote na mke aliemua ni makosa ambayo Roma alikuwa amefanya , hayo ndio yalikuwa mawazo ya mwanadada huyu mrembo , aliamini mke wa Roma sio mtu sahihi kwa Roma na yeye ndio alikuwa sahihi , kwani matukio yao ya kukutana ni kama Mungu aliwakutanisha.
Hata pale alipopata taarifa ya Roma kulala na mwanamke Neema Luwazo Mwanamke ambaye alikuwa akimjua sana tu, kwa kuwa na mahusiano na Raisi mstaafu , alijiambia kuwa ni mihemko tu ya Roma ya kukosa mtu sahihi wa kumtuliza na kama atampata basi Roma angetulia kwake na kuachana na mambo ya wanawake , kwani angempa kile kitu ambacho anakitafuta nje , kitu ambacho aliamini ni kwamba alikuwa akikikosa kwa mke wake.
Siku ya Jumapili ndio siku ambayo alipanga kutimiza jambo lake la kuanza kuweka ukaribu na Roma , aliamini anapaswa kufanikisha swala la yeye kuwa karibu kabla ya kwenda safari ya kikazi Japani , alitaka katika safari hio waitumie kama sehemu yao ya matembezi kama wapenzi , na ili kukamilisha swala hilo anachotakiwa kufanya ni kuhakikisha Roma anakuwa karibu yake anamzoea na hatimae kumpenda.
Baada ya kuwaza hayo , hatua ya kwanza aliofikiria ni kwenda kutafuta zawadi yoyote ambayo aliamini itamfurahisha Roma na eneo pekee alipoona panafaa kupata zawadi hio kwa siko hio ya jumapili ni Mlimani City.
Nwanadada huyu alijiandaa , alichukua kadi yake ya benki aina ya ‘Black Card’ kadi ambayo ilikuwa ikimruhusu kutoa kiasi chochote kile cha pesa na kuiweka katika mkoba wake , na kisha akachukua ufunguo wa gari yake na kutoka ndani ya jumba hili la kifahari alilokuwa akiishi mwenywe na wafanya kazi.,Jumba ambalo alikuwa amenunuliwa kama zawaidi na baba yake .
Lakini baada ya kufanya safari yake na kufika Mlimani anajikuta akishuhudia kitu ambacho moyo wake haukutarajia kukiona , alimuona mwanamke ambaye aliamini sio sahihi kwa Roma akiwa ni Edna , Rafiki yake kipenzi , bosi wake kazini, moyo wake ulipigwa na ganzi.
“Doris!!”Ilikuwa ni sauti ya mwanaume iliosikika nyuma yake na kumfanya mwanadada huyu ageuke ni nani anamuita , lakini ile anageika alikutana na uso wa Abu.
“Abu vipi , kwanini uko hapa ?”Aliuliza Doris kwa namna ya kushangaa.
“Nimekuja kupunga upepo kama wengine Doris , wewe vipi , kwanini uko hapa?”.
“Namini nipo kwa ajili ya kupunga upepo “Abu alijikuta akitabasamu .
“Doris najua unaonekana kuwa katika hali ya mawazo , lakini nimekuwa nikisubiria sana jibu lako”
Doris alishangaa na kuanza kuvuta pumzi kwa nguvu na kumgeukia Abuu….
Ni jibu gani ??
Comments