SEHEMU  YA 33

2010 -KIGALI  STATE HOUSE

Ni  mwaka 2010 muda wa  saa tano za Asubuhi  mheshimiwa Jeremy alionekana ndani ya ofisi yake akifanya kazi kama kawaida,  katika kuwatumikia wananchi wa Rwanda, lakini siku hii kwa mheshimiwa huyu   hali yake ilionekana kuwa  sio ya kawaida , kwani alionekana kuwa ni  mwenye wasiwasi sana kuliko siku zote hali ambayo ilimfanya kukosa utulivu , kila saa alionekana kuangalia saa ya ukutani kama mtu ambae alikuwa na  jambo ambalo alikuwa akilisubiria.Ilivyofika saa  sita na nusu  aliingia Linda  mlinzi  wa karibu wa Mheshimiwa Jeremy.

“Mheshimiwa Ashafika”Aliongea Linda na kumfanya mheshimiwa Jeremy avute pumzi .

“Mruhusu aingie”Aliongea mheshimiwa na kisha akatoka kwenye meza yake  na kwenda kwenye masofa na hapo hapo mlango ulifunguliwa na aliingia mwanaume mmoja  wa kizungu alievalia shati la Blue bahari na suruali ya kadeti , muonekano wa huyu jamaa ni kama vile hakuwa akiingia kuonana na  mheshimiwa , kwani alivaa kikawaida sana kama muhuni flani hivi.

“Welcome Mr  Viladkov”Aliongea mheshimiwa kwa kingereza.

“Asante sana mheshimiwa”Aliongea na kisha alitoa  karamu nyeusi  flani hivi pana kidogo lakini ya kawaida , kama zile za rangi na kisha alianza kuifungua kama mtu ambae anatoa  ule mrija wa wino, na akatoa kifaa Fulani hivi kama kile  kichwa cha kuchomekea kwenye Earphone  lakini hiki kwa juu mwisho kina kitu kama kigoroli.

“Hili ndio faili mheshimiwa”Aliongea na kisha  alimpatia  Jeremy  kile kidude na mheshimiwa alishangaa m inakuwaje kadude kama hako kawe ndio faili ambalo alikuwa akilisubiria kwa hamu.

‘”Usishangae mheshimiwa Hata Urusi  sasa imeendelea kwenye teknolojia , na hio ni mbinu yetu mpya kuficha taarifa wakati wa kuzisafirisha” ’Mheshimiwa Jeremy hapa alishangaa na akachukua Tablet iliokuwa kwenye meza yake na kuchomeka kale kadude na baada ya tablet ile kusoma kama Earphone ilisoma kama  memori , alishangaa  na Viladkov akatabasamu.

“Ni taarifa nyeti sana hio , na serikali ya Urusi imelipa kiasi kikubwa kuinunua kwa mtu aliekuwa akiuza”Aliongea bwana huyu  na mheshimiwa Jeremy  aliifungua  na ajabu ni kwamba alikutana na picha.

“Mbona ni picha sio kama  faili nilivyokuwa nikitegemea?”

“Angalia kwanza hizo  picha  mheshimiwa kwa umakini na  uniambie umegundua nini?”

Alianza kuangalia hizo picha kwa kuzizoom  na katika picha hizo kulionekana  meli kubwa ya mizigo ikiwa inashusha  mavyuma , lakini baada ya mheshimiwa kuangalia kwa  ukaribu Zaidi aligundua ni bawa la Ndege.

“Linaonekana  kama bawa la Ndege”

“Angalia na hio nyingine” Aliangalia na pia yenyewe ilionekana kama baadhi ya vipandevvipande vya mabaki ya ndege.

“Hio meli inamilikiwa  na kampuni Neptune , kampuni ambayo ni sehemu ya  kampuni kubwa ya kuzalisha   ndege ya  kimarekani inayofahamika kwa  jina la  Ngebo Aeronautical”Mheshimiwa alionekana kushangaa , lakini pia alizidi kuongeza umakini.

“Hizo picha zilipigwa Tarehe saba  March 1998”Aliongea na mheshimiwa huyu alishangaa sana.

“Unataka kumaanisha kwamba  ni siku moja kabla  ya ndege ya Malaysia kupotea?”

“Ndio  kutoka sehemu ambayo meli hio ilipo na sehemu ambavyo ndege  ya shirika M ilipotea  ni umbali wa kilomita ishirini tu , kwa maana hio  hayo ni mahesabu ambayo yamepigwa kabisa na hio meli ilitupa mabaki  hayo unayoyaona kwenye hizo picha eneo hilo”Mheshimiwa Raisi alijikuta akitetemeka maana anacho ambiwa hapo ni taarifa nzito sana , tena nzito kweli kweli.

“Mheshimiwa  hii ni siri ninayokupatia ambayo ni siri kubwa ndani ya  taifa la Urusi na ni kama Asset  kwetu , hivyo taarifa hii inapaswa kuwa siri , mheshimiwa Raisi Viladmn  karuhusu upatiwe taarifa hio ili kwa ajili ya kushawishi mataifa ya Afrika  kuingia kwenye Mpango TASAC”Mheshimiwa alishangaa  Zaidi.

:Mheshimiwa chomoa hio flash na uichomeke tena” aliongea  Viladkov na mheshimiwa alichomoa na kuichomeka tena na ikasoma tena kama memori  , aligusa  ten ana zile picha zikawa zimefutika ils sasa kulionekana faili lililokuwa  kwa mfumo wa ‘Xml’ , mheshimiwa alilifungua na  kuanza  kusoma na hapa ndipo aliposhangaa.

“Hio ni barua  ya wito iliotumwa kwa mashirika ya kijasusi  makubwa yote duniani na katika hio barua inaonesha kulikuwa na makubaliano ambayo yalikuwa  yanatakiwa kufanyika  juu ya mpango  ambao ulipewa  jina la LADO  ambapo sisi  tulishindwa kung`amua kirefu cha   neno hilo  , na shirika letu pekee ndiio  halikutuma muwakilishi kwenda kuhudhuria kikao hiko ambacho kilifanyikia nchini Italy”Mheshimiwa jasho lilimtoka  maana kadiri anavyoambiwa ndio anavyoona siri hii kuzidi kuwa nzito na kuhofia Maisha yake.

“Kwa hio unamaanisha kwamba LADO na kupotea kwa ndege ya shirika la M  ni swala ambalo lina muunganiko na limeratibiwa kwa makubaliano ya mashirika makubwa ya kijasusi duniani?” Aliuliza  na jamaa alitingisha kichwa  kukubaliana nae.

“Kwanini   mmeamua kunipa hii taarifa?”

“Mpango TASAC ni mpango ambao unahusisha serikali ya Urusi  kurudisha umoja wa Kisoviet , lakini hili ili liweze kufanikiwa  , tunahitaji sapoti  kutoka Afrika , tunahitaji udhaifu kutoka kwa mataifa makubwa ambao utatusaidia pale itakapobidi serikali   yetu kuingia vitani , mataifa haya hayatoi msaada   , lakini nyie wa mataifa ya Afrika  mnapaswa kutuunga mkono  kwa kukaa kimya.”

“Na ili swala hili lifanikiwe unapaswa kuhakikisha   asiliamia sabini ya mataifa ya Afrika yanakuwa kwenye huu mpango TASAC  na mheshimiwa Raisi wa Urusi amekuchagua wewe kutokana na uzoefu wako  katika uongozi,  ukifanikisha mpango huu basi serikali  ya Urusi itafanya juu chini kubaini ni nini kipo ndani ya operesheni iliopewa jina la LADO”.

“Natakiwa kukubali swala hili hapa hapa?”

“Hapana mheshimiwa , swala hili lina umuhimu sana kwa   nchi yetu na mheshimiwa Raisi atakupigia simu na mimi nipo hapa kwa ajili ya kukueleza haya , kwani tunajua kuwa wewe ni mmoja ya wahanga wa AJali ya  ndege  na unataka kulipiza kisasi , lakini kutokana na ukubwa wa tukio lenyewe  na udogo wa taifa lako, hautoweza kupata hio nafasi  ya kuujua ukweli”Aliongea bwana huyu na heshimiwa Jeremy alikubali kuwa kiongozi wa juu wa mpango TASAC.

****

“Sauron  habari za muda huu?”

“Salama  kabisa mfalme  Pluto, habari za Tanzania?”

“Hapa ni kwema kabisa Sauron , nimekupigia kupata ripori ya yale tilioongea jana”

“Mfalme Pluto , nimeshayakamilisha yote na nimepanga vijana kumi wenye uwezo wa hali ya juu kwa ajili ya kuja nchini Tanzania, lakini kuna jambo  moja nimeona nitoe pendekezo”

“Edelea kuongea Sauron nakusikiliza”

“Nimeona makomandoo hawa wakiingia nchini kama watalii  hawatapata kibali cha muda mrefu cha  kukaa  hapo Tanzania ,  hivyo nimejaribu kuwasiliana na balozi ya Sweeden  nchini Tanzania na kuwaomba watufanyie mpango wa kuwaingiza  wanajeshi wetu  kama wafanya kazi wao”Roma Alitabasamu.

“Sauron wewe  unakili sana , hili sikulifikiria , ni kweli watapaswa kukaa  nchini muda mrefu kidogo kwani pia nataka wamlinde mke wangu”Sauron alishangaa.

“Mfalme Pluto usiniambie umepata mke?”

“Ndio Sauron , sio muda mrefu sana  nimefanikiwa kupata mke”

“Hongera sana mfalme Pluto , ila kwa hatua hio sidhani kama utarudi  huku kisiwani”

“Yanayotokea kesho hatuyajui Sauonoi hivyo siwezi kuongea lolote juu ya hili”.

“Ni kweli Mheshimiwa Pluto  , ila nitatamani kumuona malkia wetu”Roma alitabasamu

“Utamuona Sauron nitakuja nae  siku moja , Sauron kuna jipya lolote kutoka The Zeros?”

“Mfalme Pluto vijana  bado wanaendelea kufuatilia na naamini muda si mrefu watatupatia taarifa “

“Sawa Sauron  , nadhani tutawasiliana  baada ya vijana kufika Tanzania”Baada ya hapo waliagana na Roma  akakata  simu .

Muda huu Roma anawasiliana na   Sauron ilikuwa ni saa moja kwenda saa mbili hivi , hivyo baada ya kumaliza tu aliitwa na Bi wema kwa ajili ya chakula cha usiku.

Baada ya kufika tu chini na Edna alikuwa akishuka  alievalia kigauni kilichokuwa kikipeperuka  kiasi kwamba kilimfanya Roma aliekuwa chini  ya ngazi aone  mapaja ya   malaini ya Edna na alijikuta hisia za mapenzi zikimuandama.

“Kukaa na mwanamke kama Edna halafu hupati kitumbua chake ni swala ambalo  nina uhakika madaktari wataniambia ni sumu kwa Afya yangu , nikimaliza hapa nduki  kwa Rose nikapunguze kichupa”Aliwaza Roma huku akivuta  kiti na kuketi.

Edna na yeye alijikuta  akitabasamu baada ya kumuona Roma leo hajatoka  kabakia nyumbani , kwani mara nyingi hakuwa akipenda sana Roma a tabia yake ya kutoka na kurudi  asubuhi yeye  kama mke aliona sio vizuri.

Wanafamilia hawa walikula  wakashiba na baada ya hapo Edna aliungana na Bi wema  kusafisha vyombo , lakini wakati Edna akiwa bize na vyombo upande wa jikoni Roma alimchungulia kwenye mlango.

“Bebi ndio natoka hivyo , hapa hadi kesho”Aliongea Roma na Edna ambaye alikuwa ameweka mikono yake kwenye Sink alijikuta  akikunja ngumi kwenye maji na kung`ata meno , kwani kila ambacho kilikuwa kikimfurahisha dakika chache nyuma  kimegeuka ndivyo sivyo,Edna aliishia kutingisha kichwa na Roma hakujali  aliondoka.

“Yaani huyu mwanaume hatulii nyumbani”Aliongea Edna kwasauti  pasipo kujua nyuma yake kasimama jasusi mbobezi wa  mapenzi Bi Wema.

“Miss ulifikiri sasa atafanyaje , mmeoana lakini  hamlali  chumba kimoja , yule ni mwanaume na wanaume tendo la nndoa  ni kama  hitaji lao la msingi hawezi kukaa na mtoto mrembo kama wewe halafu akuangalie kama picha ya ukutani”Edna alifikiria kidogo.

“Bi Wema nitafanyaje  , bado sina hisia nae na wewe unaelewa tumeoana kimkataba”.

“Naelewa ndio , lakini miss angalau  jaribu kuufungua moyo kwa Roma , huenda ukampenda na mkawa Mume na mke  kimapenzi  sio kimkataba”Edna alitingisha kichwa  kuelewa

Baada ya kufika  chumbani kwake alionekana kuwaza maneno ya Bi Wema  na kuona kidogo yana maana.

“Au nijaribu kumpa?”Aliwaza Edna akimaanisha ajaribu kumpa Roma kitumbua.

Previoua Next