Ni jumatatu asubuhi iliokuwa imekucha na makucha yake , wengi huwa hawaipendi hii siku kutokana na mambo mengi ambayo huwa yanatokea wikiend , sio wanafunzi , sio waajiriwa kila mtu anasababu yake ya kutokuipenda hii siku , lakini kwa mwanadada Edna alikuwa na motisha , kwake jumatatu aliichukulia kama safari ya wiki ya kimafanikio.
Mwanadada huyu alikuwa na jambo kubwa sana mbeleni ambalo alikuwa akilipanga kulifanikisha , dili ambalo kama likienda kama alivyokuwa amepanga , lingezidi kumfanya kuwa mwanamke Tajiri Zaidi , lakIni pia kampuni yake ingezidi kuchanja mbuga na kufahamika duniani kote na ndio maana hakutana ‘glitches’ za aina yoyote katika mkataba anaokwenda kusaini na kampuni ya Yamakuza , kampuni kubwa ndani ya taifa la Japani.
Kwake uwekezaji huo ndio mkubwa Zaidi kuwahi kuutekeleza tokea aichukue kampuni hio kutoka kwenye mikono ya mama yake na kama dili hilo pia litafanikiwa ndio dili ambalo litaifanya kampuni yake kuwa na mafanikio makubwa ndani ya mwaka huo.
Asubuhi ya leo alikuwa ameketi kwenye kiti akipata ;Breakfast’ , huku Roma akiwa mbele yake , upande wa kushoto kwake kulikuwa na Bi Wema ambaye muda wote alikuwa akimwangalia Roma kwa tabasamu akiwa ni mwenye kufurahishwa na uwezo wa kula wa Roma.
“Siku zote nyumba ikiwa na mwanaume inaonekana kuwa hai”Aliwaza mwanamama huyu Mzungu wa Roho.
Upande wa Edna , macho yake yalikuwa kwa Roma , aliwaza Roma ni mwanaume wa aina gani , kwanza amerudi asubuhi hio akitoka kwa wanawake wake , lakini alionesha kutokuwa na hatia hata kidogo , ndio ndoa yao ni ya mkataba lakini angalau aonyeshe ile heshima ambayo ambayo ipo ndani ya neno ‘Ndoa’ lakini kwa Roma hakuwa ni mwenye kujali.
Edna aliendelea kutafakari , kwanini Roma yupo kama alivyo Roma , kwanini hakuwa siriasi na Maisha , haoneshi kuwa na mipango ya kimaisha ya baadae , yeye anafikiria kufanya mageuzi katika biashara lakini mume wake wa mkataba yeye anafurahia chakula na wanawake pasipo mpango wowote alikuwa akishangaa na kujiuliza maswali lakini alikosa majibu.
“Mke wangu , itoshe kusema najivunia sana kuwa mumeo ,maana hii ‘breakfast’ ni nzito , wakati nabeba mizigo kwenye soko la Mbagala kuna siku nilikuwa nashindia mihogo”Aliongea Roma na kisha alibeba bakuli iliokuwa na mchuzi na kupeleka mchuzi wote tumboni.
“Roma unaonaje kwanzia sasa ukiwa siriasi na kazi?”Aliongea Edna aliekuwa akimwangalia ,Roma kabla ya kujibu alichukua yai la kuchemsha na kuligonga mezani na kisha akaanza kulibandua na kisha akalipeleka mdomoni lote , akavuta kikombe cha chai na kushushia..
“Aargh … mke wangu umeng`ang`ania na mimi kuwa siriasi na Maisha , lakini mimi najiona niko siriasi”.
“Uko siriasi kivipi Roma , kila siku naletewa ripoti ya wewe kucheza magemu tu kazini na kwenda kula , huo usiriasi unaozungumzia ni upi, haya ukirudi nyumbani badala ya kukaa kutulia na kuwaza siku ya kesho ,ila wewe unawaza wanawake na unaenda huko unalala na unarudi asubuhi kweli Roma”Edna leo hii asubuhi alionekana kuwa na nongwa sana , kiasi ambacho kilimfanya Roma kushangaa nini kimempata mke wake mpaka kuanza kulalamika.
“Mke wangu wewe piga kazi , mimi nitaishi kama mtoto wa Tajiri , nitafute mapesa mengi ya nini wakati hizi hatutazimaliza …Bebi Edna labda tukipata mtoto na nikiitwa baba naweza kuishi kama baba”.
Edna hakutaka kuongea maana aliona kuongea na Roma hakuna heri yoyote , alichukua mkoba wake na kumuaga Bi Wema na kisha akatoka.
“Sijui ninamfanya nini angalau awe siriasi na Maisha?”Aliwaza Edna wakati akiwasha gari yake .
Roma alifika kazini kama kawaida , na kuingia kwenye jengo hili ambalo kwake kila siku sehemu hii ilizidi kumvutia kutokana na harufu nzuri za pafumu za warembo.
“Romaa..”Ilikuwa ni sauti iliomwita Roma akiwa anaingia kwenye Lift na mwanadada aliekuwa akimwita alikuwa ni Benadetha.
Benadetha kwenye macho ya Roma alikuwa mrembo sana ambaye alitamani pia angalau apate wasaa mzuri wa kumjua nje na ndani , hayo ndio yalikuwa mawazo yake , lakini mwanadada huyu alionekana kuwa bize sana na kazi , muda mwingi hakuwa akipenda sana kupiga Stori kama ilivyokuwa marafiki zake.
“Niambie mrembo, za wikiend?”
“Nzuri vipi wewe?”
“Njema kabisa”Alijibu Roma wakati wakiwa wamesimama wakisubiria Lift ifunguke waingie , lakini mara nyuma yao wakasimama wanaume wawili na wanaume hawa hawakuwa wengine bali alikuwa ni Abu na Elvice .
Elvice baada ya kumuona Roma alijikuta akikumbuka tukio ambalo alifanyiwa na Roma na alijikuta hofu ikianza kumjaa,Benadetha alisalimiana na Abu pamoja na Elvice , ila Roma alionyesha hali ya kutofurahia uwepo wa mabwana hawa.
“Mmekuja kufanya nini hapa?”Aliuliza Roma pasipo kusalimia , huku Benadetha yeye akitangulia akiwaacha Abu na Elvice wanamwangalia.
“Mr Roma nadhani uwepo wetu hapa haukuhusu , kwanza nasikia una nafasi ndogo sana kwenye hii kampuni kwanini tuongee na wewe juu ya swala lililotuleta hapa?”Aliongea Abu kwa kejeli na Roma kwanza alitabasamu.
“Ni kweli sipaswi kujua nini kimekuleta hapa , lakini naamini unakumbuka onyo nililokupa mara ya mwisho , hivyo kuwa makini”Aliongea Roma na muda huo huo Lift ilifunguka na Roma aliingia huku Abu na Elvice wakiwa wamesimama wakiangalia Lift hio inajifunga taratibu na Roma akamwangalia Elvice na kumkonyeza.
“Hawa mafala wote wamekuja kufanya nini hapa?”Alijiuliza Roma wakati akiingia ndani ya ofisi aliokuwa akifanyia kazi na aliiendeea meza yake , huku akisalimiana na baadhi ya wafanya kazi wenzake ambao walikuwa bize , isipokuwa tu Recho pekee ambaye hakuonekana kwenye meza yake na alijiuliza ni kwannini mwanadada huyo hakuwa amefika kazini , lakini alipotezea.
“Hapa nicheze EuroTrack simulator nipoteze poteze muda , hii kazi siipendi , sema ndio hivyo kuna warembo wanaonipa motisha lakini pia nataka kumridhisha mke wangu”Aliwaza Roma na kuwasha gemu na kuanza kucheza , lakini bado akili yae ilionekana kutofarahia gemu hilo , ni kama moyo wake haukuwa na amani , baada ya kuona hafurahii aliinuka kwenye meza yake na kutoka nje ya ofisi, huku wafanyakazi wenzake wakimshangaa , aliingia moja kwa moja kwenye Lift na kwenda juu.
“ Miss Airport nahitaji kuonana na CEO”Aliongea Roma mara baada ya kumfikia Monica mwanamke ambaye alikuwa sekretari wa Edna , kwa Roma mwanadada huyu alimuona kama mbaya kuliko wanawake wote wa hii kampuni , kwanza kabisa alimuona kuwa na kifua ambacho hakikuwa na manyonyo na kilikuwa Flati kama vile barabara za Airport.
Kwa huyu Monica na yeye hakuwa akipendezwa kabisa na Roma , alionekana kutompenda kwenye hii kampuni na alitamanni awe na uwezo amfukuze , lakini licha ya kutokumpenda hakuwa akijua kuwa Roma ni mume wa Boss wake.
“Yupo ila ana wageni huwezi kuingia”Aliongea Miss Airport .
“Miss Airport haujui kujibu maswali , darasani ulikuwa unapata ngapi mimi nimeuliza swali moja ila wewe umajibu mawili”Aliongea Roma na kuuendea mlango wa CEO na kuufungua na kuzama ndani na Monica alipandwa na Jazba na kumfuata Roma.
Roma baada ya kuingia alikutana na Sura tano , ya kwanza ilikuwa nni ya Mke wake ambaye yuko ‘Composed’ kama ilivyokuwa kawaida yake ya kujiamini akiwa amekunja nne na suti yake ya rangi nyeupe , wa pili alikuwa ni Nadia mwanasheria Mpya wa kampuni na Roma hakumtaraia ndani hapo na watatu alikuwa ni Doris ambaye alikuwa amependeza kama kawaida , lakini alikuwa na uso wa usiriasi, wawili wa mwisho ni wanaume ambao Roma hakuwa akiwapenda hasa wakiwa karibu na mke wake yaani Abubakari Hamadi na Elvice Temba.
Kwanza wote watano walijikuta wakimwangalia Roma ambaye aliingia bila hodi na muda huo huo na Monica aliingia.
“Boss nisamehe nimejaribu kumzuia lakini hakunielewa”Aliongea Monica kwa wasiwasi mno , aliogopa kumkasirisha bosi wake.
“Unaweza kwenda kuendelea na kazi Monica”Aliongea Edna ambaye alionekana kuwa kawaida , lakini alikasirishwa na kitendo cha Roma kuingia hapo ndani moyoni kwani alikuwa na kikao muhimu sana na wageni wake, baada ya Monicca kutoka Roma alijongea mpaka upande wa kiti anachokaa mke wake na kisha akaketi huku akizunguka zunguka , hakuwa na wasiwasi hata kidogo, Abuu alikuwa na hasira alitamani afanye shambulizi palepale kwa Roma , kwani alikuwa akimchukia sana bwana huyo , lakini hakuwa na ujasiri wa kupambana na Roma ana kwa ana , alijua sio saizi yake , kwa upande wa Elvice na yeye alikuwa hampendi kabisa Roma , hasa akikumbuka bwana huyo ni mume wa Edna alijikuta akitaka kuonyesha uwezo wake wa kimapigano aliokuwa ameupata akiwa jeshini , lakini alivyokumbuka namna ambavyo Roma macho yake yalibadilika na kutaka kunyongwa na mkono mmoja aliogopa na kuona atulize mshono
Upande wa Doris na Nadia haikuelewaka walikuwa na mawazo gani ila walimwangalia Roma kwa macho ambayo yalikuwa na maswali mengi , upande wa Edna alikuwa akimwangalia kila mmoja aliekuwa hapa muonekano wake , na kisha akamgeukia Roma.
“Mke wangu kipenzi , Endelea na kikao chako sijaja kukuvuruga”Aliongea Roma na kisha aligeuza kiti chake na kuangalia upande wa nje kwa kutumia Dirisha akiangalia upande wa bandari hii ya Dar es salaam ilivyokuwa bize.
Edna hakuwa na chakumfanya Roma , kwanza angeonekana sio mke bora kama angemfukuza , lakini pia lilikuwa ni jukumu lake kumlindia heshima Roma kama mume wake , walikuwa wameoana kwa mkataba lakini alikuwa akiheshimu sheria za ndoa , hivyo aliwasihi wenzake waendelee na kikao.
“Tunaweza kuendelea , Roma ni mume wangu hivyo hakuna kinachoharibika akiwepo hapa , labda kama kuna mwenye shida na uwepo wake”Aliongea Edna na kuwaangalia wenzake na Nadia ndio aliekuwa wa kwanza kutingisha kichwa chake kuonyesha anakubaliana na Edna , na wengine wote wakaonyesha sura za kwamba hakuna tatizo , ila ukweli kila mmoja hapo ndani hakufurahishwa na kauli ya Edna , kila mtu aliona kauli hio kama Risasi iliozama moja kwa moja moyoni na kutibua chemba za moyo.
Kikao kiliendelea na Roma aligeuka na kuanza kutumia Computer ya mke wake , kama kawaida alikutana na gemu la nyoka na kuanza kucheza huku akila Karanga zilizokuwa kwenye kibakuli.
“Kutokana na ukubwa wa uwekezaji huu naamini viongozi wote wa juu tunapaswa kwenda Japan kusaini huu mkataba na hayo pia ni mapendekezo ya Viongozi wa Yamakuza”Aliongea Abubakari.
“Kuna ulazima wa CEO wote kusafiri mpaka Japan ?”Aliuliza Edna.
“Ndio Edna” Maagizo niliopewa na Yamakuza ni kwamba CEO Abubakari na wewe lazima muwepo , hili ni dili kubwa sana ambalo kampuni ya Yamakuza inafanya kwa mara ya kwanza na kampuni za Afrika ,tusilichukulie kwa wepesi”Aliongea Elvice na alionekana yupo hapo ofisini kuwakilisha kampuni ya Yamakuza.
“Kuna ulazima gani wa mke wangu kwenda?”Aliuliza Roma kwa sauti na alionekana kukerwa sana na Elvice kwani aliona hakukuwa na sababu ya Edna kwenda kama tu anataka kuwakilishwa na mtu mwingine.
“Mr Roma hili ni swala ambalo linahusu uongozi wa juu wa kampuni , hivyo unatakiwa ukae kimpya mabosi wako tukiongea”Aliongea Abubakari na Roma kwanza alitabasamu.
“Kwanza nikurekebishe , unaonekana hauko profesheno na kazi yako , mimi sio boss wako , pili sioni haja ya Edna kwenda kama anataka kuwakilishwa na mtu kutoka kwenye kampuni , sioni utofauti mtu mwingine akienda , kwani mazungumzo ya kibiashara yashafanyika kupitia mkataba na kule ni kitendo cha kutia sahihi , kuna tatizo gani hapo , au shida tu uende na mke wangu”
Abu na Elvice walionekana kukasirishwa sana na Roma , ni kweli hakukuwa na shida ya Edna kwenda ila Elvice alitaka atumie nafasi ya kwenda Japan na Edna ili akajiweke karibu na angalie namna ya kumpata mrembo huyo, na mpango wa Elvice na wa Abuu hakukuwa na utofauti na kila mtu aliona hio ndio nafasi ya kuongeza ukaribu na Edna , lakini waliona mipango yao Roma anaingilia , kwanini wafurahi.
“Alichongea Roma ni sahihi , hakuna haja ya CEO kwenda kama anataka kutuma mwakilishi naweza kwenda mimi au Doris na hata Nasra ambaye ni mhasibu mkuu wa kampuni”Aliongea Nadia na Roma alikumbuka kwanini Nasra hakuwa kwenye kikao hicho kwani na yeye pia swala hili la mkataba lilikuwa likimhusu.
“Swala hili sio nani kwenda , swala ni kwamba kampuni ya Yamakuza wamotoia ombi hilo kama Sharti”Aliongea Elvice na alimfanya Roma akasirike Zaidi , jambo ambalo kwa Nadia na Doris hawakulipenda , kwani Roma alikuwa akionyesha wivu waziwazi.
“Mimi Roma Ramoni .. Edna ni mke wangu licha ya kwamba ni kiongozi mkubwa wa kampuni hii lakini pia lazima apate baraka zote kutoka kwangu hilo ni la kwanza , la pili naomba nimuulize mke wangu ..” huku akimwangalia Edna
“Mke wangu kwenye huo mkataba kuna kipengele chochote ambacho kinakulazimisha wewe kwenda Japan??”Edna alitingisha kichwa kama hakuna na Roma alitabasamu.
“Sasa nasema hivi nisikie mtu anaongea tena kuhusu Mke wangu kwenda kusaini huo mkataba uone ..”
Aliongea Roma na kurudi kwenye kiti na kuendelea kucheza gemu baada ya kutoa biti ambalo lilimkasirisha kila mmoja Abu na Elvice walikasirishwa na kitendo cha Roma kuharibu mipango yao na Doris na Nadia walionekana kuwa na wivu wa Roma kumlinda Edna , walitamani nafasi hio iwe ya kwao.
Elvice na Abuu japo ya kukasirika walipiga kimya , hakutaka tena kuongea swala hilo, kwani waliogopa.
“Okey kwa upande wangu ataniwakilisha Doris pamoja na Mume wangu”Aliongea Edna na kufanya hali ya hewa ibadilike.
Comments