Reader Settings

Roma alishangazwa na mke wake kumpendekeza kwenda Japani na Doris kwa ajili  ya kusaini mkataba huo , lakini sio kwake tu alieshanga , kila mmoa hapo ndani alishangaa isipokuwa Dorisi.

“Naona mmeshangaa , lakini nimemchagua mume wangu kuniwakilisha  kwakua  anafahamu vizuri kuzungumza kijapani  , itakuwa msaada mkubwa kwa Doris  pia”Aliongea Edna na na alionekana maamuzi yake ni ya mwisho  na hakukuwa na wakupinga , ila Roma bado alikuwa akiwaza  kwanini mke wake anafanya hayo pasipo kumuambia kwanza kama anataka kwenda Japani  au la.

Kikao kiliisha  na Edna aliwaambia waondoke  kwani alikuwa  na mazungumzo na mume wake na hakukuna aliekuwa akipinga wote walikuwa  ndani ya ofisi ya  mwenye kampuni na pia Edna na Roma  ni mume na mke hivyo  ni haki yao kuongea hata kama hawapendi.

“Mke wangu kuna ulazima mimi wa kwenda  Japani ,Doris  anaweza kufanya vizuri tu kwani anajua kingereza”.

“Mimi ndio bosi wako na nishafanya maamuzi  hivyo, Kwanza inuka kwenye kiti changu”Aliongea na Roma hakuleta ubishi alinyanyuka.

“Lakini hata kama, kwanini haukuniambia mapema , tokea nyumbani  , jana tumeshinda wote  hausemi”Edna alinyamaza hakujua aseme nini , ukweli Edna alitaka kumwambia Roma jana yake usiku lakini Roma aliondoka kwenda kwa mahawala wake hivyo alikosa nafasi.

“Kama hutaki kwenda nitaenda mimi  mwenyewe”

Roma alijikuta akianza kufkiria , aliwaza kama Edna akienda wale mamluki lazima wangetumia nafasi hio kuweka mazoea na mke wake , lakini pia aliamini huenda Edna hakutaka kwenda kutokana na kuwakwepa Abu na Elvice , aliona huenda ni maamuzi sahihi mke wake ameyafanya.

“Okey mke wangu nitaenda kukuwakilisha vyema na kuhakikisha  dili lako linafanikiwa”.Edna alitingisha kichwa.

Na Roma aliona asiendeleea kukaa hapo ndani  na aliusogelea  mlango kwa ajili ya kutoka.

“Roma..! “Aliita Edna na kumfanya  Roma ageuke amwangalie

“Nini mke wangu?”.

“Najua siku tuliosaini mkataba  haukuusoma licha ya kwamba nilikuambia uusome”

“Ndio , lakini mkataba unaingiaje hapa Edna?”Edna alifikiria  kidogo kwa kukaa kimya  na kumwangalia Roma .

“Basi unaweza kwenda tutaonana nyumbani”Aliongea na Roma alitingisha kichwa na kisha akatoka.

“Ningemwambia mkataba wetu  unakipengele cha kutoingiliana  kwenye maswala ya kikazi  huenda angekasirika nadhani nimefanya jambo zuri kutoongea , ningezidi kujiweka mbali  na yeye na ushauri wa Bi Wema  pia   ni wa maana lakini pia nataka kujua kwanini macho yake yanabadilika”Aliwaza Edna.

“Miss Airport kazi njema” Aliongea Roma huku akimpita Monica ambaye aliishia kubenua midomo, hakupendezwa na Roma lakini pia alijiuliza kwanini anamwita “Miss Aiport’ .

Roma baada ya kutoka moja kwa moja alienda kwenye ofisi ya Doris, alitaka kwenda kumpetipeti mwanamke huyo kwani  alijua alikuwa na hasira nae , kwani macho yake wakati wakiwa ndani ya ofisi yalikuwa yakionyesha kabisa , hali iliokuwa ikiendelea kwenye  kichwa cha mrembo huyo .

Aliingia na kumkuta akiwa bize kama kawaida  akiwa na miwani  ya kuzuia mwanga wa Bluu wakati wa kutumia  tarakishi,licha ya kumuona Roma ameingia lakini hakutaka kumuongelesha Roma , bado alikuwa na chuki nae.

“Bebi Doris , acha kujifanya haujaniona”.

“Roma niko bize  kwasasa naomba kama hauna jambo la maana usinisumbue”Roma alitabasamu na kisha  akasogea   mpaka kwenye kiti cha Doris na  kukigeuza na kikazunguka na wakaangaliana.

“Roma nimekuambia nina kazi naomba utoke ofisini kwangu , jaribu kuwa muele..” Kabla  hajamaliza  Roma alikuwa ashanasisha mdomo wake kwa Dorisi na kumfanya mwanamke huyu atoe macho  na kuanza kumsukuma Roma , lakini alishindwa kwani Roma alikuwa amembana haswa , na alishitukia mkono umetua kwenye suruali yake, kwenye kitumbua chake  na alihisi shoti ikisambaa mwili mzima  na Roma aliendelea kufokonyoa.

Dakika mbili mbele Doris hisia zilimzidia na alishindwa kujizuia , akili ilikuwa inamwambia unachofanya sio sahihi na hapo ni ofisini lakini mwili haukuwa tayari kuacha na Roma alitumia udhaifu huo haswa kwani aliongeza mashambulizi  na kuendelea kufokonyoa.

Dakika tano  mbele Doris alimvua surali Roma mwenyewe na kutoa Mchi wa Roma  , huku akisimama kabisa na waliendelea kunyonyana midomo , hakuna aliewaza kabisa hapo ni ofisini  , akili zao zilikuwa mbali kabisa , baada ya  Roma kuona  jaribio lake limefanikia  alifyatua  suruali ya Doris na kuishusha akikusanya na nguo ya ndani kwa wakati mmoja  na Dorisi alielewa somo kwani alishikilia kiti  na kubinuka kimbuzi mbuzi na Roma akauzamisha mpini na kilichosikika hapo ni miguno  ya kuzidiwa kutoka kwa Dorisi.

“Romaa..Arrgh..”

Doris hakuamini kama amefanya uzinzi kwenye ofisi yake , siku zote alikuwa ni mwenye kujiambia kwamba hata iweje  hawezi kupanajisi  sehemu yake anayofanyia kazi , lakini siku hii ya leoalikuwa  amefanya kile alichokuwa  hataki kitokee.

“Naomba utoke niendelee na kazi”Aliongea  Doris huku akimwangalia Roma.

“Seme bebi cha ofisini ni  kitamu balaa”.

“Roma naomba  utoke”Alitumia kauli ya kibabe  na Roma hakuwa na ubishi alitoka zake  na kurudi kwenye  ofisi yake anayofanyia kazi  kuendelea na kucheza gemu.

Ile anakaa na kutulia  tu simu yake ilianza kuita na alipoangalia anaepiga alikuwa ni Najma ,  alijikuta akijilaumu  kwa wakati mmoja kumsahau Najma kwani tokea amuache hospitalini  hakuwa amemtafuta hata kidogo.

Alipokea na Najma alionekana kumlalamikia Roma kwamba  kamdanganya  , kwani alimuahidi kwamba atarudi  na Roma nae hakuwa nyuma alimpa habari za kiuongo  uongo na mwanadada huyo alikubari japo kishingo upande.

Ki ufupi ndani ya moyo wa Roma alikuwa akimpenda Najma lakini alikuwa mzito sana  kuuanzisha mahusiano nae , hakujua ni kwanini  lakini aliona kukaa mbali na Najma ni heri Zaidi kuwa nae na ndio maana hakuaka sana kuonekana mbele ya Najma.

****

Ilikuwa ni muda wa  usiku saa nne  hivi kwenda saa tano , ndani ya jiji la Mwanza ,alionekana mwanamke ambaye alikuwa akikimbia huku akiwa ameshikilia tumbo kwa mkono mmoja , huku mkono mwingine ukimsaidia kumpa sapoti ya kutembea katikati ya chochoro zilizokuwa ndani ya eneo la Mabatini.

Mwanamke huyu alionekana kupitia maumivu mengi , kwani damu nyingi zilikuwa zimeganda kwenye  nguo zake hasa upande wa tumbon na kwenye kifua  ,  alikuwa amevalia suruali ya jeans rangi nyeusi  na  viatu vikubwa kama Mabuti vyeusi  , huku akiwa na blazia ya rangi nyeupe ambayo ilimfanya  damu iliokuwa imemtoka na kusambaa  na kuonekana vyema.

Watu waliokuwa kwenye hili eneo  walionekana kumshangaa mwanamke  , licha ya kwamba alionekana kutaka msaada kutoka kwao kutokana na hali yake ila hakukuwa na mtu mwenye ujasili wa kumsaidia  na pia kwa mwanamke hakuonekana kuwa tayari kuomba msaada kwa watu waliokuwa ndani ya hili eneo ,ni kama mtu ambaye hakutaka kumbebesha mtu mzigo juu ya mazira yake.

Baada ya mwanamke  kutembea kwa umbali mrefu , akikaribia kutoka  ndani ya sehemu hii iliokuwa ikifahamika kwa jina la Mabatini kuingia mtaa mwingine upande wa kushoto , alijikuta akidondoka  pembeni  ya bababara    , sehemu ambayo ilikuwa na nyasi ndefu kidogo  zilizomfanya kumzibia kwa mbele asipate kuonekana kwa wale wanaopita , lakini sehemu hii  pia kulikuwa na mti   mkubwa  ambao ulifanya hili eneo liwe na kivuli kilichofanya giza kuwa kubwa kuliko maeneo mengine .

“Atakuwa ameelekea wapi?” Aliuliza kijana mmoja  kati ya watatu  walikuwa barabarani mita kadhaa kutoka alipodondokea Mwanamke , walionekana walikuwa wakimfafuta , wanaume hawa walikuwa wameshikilia siraha mkononi na walionekana walikuwa wakimtafuta mwnamke   kwa ajili ya kumfanyia shari.

“Ngalu  ana jeraha la risasi ,  hawezi kwenda  mbali maana amepoteza damu nyingi “Aliongea lakini moja ya wale wanaume aliona  majani yaliokuwa upande wake yakitingishika , huku akiwa ameona kivuli cha mtu lakini  ni kama hakuwa na uhakika.

“Oya pale” Aliongea na wenzake wote wakageuza macho kuangalia na hawakutaka  tu kuangalia kwa umbali , walianza kusogea ndani ya  eneo hilo  , ili kuhakiki kile wanachodhania.

Walijongea kwa tahadhari kubwa  sana , lakini kabla hata hawajaafika ile sehemu , mmoja  aliangalia chini  na kuona kitu .

“Oya Kishoka angalia hiki”Aliongea  bwana huyu mfupi kuliko wenzake wote huku akiwa ameshikilia kitambaa  aina ya Bandama , walianza kukikagua.

“Ndio ni  damu hii , hayuko mbali “ waliongea huku wakianza kutawanyika , kwani waliona mtu ambaye walikuwa wakimtafuta alikuwa  maeneo hayo .

Upande mwingine  , wakati vijana hawa wakiendelea  kutafuta , Mwanamke alikuwa mita kadhaa kutoka walipokuwa wamesimama  na alionekana kuvumilia kutoa kelele kwani maumivu yalikuwa makali , ni kweli alikuwa amedondosha kitambaa alichokuwa akitumia kuzuia sehemu ya jeraha la risasi na kufanya  kidonda kizidi kuvuja damu huku maumivu yakiwa ya hali ya juu.

“Hatimae nimekupata” Aliongea bwana huyu aliekuwa anaitwa Kishoka   na kuwaita wenzake , Mwanamke   hakutaraia kukamatwa mapema hivyo licha ya kuvumilia sana maumivu alitamani kuongea neno , ila nguvu  zilimuishia  kabisa.

“Oya kishoka mpige risasi tuondoke”

“Unaonaje tukimpeleka kwa boss kwanza akafanya maamuzi, huenda akawa  na maamuzi mengine kuliko aliotoa mwanzo”

“Kishoka  boss alituambia tukimkamata tumpige risasi , tumpeleke wa nini sasa mtu mwenyewe anakaribia kufa , wewe mmalizie , kama unashindwa lete nifanye mimi”

“Okey Ngalu wewe mmalize” Aliongea na kisha akampatia  siraha alioshika mkononi kijana mnene kidogo alieenda hewani ambaye alikuwa akifahamika kwa jina la Ngalu na alionekana kutokuwa muoga na kuwa katili  kuliko wenzake , alinyoosha bastora kwa ajili ya kumpiga  mwanamke  aliekuwa chini akiwaangalia kwa tabu , Mwanamke alionekana kuwa nusu mfu hakuweza kujitetea hata kwa kuongea.

Mwanamke , alionekana kukata tamaa kabisa , alianza kuona  picha picha wakati akiwa mtoto  akicheza na mama yake huku akiwa na furaha sana  , alianza kuona  kumbukiumbu nzuri ambazo kwake zilionekana kuwa  ndio nyakati aliopokuwa na furaha sana katika Maisha yake alipokuwa na mama yake  ,alijikuta akilazimisha tabasamu hakutaka kufa akiwa na sononeko moyoni , tabasamu la mwanamke huyu liliashiria  hali ya kufuta yote na yupo tayari kupokea kile   ambacho Mungu amemuamulia. 

“Nisamehe mama  , sijafanikiwa kulipiza kisasi”

Aliwaza mwanadada huyu na kisha akafumba macho kusubiria saa yake ya mwisho , aliendelea kufumba macho kwa takribani dakika mbili ,  lakini bado alijiona mzima  , alifungua macho huku akiwa anadhania labda wanaume  hao wameghairi kumuua kama ambavyo wametumwa na bosi wao ,  lakini ile anafungua  macho  anakutana na sura nyingine kabisa , licha ya kwamba macho yake yalikuwa na ukungu , lakini aliweza kutambua kuwa mtu aliekuwa mbele yake alikuwa ni  mwanaume ambaye hakuwahi kumuona  mahali kutokana na mavazi yake, aliangalia pembeni na kushangaa Zaidi baada ya kuona wale watu waliokuwa  wakitaka kumuua dakika chache nyuma wanatapatapa  huku miili yao  ikishindana na  kifo , lakini licha ya mapambano hayo ya kimwili ,kifo kilionekana kuwa na nguvu  Zaidi na wakatulia tuli.

Mwanaume yule alichuchumaa na kisha alishika mkono wa mwanamke  na kisha akatoa mkono aliouweka katika  jeraha lake , na kitendo cha kutoa tu mkono damu zilianza kutoka mfululizo.

“Inaonekana umeumia sana , inashangaza mwanamke kama wewe kuwa na uwezo mkubwa wa kuvumilia maumivu” Aliongea mwanaume huyu huku mwanamke akiendelea kumwangalia kwa mshangao ,alishindwa kuongea lolote kutokana na hali yake ya kimwili kukosa nguvu hata ya kutamka neno , alichofanya ni kumwangalia   tu pasipo kusema lolote.

Yule mwanamke nguvu zilizidi kumuishia na alijikuta macho yakijifumba yenyewe pasipo yeye kuyaruhusu na mpaka hapo hakuelewa nini kiliendelea.

Baada ya kufumba  macho muda mrefu huku akishindwa kuelewa nini kiliendela , hatimae aliweza kuyafumbua , aliangaza  eneo alilokuwepo  na kujiona yupo ndani ya chumba chenye harufu nzuri , sehemu ambayo hakuwa akiijua  kabisa.

Wakati akiendelea kuangalia mandhari ya hili eneo  , huku akijihisi kuwa na nguvu kuliko alivyokuwa mwanzo , alizidi kushangaa , chumba kilikuwa kizuri  lakini  alikuwa pake yake na hakujua ni kwa namna gani alifika mahali hapo , alinyanyuka na kukaa kitako huku akianza kukumbuka  matukio yaliomtokea  na picha mbalimbali zilianza kumtokea , alikumbuka alivyokuwa akipambana na mpaka kupigwa na Risasi  tumboni, namna ambavyo alikuwa akikimbia huku akivuja damu na kusikia maumivu makali  na watu walioagizwa kummaliza wakiwa nyuma yake wanamfukuzia , alikumbuka yote hayo  lakini mwisho kabisa alikumbuka alipokuwa amekamatwa tena na wanaume  ambao walikuwa wanataka kummaliza na akafumba macho kwa mara ya mwisho kusubiria kifo chake , aliendelea kukumbuka  alipofungua macho yake na kumuona mwnaume ambaye hakuwa akimtambua  na baada  ya hapo hakuelewa  ni nini kiliendelea .

Baada ya mwanamke kukumbuka hayo , alijikuta akijiangalia tumboni   na kujiona akiwa msafi huku akiwa na mavazi mengine  kabisa , alitoa blazia ya rangi ya pink aliokuwa amevalia na kuangalia eneo la tumboni , lakini  kilichomshangaza huyu mwanamke ni kwamba sehemu yake ya tumbo ilikuwa ikifanana na sehemu nyingine za mwili , kwa maana kwamba hakukuwa na jeraha la aina  yoyote.

“Imekuwaje? Ni swali la kwanza la mwanamke huyu kujiuliza , kwani alikuwa akikumbuka kabisa kuwa alikuwa na jeraha  tumboni.

“Au nimepona , inamaana nimelala muda mrefu kiasi kwamba  hata jeraha langu limepona na kutokuacha kovu?”Aliendelea kujiuliza maswali kedekede yaliokosa majibu.

“Hapana hata kama nimepona , lazima kuwe na alama  au kovu siwezi kupona haraka sana  kwa namna hii”Aliendelea kujiuliza  mwanamke maswali meengi , lakini yasio kuwa na majibu , wakati akiendelea  kuwaza mara mlango ulifunguliwa na akaingia mwanamke mwingine.

“Habari yako dada, umeamka?”

“Hapa ni wapi na nimelala kwa miezi mingapi?” Mwanadada yule alievalia sketi  ya rangi ya bluu na tisheti ambayo kwa kumwangalia mara mmoja tu ungejua  ni muhudumu wa hoteli.

“Upo Iringa dada  , hapa ni Camp Nine Motel  , umeletwa jana na mwanaume alietambulisha kwa jina la Roa Ramoni”

“Roma Ramoni , jana???!!!”Mwanamke alishangaa  yaani  kama ni kweli aliletwa jana , inamaana ni jana yake alipigwa risasi na kuokolewa lakini pia ni jana yake ameletwa hapa Moteli na mtu anaefahamika kwa jina la Roma Ramoni akiwa na jeraha tumboni.

“Dada leo ni tarhe ngapi  na ni siku gani?”Mwanadada muhudumu alishangaa.

“Leo ni Jumanne na  ni tarehe ishirini  mwezi wa kumi  mwaka 2021”Alizidi kushagaa Zaidi na Zaidi , aliinua tena blazia aliokuwa amevaa na kuangalia sehemu ambayo anakumbuka kabisa amepigwa risasi   lakini  bado ni vilevile.

“Dada hebu kwanza naomba unieleze , wakati naletwa  hapa nilikuwaje   kuwaje yaani sikuwa nimeumia?”Mwanadada muhudumu bado aliendelea kushangaa , kwanini mteja wake ana maswali mengi , kwani alichokuwa akikumbuka kwenye akili yake ni kwamba mwanaume aliemleta  alimuachia tu maagizo kwamba mtu wake anapaswa kupewa huduma kwa uangalizi mpaka pale atakapo amka lakini hakuwa na shida yoyote Zaidi ya kuwa usingizini.

“Uliletwa kama ulivyo tofauti ni kwamba  ulikuwa tu umelala , mbona maswali mengi  dada kwani aliekuleta sio mpenzi wako?”

Mwanamke bado alishangaa maswali ya mhudumu na kuzidi kuchanganyikiwa Zaidi , alitaka kuthitbitisha kile ambacho anawaza , hakuamini kwamba  yupo ndotoni na kupigwa kwake risasi kulikuwa ni ndoto.

“Jana nimeletwa hapa saa ngapi ?”Aliuliza  mwanamke na mhudumu akafikiria kuonekana alikuwa akikumbuka.

“Umeletwa hapa kati ya saa tano  na nusu hivi”Mshangao mwingine  ulimpata mwanamke .

“Kama nililetwa saa  tano na nusu  na nilikuwa Mwanza wakati  napigwa risasi amenisafirisha vipi mpaka kunileta  Iringa ndani ya nusu saa” mwanamke aliwaza .

“Dada mini nina wateja wengine wa kuwahudumia , hizi ni pesa ambazo mpenzi wako kakuachia kaniambia ni kukabidhi baada ya kuamka  , alisema zitakusadia katika matumizi”Aliongea mwanadada yule huku akitoa kibunda cha pesa zilizokuwa kwenye mfumo wa Euro na kumkabidhi  mwanamke na mwanamke alizidi kushangaa maradufu.

Baada ya  mhudumu kutoka , mwanamke alijiramba kofi moja zito ili aamke katika ndoto , lakini haikuwa ndoto , bado  alihisi maumivu na kujiona kinachotendeka kwa wakati huo ni uhalisia.

“Rose amka kwenye usingizi , Rose unaota amka” Mwanamke alijiambia  kwa kujiita jina  lake , ili aamke katika ndoto , lakini bado  mwanamke hakua akiota kila kitu kilikuwa ni uhalisia na mwanamke katika kichwa chake  likabaki jina la Roma Ramoni .

Naam mwanamke ndio Rose wa Club B ilikuwaje  inaendelea

Kiliendelea nini baada ya  hapo  .. tunaendelea…

Previoua Next