RWANDA -KIGALI  2014

Ni ndani ya hoteli kubwa iliokuwa ndani ya jiji hili la Kigali , hoteli iliokuwa ikifahamika kwa jina la The Aquad  alionekana mwanamke  na mwanaume wakiwa ndani ya chumba kikubwa cha hoteli hii ,  katika floor ambayo ilikuwa ikihudumia VIP , huku nje ya Floor hii  wakiwa walinzi wengi waliokuwa wamevalia suti.

Ndani ya chumba  hiki mwanaume alionekana akiwa amepiga magoti chini , huku mwanamke mmmoja mrembo wa  mweupe  wa kabila la  wanawake  wa Babati  yaani Wairaq  akiwa amesimama huku akiwa na machozi mengi  usoni , alionekana kulia mfululizo  huku akiwa ameshikilia moyo wake.

“Nisamehe sana Raheli, naomba unisamehe  mpenzi ,,, sikudhania haya yote yatatokea”

“Jeremy  acha kuomba msamaha wako wa kipuuzi mbele yangu , unazidi kuniumiza , kwanini ulinificha muda wote kama  Lorraine alikufa , kwanini Jeremy haukuniambia hii.. hiii…kwanini Jeremiiii…..”Mwanamke alionekana kulia kilio ambacho hakikiwa cha kawaida   huku akimshutmu Jeremiii.

“Sikuwa na jinsi Rahel , sikutaka  upitie maumivu niliopitia mimi”.

“Hata kama Jeremy  , Lorraine ni mwanangu  nilipaswa kujua  haya yote ,hivi unajua ni siku ngapi nilitumia kuchukua maamuzi ya kukukabidhi Lorraine na kubaki na Edna  eeh , unajua ni uchungu gani niliopitia kuwa mbali na mwanangu , hayo yote nilifanya kwasababu nakupenda  Jeremy .. lakini kwanini ulishindwa  kumlinda…..”Kilio kilikuwa ni cha aina yake kwa mwanamama huyu   alionekana kumlaumu Jeremy kwa   yale ambayo yamemtokea Lorraine , lakini pia anamlalamikia  Jremy kwa kutompa taarifa ya kifo cha mwanae ,

“Rahel naomba unisamehe , najua ni maumivu gani unapitia baada ya  taarifa hii , najua ulitarajia kumuona Lorraine akiwa na furaha ndani ya mikono yangu , lakini mimi  pia kama baba yeke nilikuwa  nikimpenda sana Lorraine na nilipanga kumpa  Maisha mazuri , lakini haya makafir.. ya Dunia yamenichukulia mwanangu”.

“Unamaanisha nini Jeremy?”Aliuliza mwanamama huyu huku akisimama , hakumuelewa Jeremy baada ya kusema makafir alitaka kujua anamaanisha nini, Na kwa Jeremy alijikuta akijilaumu kwa kuropoka.

“Unamaanisha nini Jeremy ukisema Makafir ndio waliomchukua Lorraine?”

“Sijamaanisna hivyo Lorraine.. ni …”Kabla hajamaliza kuongea alikuwa ashashikwa  tai   na Raheli , mwanamama huyu alionekana kuzingatia kila neno mtu analoongea na ndio maana aliweza kumsikia vyema Jeremy alipo sema Makafir .

“Rahel namaanisha ,,”

“Usipo nipa maelezo ya kutosha leo Jeremy nakwambia hapa hutoki …”Jeremy alikuwa akimjua sana Rahel akiamua lake jambo  lazima litimie , lakini  hakutaka kumwambia  Rahel juu ya  kile anachokijua na anachoendela kukitafutia ukweli wake.

Jeremy aliamini kwa asilimia mia moja Ndege ile haikuanguka , bali kuna mpango  wa siri  ambao ulikuwa ukiratibiwa na  mataifa yenye nguvu duniani , mpango ambao  ulihusisha ndege hio kupotea, aliogopa  kumwambia Rahel ukweli.

“Jeremy umenificha kwa miaka kumi na sita juu ya kifo cha mtoto wangu .. ukinificha jambo lolote na nikagundua  jua sitokuja kukusamehe mpaka naingia kaburini”Aliongea mwanamama huyu huku akionesha hasira zake waziwazi.

Jeremy hakuwa na jinsi  aliona  Rahel anapaswa kuujua ukweli ule ambaye yeye alikuwa akiufahamu  , aliona haina maana ya kumficha.

“Rahel  tokea siku ambayo  ndege ile ilipotea  moyo wangu haukuwa na Amani kabisa , niliona kabisa kuna jambo ambalo  halikuwa sawa , sikuwa na amani  nilikuwa nikiota kila siku Lorraine  yupo hai  lakini sehemu aliokuwepo anateseka..”Alitulia kwanza na kufuta machozi na kisha  akasimama  huku akiwa anaangalia dirisha kama mtu aliekuwa akitafuta kitu.

“Kupotea kwa ndege ya shirika la M ilikuwa ni mpango wa wazungu”Rahel ni kama hakuwa amemsikia vizuri , kwani alinyanyuka na kwenda mpaka mbele ya Mheshimiwa Jeremy na kumwangalia vizuri usoni.

“Nieleze vizuri  nielewe Jeremy .. mpango wa Wazungu ,, unanichanganya hebu eleza nielewe”

“Siwezi kukueleza mengi Rahel lakini naamini Lorraine yupo hai  .. hakuna ushahidi wowote wa ile ndege kuanguka  Rahel , yote ni mipango na mahesanu ya wazungu  juu ya mpango ambao mpaka sasa hatuujui  , mpango ambao umeratibiwa na mataifa makubwa yenye nguvu.. hii ni siri  kubwa Rahel na sitaki kukuambia Zaidi ila naomba uelewe nitahakikisha naujua ukweli wote , nitatumia nguvu zangu zote kuhakikisha naupata ukweli wote na kama Lorraine yupo hai nitamrudisha “.

Taarifa  hio ilionekana kuwa nzito sana kwa mwanamama Rahel , alikuwa akimjua Jeremy  kwa muda mrefu tokea walivyokutana  miaka kadhaa nyuma na kuanzisha mahusiano yao , alikuwa akimjua  kuwa hawezi kuongea jambo ambalo hana uhakika nalo , alijikuta nguvu zikimuishia na kurudi kukaa kwenye sofa huku machozi yakiendelea kumbubujika.

Ukweli ni kwamba mwanamama huyu  sababu ambayo ilimfanya asigundue kuwa   Lorraine  amekufa ni kutokana na kwamba Jeremy alitumia Mchezo wa kumuigizia kuwa anamchukia  , kipindi chote ambacho Rahel alijaribu kuwasiliana na Jeremy , mheshimiwa huyo alionyesha kumchukia sana Rahel na  hakutaka mazungumzo, na hata pale ambapo aliomba  kuonana  na Lorraine mheshimiwa alimtishia  Rahel kukaa mbali na Lorraine la sivyo ataongea ukweli wote na dunia ijue kuwa Edna ni mwanae.

Kwa upande wa Rahel hakuwa tayari  kwa  watu kujua kuwa  Edna sio mtoto wa Adebayo  kwani kulikuwa  kuna mkataba wa siri ambao  alisaini na familia ya  Adebayo , mkataba ambao Raheli alisainishwa na  mama yake Adebayo.

“Jeremy una uhakika  ndege ile haikudondoka na yote uliosema  juu ya mpango ya wazungu ni kweli?”Aliuliza  kwa sauti ndogo iliokuwa dhaifu  na Jeremy  alimuonea huruma sana Rahel , alijua ni afadhali kwake maumivu  ya kumpoteza Lorraine yamezoeleka  kwani tukio lilikuwa ni la muda mrefu tarkribani Zaidi ya miaka kumi na sita  , alimsogelea Rahel na kisha akamkumbatia na walianza kuambizana kulia.

Kwa  namna ambavyo  Jeremy alikuwa akillia usingedhania ni kiongozi mkubwa wa  taifa , kiongozi ambaye wananchi wa Rwanda wanamtegemea  sana kuwafikisha katika nchi ya Ahadi.

“Ni kweli  Rahel nina amini kwa asilimia kubwa  Lorraine yupo hai na ninaompango wa kuhakikisha namrudisha”.

Rahel alifuta machozi na kisha alijitoa kwenye mikono ya  Jeremy  na akaweka sura ya usiriasi .

“Jeremy  kama haya unayoyasema ni ya kweli hakikisha unaujua ukweli la sivyo sitokusamehe kwa kumpoteza mwanangu Lorraine”Aliongea mwanamama huyu na akafuta machozi na kuchukua mkoba wake na kutoka ndani ya chumba hiko.

****

Ilikuwa ni muda wa saa  sita kamili za mchana alionekana Roma akiingiaa maeneo ya Club B , alikuwa na muda mrefu hajaingia  ndani ya hii  club , kwani tokea apate mke  mara nyingi alikuwa akienda moja kwa moja nyumbani kwa Rose , lakini leo alikuwa amewahi sana kuja haya maeneo na alijua kabisa Rose hakuwa kwake na atakuwa ofisini na mawazo yake yalikuwa sahihi kwani alimkuta mwanada huyo akiwa kazini   kama ilivyokuwa kawaida yake na kwa Rose alishangaa ujio wa Roma muda huo wa mchana.

“Hubby karibu” Aliiongea Rose huku akitoka kwenye  meza na kuja kukaa kwenye masofa  , huku akimwangalia Roma kwa  kumsanifu , aliwaza Roma  kaja muda huo  kwasababu gani.

“Bebi Rose nimekuja leo nina shida”Aliongea Roma mara baada ya  kuketi.

“Shida gani mpenzi , ongea tu nipo tayari kukusaidia”

“Unamiliki nyumba ngapi?”

“Bebi kwanini unauliza hivyo nina nyumba  nne mbili hapa  Dar na nyingine zipo nje kidogo ya Dar , kuna  ambayo ipo  Kisarawe  na Bagamoyo “

“Kwa hapa Dar ukiachana na unayoishi  hio nyingine ipo maeneo gani?”

“Ipo Kigamboni Mbutu  huko”

“Hio ndio shida yangu , nahitaji nyumba nina marafiki zaku  kutoka nje ya nchi ambao wanaingia leo nchini nataka niwahifadhi kwa muda , ila sina nyumba kwa sasa”Aliongea Roma  na Rose alitabasamu.

“Hubby chukua ya Kigamboni itakufaa , pia ni sehemu nzuri kwani  ipo  ufukweni  na isitose ni mpya na nilikuwa nikipanga kuipangisha lakini sikupata mtu”Aliongea Rose na Roma alitabasamu na kumkiss Rose.

“Nataka nikaione leo maana  marafiki zangu wakifika nchini moja kwa moja nataka niwapeleke na wanaingia leo usiku”Aliongea Roma na Rose hakukataa , kwanza alijisikia fahari kwa Roma kumuomba msaada yeye, msaada ambao Roma ameomba kwake ulikuwa na maana kubwa.

Ni ndani ya dakika chache tu walikuwa washafika Mbutu , hii sehemu ilikuwa nzuri licha ya kwamba haikuwa na  nyumba nyingi   , lakini mazingira yake yalikuwa safi sana kiasi cha Roma kupapenda na kuona wanajeshi wake kukaa hapo ni chaguzi  sahihi.

Waliona jumba hili ambalo lilikuwa kubwa sana kiasi kwamba hata Roma mwenyewe alishangaa , licha ya kwamba alikuwa akijua Rose ni Tajiri kwa  kufanya biashara yake ya kuuza madawa ya kulevya , lakini hakujua kama anapesa kiasi hiko cha kumiliki mjengo kama huo. Walikabidhiana nyumba hio na Roma akamrudisha Rose nyumbani.

Saa mbili kamili Roma alikuwa nyumbani  kwa ajili ya chakula , sebuleni alimkuta Bi Wema pamoja na Edna kama kawaida na  walikuwa washaanza kula, alimsalimia Bi Wema na kisha akamgeukia mke wake  na kumwangalia anavyokula kimapozi , Edna alikuwa bize na chakula chake , lakini ile anapeleka kijiko mdomoni alimwangalia Roma na kukuta Roma anamwangalia.

“Mbona unaniangalia hivyo?”

“Bebi unajua   hata staili yako ya kula inakufanya uwe mrembo kuliko wanawake wote duniani”Edna alijikuta akimwangalia Bi Wema  na kuona  aibu kiasi kwamba mwili wake ulipata uwekundu.

“Kaa pakua chakula kula”Aliongea Edna na kumfanya Bi wema aliekuwa pembeni atabasamu  kwa kushuhudia aibu za Edna.

Roma  alipakua chakula chote kilichokuwa kwenye mabakuli  na kujaza kwenye sahani kama mlima Kilimanjaro na kuanza kula ,  bila habari .

“Roma..!”Aliita Edna huku akimwangalia Roma na sahani yake na Roma alimwangalia Edna bila kuongea.

“Kesho kutwa ndio siku ya kwenda Japan , ujiandae  basi nitakupatia baadhi ya karatasi za mkataba uzisome”.

“Mke wangu mimi naenda kama mkalimani kuna haja gani ya kuzisoma?”

“Ndio  najua lakini huu mkataba  ni muhimu sana kwa kampuni na kukitokea tatizo lolote  ninaweza kufirisika moja kwa moja , ni vizuri ukijua nini kinaendelea  ili  kama  ikitokea tatizo iwe rahisi ya wewe kuligundua  kuliko  kumwachia kila kitu Doris”.

“Sawa nitazipitia mke wangu”.

Baada ya Roma kushiba , aliangalia saa  yake na kuona ni muda muafaka wa kuelekea  uwanja wa ndege kwa ajili ya kupokea wageni wake , kwani mchana alikuwa ashawasiliana na Sauroni na kumpa taarifa kuwa wataingia Tanzania saa nne usiku.

“Wife ninatoka kidogo”

“Leo naomba  usiende”Aliongea Edna na kumfanya Roma ashangae na sio  Edna tu hata  Bi Wema alishangaa , lakini alitabasamu moyoni .

Ukweli ni kwamba Edna mchana yote alikuwa akifikiria swala la kujaribu kumpa  Roma  kitumbua na alishinda kwa kutafuta mitandaoni  jinsi ya kumuanza mume wake maana alikuwa na aibu sana , alitamani kumuuliza Bi Wema ampe mbinu lakini aliona aibu na msaada  pekee aliona ni kuingia mtandaoni na kutafuta  namna ya kumuanza Roma.

“kama nitakuwa nampa maramoja moja  anaweza kutulia nyumbani”Aliwaza  wakati akiendelea kusoma mbinu mtandaoni.

Na alijikuta akipata mpango kabambe  wa kumpagawisha Roma huku akiamini  kama atafanikiwa katika mpango huo basi anaweza kumtuliza Roma nyumbani.

Na alipanga mpango wenyewe ili ukamilike lazima Roma alale nyumbani  na ndio maana baada ya Roma kumwambia anataka kutoka aliona  mpango wake hautofanikiwa na alitaka kuukamilisha kabla ya Roma na Dorisi kwenda Japani.

Previoua Next