Roma hakujua sababu ya Edna kumwambia abaki nyumbani ,lakini kwake yeye alikuwa na jambo muhimu sana la kufanya usiku huo na kwa vyovyote vile asingeweza kukubaliana na mke wake.
“Mke wangu ninatoka ila nitarudi”Aliongea Roma na akanawa mikono na kuchukua ufunguo wa Gari yake na kuondoka.
Edna aliishia kusikilizia tu mngurumo wa gari ukifubaa kwenye masikio yake , Bi wema hata yeye alijisikia vibaya , alitamani Roma abaki nyumbani kama Edna alivyopendekeza lakini hakubaki , aliwaza ni jambo gani la muhimu ambalo Roma anaenda kulifanya nje kuliko kubaki na mke wake , hakujua lakini hakutaka kuwaza Zaidi , kwani Roma alikuwa ni mwanaume na pia hakutaka kuangilia katika mahusiano yake yeye na Edna.
Edna alirudi chumbani kwake , huku akijisikia mnyonge sana lakini pia akiwa na hasira nyingi , katika akili yake alijua kabisa Roma alikuwa akienda kuonana na wanawake wake.
“Mimi sio muhimu kwake , wanawake wake ndio muhimu ..Damn you Roma .. nimejipanga vyote hivyo leo kwa ajili yako halafu unaniona sina thamani… shenz kabisa , nakuambia hivi Roma utanisikia kwenye bomba ,Kwanza nini kilinipata mpaka nikawa na mawazo ya kijinga ya kumpa mwili wangu …Aaah Edna wewe mjinga kweli, Roma sio wa kumpa mwili wako ni Malaya yule mwanaume”Ungemuona Edna anavyoongea na mto usingemdhania ni yule CEO mwenye heshima zake , alikuwa akiongea mweyewe huku akiangalia mto uliokuwa kitandani kwake.
“Ila mimi mjinga sana hadi aibu ..Aaa nisingemwambia abaki nimejidharirisha leo …Edna usie ukarudia tena”Aliendelea kuongea mwenywe na kisha akachukua shuka na kujifunika gubigubi.
Upande wa Roma alifika Uwanja wa ndege kama kawaida muda ulikuwa ni saa tatu hivi kama na nusu , baada ya kusimama nje ya jingo la Terminal 3 akisubiria wageni wake , alikuja mwanaume mmoja wa kizungu alievalia suti bila tai huku akiacha vifungo viwili vya shati lake kuwa wazi na kumfanya nywele za kifuani kuonekana, aligonga gari la Roma mara mbili kwenye kioo cha mbele.
“You are Mister Roma ??”Aliuliza yule mzungu na Roma alitingisha kichwa kukubali kuwa ni yeye , yule mzungu alitoa ufunguo mfukoni na kumpatia na Roma alitabasamu na kisha akauchukua ule ufunguo huku bwana yule wa kizungu akiondoka mbele ya gari la Roma , alionekana kazi ambayo ilikuwa imemleta mahali hapo alikuwa ashaimaliza.
Baada ya dakika kama mbili hivi kupita ,Roma alitoka kwenye gari yake akiwa ameshikilia ile funguo ya gari na kisha alianza kubonyeza bonyeza kitufe cha rimoti iliokuwa imeambatana na ufunguo na gari lilitweak na kuwahsa taa za mbele na Roma alitabasamu na kuisogelea.
Ilikuwa ni gari kubwa kutoka kampuni ya Toyota , iliokuwa na uwezo wa kubeba Zaidi ya watu kumi na tano na ilikuwa imeletwa hapo na Ubalozi kwa ajili ya kuwasafirisha wageni kutoka uwanja wa ndege kwenda kwenye makazi yao.
Roma baada ya kuikagua na kuridhika , alitoka nje na ndani ya dakika chache tu , alishuhudia ndege kubwa kampuni ya KLM ikiiambaambaa kwa kushuka ndani ya uwanja huu wa Dar es salaam, aliendelea kusubiri kwa takribani dakika kumi na tano na hatimae alianza kuona wageni wake wakitoka nje kabisa ya mlango wa ‘Arrivals’.
Wa kwanza kabisa alikuwa ni mwanamke mzungu aina ya Cauccasian aliekuwa amevalia surali ya jeans rangi ya bluu n araba nyeupe huku akiwa amefunga kiunoni shati moja ya draft akiwa amevalia miwani , alionekana mrembo.
Wasichana wengine watatu walitoka huku nyuma yao wakifuatiwa na wanaume sita wote walionekana kuwa katika lika moja la ujana kati ya miaka 25 kwenda 30 , Roma aliwaona wazungu hao na kutabasamu , kwa namna ambavyo walikuwa wamebaba mabegi yao walionekana kama watalii , karibia wote walikuwa wakitafuna bublish.
“Your Majest Pluto”Aliongea yule mwanamke kwa mshangao , huku akionesha heshima ya hali ya juu kwa Roma lakini Roma alimpa ishara na mzungu yule alielewa na wenzake walielewa na kutulia .
“Welcome in Tanzania guys”
“Thank you” waliitikia wote kwa pamoja na Roma alitabasamu na kumrushia kijana mmoja funguo ambaye alikuwa mwembaba.
“You will drive along with me”Aliongea Roma na kuwaonyesha gari iliokuwa upande wao wa kushoto na wote wakatabasamu na kuisogelea na wote wakaingia ndani , lakini wakati Roma ashaanza kulisogeza gari lake kuingia barabara kuu , mara zilikuja gari tatu diffenda na kusimama barabarani na palepale walionekana wanajeshi wakiruka kwa ustadi mkubwa kwenye gari wakiwa na siraha na kisha kulizunguka gari lile walilopanda wazungu , walionekana walikuwa wamejipanga kweli.
Roma alishuhudia kitendo kile akiwa ndani ya gari yake na kujikuta misuli ya uso ikisimama , kwa namna wanajeshi hao walivyokuwa wanaonekana mahali hapo ilionesha kabisa walikuwa na taarifa za kutosha na ndio maana walionekana kujipanga.
Baada ya kuona gari lile limezingirwa Roma alishuka kwenye gari yake na kusogea upande wa wale wanajeshi walipo , lakini kabla hajawafikia gari iliokuwa mbele yake mita kadhaa , gari ambayo ilikuwepo hapo muda mrefu kidogo kwani aliiona , ilifunguliwa na akatoka mzee mmoja hivi mwenye mwili mkubwa wenye afya alievalia miwani pamoja na suti ,Roma hakumjua mzee huyu.
Yule mzee alimsogelea Roma huku wanajeshi watatu wakimzingira upande wa kulia na kushoto na nyuma wakionesha kumlinda ,Roma aliendelea kujiuliza mtu huyu ni nani na kwanini amewazingira wageni wake , kwani swala la wageni wake kuja ndani ya taifa la Tanzania lilikuwa ni siri sana na waliokuwa wakijua ni watu wachache sana ndani ya ubalozi wa Sweden.
“Tunaomba mshuke kwenye gari”Aliongea kwa kingereza moja ya wanajeshi ambae alikuwa na nyota tatu begani na wale wazungu waliangaliana na jamaa mmoja mwenye mwili mkubwa aliwapa ishara wenzake washuke na wakashuka huku wakiwa wamenyoosha mikono juu kuonesha kwamba hawapo kishari.
“Tupo hapa baada ya kupata taarifa ya nyie kuwa wanajeshi mnaokusudia kuingia ndani ya nchi yetu bila ruhusa”Aliongea yule Mwanajeshi alieonekana kuwa kiongozi na wakati huu Roma alikuwa ashafika upande aliosimama mzee ambaye alikuwa amevalia suti na yule mzee alimwangalia Roma na kisha wakasogeleana.
“Habari yako mzee , unaonakana wewe ndio kiongozi mkuu hapa , nini kinaendelea mbona wageni wangu wanazuiwa”.
“Nadhani mpaka sasa ushajua kwanini wanazuiwa Mr Roma Ramoni , Sisi ndio walinzi wa mipaka ya taifa hili na tunajua kinachoendelea nje na ndani ya mipaka yetu na hatupo tayari kuona wanajeshi wanaingia ndani ya taifa hili bila kuwa na kibali maalumu”
“Una Ushahidi gani kama wakujitosheleza kama hawa ni wanajeshi?”Mzee huyu alitabasamu.
“Hawa ni wanajeshi kutoka kundi la The Eagles na taarifa za ujio wao tulizipata kutoka kwa watu wetu ndani ya ubalozi”.Aliongea mzee huyu na Roma alimwangalia na kuwageukia wanajeshi wake waliokuwa katika hali ya wasiwasi.
“Mr Roma tunajua wanajeshi hawa wanauwezo mkubwa wa kimapigano , lakini leo lazima sheria za nchi zifuatwe hatuwezi kuwaachia wakaingia uraiani pasipo kujua ni sababu zipi zimewafanya kuingia hapa nchini , hivyo tutaenda nao pamoja na wewe kambini kwa ajili ya mahojiano”
“Hapana,naondoka na wageni wangu”Aliongea Roma na kumfanya mzee huyu amshangae na kisha akatabasamu
“Hauna uamuzi katika hili”: aliongea na kisha aliwapa ishara wanajeshi wafanye kazi , lakini ile wanataka kuwasogelea wale wanajeshi wa kizungu walishusha mikono chini na wanajeshi wa kitanzania walikuwa fasta sana kwani walikuwa ashakoki siraha zao tayari kwa mashambulizi.
Wanajesh wale wa kuzngu walimwangalia Roma huku wakionesha wanataka Ruhusa kutoka kwake , ila Roma aliwaangalia na kisha akamgeukia huyu mzee huku akiwaza jambo la kufanya , lakini kabla hajaongea ziliingia ndani ya eneo hili gari nyingine mbili moja Range Vx na moja difenda na baada ya gari hizi kusimama alishuka mzee mwingine alievalia gwanda huku mabega yake yakiwa yamechafuka kwa vyeo vingi, wale wanajeshi baada ya kuona mtu huyo ametoka kweye gari na na kumtambua walijikuta wakitoa heshima na kushangaa kwa wakati mmoja kwanini mkuu wao yupo hapo.
Upande wa huyu mzee aliekuwa akiongea na Roma pia alishangazwa na ujio wa mkuu wake , ghafla tu alikakamaa mwili.
“Jambo Afande” lakini Mzee huyu hakuongea chochote Zaidi ya kuinua mkono ya kumwambia alegeze na kumsogelea Roma.
“Mr Roma unaweza kuondoka na wageni wako , mengine tuongee siku ya kesho baada ya kuwasiliana ”Aliongea huyu mzee mwenye manyota mengi na Roma alitingisha kichwa pasipo kusema lolote na kisha akawapa ishara wanajeshi wa kizungu na wote wakaingia kwenye gari na kuondoka eneo hili Roma akiwa ametangulia.
Comments