Reader Settings

Ni ndanni ya dakika chache tu Roma alikuwa ashafika Mbutu akiwa na  wageni wake  ,  aliingiza  gari  na kuegesha na kisha  akawakaribisha ndani , Wageni hawa walipendezwa sana na nyumba , hio licha kwamba ilikuwa usiku , lakini  ilionekana kuwa nyumba nzuri kwao yenye mazingira ya kuvutia.

“Guys here is now your home , all your missions will be  operated  here , feel free and welcome again  in Tanzania”.

“Thank you! ,Your Majest Pluto , it`s  has been our dream working with you personally and we ready for any instructions”

Aliongea kijana mmoja kibongea ambaye  ndio alionekana kuwa kiongozi katika hili kundi la wazungu na Roma alitabasamu.

Kwanza kabisa aliwanza kuwakagua mmoja mmoja  kwa dakika kama nne hivi , akiwazunguka nyuma na mbele na kisha akatabasamu  baada ya kuona ya kuridhishwa  nao , lakini bado  vijana hawa wa kizungu walionesha hali ya wasiwasi , walionekana kukosa kujiamini.

“Okey nimeridhishwa na uwezo wenu, tuingie ndani  kwanza”Aliongea Roma kwa kingereza Safi na wakatabasamu na kisha wakamfautisha kwa nyuma na wote wakaingia ndani na kuweka mizigo yao chini  kwenye sebule hii kubwa ambayo ilikuwa na furniture za bei kubwa , mabwana hawa waliangaliana na kisha wakatabasamu.

“Kwanza kabisa nataka niwatambue majina yenu mmoja mmoja na   kila mmoja kwa uwezo wake cheo ndani ya The Eagles”

Aliongea  na wakaanza kuangaliana ni kama kila mmoa alitaka mwenzake aanze  huku wakiwa wamesimama na Roma akiwa amekaa huku amekunja nne , alikuwa ni kama bosi  hapa ndani kwa muonekano wake na waliokuwa mbele yake walikuwa vijakazi wake.

“My name is Bram Garcia, I am an expert in computer , with various records in hacking issues, in 2016 I managed to hack the communication system of the international space station, also.....”( jina langu Bram Garcia ni mtaalamu katika maswala ya Computer  , nikiwa na rekodi mbalimbali katika  maswala ya Hacking , mwaka 2016 nilifanikiwa kuhack  mfumo wa  mawasiliano wa international space station, na pia ..) Roma alimwambia asiendelee  kwani asharidhika na kuashiria mwingine aendelee

Baada ya dakika chache Roma  aliridhika na utambulisho wa kila mmoja  na kusimama na kuwaangalia  mmoja mmoja.

“Okey Liutenant Diego utakuwa kiongozi wa kundi hili na utapokea maelekezo yote kutoka kwangu .. kuna mwenye pingamizi?” Wote walipiga Salute.

“Chiara  na John mtakuwa  na  jukumu la kuhakikisha  usalama wa mke wangu popote pale anapoenda na iwe kwa siri sana , akiwagundua mnalinda  kazi hamna” Walipiga wote saluti.

“Wote nane mliobaki kwanzia leo hii kazi yenu ni kuhakikisha  mnajua  kila kinachoendelea kwa watu ninaoneda kuwatajia… “alisimama kuongea na  akawaangalia  wote na wanajeshi hawa walianza kujishuku .Na Diego alijua   kwanini Pluto anawaangalia na alimpa ishara Chiara mwanadada ambaye alikuwa  ndio  aliekuwa amefunga shati kiunoni  na Chiara alielewa ishara hio na haraka haraka akatoa notebook na kalamu.

“Nataka muanze kumfatilia mtu anaejiita kwa jina la The Don  kwanzia nani anaongea nae , ratiba zake za kila siku na mtandao wake wote wa kibiashara ndani na nje ya nchi , wa pili  nataka taarifa za mheshimiwa Senga  watu wote ambao anawasiliana nao kwa siri  na  kila kitu kinachoendelea Ikulu ambacho  kina muunganiko na mimi, naomba taarifa hio ipewe kipaumbele na kuchambuliwa vyema , nikija kwenu nitahitaji ripoti tu , kazi ya tatu ambayo nadhani wote mnamfahamu Seventeen nafasi yake ndani ya kikosi na sehemu yake katikamaisha yangu? , nataka  mchimbe na mnipatie muunganiko wote uliopo kati ya mke wangu na Seventeen”Walishangaa na Roma akatabasamu.

“Haina  haja ya kushangaa maafande  , mkishamuona mke wangu mtajua kwnini nawapa hio kazi ,na yangu kwa leo ni hayo tu  nasisitiza ulinzi kwa mke wangu lazima upewe kipaumbele naelewa The Eagles tuna teknolojia kubwa , hivyo teknolojia hio nataka itumike  katika kumpa ulinzi Edna tumeelewana”

Wote waliitikia kwa  kupiga saluti na Roma alinyanyuka  na akamwangalia Diego.

“Utawasiliana na Sauron kwa mahitaji yote mtakayohitaji mkiwa hapa nchini , lakini pia mishahara yenu itaongezeka kwa asilimia ishirini  kutokana na kazi hii , niwatakie usiku mwema na maukumu mema”Wote walitabasamu  kwa shangwe .

Baada ya kusema hayo Roma alitoka na kuwaacha  na kugeuza kwenda nyumbani kwake , na muda ulikuwa umeenda kweli , lakini kutoka Mbutu na Sunlight Villa palikuwa ni  umbali mdogo sana.

Kama kawaida alikuta walinzi wako macho na kikama walikuwa wanamsubiria kwani ile anafika tu alifunguliwa geti na kuingia ,taa  za ndani zilikuwa zimezimwa kuonesha Bi Wema na ,mke wake walikuwa washalala kitambo , na  hakujali sana , alijirusha kitandani baada ya kupunguza nguo na kuangalia gypsum.

“Kazi yangu ilionirudisha hapa nchini imeanza  na  nitaujua ukweli wote kwanini Seventeen na Edna wanafanana na kwanini mimi na Seventeen tukawa peke yetu kwenye kile kisiwa”Alijiongelesha Roma na kisha akalala.

****

Ratiba za asubuhi zilikuwa kama kawaida kwa Roma , alianza kwenda   kufanya mazoezi  ya kuuweka mwili  sawa na baada ya hapo alirudi chumbani kwake baada ya kusalimianan a na Bi Wema ambaye alikuwa bize na usafi pamoja na kuandaa  kifungua kinywa.

Baada ya kujiweka sawa kwa  ajili ya kuelekea kazini  alishuka na  ufunguo wake  chini kwa ajili ya kifungua kinywa , leo alikuwa amechelewa kidogo kufika mezani kwani Edna alionekana  kwenye meza akiwa amenuna , na hakutaka kabisa hata kumwangalia  usoni Roma na hata pale Roma alipomsalimia aliishia kutingisa kichwa tu kama salamu na Roma hakujali sana  , alikua akijua kwanini Edna amenuna na hakuwa na namna ya kujitetea mbele  yake , alichokifanya ni kunywa chai ilioandaliwa.

Wa kwanza kumaliza alikuwa ni Edna  alimuanga Bi Wema na  mama huyo kumtakia siku njema na kisha kuondoka na ni mgurumo wa  gari pekee uliokuwa ukisikika ukifubaa kwenye masikio ya Roma na Bi wema.

Bi wema alimwangalia Roma aliekuwa akimalizia   mayai yakukaanga yaliokuwa kwenye sahani  , mwanamama huyu alitamani kumuuliza Roma jana kulikuwa na umuhimu gani wa kutoka  , kwanini asingebaki nyumbani kama Edna alivyo omba kama  Edna , lakini ile anataka kuinua mdomo…

“Bi Wema  Asante kwa chai na usiwaze sana kuhusu Edna..”Aliongea Roma na kumfanya mwnamama huyu amuangalie na kujiuliza amejuaje kama alikuwa akiwaza kuhusu Edna , ila Roma hakujali mshangao wa Bi Wema Zaidi ya kufungua mlango… lakini alikumbuka jambo na kusimama.

“Bi Wema  kama kuna mtu yoyote akifika hapa wa kizungu naomba umpe nafasi ya kufanya kazi yake  , ni maswala ya kiulinzi  hivyo haina haja ya kumwambia Edna”.

“Sawa mr Roma kazi njema”Roma alitabasamu na kisha akaondoka  na kuchukua gari  yake aliodhurumu kule PANZ security  Aud Q7 rangi ya Silver , ilikuwa gari nzuri kweli ambayo Roma alikuwa akiendesha , kwa muonekano wa Roma wa sasa usingemdhania kama alikuwa akibeba mizigo  siku kadhaa nyuma ndani ya soko la Mbagala , licha ya sasa kuonekana  kawaida kimtindo   lakinni  alikuwa na utofauti mkubwa , uso ulikuwa unang`aa.

Baada ya kufika getini alisimamisha gari na kushusha kioo  na kumwangalia Derick aliekuwa ameshikilia gati  , licha ya kwamba geti  hili lilikuwa likitumia umeme lakini bwana huyu alikuwa akilifungua kwa kulisukuma  ili kuonyesha juhudi yake kazini kwa mabosi wake.

Baada ya Derikc kumuona boss wake kasimamamisha gari alimsogelea kwa heshima, huku akipanga ayajenge na Roma kwani tokea siku ambayo  alimwita kichaa msafi hawakuwahi kuongea nae tena, kwani muda wote Roma  akitoka  alikuwa ndani ya gari na hakuwa na ruhusa ya kuingia ndani ya Jumba hilo kwa ajili ya kuongea nae  , lakini leo hii bosi wake amesimamisha gari  , aliona  hio ndio nafasi nzuri.

“Hivi unaitwa nani vile” Aliuliza Roma  na ni kweli alikuwa amemsahau  jina kwani siku ile  alimsikia Edna akimuita ila hakulishika vizuri.

“Naitwa Derick Bosi”.

“Sawa Derick , hebu  acha kukakamaa mwili  kwa namna hio unaweza ukajamba , kuwa kawaida tu , haina haja ya kuniogopa”

“Sawa bosi” aliongea Derick huku akijiweka sawa kwa kufunga suti yake vizuri .

“Okey kuna watu watakuja hapa  wazungu , wakiomba kufanya mambo yao hapa waruhusu nni maswala ya kiulinzi sawa”

“Sawa bosi”

Roma alifika  kazini  akiwa ni wa mwisho  kuliko  wafanyakazi wote , lakini leo kulikuwa na mabadiliko kidogo , wafanyakazi walionekana kumuangalia  sana kiasi cha kuiuliza kuna nini kwanini wenzake wanamwangalia.

“Recho mambo?”

“Poa Vipi Roma”

“Gudi , kuna nini mbona mnaniangalia sana , au nimezidi kuwa handsome”

“Hongera , tumesikia unaenda Japan kesho kikazi , tumeshangazwa na taarifa hio  na kila mmoja anashangaa kwanin umechaguliwa , maana tokea ufike haukuwahi kufanya kazi zaidi ya kucheza gemu , na isitoshe hauna uzoefu wa kutosha na Kampuni , lakini wote hapa ndani  hatujawahi kupewa  hata kazi ya kwenda nje ya mkoa lakini wewe huna hata mwezi umepata nafasi hio , lazima tukuangalie kwa mshangao”

“Sasa mnachoshangaa nini hapo , ushasahu mimi ndio mwanaume  peke yangu ndani ya hii idara, hehe ukute CEO mwenyewe kapagawa na uwepo wangu anataka kuniweka karibu , kwahio msiwaze sana pigeni kazi”Recho alibetua midomp  na Roma  akageukia  tarakishi yake , alitoa  headohone kwenye droo ya meza na Pad za kuchezea gemu ,haikueleweka ni lini alizinunua, alichomeka na kuanza kucheza gemu la Mpira PES 2021 , huku wafanya kazi wenzake  wakizidi kushangaa, maana mtu kazi yake ni kucheza gemu , lakini kapewa kazi ya kwenda Japani kumwakilisha bosi wa kampuni , jambo hilo kwao liliwashangaza na kuona kuna walakini na uongozi wa kamouni.

Licha ya kujua  Roma ni mhitimu wa chuo kikuu cha Harvard lakini bado hawakukubali , kwani ndani ya kampuni hio kulikuwa na  wasomi wakubwa   tu akiwemo Nasra ambaye alisomea  masomo yake yote Cambridge Marekani.

Wakati Roma anaendelea kucheza gemu alikuja Miss Airport  na kwenda kusimama kwenye meza yake na kumwangalia Roma kwa sekunde namna ananyofurahia gemu  , huku baadhi ya wafanya kazi wakishangazwa na uwepo wa Monica hapo ndani , kwani ni mara chache sana kwa Monica  kuja kwenye ofisi yao.

Miss Aiport alionekana kutompenda kweli Roma , na alikasirika Zaidi baada ya kuona  Roma anacheza gemu  wakati wenzake wote wako bize  kufanya kazi , alitamani awe na cheo kisha amfukuze. Alimsogelea Roma na kisha akamvua Headphone na kumfanya Roma ageuke.

“Miss Airport!”Alishangaa roma mara baada ya kugundua mtu aliekuwa  amesimama nyuma yake ni  Monicca.

“Unaitwa na CEO”aliongea Monica na kisha akageuza na kuondoka kwa maringo  , huku viatu vyake vikitoa sauti ya ‘kwaa.. kwaaa..   huku sehemu  katikati ya mapaja yake ikionekana  kutokana na  pasua ya sketi nyeusi aliovalia , alionekana  kujisikia kweli kwa mnafasi yake alionayo kwenye kampuni.

Previoua Next