Roma alisubirisha gemu lake na kisha akainuka kwenye meza na kujivuta na kuianza safari , huku nyuma akiwaacha Recho ,Tina na warembo wengine wakimwangalia kwa nyuma mpaka pale kisogo chake kilipotokomea nje , walitingisha vichwa vyao na kuendelea na majukumu yao.
Roma baada ya kutoka kwenye lift alitembea kuelekea ofisi ya CEO lakini njiani alikutana na watu wawili , wa kwanza alikuwa ni Dorisi ambaye alikuwa ametangulia kwa mbele mita kadhaa akimuacha Nadia nyuma ,Doris baada ya kukumfikia Roma alimkonyesha na kumpa busu la hewani na kisha akampita , lakini kitendo hiko kilishuhudiwa na Nadia aliekuwa nyuma na hakufurahishwa na jambo lile , alimwangalia Roma kwa hasira na kisha akampita na Roma aligeuka na kumwangalia Nadia na kutabasamu na kuendelea mbele , mpaka kuingia kwenye ofisi ya mke wake.
“Bebi Nishafika”Aliongea Roma mara baada ya kuingia na kumshuhudia mke wake kama kawaida akiwa bize na tarakishi yake , licha ya kwamba Edna alionekana kauzu lakini muonekano wa yeye kuwa bize na kazi ulikuwa ni wa kipekee kabisa na Roma alitaman kuwa na picha ya mke wake akiwa anafanya kazi ilia awe anaikodolea macho.
Edna hakujibu mara moja aliendelea na kazi na Roma alikaa kwenye sofa akimsubiria mke wake amwangalie , baaada ya kuwa bize kwa dakika mbili Edna aliinua macho yake na kumwangalia Roma ambae amepandisha miguu kwenye sofa akiegemea sehemu ya kuwekea mkono na miguu kuning`inia upande mwingine, Roma hakuwa na tofauti na mtoto kwa mambo ambayo alikuwa akifanya , Edna alitingisha kichwa kwa kusikitika na kisha aliangalia pembeni kwenye kitrei flani hivi cha chuma kinachong`aa na kutoa karatasi.Alinyanyuka kwenye kiti chake na kisha akamsogogelea Roma.
“Angalia hizo karatasi , naomba uzisome zote na uelewe , ni sehemu ya vipendelea vya mkataba ambao mtakwenda kusaini huko Japani”.Aliongea Edna huku akiwa Siriasi na Roma aliinua uso wake na kumwangalia Edna.
“Mke wangu , unaonaje kwanza ukinitengenezea kahawa uniletee niwe na kunywa taratibu wakati nikiendelea kusoma hizo karatasi”
“Huo muda sina , katengeneze mwenywe na karatasi hizi utazisoma mpaka uzimalize ndio uondoke”.
“Bila kahawa nakwambia hivi , sizisomi na nalala hapa mpaka muda wa chakula cha mchana na sitaki kahawa iliotengenezwa na Monica nataka uliotengeneza na wewe mke wangu” Aliongea Roma na kisha akarudia staili yake ile ile na kufumba macho , Edna alijikuta akichemka kwa hasira , alimwangalia Roma namna ambavyo amelala , huku akishindwa kuelewa ni kitu gani akifanye. , aliinua karatasi alizoshikilia mkononi na kuziangalia kwa sekunde na kisha akakunja ngumi kwa hasira na kuziweka kwenye meza na kutembea kihasira hasira na kutoka nje ya ofisi yake.
“Boss unahitaji nini?” Aliongea Monica akiwa amekakamaa kwa heshima.
“Unaweza kuendelea na kazi Monicca natengeneza kahawa”Aliongea Edna na kupita kushoto huku akimuacha Monnica ambaye alikuwa kwenye mshangao , maana kwa mara ya kwanza tokea aanze kazi yeye ndio aliekuwa akimtengenezea Edna kahawa , inakuwaje leo , alitingisha kichwa na kisha alikaa chini na kuendelea na kazi.
Roma na yeye baada ya kusikia mlango ukifunguliwa na Edna kutoka nje , aligeuka na kuangalia na kujikuta akitabasamu na kujisemea moyoni kwamba amemuweza leo.
“Nimemuweza na asipoleta kahawa hapa nzuri sizisomi karatasi zake” Alijiwazia na kisha aliendelea kukaa vile vile akisikilizia kaubaridi kakiyoyozi pamoja na harufu nzuri ya ofisi hii ya mke wake.
Dakika tano mbele Edna alirudi akiwa ameshikilia kikombe na kwenda kusimama mbele ya sofa akiwa anamwangalia Roma kwa hasira na Roma aliinua uso wake na kumwangalia Edna na kisha alitabasau na kupokea kikombe.
“Asante mke wangu kipenzi”aliongea Roma huku akitabsamu na kunywa kidogo na kisha akafumba macho akifurahia burudanni ya utamu wa kahawa.
‘kumbe ni mtaalamu kwenye utengenezaji wa kahawa nitakuwanakuja uwe unanitengenezea mumeo mara kwa mara”Edna hakujibu kitu alilirudi kwenye meza yake kuendelea na kazi na Roma alichukua karatasi na kuanza kuzisoma.
Baada ya dakika kumi kupita Edna aliinua shingo yake na kumwangalia Roma na kumuona yupo bize akisoma karatasi hizo kwa umakini mkubwa na alijikuta moyo wake ukipata joto na alishindwa kujizuia na kutabasamu.
“Anaonekana mwanaume aliekamilika akiwa siriasi”Aliwaza Edna na kuendelea na kazi.
Baada kama ya dakika arobaini na tano hivi za mara ya kwanza kwa Roma kuwa siriasi tokea aanze kuingia kwenye hii kampuni , simu yake ilipata uhai , na simu hii ilikuwa na kelele maana ilikuwa ni simu ya Tecno batani kitochi aliotoka nayo Mbagala, na kama unavyojua simu hizi kwa makele .
Roma alitoa simu yake mfukoni na kuangalia nani anapiga na namba ilikuwa mpya , alimwangalia mke wake ambaye alijua anajifanya kuwa siriasi na kisha akapokea.
“Mr Roma Ramoni , unaongea na Meja Generali Maeda Mkwizu , tulionana jana Uwanja wa ndege , nimepiga tuonane ofisini kwangu saa sita kamili Lugalo”Ilisikika sauti nzito upande wa pilili.
“Sawa Mr Maeda nitakuwa hapo ndani ya muda”
Baada ya kukata simu , Roma aliangalia muda na kuona ni saa tano na dakika iishirini na saba ,aliangalia karatasi zilizokuwa kwenye meza na kisha akainua macho yake na kumwangalia Edna.
“My Wife utakuja nazo nyumbani hizi karatasi nizimalizie , kuna sehemu naenda”Aliongea Roma na kisha alinyanyuka na kupiga hatua kuelekea nje.
“Romaa.. !, kwanini usizimalizie kabisa”.
“See you at home babe , uje nazo”Aliongea Roma Nakisha akafungua mlango na kutoka , akimuacha Edna alikuwa amekodolea macho mlango.
****
Roma aliendesha Gari yake huku akiwa anasikiliza mziki mdogo mdogo , alitaka atumie muda mwingi mpaka kufika Lugalo , alichukua barabara ya Morogoro na kuendesha mpaka Ubungo na kuchukua barabara ya Mawasiliano ,Sam Nujoma na akaja kutokezea Mwenge na kuingia kwenye barabara ya Bagamoyo , aliendesha kwa utaratibu huku akiendelea kula mziki na pia alifurahishwa na madhani ya jiji.
Dakika chache mbele alikunja kushoto na kusimamaisha gari yake na kisha aliangalia saa na kuona alikuwa na dakika kumi kabla ya muda , alitulia kwa dakika kadhaa na zikiwa zimebaki dakika mbili aliingiza gari yake ndani ya eneo la Brigade baada ya kujitambulisha getini.
Ndani ya ofisi ya uongozi wa juu wa jeshi alionekana Meja General Maeda akiwa kwenye mavazi yake ya Gwanda iliokuwa imechafuka na manyota manyota na mwenge na alama ya x iliokuwa na visu, huku mbele yake akiwa Kanal Augustin Tobwe akiwa ameketi kwa heshima ndani ya ofisi hii
Ilikuwa ni ofisi kubwa iliokuwa na kiyoyozi na harufu nzuri na kufanya eneo hili kuzidi kupendeza , ukiongezea na fanicha za hapa ndani pamoja na kapeti la unyoya lililotandazwa chini , palikuwa panavutia na kuonyesha hadhi ya ofisi ya cheo cha mkuu huyu wa jeshi.
Baada ya dakika chache tu aliingia mwanajeshi cheo cha luteni kwa nyota zake mbili na kutoa saluti kwa wakuu wake .
“Mr Roma amefika”
“Okey! Mruhusu aingie”.
Roma aliingia ndani hapa kama kawaida yake ,sura kutokuwa na wasiwasi na kujiamini ndio ilikuwa imemvaa , alikuwa ni Roma yule yule ambaye hakuw akibadilisha na mazingira, watu walokuwa ndani ya hii ofisi wote alikuwa akiwajua , wa kwanza aliekuwa amekaa upande wa kulia , alikuwa ni mzee aliekutana nae jana na kumpiga biti la kutaka kuondoka nae kwenda kambini pamoja na wageni kwa mahojiano na aliekuwa kwenye meza alikuwa ni Meja jenerali mwenyewe Maeda Mkwizu.
“Karibu Mr Roma , naitwa kanali Augustin Tobwe”Aliongea mzee wa jana aliempiga biti na Roma alitabasamu na kupokea mkono wake.
“Unaitwa Tobo au Tobwe”Mzee yule aling`ata meno kwa hasira na kisha akatabasamu .
“Naitwa Augustin Tobwe sio Tobo tafadhari”
“Sawa Afande Tobo nishalinakiri jina lako hivyo ili iwe rahisi kukumbuka”Aliongea Roma na kumfanya Afande Maeda atabasamu na kuona Roma alikuwa akilipiza kisasi cha jana na hakutaka kutia neno na mzee alietwa Tobo alikuwa ni mwenye bisara hakutaka kuonesha hasira zake waziwazi.
“Karibu sana mr Roma , nadhani sina haja ya kujitambulisha kwani nishafanya hivyo kwenye simu”Roma alitingisha kichwa na wote wakaketi kwenye masofa yaliopo hapo ndani.
“Mr Roma nadhani niende moja kwa moja kwenye jambo ambalo limefanya tuonane , na kabla ya kuendelea naomba tusahau ya jana”.
“Meja nishasahau yote mimi na Afande Tobo hatuna shida kabisa , yaliotokea na ni sehemu ya majukumu yake ya kikazi”
Aliongea Roma huku akitabasamu , lakini bado alikuwa akishangazwa na namna Meja alivyokuwa akiongea hakuwa akifanannia na cheo chake , kwani aliongea kama mwanasiasa.
“Mheshimiwa Afande twende sasa moja kwa moja kwenye maongezi , tusiwe kama wanasiasa , nimeondoka bila ruhusa ya mke wangu nataka nirudi nikampet peti” Aliongea Roma na Meja jenerali alitabasamu na kisha aligundua alikuwa anaongea na mtu wa aina gani , kwani alionekana kujiamini mno.
Baada ya Roma kuongea hivyo Afande Maeda alimpa ishara Kanali na akaibua fomu iliokuwa pembeni yake na kisha akatoa karatasi na kumkabidhi Roma ambaye alizichukua na kuanza kuzipitia.
“Hio ni katatasi ya kikosi chetu maalumu kinachoendelea na mafumbo ndani ya kambi ya Mirambo”
“ Mr Meja ndio ni kikosi , lakini sijaelewa kwanini umenipa majina yao?”alitabasamu.
“Mr Roma miezi miwili iliopita tuliomba msaada wa wakufunzi kutoka jeshi la Urusi kwa ajili ya kuwafundisha wanajeshi wetu mbinu maalumu za kivita kupitia ofisi ya CDF lakini ombi letu lilikataliwa kwa pendekezo”
“Unamaanisha nini kwa Pendekezo”
“Uongozi wa Jeshi la urusi walipendekeza tukuombe wewe usaidie katika kufundisha wanajeshi wetu baada ya kutupitishia taarifa ya ujuzi wako wa kimapigano , lakini pia uongozi wako wa juu ndani ya Kikosi cha The Eagles na nadhani dunia nzima inajua umahili wa kikosi cha The Eagles , hivyo hata sisi tulishangaa baada ya kusikia kuwa wewe ni sehemu ya wanajeshi kikosi hiko”Alitulia na kisha akamwangalia Roma , ila Roma hakuonesha mshangao , wala hakuonyesha mabadiliko yoyote.
“Lakini swala hili hatukuombi ulifanye bure , sisi kama jeshi tumekaa tukaridhia wanajeshi wako kuendelea kukaa hapa nchini lakini wewe utatusaidia kuwafundisha vijana wetu mbinu mpya ambazo sisi jeshi la Tanzania hatuna , ikiwemo baadhi ya siri mnazotumia ndani ya jeshi la The Eagles”Aliongea Afande Maeda na kumwangalia Roma.
“Kwa hio Afande milikuwa mnasubiri mpate Collateral ili uandae haya mazungumzo na mimi?”
“Ndio hivyo Mr Ramon licha sisi ya kuwa wanajeshi ila tunaelewa kanununi za kuwa katika nafasi nzuri katika mazungumzo”
Roma alifkiria kwa dakika kadhaa na kuona jambo hilo sio baya , kama ni kuwafundisha tu anaweza kawapa kazi hio wanajeshi wake , na asiende yeye lakini pia alikuwa akihitaji sana wanajeshi wake kuwa ndani ya taifa la Tanzania kwa kazi yake iliomleta.
“Sawa meja , lakini kabla ya kukubaliana na ombi lenu nina masharti makuu mawili , kwanza kabisa nataka nijue , ilikuwaje mpaka afande Tobo hapa kupata taarifa zangu na kuintercept wanajeshi wangu , kwani kwa maelezo yako na kwa tukio lile inaonekana kabisa hakukuwa na muunganiko wa taarifa kati yenu”
“Ni kweli Mr Roma , kilichotokea ni Misunderstanding kati yetu , Project ya kikosi kinachoendelea na mafunzo huko Mirambo haikuwa imemfikia kanali hapa na niseme tu kuwa kanali ni moja ya wanajeshi wenye weledi mkubwa ndani ya jeshi letu na ndio maana licha ya kukosa taarifa kamili kutoka kwetu aliweza kunusa harufu ya wanajeshi wanaozamia ndani ya Tanzania”.Roma alikubali maelezo
“Sharti langu la pili ni hili Afande Meja jenerali , nataka unihakikishie jambo lolote kutonikuta nikiwa hapa Tanzania , ikiwa nitafanya maauzi ya kuua mtu , hapa naomba usinielewe vibaya ila ni kwamba kuna watu ni wachokozi sana ndani ya taifa hili na mimi sipendi mtu anaenichokoza , hivyo afande ikitokea nimeua you have to clean up the mess for me”Aliongea Roma na Mzee huyu alitoa macho , kwani aliona sharti hilo kuwa kubwa na Roma aliona kusitasita kwa Meja.
“Meja ombi langu ni hilo , kama haliwezekani sinabudi pia kukataa ombi lako na kuhusu wanajeshi wangu nitatafuta namna ya kuwabakisha Tanzania maana hilo lipo ndani ya uwezo wangu”Aliongea Roma na Afande Maeda alifikiria ombi hilo kwa dakika kadhaa.
“Okey Deal Mr Ramoni , utafundisha jeshi letu mafunzo ya hali ya juu na mbinu zote zinazomilikuwa na jeshi la The Eagles na mimi nitahakikisha na ‘Clean up the Mess’ lakini licha ya hivyo Mr Roma nataka kukuambia kuwa hii nchi inaendeshwa kwa sheria , hivyo hatutakuwa tayari kuona unavunja sharia kwa namna ambavyo unapenda”Roma alitabasamu na kisha alipeana mkono na Meja Generali Maeda.
“Kanali hapa atakuwa na wewe bega kwa bega katika zoezi hilo , na tunatarajia mafunzo hayo yaanze mwenzi ujao yaani baada ya wiki tatu kuisha kutoka leo”
“Hakuna shida Meja”Aliongea Roma na kisha wakaagana huku akisindikizwa mpaka nje eneo la kuegesha Magali , jambo ambalo kwa wanajeshi walikuwepo eneo hili kushangaa.
Wakati wanapeana mikono mara iliingia pikipiki na kwenda kusimama mita kadhaa umbali walipokuwa wamesimama Roma.
Na dereva wa pikipiki alitoa helmeti na hapo ndipo Roma alipomshuhudia Mage mwanadada mrembo ambaye kila siku wanapokutana ni kwa shari., alijiuliza mrembo huyu kaja hapa ndani kufanya nini maana kwa kumbukummbu zake alikuwa anaelewa kuwa Mage alikuwa ni polisi na hapa ndani hapakuwa pakimuhusu.
Comments