Roma aliendelea kumshangaa Mage mpaka pale alipowafikia, huku akiendelea kujiuliza maswali ni jambo gani limemleta Mage makao makuu ya jeshi , baada ya Mage kuwafiikia , alisimama wima kama mwanajeshi na kisha akakakamaa mwili maarufu kama kubana ta*ko.
“Jambo Afande , jambo afande ,Ajenti Flamingo kutoka kikosi cha wachawi naripoti”
“Karibu tena Tanzania Ajenti Flamingo”
“Asante sana Afande” Huku akilegeza , huku upande wa Roma akishangazwa na kitendo hiko inakuwaje Mage akawa mwanajeshi ghafla tena ndani ya kikosi cha wachawi.
“Meja naomba niulize kwanza”Aliongea Roma na kuwafanya maafande hawa wamwangalie na kumpa ruhusa .
“Huyu si Mage , polisi namba moja kwa kunichukia hapa Tanzania , mbona ni mwanajeshi?”Aliuliza Roma na Afande Maeda alitabasamu baada ya kuona Mage na Roma washakutana na kisha akamwangalia Afande Tobwe.
“Magreth ni polisi ndio , huyu ni pacha wake anaitwa Magdalena Tobwe ni Special Ajenti kutoka kitengo maalumu cha kupambana na maadui wanaotumia nguvu za giza na alikuwa nchini China kwa miaka minne akisomea mafunzo ya uchawi wa kachina na kijapan”.
“Kwa hio Afande Meada Mage na huyu Magadalena baba yao ni Kanali Tobo?”
“Kijana kuwa na Adabu nishakwambia naitwa afande Tobwe sio Tobo “Kitendo kile cha Roma kumuita baba yake Magdalena Tobo kilimuuzi.
Roma alimwangalia mwanadada huyu ambaye alikuwa akifanana kwa kila kitu na Mage na kisha akatabasamu na kisha akaagana na maafande na kuingia kwenye gari yake kuondoka.
Baada ya Roma kuondoka Afande Maeda alimwangalia Ajenti Flamingo na kisha akamgeukia kanali.
“Ajenti Flamingo wewe ni invicible Solder na kwanzia sasa utakuwa unafanya kazi kwa ukaribu na Pluto”.
“Afande unamzungumzia Pluto gani?”Aliongea Flamingo kwa mshangao na Afande Maeda alitabasamu
“Unaonakena kuwa na habari za kutosha kuhusu Pluto ulipokuwa kwenye mafunzo si ndio?”
“Ndio Afande , nimesikia sana habari zinazomuhusu Mrithi wa Mfalme Pluto Hades , hakuna mwanajeshi yoyote wa kitengo cha uchawi ndani ya China asiemfahamu Hades”Aliongea Ajenti Flamingo huku wakiwa wanaingia ndani ya ofisi.
Na baada ya mkuu wa Afande Maeda kukaa kwenye kiti chake , huku kanali Tobwe alikuwa asharudi kwenye ofisi yake kuendelea na majukumu.
“Okey Ajenti Flamingo , ninachokuambia hapa ni siri za jeshi na wewe kama mwanaeshi unapaswa kutotoa siri hii , hata Raisi amiri mkuu wa jeshi hajui hili ninalokuambia niswala linalojulikana na watu wachache sana ndani jeshi”Alitulia kidogo na kuvuta pumzi.
“Kijana tuliekuwa tumesimama nae hapo nje ni Pluto mwenyewe , ambaye umezisikia sana habari zake”Ajenti flamingo alijikuta akishangaa mno na alionekana kutokuamini maneno ya Mkuu wake.
Naona umeshangaa , lakini pia utakuwa unajiuliza kwanini na kuambia siri hii , nimekuambia kutokana na kujua uwezo wako wa kimapigano , wewe ni komandoo , lakini pia unajua mbinu zote za kichawi na uwezo wako unakufanya kuwa mtu sahihi wa kufanya kazi na Pluto”Ajenti Flamingo alizidi kushangaa .
Ukweli ni kwamba tokea aende kwenye mafunzo kichawi (Cultivation training) nchini china alikuwa akiskia habari nyingi zilizokuwa zinamuhusu Hades au pluto kama moja ya macultivator wakubwa waliovuka steji za juu kabisa za kucultivate.
Pluto na Hades ni majina sawa , Pluto ni jina ambalo miaka ya nyuma mtoto Venetia Burney aliekuwa mpenzi wa kusoma hadithi za Ugiriki alipenda kumuita Hades kama Pluto na kuanzia kipindi hiko jina la Pluto likawa maarufu Zaidi kuliko hades.
Licha ya mshangao wa Ajenti Flamingo na kukubali kazi hio , hakuwa akiamini kwamba mtu aliekuwa akisifika kwa ulozi wa kachina na Japani Mfalme Pluto kutoka jeshi la The Eagles ndio Yule mwanaume aliekuwa hapo nje , akili yake ilikataa kabisa , lakini akajiambia kwenye nafsi yake kwamba ataendelea kulithibitisha hilo kwa kumfatilia Roma kwa kila atakachokuwa anafanya
Ni muda wa saa nane nane hivi , wakati Roma akiwa ameshusha kiti cha gari yake na kuuchapa usingizi ufukweni kilomita chache kutoka lilipokuwa Daraja kubwa la Tanzanite , simu yake ilitoa mlio na aliinua na kuangalia na kujikuta akitabasamu.
“Hehe.. kwa mata ya kwanza Edna kanipigia” aliiongelesha Roma huku akipokea simu baada ya kuona jina la ‘My Wife’ kwenye kioo.
“Ndio wife , usiniambie umenimiss mume wako?”.
“Uko wapi?”
“Ufukweni bebi”.
“Njoo tukutane My World Fashion Mall pale”Na simu ikakatwa, Roma alitabasamu huku akifikiria ubabe wa mke wake , ila hakujali sana aliwasha gari na kisha alielekea lilipo jengo refu sana ndani ya Posta lililokuwa likifahamika kwa jina la My World Fashion Mall
Roma ndani ya madakika kadhaa tu alikuwa ashafika na nikama walikuwa wameambizana , kwani wakati Edna anaegesha gari na Roma alikuwa akiingiza gari maegeshoni, alisimamisha na kufungua mlango na kisha akamrushia ufunguo Valet(mtu uanaehusika na kupaki magari) na kumsogelea Edna.
“Bebi hapa tumekuja kufanya nini?”Edna hakujibu Zaidi ya kutangulia na Roma alimsogelea na wakaingia kwa pamoja na kama kawaida watu wengi wlaikuwa wakimshangaa Edna kwa uzuri aliokuwa nao , kuna waliokuwa wakimjua kama mfanyabiashara mkubwa , lakini pia kuna ambao hawakuwa wakimjua.
Edna hakuwa mtu wa kupenda sana kunyionyesha kwenye mitandano na vyombo vya habari , hakuwa hata na akaunti yoyote katika mtandao wa kijamii na ni watu wachache sana waliokuwa wakimfahamu na hata mara nyingi kama tu atasaini mkataba ambao utahusisha waandishi wa habari mara nyingi Dorisi ndie aliekuwa akimuwakilisha , hivyo ndani ya Tanzania imemfanya kutotambulika sana licha ya kuwa mwanamke ndani ya taifa mwenye pesa nyingi kuliko mtu yoyote.
Baada ya kuingia kwenye duka moja kubwa ambalo lilikuwa limesheheni nguo za kiume , Edna alianza kupita taratibu upande wa suti na alionekana alikuwa akichagua , huku wafanyakazi hapa ndani wakionekana kutoa heshima kubwa kwa Edna.
Aliangalia baadhi ya suti karibia zote za Brand tofauti tofauti za ndani ya nchi na nje ya nchi na kila aliokuwa akivutiwa nayo aliinyoshea kidole na mfanyakazi wa hapa ndani alichomoa na kuishika mkononi.
Wakati huo Roma hakuwa na habari kwani alikuwa amekaa kwenye masofa , akimwangalia mke wake na kutabasamu , baada ya dakika kadhaa Edna alikuja akiwa amebeba suti na mashati mpaka alipokaa Roma.
“Kajaribu hizi nione zinakaaje kwenye mwili wako”Aliongea Edna kama kawaida na sura yake ya usiriasi.
“Bebi kwakua umezichagua wewe zitanipendeza haina haja ya kujaribu”
“Nimekuambia kajaribu”
Roma aliinuka huku akiangalia baadhi ya watu waliokuwa na wapenzi wao wakiwaangalia , na Roma alijua tu kuwa walikuwa wakimwangalia mke wake alivyokuwa mzuri.
“Kaka una mke mzuri , ukimsaliti utaonekana kichaa kaka , mchunge sana”Aliongea jamaa mmoja ambaye na yeye alikuwa akibadilisha.
“Jua mambo yako braza”Aliongea Roma huku akimpita na kwenda kubadilisha.
Walitumia takribani nusu saa ya kununua nguo viatu na saa .
“Bebi hivi vyote vya nini sasa?”
“Ni vya kwako na kesho utavaa hii na hii nyingine tukienda kwenye kusanyiko la wafanya biashara”Alionyesha moja moja.
“Kusanyiko la wafanyabiashara , mbona sijui kama tuna ratiba ya kwenda kwenye kusanyiko la wafanya biashara”
“Ndio nakuambia , ukisharudi inabidi nikakutambulishe kwa wafanyabiashara wenzangu”
Lakini wakati wakiwa wanaendelea kuongea , mara aliingia mwanadada mwingine hapo ndani akiwa ameongozana na mabaunsa kama manne hivi na kufanya hali ya hewa kubadilika kwani watu wote waliwakodolea macho.
“Donyi Donyi”Aliita Roma mara baada ya kumuona mwanamke aliekuwa mbele yake ni yule aliekutana nae siku kadhaa nyuma ufukwen, sasa Roma alimwita huyu mwanadada lakini huyu mwanadada ni kama hakuwa amemuona vizuri Roma na ile anageuka vizuri kumwangalia Roma alijikuta akipatwa na mshangao na kumkimbilia Roma na kumvaa mzima mzima mwilini na kumkumbatia , kitendo ambacho kilimfanya Edna na baadhi ya watu waliokuwa hapa ndani washangae , ikiwemo yule bwana aliempa ushauri Roma dakika chache nyuma.
Roma mwenywe ni kama tukio hilo kwake lilikuwa ghafla sana kwani alishindw akulizuia na aliona Donyi kaharibu Zaidi alivyoanza kumbusu mashavuni.,Roma alimwangalia mke wakena kumuona akianza kukunja sura kwa hasira na Edna alichukua mkoba wake na kupiga hatua kuelekea nje , huku akiona aibu , kwani aliona kitendo kile kimemdharirisha mbele ya watea waliopo hapo ndani kwani ni dakika chache nyuma tu walionekana kama mume na mke kweli lakini dakika kadhaa mbele kila kitu kimebadilika na mchepuko kwa Roma amemvaa.
“Sema wanaume hawajahi kuridhika , kwa jinsi yule mrembo alivyomkumbatia yule kaka ni lazima ni wapenzi”Aliongea mwanadada mmoja aliekuwa pembeni akilipia nguo alizonunua
“Tokea tulivyoachana nilishindwa kulala , kabisa nimekuwa nikikufikiria kila dakika kila sekunde kila saa , niliilaumu sana kwa kusahau kuchukua namba yako”Aliongea Donyi na kuzidi kumchangaynya Roma , alimtoa kwenye kifua chake na kisha akamwangalia.
“Donyi naomba nimuwahi mke wangu kwanza na naomba Mungu asije kutukutanisha tena”Aliongea Roma na kujitoa kwenye mwili wa mrembo huyu na kisha akachukua nguo walizonunua na kuwahi nje , lakini alikuwa amechelewa kwani ile anatoka aliona gari ya Edna ikitokomea nje kabisa ikiingia barabara kuu.
****
NEW YORK
Ni ndani ya chumba cha hoteli katika floor inayohudumia VVIP alionekana The First Black akiwa ameketi kwenye masofa ndani ya chumba hiki , huku mbele yake kukiwa na mwanaume mwingiene wa kizungu mwenye umri kimakadirio kama miaka arobaini hivi , aliekuwa amevalia suti na shati la blue na tai nyeupe .
Bwana huyu alifungua mkoba wake mweusi aliokuwa ameuweka pembeni na kisha akatoa picha na kumpatia mheshimiwa Mstaafu na Mheshimiwa alizipokea zile picha na kuanza kuangalia moja moja pasipo kubadili muonekanao wake , baada ya kuridhika na picha zile aliziweka kwenye meza ya kioo na kuinua macho nyake kumwangalia huyu bwana.
“Futeni Ushahidi wote , ambao unaweza kumfanya akafahamu ukweli , hakikisheni anajua kile ambacho tunataka sisi akijue na sio Zaidi ya hapo”Aliongea The first black huku akiangalia picha iliopo mezani , ni picha ambazo zilikuwa zikimuonesha Roma akiwa na Edna na picha hizi kwa haraka haraka zilionekana zilipigwa siku ambayo Roma na Edna walienda kusajili ndoa yao Bomani.
“Sawa mheshimiwa ila Mr President anataka nyaraka zote ambazo zinahusiana na Project LADO , maana kwa taarifa tulizonazo mpaka sasa inaonesha Urusi inataka imshawishi Agent !3 kujiunga nao , jambo ambalo kama litafanikiwa itakuwa hatari kwa upande wetu”.
“Kuhusu mikataba ile , nitakaa nayo , naelewa ni mali ya taifa , lakini mpaka sasa sina ninaemuamini nitaongea na Mr President mimi mwenyewe na kumuelewesha juu ya hilo , kuhusu Agent 13 acheni shaka kabisa , hawezi kujiunga na upande wowote, kabla ya kwenda Tanzania alisaini ‘The Gods Treaty’ na huu mkataba unamtaka kuwa Neutral , ninachowaasa ninyi kama CIA hakikisheni hamfanyi jambo lolote la kijinga na akafahamu kama mnafuatilia , itakuwa hatari kwenu na kwa taifa”Yule mzee alishangaa kidogo , lakini hakuweza kuongea chochote.
“Rogani Project LADO ilitugharimu kiasi kikubwa sana cha pesa na mpaka sasa mimi ndio mkuu wa Project hio , hivyo Raisi kusema kuwa anataka nyaraka ni swala ambalo haliwezekani , licha ya kwamba nchi yetu iliwekeza sehemu kubwa kuliko taifa lolote , lakini bado Project LADO ni ya kimuungano”
“Nimeelewa mheshimiwa na sisi kama CIA tutakaa mbali na Hades”The First Black alitabasamu na kisha alinyanyua glass ya wine na kunywa kidogo.
“Itakuwa vyema sana kama utawaweka vijana wako under Control , labda nikudokezee tu Project LADO inaendelea na sasa tupo kwenye Testing Phase(Hatua ya majaribio)
Rogani alionekana kumuelewa vizuri mheshimiwa na hakutaka kuongea neno lolote kumpinga The First Black.
Comments