Reader Settings

Ni siku nyingine  kabisa , siku ambayo Roma alikuwa akielekea nchini  Japani  kwa ajili ya kumuwakilisha mke wake katika dili nono  kati ya kampuni ya  Yamakuza  , Vexto na JR , ni muda wa asubuhi kabisa  saa mbili  kamili  Roma alikuwa ashajiandaa kwa kila kitu na kilichobaki  ilikuwa ni kuelekea  nchini Japan.

Edna alishuka  kutoka kwenye chumba chake akiwa tayari ashajiandaa kwa ajili ya kumsindikiza Roma mpaka uwanja wa ndege, baada ya wawili hao kuungana huku Edna akionesha  ukauzu wake kama kawaida mbele ya Roma ,alitangulia na kuingia  kwenye gari yake  ya Mercedenz aliokuwa akipendelea,na Roma na yeye akaingia na Edna kama dereva alitoa gari hio taratibu na wakatoka nje ya Geti na kuingia barabarani.

Muda mchache tu walikuwa washafika ndani ya uwanja huu wa ndege wa JNIA ,Doris alionekana kuwahi , kwani alikuwa ashafika tayari na alionekana alikuwa akiwasubiria , alikuwa amependeza kama kawaida kuzidi wanawake karibia wote walikuwa ndani ya uwanja huu wa ndege  na kufanya baadhi ya wanaume wamkodolee macho.

Wakati wanaendelea kuongea ,  mara walisogelewa na  watu wawili , mmoja akiwa ni mwanaume na mwingine alikuwa ni msichana mrembo hivi alievaaa akapendeza na hata kwa mwanaume alikuwa amependeza pia.

“Naitwa Isack Bathomayo ,Assistant CEO kutoka JR Group  na huyu ni Sasha sekretari wangu na mpenzi wangu ”Aliongea bwana huyu kwa kujitambulisha na kuwafanya Dorisi , Edna na Roma kushangaa  na Roma alijikuta akitukana matusi ndani kwa ndani Abuu , alikumbuka ile siku ambavyo Abuu alivyokuwa aking`ang`ania Edna aende huku akisema ni  masharti kutoka kwa Yamakuza , lakini leo hii alikuwa ametuma muwakilishi alijua yote yale yalikuwa ni mipango yao na anashukuru aliifahamu mapema .

Edna alimwangalia Roma kwa kuibiaibia na Dorisi pia alimwangalia Roma  na hawakutaka kuongea mengi ,Edna aliwapa  maelekezo ya kuwa makinni katika kusaini mkataba huo na kisha wakaagana na  ndani ya madakika  kadhaa tu ndege ya Emirates  iliapaa kuelekea Japan.

Kwenye ndege hakukuwa na maongezi mengi sana , kwani Dorisi  alilala mapema sana , aliekuwa macho alikuwa ni Roma ambaye alikuwa akiwakagua wahudumu wa ndege  kila aliekuwa  akija kumhudumia  ndani ya daraja la Kwanza la wafanyabiashara.

****

KANSAI -INTERNATIONAL AIRPORT,JAPAN

Saa kumi na moja kamili za Asubuhi Ndege  ya shirika la Fly Emirates iligusisha taili zake ndani ya uwanja wa kimataifa  wa Kansai  ndani ya jiji hili la Osaka.

Osaka ni moja ya miji mikubwa sana ndani ya Japani  ni mji ambao  ni mzuri sana kutokana na uwepo wa safu za milima ndani ya  jimbo lote la  Honshu, na ni sehemu pekee ambayo watu wengi wanaosafiri kwa ajili ya kutalii hupendelea sana kufika.

Osaka ni maarufu sana kwa raia wake kuishi watakayo , lakini pia  upatikanaji wa aina  nyingi ya vyakula na hili lilivutia sana watu na kwa kwa kiasi Fulani unaweza kuufananisha mji huu na Los Angels Marekani. Kutokana na mazingira yake na pia namna watu wanavyokula bata ndani ya hili jiji.

Muda huu wa  Saa kumi na moja  Roma , Dorisi pamoja na  wafanyakazi wawili wa JR Grupu   walikuwa washakamilisha taratibu zote na sasa walikuwa wakitoka  nje ya jengo hili  la kufikia wageni , baada ya kutembea na kufika  nje sehemu maalumu kwa  ajili ya kupokelea wageni , hatimae waliweza kumpata mwenyeji wao ambao alikuwa amekuja kwa ajili ya kuwapokea baada ya kuona bango la JR  na Vexto likiwa limeshikiliwa na kijana mmoja wa  Kijapani ambaye alikuwa amesimama na  bwana mmoja ambaye alionekana  kibosibosi kutokana na aina ya mavazi yake, alikuwa amevalia Navyblack suti  ambayo ilionekana kuwa ya bei kubwa  , pamoja na saa kampuni ya Brand ya Radeon.

“We’ve been expecting you, friends of Vexto and JR Group . I’m Yamakuza  Corporation’s Vice-CEO, Tikayi . My father, Yamamoto  was unable to make the trip down due to sickness, so I am welcoming you on his behalf, and also express his apologies.”

“Tulikuwa tukiwasubiria ndugu zetu kutoka Vexto grupu na JR grupu , mimi ni  CEO msaidizi wa  Kampuni ya Yamakuza  naitwa Tikayi , baba yangu  ameshindwa kuja kuwapokea  kutokana na maradhi yake na nipo hapa kuwakaribisha kwa niaba yake , na niombe Radhi kwa kutokuwepo kwake”:Aliongea Tikayi kwa kingereza safi.

“I never expected to be received so warmly, sorry to make you wait”(Sikutarajia mapokezi haya ya kikarimu  tusamehe kwa kukufanya  usubiri kwa muda mrefu” aliongea Doris .

“Tunafurahi  kukufahamu bwana Tikayi , Niite Roma  ni mkalimani kutoka kampuni ya Vexto”Aliongea Roma na kumpa mkono Tikayi na bwana huyu akatabasamu

“Nilikuwa nikisikia taarifa Tanzania kuna wanawake warembo   nadhani leo ninaamini fununu hizo ni za kweli”Aliongea na Dorisi alitabasamu , ila Roma hakupendezwa na namna ambavyo Tikayi alikuwa akimwangalia Doris.

“Ni kweli kabisa bwana Tikayi ,Tanzania  imebarikiwa na kuwa na wanawake warembo ila wanapendelea  wanaume wenye mashine kubwa sio kama wajapani na vipenseli  vyenu”Aliongea Roma kwa Kijapani na kumfanya Tikayi akunje sura , kwa dakika na kisha akatabasamu , huku Dorisi na wenzake wakishangaa ni nini Roma alimwambia mkaka wa watu mpaka akakunja sura.

Basi  waliongozana na kuingia kwenye magari  mawili  yote yakiwa ni Caddillac limousine ambayo yalikuwa yameandaliwa kwa ajili yao na kisha wakatoka nje kabisa ya uwanja  huu wa Ndege.

Jiji lilionekana kuwavutia sana Doris na  wafanyakazi wa JR kweli , kwani walikuwa wakishangaa miundombinu na kujikuta kutabasamu  bila kupenda, majengo ya Japani hayakuwa yameenda  hewani sana ,  lakini yalikuwa yakipendezesha mji kutokana na mpangilio.

Ndani ya dakika chache walifika ndani ya eneo moja lililokuwa likifahamika kwa jina la Ashiya , hii ni sehemu ambayo  inaishi matajiri wengi ndani ya Osaka na ni sehemu ghari sana kupata nyumba ya kuishi ndani ya eneo hilo  ni kama hapa Tanzania useme Osterbay ndio ilivyokuwa kwa Ashiya.

Sehemu hii ilikuwa katikati  ya Kobe na Osaka , na upande wa kushoto kulikuwa na fukwe ambayo ilizidi kupendezesha eneo hili.

Doris alionekana kupenda sana hili eneo na alishindwa kuzuia furaha yake na  kumwangalia Roma aliekuwa pembeni yake na kutabasamu.

Upande wa  Roma hakuonekana kushangaa sana , ila alionekana kama ni mtu ambaye  alikuwa akikumbuka   mambo mengi sana ya nyuma akiangalia maeneo haya.

Dakika chache mbele gari zote mbili zilikuja  kuingia ndani ya kizuizi  kilichokuwa kikipakana na barabara upande wa kushoto.

“Imekuwa heshima kwetu sana kufanya kazi na Kampuni kutoka Tanzania na kwasababu ya hilo tumeona ni vyema mkiishi kwa muda wote mtakaokuwepo hapa japani ndani ya Twillight  Villa ya kifamilia”Aliongea Tikayi  kwa kingereza na Dorisi alitabasamu na kisha akasema ‘Thank you’.

Hii sehemu ilikuwa nzuri mno na  ilikuwa ikiendana na sifa ya eneo hili kuitwa sehemu wanayoishi matajiri , licha ya ukubwa wa  eneo hili lakini pia  unadhifu wake ulifanya kuvutia sana , bustani zilikuwa zimejengewa kwa ustadi mkubwa na miti yake mirefu ya wastani  aina ya Italian  Cypress Tree ilizidi kupendezesha macho.

“Karibuni Sana”

“Asante” Alijibu Doris huku akivuta pumzi ya hewa iliokuwa ikinukia ndani ya eneo hili , na mbele yao kulikuwa na jengo ambalo lilikuwa limejengwa kwa muundo wa Nyota ,  lilikuwa ni jengo kubwa na la kuvutia sana ,  kwa mbele kulikuwa  sanamu  la Samurai lililokuwa limejengwa na kunakishiwa kwa madini ya Dhahabu   na kufanya sehemu hii kupendeza Zaidi.

Wakati wakiendelea kushangaa , uzuri wa hili  eneo ziliingia gari mbili za kifahari MBW 7  na kwenda kusimama mita kadhaa kutoka walipokuwa wamesimama  na akashuka mzee mmoja  hivi makadirio ya miaka sabini hivi akiwa na fimbo ya kutembelea na akawasogelea huku akiwa ameweka tabasamu pana usoni.

Aliwasalimia kwa ukarimu sana na kuwakaribisha  Japani ,Mzee alikuwa akiongea vizuri  kingereza kwa rafudhi nzuri  tofauti na Tikayi , huyu mzee ndio anafahamika kwa jina la maarufu la Yamamoto na ndio alikuwa  mmiliki wa kampuni ya Yamakuza na pia alikuwa Tajiri mkubwa ndani ya jiji hili.

“Mr Vice ni muda gani mazungumzo yetu ya kibiashara yataanza?”Aliuliza Doris na alionekana alikuwa akitaka mazungumzo ya kibiashara yaanze  wamalize ili wajue  mambo mengine

“Miss Doris , please rest assured, you’re all fatigued from the flight today, so please rest at our Villa for hours  My father and the others would also relax, and we will only begin the talks Tomorrow. Then, there will be two days of visits to the research facility, and exchanges with the researchers. Then, we will draft up a collaboration document.”

Hapo akimaanisha kwamba wapumzike kwanza ndani ya nyumba hio kwa masaa kadhaa kuondoa uchomvu unaotokana na safari  na  kesho wataanza  maongezi ya kibiashara  halafu baada ya hapo watatembelea  taasisi ambazo zinahusika na utafiti wa Material hayo mapya  na  pia mabadilishano ya watafiti  halafu watakaa mezani kwa ajili ya kujadiliana juu ya makubaliano ya pande zote .

Kwa mtiririko mzima wa kikazi itawachuku jumla ya siku tatu kukaa ndani ya nchi hii  ya Japani  na Doris alitabasamu , aliona atapata wasaa  mwingi wa kukaa na Roma na kufurahia Maisha.

“Roma ushawahi  kufika Japan?” Aliuliza mzee Yamakuza na Roma alimwangalia na kutabasamu na kisha akasema hakuwahi kufika , ila  ukweli Roma kwenye moyo wake alikuwa amekuja ndani ya Japani mara kibao na mara zote alizoingia ndani ya hili taifa ilikuwa ni kwa kazi maalumu.

“Waheshimiwa mnaonaje kwanza tukiachana na maongezi na mkafanya mpango wa chakula maana nahisi njaa sio ya kawaida” Aliongea Roma mara baada ya  kuona mzee huyu alikuwa bize kuongea na Dorisi juu ya  umaarufu wa Japani na mambo yake ya kipekee  yanayopatikana na Roma mambo hayo yalimchosha maana kwake hayakuwa na maana.

Msosi uliandaliwa baada ya mzee huyu kuwapa ishara wafanyakazi wa hapa ndani na ndani ya madakika kadhaa tu  Meza ilichafuka kwa aina  mbalimbali ya mapishi . jambo ambalo lilimfurahisha sana Roma.

Baada ya kupata chakula  ambacho haikueleweka ni chakula cha asubuhii au cha mchana  , Roma na Doris na wale wapenzi kutoka JR grupu walionyeshwa sehemu  zao za mapumziko.

Dorisi na Roma kama kawaida walipewa chumba kila mmoja cha kwake , lakini waliishia kuwa ndani ya chumba kimoja na kuanzia asubuhi mpaka muda wa jioni  ilikuwa ni kukiamsha na hata chakula cha mchana walikula  humohumo.

Saa mbili kamili za jioni Roma  , Dorisi na wale wapenzi kutoka JR  walitoka kwenye vyumba vyao mara baada ya kuitwa na wahudumu  kwa ajili nya chakula cha  usiku , na walijikuta wakishanngaa mara baada  ya kukuta watu wengi waliokuwa kwenye meza tofauti na ilivyokuwa asubuhi.

Baada ya kuketi kwenye nafasi ambazo walionyeshwa na wahudumu , Mzee Yamamoto alianza kuwatambulisha kwa wageni hao waliokuwa  wanaonekana kuvaa mavazi ya suti na hapo Roma na Dorisi ndipo walipowatambua kuwa hao ni moja ya wafanyakazi wakubwa wa kampuni ya Yamakuza na  wamealikwa kwa ajili ya chakula cha jioni kama sehemu ya kujipongeza katika mafanikio ya kuelekea kusaini mkataba kati ya Yamakuza na Kampuni mbili kutoka Afrika.

Msosi wa nguvu  uliandaliwa  , jambo ambalo lilimfurahisha sana Roma  kiasi cha kutoa tabasamu, wageni hawa  walitoa mshangao mara baada ya Roma kuanza kula  bila habari , kwani wote walikuwa hawajaanza na ni kama walikuwa wakisubiria kukaribishwa na mzee Yamamoto , ila  wakati wao wanasubiria Roma yeye alikuwa tayari ashaanza yake na hata Dorisi alimshangaa Roma ila aliishia kutabasamu na hata kwa mzee  Yamamoto aliishia kutabasamu na ilibidi wote waanze kula.

Wakati wanaendelea  kula mara aliingia bwana mmoja ambaye alikuwa amevaa  suti lakini kwenye mfuko wa suti yake kukiwa na kibango kidogo kilivhokuwa kikionesha nafasi yake ya kazi ndani ya nyumba hii  yaani ‘House’ Meneja  na kumsogelea mzee Yamamoto na kumnong`oneza jambo na mzee huyu aliweka vijiti(chopstick) vyake alivyokuwa anatumia  kula.

 “Huu ni ujinga” Aliongea kwa  sauti na kwa hasira  na kufanya waliopo hapa ndani washangae.

Previoua Next