Reader Settings

Kila mmoja alishangaa kwanini mzee huyu alipandwa na  jaza ghafla namna hio mara baada ya kunong`onezwa jambo na muhudumu wa nyumba.

Tikayi aliekuwa amekaa  pembeni na baba yake alionekana kutokuwa na  wasiwasi kabisa ni kama mtu ambaye alikuwa akijua ni taarifa gani baba yake ameambiwa.

Na wakati wakiendelea kujiuliza ni kwanini mzee Yamamoto kapandwa na  Jazba mara aliingia bwana mmoja mkumkukuku  , bwana ambaye alikuwa amevalia shati lake rangi ya maua maua  na suruali ya Jeans.

Bwana huyu ukimwangalia  mara moja tu utagundua kuwa Tikayi na huyu bwana  ni ndugu kimuonekano, jamaa huyu baada ya kuingia  alijikokota na kudondoka kwenye miguu ya Yamammoto na kisha akaanza kulia  kwa sauti  na alionekana kulewa pia , jambo ambalo lilifanya hali ya hewa kuwa mbaya.

“Wu.. baba .. ninafanya nini mimi..  aaaaaah Dina kaniacha baba ..iiii .. Dina..weeee… aaaa”

Jamaa alikuwa akilia mpaka anatema mate kitendo kilichozidi kumkasiriasha mzee Yamamoto  na alichokifanya ni kumpiga teke na akadondokea upande mwingine  , lakini huyu bwana  aliamka tena na kukamata  mguu wa baba yake na kuanza kulia tena huku akiwa anamtaja mwanamkie anaeitwa Dina akilalamika ameachwa , na kila mmoja aliekuwa hapa ndani alikuwa ashajua ni nini kinaendelea kwa huyu bwana, walijua yote hayo ni sababu ya kimapenzi. Na bwana huyo alikuwa ameachwa.

“Jamani naomba mniwie radhi kwa jambo hili , huyu ni mwanangu mkubwa Tikayeshi , lakini licha ya kuwa mkubwa katika familia  , ndio  mpumbavu kuliko wanangu wote”Aliongea mzee huyu  wa kijapani huku macho yake  yakiwa  mekundu kwa hasira.

“Hakuna shida mzee ni jambo la kawaida kwa vijana” Aliongea moja ya wafanya kazi wa kampuni na mzee huyu aliwapa ishara walinzi wamtoe eneo hilo na bwana huyu alikokotwa na kutolewa huku akiendelea kulia kwa sauti kama toto jinga , na kwa kumuangalia tu ungejua kuwa  ni sahihi kwa  mzee Yamamoto kumuitwa Tikayeshi mtoto mpumbavu kuliko Watoto wake wote.

Tikayi alionekana kutabasamu na kufurahishwaa na tukio hilo , ali mwangalia  baba yake alivyokuwa na hasira na  kuridhishwa na hali hio.

Basi baada ya chakula wageni wale walitawanyika na  hata kwa Mzee Yamamoto waliagana na Roma na kuwatakia usiku mwema huku wakiwaahidi kuonana keshi kwa ajili ya mazungumzo ya kibiashara.

Roma aliingia kwenye chumba chake  na hata kwa Dorisi hivyo na wale wawakilishi wa JR pia kila mmoja aliingia kwenye chumba chake .

Roma  baada ya kuingia alipunguza nguo na kisha akajilaza kitandani kuutafuta usingizi kwani muda hio ilikuwa yapata  saa nne usiku.

Roma alitumia nusu saa tu kujipumzisha mara mlango uligongwa na kujikuta akishangaa nani anagonga, kwani  walikuwa washaagana na hata na Dorisi pia , akiwa na singlendi yake pamoa na pensi , alisogelea mlango na kufungua na mbele yake alikuwa mhudumu wa kiume ambaye alikuwa ameshikilia sahani ambayo ilikuwa imefunikwa na kitambaa cheupe  na Roma akamwagalia huyu mhudumu pasipo kumsemesha chaohcaote na kushangaa ameleta nini kwani hakuwa amegiza aina yoyote ya huduma  , lakini ghafla tu muhudumu huyu wa alievalia sare za hili jumba alitoa kile kitambaa kwa kasi na kwenye ile sahani kulikuwa na kisu na alikishika haraka sana kwa ustadi na kumrushia Roma kwa madhumuni ya kumdhuru  ,  lakini Roma ni kama vile alitegemea , kwani ile kisu kinarushwa alihepa kushoto na  kisu kikapita nusu inch na umbali wa kidevu chake kiasi kwamba hata ndevu ziliguswa  kiana na Roma hapo hapo akajua huyu ni mhudumu feki na ametumwa kwa ajili ya kuua.

Baada ya mhudumu huyu feki kuona Jaribio lake limefeli , alirusha ngumi lakini kwa Roma alimuona kama mtoto anaejifunza kurusha ngumi  kwani aliushika mkono na kuuzungusha  na kilichosikika ni mlio  wa mifupa kukatika  , na Mhudumu feki akaachia  mguno wa maumivu , lakini Roma hakuishia hapo tu , alimpiga kwenye koo kwa mkono , kama vile alikuwa akimchinja  , kwnai pigo hilo lilikuwa ni la Karate na mhudumu  feki   aliregea na kudondoka chini.

“Shi*t watakuwa wengi hawa ,Dorisi atakuwa kwenye matatizo”

Aliongea Roma na kuchomoka kwa spidi kuwahi kwenye chumba cha Dorisi na ile  anafika tu alimuona mhudumu akiingia ndani ya chumba cha Dorisi  huku akiwa na sahani kama ile ile  ya mhudumu aliemuua  ikiwa imefunikwa na kitambaa cheupe.

Roma alikimbia kwa kasi na kuzama na ile anafika  mhhudumu alikuwa tayari ashashika kisu  na kumlenga nacho Dorisi kooni  na Dorisi aliishia kufumba  macho huku akiwa anatetemeka mwili mzima akisubiria kifo , lakini mhudumu baada ya kufikisha sentimita mbili karibu na koo la Dorisi alidakwa mkono na kuzungushwa kwa nguvu ambayo hakuwa ameitegemea  , na baada ya kugeuka  tu, aliopigwa na mikono miwili  kwa wakati mmoja na Roma kwenye mbavu na mhudumu yule wa kijapani aliishia kuachama na kukosa pumzi na kisha akadondoka chini kwani mbavu zilikuwa zishakatika.

Dorisi alihikuta akimkimnbilia Roma na kumkumbatia huku akianza kulia kama mtoto na Roma alimtuliza na walati huo huo aliingia ndani ya chumba cha Dorisi Tikayi.

“Mko salama?” ndio swali la kwanza kutoka kwa Tikayi  huku akimwangalia Roma  kwa macho ya kumsanifu.

“Naona mmetuleta Japani kwa ajili ya kutua”Aliongea Roma kwa hasira na Tikayi alianza kuomba msamaha kwa tukio hilo  na wakasema kwamba hawahusiki nalo.

“Mr Roma hili swala halituhusu hata kidogo na tutahakikisha tunawakamata  wahusika , kwani tunaamini ni watu ambao wametumwa”:

Aliongea Tikayi  na muda huo huo aliingia  bwana mmoja alievalia Robes za kitamaduni za Japani huku akiwa ameshika upanga kwenye mkono wake na Roma kwa kumuangalia tu aliuona huyo jamaa anajua mapigano.

“Yoshida  hakikisheni  mnamkamata aliehusika na  hili jambo haraka , naamini ana watu wake humu ndani na bado wapo, kagua wahudumu  wote mmoa mmoja” aliongea Tikayi na bwana huyu aliamrisha walinzi waliokuwa wamevalia mavazi ya majoho meusi kama yeye  na kuanza kutawanyika kumtafuta muhalifu.

Dorisi na Roma walitolewa na kupelekwa  kwenye chumba maalumu cha usalama Zaidi na wakati huo huo mzee Yamamoto na yeye aliingia kwa spidi na kuanza kuasihi Roma, Dorisi na  wawakilishi wa JR grupu watulie   mpaka pale mtuhudumiwa atakapo kamatwa huku akiomba msamaha kw akujitetea jambo hilo hawakuwa wakihusika nalo.

Wote walikusanyika na  kukaa kwenye masofa haya , akiwemo Tikayi ,Yamamoto Roma ,Dorisi pamoja na wawakilishi wa JR Group , wakati wakiendelea kuongea juu ya tukio hilo ambalo halijawahi kutokea ndani ya hii nyumba kutokana na ulinzi wake , mara  aliingia meneja  wa nyumba , yule ambaye alimnong`oneza Yamamloto kuhusu ujio wa kilevi wa Tikayeshi.

“Kuna nini  meneja?”

“Boss kuna simu yako hapa kutoka kwa mtu ambaye  hatumjui na anadai humu ndani  ametegesha  mabomu”

“Mabomu!”Aliongea kwa kupaniki  huku akichukua ile simu na kusikiliza.

“Mr Yamamoto , nyumba yako yote  imejaa mabomu ambayo yataripuka baada ya nusu saa , na hata ujifanye kuyatafuta  hautoweza” ilisikika sauti  hio ya kijapani kwenye simu na Roma aliisikia vyema kwani na yeye alikuwa akijua kijapani.

“Unataka nini katika familia yangu”Aliongea Yamamoto kwa  hasira kwa kijapani.

“Kwanza kabisa  nikwambie tu kwamba mabomu yatalipuka  baada ya nusu saa na hata kama ulete wataalamu wa uwezo wa juu hatoweza kufanikisha hilo ndani ya nusu saa , na mabomu hayo ni ya sumu kwa maana hio nikibonyeza kitufe ambacho nimeshikilia hapa , itawachukua dakika tano kwa kila kiumbe ndani ya nyumba kufariki”

“Sema unataka nini acha maneno mengi”

“Ni jambo rahisti tu nahitaji Yen Bilioni kumi zinifikie mahali ambapo nitawaambia  na  nataka Cash….” Aliongea bwana huyo , lakini muda huo huo aliingia Tikayeshi huku akilia.

“Baba .. mabomu … mabomu baba… tunakufa .. Mama wee.. babab niokoe sitaki kufa sitomuaona tena Dina mimi ,,,,aaaaaa” Alilia  bwana huyu  kama chizi kiasi kwamba Yamamoto alikasirishwa Zaidi na kujisemea moyoni  boar ahata abadilishane na mt una  gunia la Pumba heanda akapunguza hasara ya kuwa na toto jinga.

“Mtoeni huyu mpuuzi hapa” Aliongea Yamamoto na Tikayeshi alitolewa huku akiendelea kulia kwa sauti akitaja mabom na baada ya Tikayeshi kuondoka Yamamoto aliendele akusikiliza simu.

“Endelea na masharti yako nakusikiliza”

“Nishasema mzee kiasi ninachotaka , shariti la pili mtu atakae leta hizo pesa lazima awe wewe au Tikayi” mzee alitoa macho.

“Kwanini mimi au  Tikayi , shida yako ni pesa  na tutakupatia haina haja ya mimi kuja au Tikayi kuja”.

“Mzee nadhani  haulewi nishasema nahitaj wewe uje ulete pesa hizo au Tikayi ndio alete  na  niwaambie tu naona kila kitu mnachokifanya hapo ndani na ikitokea mtu atatoka ama kuingia ndani ya hio nyumba bila ruhusa yangu nabonyeza kitufe na  Maisha yenu yatakuwa yamefika mwisho na kama haumini mlangoni hapo kuna mtu aliesimama kama kaegeshwa” Wote waliangalia mlangoni na kuona kweli kulikuwa na mtu ambaye alikuwa ni mlinzi wa Yamamoto na wakaini ni kweli bwana huyu alikuwa akiwaona.

Mzee yamamoto   jasho lilianza kumtoka , licha ya kwamba kulikuwa na baridi kali lakini jasho lilionekana kwenye uso wake , hakuwa tayari kumuachia Tikayi aende kwani alikuwa ndio mrithi pekee na ndio mtoto ambaye alikuwa na akili , kwani kaka yake alikuwa ni kama chizi.

“Okey  tupe dakika kumi na tano  tukuandalie Cash”

“Dakika kumi zinatosha hakuna maongezi  na narudia , naona kila kitu kinachoendelea  hapo ndani mpaka panya wanaoingia na kutoka, hivyo nikiona mtu anatoka   ambaye sio wewe au Tikayi nabonyeza kutufe na kuwalipua”.

“Sawa tupe dakika  kumi tukuandalie Cash”

“Nitapiga baada ya dakika kumi , muwe na Cash  na ndipo nitawapa eneo mnalotakiwa kuja”

Baada ya simu kukatwa Yamamoto alimuuliza Tikayi kama wanashilingi ngapi hapa ndani na Tikayi alisema wana Yen bilioni kumi na nusu, mzee baada ya jibu hilo alipata ahueni na kumuagiza  Tikayi akaziweke kwenye begi na baada ya dakika kama saba hivi Tikayi alirudi akiwa ameshikilia begi  zito likiwa na vibunda vya hela .

“Nitaenda mimi baba”Aliongea Tikayi na kufanya watu wote  hapo ndani washangae.

“Hapana Tikayi , hao majambazi siwaamini kabisa  wanaweza wakakufanya kitu , kibaya na wewe ndio mrithi pekee ambaye napanga kukuachia kuiongoza Yamakuza , hapana siwezi kukuruhusu kwenda”

Aliongea Yamamoto  lakini Tikayi aling`ang`ania kwenda na baada ya malumbanio ya   dakika mbili Mzee huyu alikubali Tikayi aende lakini akimsihi kuwa makini.

Baada ya dakika kumi Jambazi lilipiga simu na kutoa maelekezo ya sehemu ambayo alitakiwa kwenda , ni sehemu moja iliokuw aikifahamika kwa JPN.

Jambazi aliendelea kuwapiga mkwara  kwamba hakuna mtu kutoka Zaidi ya Tikayi,  na mzee Yamamoto  licha ya kwamba alionekana kuwa na wasiwasi mkubwa ,  alikubaliana na Jambazi , kwani hakuwa akitaka kuona watu wote waliokuwa  humu ndani wanakufa kisa pesa,

Baada ya Tikayi kutoka  akielekea mahali ambapo  majambazi hayo ndio walisema wapo , Roma hakubaki hapo kwenye chumba  cha usalama  , alitoka  na kuelekea kwenye chumba chake na baada tu ya kufika , aliangalia nje kwa kutumia dirishani kwa sekunde kadhaa na kisha akatabasamu  na kufungua dirisha , alirudi na kuvaa  shati na suruali na kisha  akarudia dirisha na alionekana alikuwa akijiandaa kuruka.

“Unataka kuniacha sio?, ndani ya hii nyumba unajiokoa mwenywe ”Ilikuwa ni sauti ya Dorisi  iliomfanya   Roma aliekuwa amepandisha mguu kwenye dirisha ageuke na kumwangalia Doris.

“Doris narudi ,baki hapa naamini hakuna kitakacho kutokea” Aliongea Roma

“Hapana tunaenda wote na sipo tayari kubaki”Aliongea huku akionekana yupo siriasi na Roma alifikiria kwa sekunde  na kisha akamgeukia.

“Utaweza kuruka hapa?”

“Hapana”

“Sasa utaendaje na mimi kama hapa huuezi kuruka” Dorisi hakuwa na jibu na Roma alifkiria jambo  na kisha akamwangalia.

“ Natangulia kwenda chini , utajirusha na mimi nitakudaka”Aliongea lakini Dorisi alitoa mshangao , kwani alipochungulia umbali  kutoka walipo mpaka chini  aliogopa.

“Kama huwezi mimi nitaondoka mwenyewe”

“Okey nitajirusha kama kweli utanidaka”.

“Usijali nitakudaka”Aliongea Roma  na kumwnaglaia tena Dorisi.

“Nitahesabu mpaka nne usipojirusha naondoka”.

Baada ya kuongea Roma alijirusha chini na kwenda kutua kwenye bustani  bila ya kupiga kelele ya aina yoyote ile , alionekana kuwa mtaalamu kweli na baada ya kutua aligeuka na kuangalia  juu huku akimpa ishara Dorisi ajirushe , ila Dorisi alikuwa akitetemeka  ,Roma baada ya kuona Dorisi anatetemeka na hayuko tayari kujirusha , alimuonesha vidole kwa ishara na kuanza kuhesabu , na ile anafika  tatu Dorisi alimpa ishara ya kujirusha na hakuwa na jinsi alikuwa akiogopa kufa mabomu na hakutaka kubaki mwenyewe hapo ndani na ndio maana alitaka kuondoka na Roma , alifumba macho na kujiachia kwa ujasiri  na ile anafika chini alikuwa kwenye mikono ya Roma , huku akihema kwa kasi sana na Roma alimtuliza na kumwambia apunguze presha.

Previoua Next