Dorisi na Roma walizidi kushangaa kwa hali iliokuwa hapa ndani , kilichowafanya washangae zaidi ni uwepo wa Tikayeshi na Abuu.
Wakati huuTikayeshi hakuwa tena yule toto jinga aliekuwa akililia mapenzi kama alivyokuwa dakika kadhaa nyuma ,pia hakuonekana kama mpumbavu kama baba yake Yamamoto alivyokuwa ana muita , Dorisi na Roma walimuona Tikayeshi kama mtu anaejiamini.
Upande wa kulia alikuwepo Tikayi akiwa na begi lake vilevile kama alivyotoka Twillght Villa huku upande wa Tikayeshi alikuwa amesimama na Abuu ,Yoshida yule mlinzi ambae Roma alimtambua kwa uwezo wake wa kimapigano kwa kumuangalia tu , lakini pia walikuwepo baadhi ya walinzi wa Mzee Yamamoto ambao wote walionekana wapo tayari kupambana kwa ajili ya Tikayeshi..
Kwa hii hali ya hapa ndan Roma na Dorisi waligundua Abuu yuko upande wa Tikayeshi ,lakini swala walilojiuliza ni vipi akawa upande wa Tikayeshi na ni sababu gani kaamua kufanya hivyo kwani Abuu alikuwa na kiasi kikubwa cha pesa tu hivyo hawezi kutega mabomu ndani ha Twillight Villa kwa ajili ya kupata kiasi cha Yen Bilioni kumi.
"Tikayi umekuwa wa kujifanya mjanja sana na leo ndio utakuwa mwisho wako"Aliongea Tikayeshi huku akiwapotezea Dorisi na Roma kama vile hajawona , walionekana kujiamini kutokana na Sitaha walizokuwa nazo ,lakini pia walionekana kujiamini kutokana na wingi wao na pia waligundua kuwa Dorisi Na Roma wako peke yao baada ga Mlinzi mmoja kutoka na kukagua eneo la nje kujihakikishia kama kuna watu wengine waliokuja nao.
"Tikayeshi nimekufanya nini mpaka unichukie namna hii ya kunipangia njama kwa ajili ya kunidhuru mimi mdogo wako wa damu"
"Tulia acha kuongea unafiki Tikayi , unajua sana nini umefanya kwenye Maisha yangu mpaka ukanifanya kuchukua haya maamuzi magumu , siku zote baba alikuwa ni mwenye kukupendelea na kukuona una akili sana kuliko mimi na akaniita mtoto mjinga bila ya kuutafuta ukweli wote,umekuwa ukinizunguka kwa kila kazi ambayo baba alikuwa akinipatia na kuhakikisha inafeli , ili tu nionekane mjinga na uchukue nafasi yangu ndani ya urithi katika famlia"
Tikayeshi aliongea kwa uchungu sana na jambo ambalo alikuwa akiongea lilionekana kuwa kweli na kwa jinsi hali ilivyo, ilionesha Tikayeshi hakuwa mjinga kama Baba yake alivyokuwa akimuona , ila ilionekana pale ambapo Tikayeshi alikuwa akipewa Jukumu ndani ya kampuni ,Tikayi alikuwa akihakikisha jukumu hilo linafeli , alifanya hivyo ili Tikayeshi aonekane hana akili na hayuco ‘competent’ katika kuongoza kampuni.
Dorisi na Roma walionekana kushangaa , ila walikaa kimya kuangalia Drama hio ya kifamilia waone nini muisho wake ,Katika mapambano hayo ya kugombea urithi.
Kwa Roma hakuonekana kushangaa sana , alionekana kuzoea kuona mambo hayo yakitokea mara kwa mara ndani ya familia za kitajiri ,watoto kugombana mpaka kuana kisa tu kupata urithi , kwake ni mambo ambayo hayakuanza leo wala juzi ni , ni mambo ambayo yalikuwepo tokea enzi za kale na yataendelea kuwepo.
"Hahahahaha.... Tikayeshi wewe ni mjinga na siku zote utakuwa mjinga .. na nikuambie tu mimi mdogo wako nimekuzidi kila kitu"
"Acha kuongea ujinga Tikayi , leo ndio mwisho wako na kauli zako za majigambo nakuua hapa na kampuni itakuwa yangu"
"Huna uwezo huo Tikayeshi .. hauko smart kichwani kama mimi na haitokuja siku ukanizidi akili .. masikini kaka yangu , jaribu kuniua kama una uwezo huo"
Roma na Dorisi walishangaa namna Tikayi alivyoanza kujiamini , lakini pia hata kwa Tikayeshi alishangaa na kupandwa na jaziba maradufu na kupandwa na hasira, yeye alitaka amuone Tikayi akipiga magoti na aombe asimuue lakini hali imekuwa tofauti , kwanini asishangae.
"Mpigeni risasi acheni kuzubaa muda unaenda"
Aliongea Tokayeshi lakini ajabu ni kwamba vijana wake hawakuonekana kusogea wala kunyanyua siraha zao na alishangaa na wakati akiendelea kuwa katika hali yake ya mshangao Yoshida , Abuu na vijana wake wakatoka upande waliokuwa wamesimama na Tikayeshi na kusimama upande wa Tikayi na jambo hilo likawashangaza Dorisi na Tikayeshi lakini Roma akatabasamu.
"Hahaha.. brazaaa.. umejiona sasa ulivyokuwa mjinga , siku zote nimekuwa wakukuambia kuwa hauwezi kunishinda kiakili , angalia sasa ulivyoanguka kwenye mtego wangu .. hahahaha"
Tikayi alicheka kifedhuli na hapa hakuonekana mpole kama baba yake alivyokuwa akimtambua bali alionekana kama muuaji na mtu mwenye roho mbaya sana .
"Yoshida wewe sio wa kunisaliti mimi , Abuu hapana .. hii haiwezekani "
Aliongea Tikayeshi huku akionekana kuchanganyikiwa , alijikuta akiwa peke yake wale ambao alikuwa akiwaamini kama wako upande mmoja walikuwa wamemgeuka ,tena wamemgeuka kwenye wakati ambao alikuwa akiwahitaji sana , alijiona kama mtoto alieachwa katikati ya msitu mnene peke yake ,Bwana Tikayeshi chozi lilimtoka.
"Usijali sana broo .. leo nitakuondoa duniani ili kumpunguzia baba kichwa kuuma mara kwa mara ,maana siku zote umekuwa mzigo kwake"
"Hapana Tikayi naomba usiniue .. tafadhari mdogo wangu naomba usiniue .. nimekosa kuanzia sasa nitaendelea kuwa mjinga naomba usiniue"Aliongea Tikayi akiwa amepiga magoti na kupasha viganja vyake baada ya kuona hali ya hewa imebadilika na chaguo pekee ambalo aliona kwa muda huo ni kupiga magoti na kuomba kusamehewa , ungemuona usingedhania ni yule aliekuwa akiongea kwa kujigamba dakika chache zilizopita , Tikayi alionekana kumzidi mbinu na akili.
"Broo pole sana kwa kuzaliwa mjinga , unawaona hawa wote walikuwa wangu kabla ya kuja kwako na nilichokifanya nikuwapa maneno ambayo yatakurubuni na hata huu mpango niliupanga mwenyewe na nikamtumia Yoshida akuambie huu mpango na ulivyokuwa mjinga ukaufuata alichokuwa anakuambia ,huo ndio ujinga wako na usinilaumu mimi kwa kukuua ,familia yetu haiwezi kuwa na mjinga kama wewe"
Baada ya kuongea hivyo, Tikayi bila ya kumsikiliza kaka yake aliekuwa akiomba msamaha kwa kumkosea, wala kumhurumia alivuta upanga uliokuwa kwenye kiuno cha Yoshida na kisha akamsogelea kaka yake huku akiwa na macho yaliojaa roho ya kinyama na akamfyeka kaka yake kwenye shingo na damu pekee ndio zilizosambaa kwa kuruka na kutapakaa mahali hapa na kila mmoja alishangazwa na roho ya kikatili ya Tikayi.
"PAAA...PAAA ... PAPAPA .."
Roma alinyanyuka kutoka alipoketi na kuanza kupiga makofi huku akisogelea upande waliokuwa wamesimama Tikayi , Abuu na Yoshida na Tikayi aligeuza shingo na kumwangalia huku akionekana hakuwa na hatia hata kidogo ya kumuua kaka yake kifo cha kikatili .
Dorisi alijikuta akijuta kuja na Roma ndani ya hili eneo kwani alikuwa akitetemeka mno , kwa mara yake ya kwanza alikuwa akishuhudia laivu mtu akikatwa kichwa kikatili kwa namna hio , kwake alijiambia tukio hilo ndio la kwanza na ambalo halitakuja kufutuka katika akili yake ,alishindwa hata kuendelea kuangalia maiti ya Tikayeshi na kugeuzia shingo yake pembeni .
"Nishamalizana na Tikayeshi na sasa nimalizane na nyie wawili ,licha ya kwamba sikutaka yafikie hapa yalipofikia lakini sina budi , kutokana na umbea wenu wa kufatilia mambo yasio wahusu leo mmeweza kushudia jambo ambalo hakumpaswa kushuhudia na hio ni tiketi yenu ya kunifanya nisiwaache hai , mngebaki kule Twillght Villa kesho tungesaini mkataba na kumalizana"
“Hongera bwana Tikayi kwa kumuua ndugu yako , sio watu wote wanaweza kufanya hivi”Aliongea Roma na kama kawaida yake hakuwa akitishika na meneno ya Tikati , alifika aliposimama na kisha akampita na kuchuchutama huku akiangalia maiti ya Tikayeshi , aliingiza kidole sehemu ambayo panga lilipita na kama kawaida yake alitoa kidole na kukipeleka puani na kumfanya Abuu na wengine kushangazwa na ujasiri wa Roma.
Baada ua Roma kufanya kitendo chake kiilichowashangaza hawa watu , alinyanyuka na kumuangalia Tikayi lakini ghafla tu Yoshida aliekuwa mita kadhaa kutoka aliposimama Tikayi kwa spidi ya hali ya juu alikuwa ashafika aliposimama Roma na kumzibia Tikayi kwa mbele , huku bwana huyu akionekana kuwa tayari kimapigano.
****
Ni ndani ya mji wa kigamboni saa tatu kamili za usiku Edna leo hii alionekana kusimama nje ya Balconi akiwa ni kisweta chake cha Rangi nyekudu pamoja na pensi huku mkononi akiwa ameshikilia glasi ya kinywaji cha Wine.
Wakati Edna akifurahia upepo wa baharini , upande wa nje ya ukuta ilisimama gari aina ya Noah mita kadhaa kutoka lilipokuwa geti la Nyumba hii anayoishi mrembo Edna , baada ya gari hio kusimama , walishuka watu wanne waliokuwa wamevalia kofia nyeusi aina ya boshori ambazo zilikuwa zimewaziba uso mzima na kubakiza uso tu , watu hawa wanne pia walikuwa na siraha kwenye mikono yao.
Mmoja ya wale watu aliwapa ishara kwa kuwaonyeshea ishara ya Vidole viwili na kuonyesha upande wa kushoto , akimaanisha kuwa wawili wazunguke nyuma ya ukuta upande wa kushoto , eneo hili lilikuwa limetulia kama ilivyokuwa kawaida ya utulivu wa hili eneo , basi mabwana hawa walionekana kutumia nafasi hio vyema.
Wawili waliobaki wakazunguka upande wa kulia mita chache kutoka lilipokuwa geti na kisha walirusha kifaa flani ambacho hakikuonekana vizuri mfano wa chuma kinene na kutua kwenye nyaya za juu za ukuta na kuning`inia na baada ya kufanya hivyo jamaa alimpa ishara mwenzake na wote kwa pamoja wakaruka juu na kutua kwa ndani bila ya kupigisha kelele ya aina yoyote ile na walionekana kuwa wataalamu.
Edna wakati akiendelea kuangalia mandhari ya usiku ya bahari , alijikuta akigeuza shingo na kuangalia upande wa getini na hapo ndipo alipoona watu wakiruka ukuta na moyo wake kupiga paa.
Wakati akiendelea kuwa katika hali yake ya mshangao , majambazi yale yaliinama kwa ustadi mkubwa na kunyata kuelekea upande ilipokuwa nyumba ya walinzi na kwa eneo ambalo Edna alikuwa amesimama , alikuwa akiona vyema kilichokuwa kikiendelea licha ya kwamba taa za eneo la getini zilikuwa zikitoa mwanga hafifu, walinzi waliokuwa eneo la getini ni kama walikuwa wamezubaa kwani ile wanataka kufanya shambulizi walikuwa washafikiwa kitaalamu kabisa na kugongwa shingoni na kulazwa chini na yote hayo yalikuwa yamefanyika kwa wakati mmoja kati ya mabwana wale wawili waliozunguka upande wa kulia na wale waliokuwa wamezunguka upande wa kushoto na wote wakawa wamekutana getini na walikuwa washakamilisha kuwaweka chini walinzi wote wanne waliokuwa wakilinda nyumba ya Edna.
Upande wa Edna ni kama sasa akili yake imerudi na kuanza kufanya kazi kwani alijikuka akijisema.
“Majambazi!!!”Aliongea Edna kwa mshituko.
Comments