Reader Settings

Edna ile anataka kugeuka  kukimbilia ndani kufuata simu  ili apigie polisi mara  muda huohuo, bila ya kueleweka imetokeaje , waliingia  wazungu  wawili  mmoja mwanamke na mmoja  mwanaume walitokea hewani   na wakatua  kitaalamu kabisa  ndani ya eneo hili la ndani , wale majambazi yaliokuwa yamevalia  maski  yaligeuka na kushangaa uwepo wa watu waliongia ghafla na  kujiandaa kwa mapigano , lakini  mabwana hawa walionekana kukosa spidi , kwani ile wananyanyua bastora zao zilizokuwa mikonni walifikiwa kwa spidi ya hali ya  juu kabisa na siraha zile zikaenda pembeni na haikuishia hapo tu, walipigwa kitaalamu tumboni na shingoni kwa mapigo ambayo  hayakueleweka ni Karate au ni Kungfu kwani walijikuta wote wakiona nyotanyota na kudondoka chini.

Kwa namna walivyodhibitiwa na wazungu hawa ilikuwa ni ya kushngaza kwani spidi iliotumika haikuwa ya kawaida kabisa  maana wazungu walikuwa ni wawili lakini wao walikuwa ni wanne na licha ya wingi wao walidhibitiwa  ndani ya sekunde mbili tu.

Baada ya  wazungu wale kuona  wamefanikiwa kuwadhibiti  majambazi walibeba wale majambazi  mmoja mmoja na  kufunfua geti na kutoka nayo nje  na hali ikawa imetulia kama kawaida kama hakuna kilichokuwa kimetokea Zaidi ya Derick na walinzi wenzake kuwa katika hali ya kuzimia.

Lakini sasa wakati yote hayo yanatendeka Edna aliekuwa juu ya Balconi aliweza kushuhudia kila kitu  , kilichokuwa kimetokea  , hakuelewa ni nini kilichokuwa kikiendelea kwa wakati mmoja , alichokifanya ni  kukimbilia ndani  na kuchukua simu yake na kupigia polisi.

Na wakati huo huo akashuka mpaka sebuleni na kumkuta Bi Wema ambaye hakujua hata  nini kilitokea getini kwani alionekana kunogewa na tamthilia ya kimexico ilikuwa ikonyeshwa ITV.

“Miss kuna nini?”Aliuliza baada ya kumuona Edna anashuka mbio mbio.

“Bi Wema kuna majambazi yameingia ila nimeshindwa kuelewa kilichotokea”

“Yako wapi hayo majambazi?” Aliongea kwa kupaniki lakini Edna alishindwa kuongea , woga ulikuwa umemvaa na muda huo huo  gari ya polisi iliingia , na ilikuwa imewahi kweli kuliko ilivyokuwa mategemeo ya Edna, baada ya Edna kuona polisi wamefika alijikuta akivuta pumzi ya ahueni.

“Nini kimetokea hapa?”Aliuliza afande aliejitambulisha kama Koplo Juma  aliekuwa ameambatana na polisi wenzake watano na Edna alielezea kilichotokea na polisi hawa walishangaa  lakini pia waliweza kuamini kwani Derick na wenzake bado  walikuwa ndio wanaanza kurejewa na  fahamu baada ya kupulizwa na maji ya ubaridi huku wakionekana kuwa na  maumivu shingoni.

Kitendo cha Edna kumaliza kuongea  namna ya tukio lenyewe lilivyotokea Bi Wema alipata kujua  sasa tukio zima na  akili yake ikasimama kwenye neno ‘Mzungu’.

Polisi wale baada ya kuona  hawakuwa na cha ziada  hapo ndani na  hakuta uharibifu wowote uliotokea waliaga na kuondoka huku wakiahidi wataendelea kulifanyia kazi swala hilo na  kuwatoa hofu.

“Itakuwa ni walinzi  wa Roma”Aliongea Bi wema na kumfanya Edna kushangaa.

“Walinzi gani Bi wema Roma kaleta?”

“Jana wakati anaenda kazini aliniambia  kama kuna wazungu watakuja hapa niwaruhusu kufanya mambo yao  kwani ni maswala ya kiulinzi na akaniambia hakuna haja ya kukuambia lakini nilisahau na pia hawakutokea kama alivyosema”

Aliongea bi wema na  kumfanya Edna ashangae Zaidi na kutoka  tena nje na kumfuata Derick na kumuuliza kama Roma jana aliacha maagizo yoyote kuhusu  kuja kwa wazungu na Derick alisema ndio alitoa maagizo hayo  na hapo ndipo sasa akili ya Edna  ilianza kufunguka na alijua  sasa wale waliowadhibiti majambazi  huenda ni Wazungu  ambao Roma alileta , lakini swali likabaki kwenye kichwa chake , Roma kawezaje kuleta wazungu.

****

Yoshida alionekana kuwa tayari kupigana na Roma na alichokuwa akisikiliza ni oda ya bosi wake tu , lakini licha ya kuonesha kutaka kupigana kwa Roma hakuonesha mabadilio yoyote na aliishia kutabasamu baada ya kuangalia mwili wa kimazoezi wa Yoshida.

Tikayi hakuwa na wasiwasi na Roma kabisa ,alijua kabisa ataweza kumdhibiti  na ndio maana  alimpa ishara  Abu waondoke na kazi wataimaliza vijana wake.

“Nani kasema mnaweza kuondok?a”Aliongea Roma kwa sauti na kumfanya Tikayi  pamoja na Abu wasimame huku Tikayi hakuwa hata na wasiwasi  lakini kwa Abu alionekana kuwa na wasiwasi , licha ya kwamba  alishawahi kukutana na mziki w a Roma lakini hakuwa akijua uwezo wake halisi.

“Unaonekana kujiamini sana Bwana Roma , lakini ni bahati mbaya   kwamba leo hauwezi kutoka mahali hapa pamoja na huyu mwanamke , mmeona mambo ambayo hamkupaswa kuona”

Aliongea Tikayi na ile anamaliza kuongea  haikueleweka  Roma alimpita vipi Yoshida , kwani tayari alikuwa mbele  ya Tikayi , lakini tofauti ni kwamba leo hii macho yake yalikuwa kawaida tu.

“Umekosea sana  kutujumlisha kwenye mpango wako , kwanza kabisa nikwambie tu  nilikuwa nishafahamu  kuna drama iliokuwa ikiendlea kati yako  na kaka yako , lakini jambo lililoniuzi ni kuagiza watu waje kutudhuru”

Aliongea Roma huku akiwa siriasi na Tikayi alishangazwa utambuzi wa Roma mapema , lakini muda huo huo kabla hajaongea chochote Yoshida huyu hapa  na panga lake linalowakawaka  likiwa hewani  kama vile kwenye muvi za wakorea akiwa na dhamira  ya kumdhuru.

“Romaa.. angalia”

Ilikuwa ni sauti ya Doris akiongea kwa kupaniki baada ya kuona Yoshida anataka  kumfyeka Roma na panga lake , lakini  ile  panga linamkaribia Roma karibu na Tumbo alilishika kwa mkono wa kulia bila ya kujali kama ameshika upande ambao ulikuwa na makali na kisha akalipindisha kwa nguvu kwa spidi ya hali ya juu na palepale  panga  likakatika  vipande viwiwili na kumfanya Yoshida ashangae huku damu zikiwa zinatoka kwenye mikono ya Roma  , lakini pia Yoshida  hakuwa mzembe  kwa kutumia kipande  kilichobaki kwa spidi kabisa alizungusha    na kupeleka  usawa wa  shingo ya  Roma huku akiwa hewani  na ile anafikisha sentimita kama kumi na tano kutoka kwenye shingo ya Roma alijikuta kile kipande kingine kikizama  kwenye koo lake  na kutokezea upande  mwingine , jambo ambalo lilimfanya Dorisi mwili kuwa wabaridi na huo ukawa mwisho  wa Yoshida.

Baada ya wale walinzi wengine waliokuwa wamesimama mita kadhaa  kutoka mlangoni  kuona Yoshida mkuu wao kashakufa  waliinua bastoa zao na kuanza kumlenga Roma na hapa ndipo kila mmoja alijikuta  akipatwa na kiwewe kwani Roma ni kama alikuwa akijua ni nani anavuta triga na kuachia  risasi  kwani alikwepa risasi nne kwa ustadi mkubwa sana kiasi kwamba  Tikayi  hakuamini.

“Nachukia sana bunduki”Aliongea  Roma kwa sauti nzito sana kama Roboti  huku akiwa ameinamisha uso wake chini na hio ni mara baada ya kukwepa risasi  ya tano , lakini sasa sauti yake ya awamu hii  haikuwa ya kawaida na kumfanya Dorisi atoe mshangao  na kumwangalia Roma , na haikuwa kwake tu hata Abu na wengine wote walikuwa kwenye mshangao.

Roma bado alikuwa ameinama chini  vilevile  huku mwili wake ukianza kutingishika kama mtu anaepandisha mashetani na hakuna aliekuwa akielewa Roma alikuwa akifanya nini na walianza  kushangaa Nguo alizovaa Roma zikianza kuloana huku mwili wake ukitoa mvuke mwingi kama sufuria iliokuwa ipo jikoni.

“Mnashangaa nini mpigeni Risasi”Aliongea Tikayi kwa kijapani huku akianza kupiga hatua kuelekea mlangoni  baada ya kuona  hapa ndani hapakaliki , lakini kitendo cha kufumba na kufumbua  Roma kama jini vile alipotea  na kuibukia mlangoni.

“Nani kasema unaweza kuondoka”

Ilikuwa ni sauti nzito sana  ambayo ilisababisha mwangwi  , yaani Roma aliongea mara moja lakini sauti ilisikika mara mbili katika masikio ya watu wote waliokuwa hapa ndani ,Tikayi ile anainua macho na kumwangalia Roma  alijikuta akidondosha begi    la hela alilokuwa ameshikilia na hakuelewa mkojo ulitokea wapi  kwani alihisi  majimaji ya  moto yakishuka kwenye mapaja yake na hio ni mara baada ya kushuhudia  macho ya Roma yaliokuwa ya kijani huku yakiwa na michirizi ya damu iliokuwa ikionekana  kabisa na sio kwa  Roma , kila mtu alianza kutetemeka huku mwili wa Roma ukiendelea kutoa mvuke ambao ulisababisha aina flani hivi ya Harufu kama nailoni inachomwa jikoni kwenye moto.

“Paaa.. paaa , khaaa...”

Ilikuwa ni milio  ya risasi zilizokuwa zikirushwa kuelekea alipokuwa amesimama   Roma , lakini ni kama walikuwa wakipiga hewa kwani hakukuwa na risasi hata moja iliompata Roma zikaishia kwenye mlango  na ni kama walikuwa wamepandisha mashetani ya Roma kwani palepale  ni kama muvi iliokuwa ikipelekwa mbele Roma alionekana akiwaadhibu wale walinzi kwa spidi sana huku akiwavunja shingo na alitumia sekunde  therathini  tu walinzi wote walikuwa  wapo chini wakiwa hawana uhai.

Dorisi hakuwa akiamini kama mtu aliekuwa mbele yake  ni Roma aliekuwa akimjua ,  mwanaume ambaye alimsababishia hata  kudiriki kufanya nae mapenzi ndani ya ofisi , alionekana hakuwa ni mwenye kuamini kile alichokuwa akikiona mbele yake  na haikuwa kwake tu Abu na Tikayi walikuwa wamebaki na Bumbuwazi huku  suruali zao zikiwa zimeloa kwa mbele  walikuwa kwenye woga usiokuwa na kifani na kuzidiwa hat ana Dorisi ambaye   hakuonesha woga mwingi ila alikuwa na wasiwasi huku machozi yakiwa yanatiririka kwenye mboni za macho yake.

Roma aligeuka kama Roboti  baada ya kumaliza  kudili na walinzi na sasa  alisogea taratibu kumuendea Tikayi , Roma alikuwa akipiga hatua moja mbele na Tikayi alikuwa akipiga hatua mbili kinyume nyume  na ile Roma  anaongeza hatua Tikayi aligeuka na kuanza kukimbia , lakini sasa ni kama alikuwa amesahau mlango kwani kule alikokimbia ndio ukuta ulipokuwepo na kufika ukingoni.

Kwa upande wa  Abu ni kama alipata upenyo kwani  alichomoka kama  mshale kuelekea nje na Roma aligeuka na kumwangalia akitokomea lakini hakuwa na habari nae.

“Romaaa…!!”Ni sauti ya Dorisi iliojirudia rudia kama mwangwi kwenye masikio ya Roma na kumfanya ageuke na Dorisi alimwangalia kwa woga na kutingisha kichwa akimuoneshea ishara ya kwamba asifanye anachotaka kufanya na Roma aliongekana kumuelewa na hapohapo mwili wake ulipoa ghafla na mvuke kukauka  lakini kiini cha macho yake kilikuwa hakijabadilika.

Roma alimwangalia  Tikayi   aliekuwa amedondoka chini akitetemeka miguu   kwa woga.

“Naomba unisamehe?”

“Ulifikiri ni rahisi hivyo mimi kusamehe”.

“Hapana naomba unisamehe , nitafanya chochote unachotaka”Aliongea kwa pupa huku akipiga magoti kama ilivyokuwa kwa kaka yake.

Roma sasa alionekana kurejewa na fahamu zake za kawainda ,kwani licha ya kwamba rangi ya macho yake ilionekana kuwa ya kijani bado ,  lakini ilikuwa imefubaa.

“Siwezi kukusamehe kirahisi hivyo , napaswa kukuua hapahapa kwa kuvuka mipaka , sipendi kutishiwa kwenye  Maisha yangu

Previoua Next