Reader Settings

Tikayi  kwenye Maisha yake hakuwahi kuwaza kama anaweza kukutana na mtu anaebadilika  kama ilivyokuwa kwa Roma , alijiambia katika akili yake  kwamba katika siku zote alikuwa amefanya makosa na kumgusa mtu ambae hakupaswa kuguswa basi ni bwana aliekuwa mbele yake, aliamini ana asilimia ndogo  sana za kutoka hapo ndani akiwa  salama , akili yake ilikuwa ikifanya kazi kama mashine , alimwangalia  Roma ambaye awamu hii alikuwa anaonekana kawaida  na nikama alikuwa haamini  kama mtu aliekuwa mbele yake dakika kadhaa zilizopita alikuwa   kiumbe cha kutisha  kilichojaa ukatili.

“Utachukua  asilimia sitini za faida ndani ya mkataba wa kibiashara tutakaofanya”Aliropoka Tikayi  na kumfanya Dorisi ashangae , kwani katika mkataba huo wa kibiashara walikuwa wakichukua asilimia  therathini tu na JR asilimia ishirini  huku Yamakuza wakichukua asilimia  hamsini, hivyo Dorisi kusikia hivyo moyo waka ulipiga kite na kuona dili hilo litakuwa nono kama tu wangelikubali

“Unadhani ninaweza kukuacha hai kwa asilimia sitini?”Aliongea Roma kwa sauti ya kawaida  na Tikayi akamwangalia  Roma kwa wasiwasi.

“Asilimia  hizo ni nyingi sana ndani ya kampuni yenu kutokana na uthamani wa Material”

“Umefanya makosa mangapi , isije ukawa unapendekeza  asilimia sitini lakini hata makosa yako huyajui”

Tikayi alinyanyuka na kupiga magoti , huku akianza kufikiria ni  makosa mangapi alikuwa amefanya na kisha akamwangalia Dorisi aliekuwa akimwangalia kwa wasiwasi na Tikayi ni kama alikuwa akitaka kuomba msaada kwa Dorisi.

“Nimefanya makosa matatu”

“Yataje niyasikie”

“Kwanza kabisa  nilipanga kuwaua wewe na Dorisi  kule nyumbani , pili  nikataka kukuaa hapa ndani ,tatu….”Alianza kujikuna kichwa akifikiria ni kosa gani tena ambalo alikuwa amelifanya , lakini hakuelewa alikumbuka katika makosa yote alitaka tu kumuua  Roma.

“Umenikosea halafu  hukumbuki makosa yako , sasa nasema hivi mimi Roma Ramoni siwezi kukuacha hai leo na nakupa dakika  moja tu unishawishi nisikuue na kama unajiona huwezi kunishawishi niambie niivunje shingo mapema tu nisipoteze muda wangu, mimi kuua kwangu ni jambo jepesi sana”

Aliongea Roma huku akionekana kuwa  siriasi na Tikayi  alijikuta akikumbuka macho ya Roma dakika kadhaa zilizopita na mwili wake ukahisi ubaridi wa hali ya juu sana wa woga.

Dorisi alishindwa kuongea chochote , alitamani kumwambia  Roma wakubaliane na asilimia Sitini alizotaja Tikayi  lakini alishindwa kuongea , hakuelewa  kwasababu gani, lakini alikosa hali ya kujiamini kuongea na Roma.

“Bado Sekunde kumi”aliongea Roma  huku akiendelea kumuangalia na Tikai  hakujua ni namna gani anaweza kumshawishi Roma asimue.

“Tatuuu ….mbiliii ….”

“Kosa lingine tulitaka kuwasainisha mkataba feki”Aliongea Tikayi kwa kukurupuka  na kumfanya Roma atabasamu na Dorisi macho yalimtoka , hakuelewa alichozungumza  Tikayi kina ukweli ndani  yake.

“Wewe na nani mlitaka kutusainisha mkataba feki, nataka maelezo yalionyooka  la sivyo nitakunyonga hapahapa na Japani yote hii hakuna atakae kuwa na uwezo wa kunigusa”Roma alionyesha hasira zake waziwazi na kumfanya Tikayi kuanza kuogopa.

“Black Mamba kupitia muwakilishi wao  Abubakar”Dorisi alizidi kushangaa na  hakuelewa Black Mamba ni mtu gani  , lakini kwa Roma alikuwa ashasikia sana hili kundi  na pia alikumnbuka  Karimu  ndio aliekuwa kiongozi wa kundi hilo na baada ya kusikia maneno haya kutoka kwa Tikayi alijua Black Mamba walikuwa wakitafuta namna ya kulipiza kisasi kupitia kampuni ya mke wake , alijikuta akikasirika na kujilaumu kwanini alimuachia Abu akimbiena hakumua , lakini alijiambia katika nafsi yake atamkamata tu na kifo kitamuhusu.

“Kwa hio unamaanisha swala lote la Mkataba kati ya Yamakuza na kampuni yetu , yote yalikuwa ni uongo na hakukupaswa kuwa na mazungumzo ya aina yoyote yale  ya kibiashara baina yetu?”Aliuliza Dorisi  na hio ni baada ya Roma kumueleza  kinachoendelea  kwa kutafsiri maneno ya Tikayi.

“Kuhusu Material Mapya ni biashara ya kweli , lakini  kuhusu material hayo kusambazwa na kampuni ya Vexto hakuna kitu kama hiko, kampuni ambazo  tulichagua kufanya nayo kazi kwa Tanzania  ni Maple Group na  JR Group na mkataba halisi ulipangwa kusainiwa  siku  tatu mbele baada ya kusaini na nyie mkataba feki a kuhakikisha mmetupa kiasi cha pesa ambacho kipo kwenye mkataba”

Aliongea Tikayi na kumfanya Dorisi kushangaa mno  , lakini sio kushangaa tu aliogopa kwa wakati mmoja  , kwani kama  angesaini huo mkataba na kisha wakaruhusu kiasi kikubwa cha pesa kikatoka kwenye kampuni na baada ya hapo wakagundua kuwa mkataba ulikuwa ni feki huenda Vexto Grupu ingefilisika  rasmi,Dorisi alimwangalia Roma na kuzidi kushangaa na aliamini hata kama angekuja Edna mwenyewe Japani huenda asingegundua jambo hilo.

“Sasa Bwana Tikayi nyie na hawa Black Mamba mna uhusiano gani  na kwanini mkubaliane nao kwa ajili ya kusaini mkataba  feki na  kampuni yetu , ilihali  swala hili huenda lingewaletea matatizo mbeleni?”

Tikayi alifikiria kidogo na kisha  akakaa chini kabisa kwani alionekana kuchoka kwa kutumia magoti na hakujali uchafu uliokuwa chini na kisha akamwangalia Roma kwa wasiwasi ,Tikayi hakuwa na namna , aliona   bila ya kusema ukweli  asingeweza kutoka kwenye mikono ya Roma.

“Black Mamba ndio wasambazaji wakubwa wa madawa yetu ya kulevya  kwa Afrika Mashariki yote kwa Zaidi ya miaka kumi , lakini miaka mitatu nyuma kulitokea  tatizo  baada ya raisi mpya kuchukua madaraka”

“Tatizo gani?”

“Njia ambayo tulikuwa tukitumia kuingiza madawa ya kulevya  ndani ya Tanzania  Raisi Senga aliigundua na kuizuia , lakini pia sharia zake mpya na ukaguzi mkali bandarini  na njia zote za   usafirishaji tulishindwa kupata Njia salama ya kupitisha madawa na kwa Afrika mashariki soko kubwa la madawa lipo Tanzania  , hivyo uongozi wa senga ulifanya  mapato ya biashara kushuka kwa kiasi kikubwa  san ana hapo ndipo tulipokuja na wazo la kutengeneza njia mbdala ya kuingiza madawa Tanzania”.

“Hio njia yenu inahusiana vipi na kampuni ya Vexto?”

“Vexto ndio kampuni pekee ambayo imepewa mkataba wa kudumu wa kuingiza mafuta ya petroli   Tanzania kutoka India  na huo mkataba unaifanya Vexto  kuwa na nguvu  ndani ya taifa  la Tanzania”Aliongea Tikayi na kumfanya  Roma ashangae kwani hilo hakuwa akilifahamu na alimgeukia Dorisi  na Dorisi alitingisha kichwa kuashiria ni kweli.

“Saa kama ndio wanamkataba wa kudumu wa kuingiza Mafuta inahusiana vipi na madawa yenu ya kulevya?”

“Njia salama  ya  kusafirisha madawa ya kulevya  duniani kwasasa  ni kwa njia  ya Shehena ya Mafuta”Dorisi alishangaa  lakini Roma hakushangaa.

“Kwa hio mlitaka muitumie Vexto kuingiza madawa Tanzania kupitia shehena ya  Mafuta wanayoingiza?”Alitingisha kichwa kuashiria ni kweli.

“Black Mamba  mkuu wake ndani ya Tanzania ni nani?”

“Mkuu wa Black Mamba Tanzania simfahamu  ila ninachojua ni kwamba anafahamika kwa  jina la The Doni , ila muwakilishi wake mkuu ambaye mara nyingi ndie anaemuakilisha katika mazungumzo ya kibiashara ni Abubakari Juma”

Roma alijikuta akishangaa na kuwaza huyu The Doni ni nani , kwanini kila mtu hakuwa akimjua na ana nguvu gani ndani ya taifa la Tanzania  , ila alijiambia atayajua yote hayo taratibu huku akijipiza moyonni akimpata lazima amvunje shingo.

“Baada ya kutusainisha mkataba feki ni kipi kingefuara baada ya hapo?”

“Mpango uliokuwepo ni kwamba  kama mkataba huo ungesainiwa  na ikajulikana kwamba ni feki ,Edna angekosa  vigezo vya kuwa CEO , lakini wakati huo huo  kampuni ingefirisika na JR Group ingeinunua kampuni  ya Vexto  na JR ni sehemu ya Black Mamba na mpango ungekuwa umefanikiwa kirahisi”

Dorisi alijikuta  akivuta pumzi , hakuwa akijua kuwa kampuni ya Vexto ilikuwa ikikodolewa macho kwa namna hio  na wafanya biashara wa madawa ya kulevya , sasa alianza kuhisi ile michakato yote ya Abu kutaka kumuoa Edna ni kwasababu  ya hilo swala la uingizaji wa Madawa nchini , hakika alishangaa na kuona siku hio amejua mengi lakini pia alishukuru moyoni  kwamba swala hilo la kusaini mkataba feki halikuwa  limefanikiwa, maana kila alipokuwa akikumbuka  nguvu  na juhudi za Rafiki yake Edna  kuifikisha Vexto ilipofikia  aliogopa na aliona huenda Edna angechukua maamuzi magumu hata ya kujinyonga.

“Mpaka hapo   bwana Tikayi umenishawishi japo bado kidogo sana , nadhani mpaka sasa unafahamu kuwa mimi na Dorisi ndio tunajua kuwa wewe ndio umemuaa Tikayeshi ndugu yako , lakini pia mpaka sasa unajua fika kwamba  ulitaka  kutuua , lakini pia mlitaka kutusainisha  mkataba feki , Sasa wewe mwenyewe hebu kaa chini tena fikiria  unadhani utanipatia kitu gani cha thamani  nikusamehe?”Aliongea Roma na kumfanya Tikayi afikirie,

“Kwakua biashara ya Material mapya ni halali nitaiota JR Group  kwenye mkataba na kuiingiza Vexto , lakini katika mkataba huu Vexto mtapata asilimia  sitinni na Tano ya faida yote ya mauzo kwa bara la Afrika nadhani hilo sio dili  baya kwa kampuni ya Vexto”

Dorisi macho yalimtoka , alitamani aseme ndio hapo hapo lakini alikumbuka  dakika chache nyuma kuwa kama sio Roma wangesainishwa mkataba  feki bila wao kujua. Akaona atulie na Roma amalize kila kitu.

Basi Roma alikubaliana na Tikayi  kwa kusainishana mkataba mpya kati ya Maple Group na  Vexto Group huku kampuni ya JR ikitolewa  kwenye mkataba huo.

Roma kama kawaida yake alimpiga mkwara wa kutosha Tikayi kwa kumtishia kama tu angefanya ujinga mwingine wa kufanya janjajanja ya kumzunguka , basi angeimaliza familia nzima ya Yamamoto na kuchukua na kampuni yao na Tikayi kutokana na mziki wa Roma aliokuwa ameushuhudia kwa  macho yake , alijikuta akiapia kwa majina yote  hatokuja kumuuzi Roma tena na atafanya kama  ambavyo wamekubaliana.

Siku iliofuata Roma na Dorisi hawakulala  ndani ya Twillight villa  kutokana na mambo yaliotokea kati ya  Tikayi na Roma , lakini pia familia hio ilikuwa kwenye maombolezo ya msiba wa Tikayeshi ambaye alikuwa ameuliwa na mdogo wake Tikayeshi na kuhusu Tikayi kumuua kaka yake lilimalizwa kifamilia na hakukuwa na taarifa yoyote iliotolewa Zaidi ya kutangaza kuwa  ni ajali ambayo ilitokea  na kumuua Tikayeshi.

Dorisi aliwasiliana na Edna na kumpa  taarifa ya  kile kilichokuwa kimetokea na Edna alifurahishwa sana na taarifa hio huku akiahidi zawadi kwa wawili hao watakaporudi  nchini.

Mkataba ulikuwa ukisainiwa siku mbili mbele lakini kabla ya kusainishana mkataba huo viongozi wa Maple Group walitakiwa kufika nchini  Japani kwa ajili ya mazungumzo hayo ya kibiashara lakini pia kukagua miundo mbinu ya  kiwanda ambacho kitakuwa kikitumika kutengenezea material hayo mapya.

Ni saa Moja za jioni ndani ya uwanja wa Kansai  Tikayi alikuwa eneo la mapokezi la kufikia wageni akimsubiria mgeni  atakaeiwakilisha Maple Group katika kusainishana mkataba mpya.

Baada ya kusubiria kwa takribani nusu saa akiwa na walinzi wake , hatimae  eneo la kutokea wageni alionekana  mwanamke mrembo akiwa anatoka  huku akiwa amependeza sana , mwanamke huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni Naibu waziri wa Sanaa , mheshimiwa Neema Luwazo.

Previoua Next