Neema Luwazo waziri wa Sanaa kutoka Tanzania alionekana kufurahia ukaribisho kutoka kwa Tikayi kwani muda wote alionekana kuwa na uso uliokuwa umepambwa na tabasamu.
“Licha ya kwamba swala hili la kibiashara lilikuwa ghafla kwangu baada ya kuvuta tarehe nyuma , lakini nafurahi sana kufanya kazi na kampuni yenu”Aliongea Neema baada ya kuingia kwenye gari ile ile iliowapokea Dorisi na Roma Caddillac Limuosine
“Hata sisi pia kama kampuni tunafuraha kubwa sana kufanya kazi na Maple grupu , karibu tena Japani kwa mara nyingine”
“Nashurkuru sana , sio mara yangu ya kwanza kufika Japani lakini ni mara yangu ya kwanza kufika hapa Osaka , unaonekana kuwa mji mzuri sana , nimezoea kufika Tokyo mara kwa mara katika safari zangu zote za kibiashara”
“Ndio Osaka ni mji mzuri sana na una utulivu wa hali ya juu”Alijibu Tikayi kwa kingereza safi na safari iliishia katikati ya mji huu kwenye hoteli iliokuwa ikifahamika kwa jina la W Osaka Luxury one ni moja ya hoteli nzuri sana na ya bei ghali ndani ya jiji hili la Osaka usiku mmoja tu ni milioni nne za kitanzania.
“Wow! Its so amaizing hereTikayi”Aliongea Neema huku akifurahishwa na mandhari mazuri yaliokuwa ndani ya hili eneo na alishindwa kuzuia furaha yake na Tikayi alitabasamu na kumuongoza ndani.
Ni Siku nyingine ndani ya makao makuu ya kampuni ya Yamakuza kwenye ukumbi mkubwa wa mikutano , walionekana viongozi wa juu kabisa wa kampuni wakiwa wameizunguka meza , lakini pia kwenye meza hio alionekana mwanadada Neema luwazo alievalia vazi lake la suti akiwa ameketi kwenye nafasi yake , huku pembeni yake kukiwa na viti viwili ambavyo vilikuwa wazi ni kama watu ambao walitarajiwa kukaa kwenye viti hivyo ni kama walichelewa , kwani watu wote walikuwa washawasili akiwemo Tikayi ambaye siku hio ndio alieonekana kuongoza mazungumzo yote yaliokuwa yakihusu mkataba wa biashara kati ya kampuni ya Yamakuza Corporationi`s na kampuni mbili kutoka Afrika yaani Maple group ambayo ilikuwa ikiwakilishwa na Neema ambaye ndie alikuwa mmiliki na mwenyekiti wa kampuni hio , lakini pia Dorisi na Roma ambao ndio walikuwa wawakilishi wa kampuni ya Vexto International.
Dakika chache mbele mlango wa chumba hiki cha mikutano ulifunguliwa na akaingia mrembo Dorisi akiwa ameambatana na Roma Ramoni , wawakilisi wa kampuni ya Vexto.
Kila mmoja macho yalikuwa kwa wawili hao na kwa jinsi walivyokuwa wamependeza ni kama vile walichelewa makusudi ili kujionyesha , viongozi hawa wajuu walikuwa wanawaangalia Dorisi na Roma kwa namna ya macho ya kitathimini , upande mwingine mwanamama Neema Luwazo jicho lilikuwa limemtoka mara baada ya kumuona mtu ambaye hakuwa amemtarajia kumuona , tena kwenye nchi ya mbali kama hii ya Japani.
“How This possible?”
Alijiwazia huku akiendelea kumuangalia Roma ambaye kama kawaida yake , alikuwa akijiamini mno kiasi kwamba hata watu walijiuliza ni ninni kinamfanya kujiamini kwa namna hio , kwani kwa Roma watu waliokuwa mbele yake ni kama alikuwa akiwafahamu wote.
Dorisi akiwa nyuma Roma alitangulia na kuelekea upande ambao ndio nafasi zao zilikuwa zimeandaliwa , wakati wote huu Roma hakuwa amemuona Neema bado mpaka pale alipofikia kiti ndipo alipomuona mwanamke ambaye kwa kumuangalia tu kumbukumbu zake zilimrudisha ndani ya taifa la Tanzania kwenye hoteli ya New Afrika akiwa amemkunja kisawasawa lakini sio kwa Roma tu aliemuona Neema hata pia kwa Dorisi alimtambua mara tu baada ya kumuona na alionyesha waziwazi kutofurahia uwepo wa mwanamama huyo hapa ndani.
“Mrembo ni wewe?”
Aliongea Roma mara baada ya kumfikia huku akivuta kiti kwa ajili ya kuketi , lakini Neema alishindwa kuongea chocote kwani muda wote alikuwa akimwangalia Roma kwa mshangao mpaka pale Tikayii alipoanza kuongea na kufungua kikao hiko.
Tikayi alionekana kujiamini sana , lakini kila alipokuwa akikutanisha macho na Roma alijikuta akikosa utulivu na hali hio Roma na Dorisi waliishuhudia na Roma alimkonyeza Tikayi na akatabasamu na kuendeleza kikao.
Baada ya utangulizi wa ajenda za kikao hiko kuhusu mkataba wa kibiashara juu ya uzalishaji wa material mapya ambayo kama kampuni walikuwa wakiamini yanakwenda kuweka historia kimauzo , ilifikia wakati ambao sasa watafiti wa kampuni ya Yamakuza ambao ndio waliokuwa wakihusika kwa asilimia miamoja na gunduzi ya material hayo , walitakiwa kutoa ‘representation’ kwa ufupi.
Na Tikayi alichukua nafasi hio kumkaribisha kiongozi wa juu wa utafiti kuingia ndani ya chumba hiko cha mkutanao kwa ajili ya jambo lililokusudiwa na baada ya kutoa ukaribisho mlango ulifunguliwa na akaingia kijana mmoja wa kijapani mrefu mwembaba aliekuwa na nywele ndefu lakini zilizokuwa na staili flani hivi kama wigi, alikuwa ni kijana wa makadirio ya umri kati ya miaka si chini ya ishirini na Tano ,bwana huyu alijitambulisha kwa jina la Mori Satoshi.
“Kabla sijaanza kutoa taarifa juu ya Project hii ambayo imenichukua miaka mingi kufanya utafiti na majaribio mpaka kuikamilisha naomba kwa heshima kubwa nimtambulishe mwalimu wangu ambaye alikuwa na mimi bega kwa bega katika masomo yangu ndani ya chuo kikuu cha Oxford Dr Clark Stephanie”
Aliongea Mori na hapohapo mlango ukafunguliwa na akaingia mwanadada ambaye alimfanya Roma atoe macho.
Alikuwa ni mwanamke mzungu mrembo sana wa kuvutia mno kwa muonekano wake , mwenye muonekano ambao ukiangalia utagundua kuwa alikuwa na umri mdogo sana na hii ilifanya watu wengi hapa ndani kushangazwa na mtu ambaye anaitwa Profesa n ani mwalimu wa Mori kuwa ndio huyo mwanamke.
Profesa Clark alijikuta macho yakimtoka mara baada ya kukutanisha macho na Roma ni kama mtu ambaye hakutegemea kumuona mtu huyo hapo ndani na mshangao wake ulifanya watu hapa ndani kuangalia upande ambao macho ya Profesa clark yalikuwa yameelekea na wote wakagundua kuwa Profesa alikuwa akimwangalia Roma na huku Roma baada ya kuona macho ya Profesa yanamwangalia aliinua mkono na kumpungia huku akiachia tabasamu pana usoni na hapa ndipo watu walizidi kushangaa ,sio Dorisi na Neema waliokuwa wamekaa karibu na Roma ,lakini pia Mori mwenyewe aliemleta profesa wake hapo ndani alikuwa kwenye mshangao na pia Tikayi alikuwa kwenye mshangao.
Baada ya hali hio ya mshituko kupita Profesa Clark alianza kuitambulisha.
“I am renowned Professor Clark Stephanie, it has been an honor for me to attend this session which involves the success of my student Mori in his research which has led to development of new materials,
Despite having a tight schedule, it's a pleasure for me to be able to listen to what Mori prepared, but I'm also happy to meet each of you”.
“Mimi ni Profesa maarufu ninaefahamika kwa jina la Profesa Clark Stephanie , ni heshima kwangu kupata nafasi ya kuwa moja ya wahudhuriaji wa kikao hiki ambacho kinahusisha taarifa ya mafanikio ya Utafiti wa mwanafunzi wangu Mori , ambao umepelekea kupatikana kwa Material mapya, licha ya kuwa na ratiba iliobanana ni furaha kwangu kusikiliza kile Mori alichoandaa na pia nimefurahi kukutana na kila mmoja hapa ndani”
Aliongea kwa kujiamini kabisa , huku akionyesha ile hali flani ya mtu kujiamini anapokuwa na mafanikio makubwa.
Kila mmoja alivutiwa na sauti ya mrembo huyu na kutamamani waendele kusikiliza.
“Huyu ndio Princess wa Wales ,Mtoto wa malkia Catherine Steohanie”
Walinong`onezana mabwana wawili kwa lugha ya kijapani wakati huo Profesa Clark akienda kukaa sehemu ambayo iliandaliwa,lakini mwanadada huyu mrembo macho yake yote yakiwa kwa Roma, ambaye alionekana kuanza kuchoka kukaa hapo ndani.
Ukweli utofauti kati ya Edna Clark likija swala la uzuri kama utawalinganisha Profesa Clark na Edna wameachana kidogo sana , na kitakachombeba Edna Zaidi ni umbo.
Basi kikao kiliendelea kwa takribani saa moja na nusu jambo ambalo kwa Roma ni kama hakuwa akielewa kile kinachoendelea na kujiamulia kulala zake kwa kujiinamisha kwenye kiti huku akibenua kichwa juu na kufanya koo lake lionekane na hata pale alipokuwa akimeza mate Neema na Dorisi waliokuwa wamekaa pembeni yake walikuwa wakiona misuli ikipishana.
Waandishi walikuwepo ndani ya jengo hili refu la kampunni ya Yamakuza na kila kilichokuwa kikiendelea kilikuwa kikinakiliwa kwa ajili ya matangazo na hio ni moja ya mbinu ya kufanya kampuni ambazo zipo katika mfumo wa ‘Trading’ Hisa zao kupanda.
****
Edna leo hii alikuwa ndani ya kampuni yake ndani ya ofisi yake huku macho yote yakiwa kwenye chati ya ‘Candlestick’ ya soko la hisa ambayo ilikuwa ikishuka na kupanda . Katika tarakishi yake alikuwa amegawanya sehemu mbili.
Sehemu ya kwanza kulikuwa na chati iliokuwa ikionesha graph ya kampuni ya JR Group na upande wa pili ilikuwa ikionesha chati ya kampuni yake.
Utofauti wa hizi graph ni kwamba kuna ambayo ilikuwa ikishuka na kuna ambayo ilikuwa ikipanda , graph ambayo ilikuwa na mstari wa kushuka ni ya kampuni ya JR na hii iliashiria hisa za kampuni hio zikishuka thamanni tena kwa spidi kubwa lakini upande mwingine hisa za kampuni ya Vexto zikipanda thamani kwa siku hio , hali zote mbili zilionekana kumfurahisha sana Edna na alichukua simu yake iliokuwa kwenye meza na kutafuta namba ilioandikwa kwa jina la ATHENA na kisha akapiga.
“I think with the ongoing situation you know what to do Amiri?”
“Yes! Madam”.
“Okay!, look at the Dow Jones Line for today when it get to the lowest point where we intended to, initiate the plan”.
“Angalia Mstari wa Dow jones kwa siku ya leo ukifikia point ambayo ndio tumekusudia , Anzisha mpango wetu”
“Rest Assured Madam , leave everything to us”
“Kaa kwa kutulia Madam , tuachie kila kitu sisi”
Sauti ya mwanaume ilisikika upande wa pili , mwanaume ambaye Edna alimtamka kwa jina la Amiri.
Baada ya Mrembo huyu ambaye alikuwa akionekana kiprofesheno Zaidi baada ya kuongea na simu yake aliendelea kukodolea macho tarakishi yake na kutabasamu lakini muda huo huo mlango ulifunguliwa na akaingia mrembo Nasra akiwa amependeza kama kawaida huku mkononi akiwa ameshikilia kishikwambi(Tablet).
“Boss Taarifa ya kampuni yetu kutoka japani ipo mtandaoni”
Aliongea Nasra huku akimpatia Tablet alioshika mkononi na Edna aliichukua na kuangalia picha mbalimbali zikimuonesha Roma na Dorisi wakipeana mikono na wafanyakazi wa kampuni ya Yamakuza.
Edna alishindwa kuzuia tabasamu lake mara baada ya kumuona mume wake kwenye picha hio huku moyo wake ukipata kajimsisimko flani hivi ambako mwenyewe ameshindwa kukatafsiri kwani kalisafiri kuwanzia kichwani na kwenda kuishia katikati ya mapaja.
“Boss nadhani huu ndio mkataba ambao kampuni imeufanikisha tokea kuanzishwa kwake , shukrani ziende kwa Roma na Dorisi walioweza kupata asilimia kubwa za gawio la Faida”Aliongea Nasra huku akimwangalia Edna.
“Hakika Nasra lakini haya yote ni juhudi za kila mfanyakazi wa Vexto nitahakikisha tunaendelea kusaini mikataba mikubwa zaidi na kuipanua hii kampuni duniani kote”.Nasra alitabasamu na kisha akasema:
“Nadhani muda si mrefu Forbes watakutoa kwenye nafasi yako ya mwanamke tajiri duniani uliopo na kukupandisha juu Zaidi , kutokana na mauzo ya hisa ya leo yanavyopanda,natamani Madam Rahel angekuwepo hai Edna”Aliongea Nasra huku machozi yakianza kutoka, machozi ya huzuni.
“Ni kweli Nasra , unaonekana kummiss sana Mama eti eh?”
“Huwezi amini Edna kwenye siku mbili hizi nilikuwa nikimuota kwenye ndoto , nammissi kila siku , wema wake alionitendea kwenye Maisha yangu umemfanya kuwa mtu muhimu sana kwenye Maisha yangu”
Edna alitabasamu na kutoka kwenye meza yake na kisha akamsogelea Nasra na kumkumbatia huku na yeye akitoa machozi na walionekana kufarijiana.
Upande mwingine hapa ndani ya jii la Dar kwa upande wa Masaki alionekana mzee Alex akiwa kwenye Runinga huku akiwa na mtoto wake wa kike aliekua ameshikiria simu yake ya I phone akichati huku akiwa si mwenye kuzingatia kile alichokuwa akiangalia baba yake sebuleni hapo kwani alionekana kuwa bize , lakini Ghafla mzee huyu alirusha rimoti kwa nguvu na kuipigiza kwenye Tv iliokuwa ikionesha channel ya Bloomberg , huku taarifa mbalimbali zikiendelea ikiwemo ya kampuni ya Vexto international kusaini mkataba mnono na kampuni ya Yamakuza , lakini pia wakati taarifa hio ikiwa nzuri ,pia kulikuwa na taarifa mbaya ya Kampuni ya JR kutolewa katika mkataba huo na ilionekana jambo hili ndio ambalo lilimkasirisha sana mzee Alex.
“Dadiii…!”Aliita mrembo huyu kwa sauti yake nyororo huku akimwangalia baba yake aliekuwa akipandisha ngazi lakini mzee alimpotezea , mrembo huyu ambaye alikuwa akifahamika kwa jina la Queen alionekana kushangazwa na kitendo ambacho baba yake amekifanya na alijikuta akigeuza macho yake kuangalia kwenye TV hio kubwa ya teknolojia ya OLED na kuona taarifa ambayo ilimkasirisha baba yake na alijikuta akitoa kicheko kwa nguvu.
“Masikini Abuu… sijui awamu hii baba atamfanya nini?”
Aliongea mwanadada huyu kwa kufurahi huku akiendelea kuchatika kwa mapozi mara akae uchi mara ajibinue na simu yake hio kubwa na hakuoneskana kuguswa na chochote kilichokuwa kikiendelea kwenye kampuni ya baba yake.
Baada ya mzee Alex kuingia kwenye Ofisi yake ndani ya jumba hilo alivuta mtoto wa meza na kisha akatoa Bastora na kuchukua funguo na kushuka chini na kumfanya Queen azidi kushangaa baada ya kumuona baba yake na siraha … alishindwa kuongea chochote mpaka pale baba yake alipotokomea nje na kusikilizia mngurumo wa sauti uliokuwa ukifubaa kwenye masikio yake..
“Hahahahaha…”Lilikuwa ni cheko la kishambenga la Queen.
Nini kitendelea ….. usichoke.
Comments