Baada ya mtiririko wa matukio ndani ya kampuni ya Yamakuza kuisha , hatimae wageni walikuwa wakiagana kila mtu kurejea kwenye majukumu yake na wale ambao walikuwa ni wageni kuondoka na kuendelea na majukumu yao.
“Tunaweza kuongea Private Pluto?”Lilikuwa ni ombi kutoka kwa Profesa Clark kwenda kwa Roma na Roma alitabasamu.
“Sawa Clark hata mimi ninatamani kuongea na wewe baada ya muda mrefu kutoonana , tuelekeee juu kabisa ya jengo hili nadhani ni sehemu inayofaa”
Aliongea Roma huku akiongoza njia na wakati huu Dorisi walikuwa bize na kuagana na baadhi ya watu lakini alimuona Roma na Profesa Clark wakiingia kwenye lift na alishangaa , lakini sio yeye tu pia Neema Luwazo ambaye bado hakuongea neno lolote na Roma aliliona tukio hilo , lakini pia Mori aliekuwa akiongea na Tikayi wote kwa pamoja walimuona Profesa Clark na Roma wakifuatishana na kuingia kweye lift na kila mmoja akabaki na swali hao wawili wamefahamiana lini , kwani muonekano wa Roma ulikuwa wa kawaida sana kiasi kwamba hakuwa tishio lolote kwa jamiii , yaani alionekana kama mkulima alieziotea pesa jana yake na leo kaja kuichanganya kutoa ushamba na matajiri ambao pesa ilikuwa kama marashi kwao na kiasi kwamba hata harufu zao zilikuwa zikitoa marashi ya kidola dola na ki Euro , Euro.
“Nilipata taarifa kwa mwanafunzu wangu Ashley umepata mke pluto”Aliongea Profesa Clark aliekuwa nyuma ya Roma wakiwa juu kabisa ya gorofa hili la kampuni ya Yamakuza , kiasi kwamba walikuwa wakiliona jiji lote la Osaka , ni sehemu ambayo ilikuwa ikivuma upepo na kufanya nywele za mwanadada Clark kupepea na kumfunika uso na kwa mapozi alikuwa akizitoa usoni na kuzidi kumfanya kuwa mrembo.
Roma aliekuwa amefika mwishoni kabisa wa floor ya ufuniko wa gorofa hii alitabasamu kidogo pasipo kugeuka.
“Ndio Clark , nadhani unataarifa kama anafanana kwa kila kitu na Seventeen”.
Profesa Clark ambaye alionekana kutofurahishwa na tarifa hio alivuta pumzi na kuzitoa nywele zake ndefu zilizojaaa usoni na kisha kuangalia mgongo wa Roma kwa dakika na hapohapo alifanya maamuzi na kwenda kumkutambia Roma kwa nyuma na kupitisha mikono kwa mbele huku wote wakiangalia upande wa baharini ndani ya jiji hili la Osaka na upepo ukiwa unawapuliza.
“Niliishi kwa mateso sana ulivyoondoka Pluto kwenye macho yangu , kila siku nilikuwa mwenye kukuwazia”Aliongea mwanadada huyu huku machozi yakimtoka na kuloanisha suti ya Roma.
“Pole sana Clark , lakini ulinipa baraka zote wakati wa kuondoka na tuliagana , kwanini uwe katika hali ya mateso , maamuzi nilioyafanya kipindi kile ndio maamuzi ambayo nitayafanya pia kwa Zaidi ya mara elfu moja,Clark nimeshaachana na kuwa mashine ya kufanyia matajiri kazi kama mtumwa”
Aliongea Roma na hapa kama ungemuona usingedhania ni yule ambaye muda wote alikuwa akionekana kutokuwa siriasi , hapa alionekana Roma ambaye alikuwa na uchungu mkubwa lakini aliekuwa akidhirisha kile anachokiongea kwa muonekano wake wa sura.
“Ndio najua, najua uliopoondoka nilikupa baraka zote , lakini moyo wangu haukukubaliana na wewe kuniacha , niliteseka na kuwaza kila siku kuhusu ugonjwa wako kukurudia tena , kwani dawa ambazo nilikupatia zilikuwa ni za kuutuliza tu , uliondoka katikati ya matibabu na katikati ya utafiti wangu wa kukutafutia dawa, ni kwanini nisiwe na mawazo ilihali umekuwa mtu wa muhimu kwangu mimi na mama yangu Pluto!?”
“Kwanza ni tukiachana na hayo ,Catherine anaendeleaje?”
Aliongea Roma na wakati huu akiwa washaachiana na walikuwa wote wamesimama upande upande kuangaia upande wa baharini.
“Unamkumbuka? ,yeye yupo ni mwenye kutamani kila siku kukutana na wewe kwa mara nyingine , kila siku amekuwa wakunilalamikia kukuhusu kurudi Tanzania”Roma alitabasamu .
“Naamini siku moja tutakutana , mpe salamu zangu Clark,sidhani kama tunayo mengi ya sisi kuongea Clark mimi ni yule yule na maamuzi yangu , imekuwa jambo jema kukutana na wewe daktari wangu , umezidi kuwa mrembo”
Aliongea Roma na kumfanya mwanadada huyu atabasamu lakini pia kuhudhunika kwa wakati mmoja.
“Mimi siku zote nitakuwa mwenye kuwa upande wako kwa kila maamuzi utakayo yafanya Pluto”Roma alitabasamu na kumgusa shavu kwa namna ya kuliminya
“Okey! Clark nadhani ni muda wangu sasa wa kurudi chini , Dorisi mfanyakazi mwenzangu atakuwa ananisubiri , kwasasa nafahimika kwa jina jipya la Roma unaweza kuniita hivyo tukionana kwa mara nyingine , kwaheri Clark msalimie malkia Catherine” Aliongea Roma na kisha akageuka kuondoka .
“Wait..!!” Aliongea clark na kumsogelea kwa mara nyingine Roma na kisha alitoa Pentorch(Kalamu za mwanga wanatumia sana madaktari) iliokuwa kwenye koti lake la suti ya rangi ya bluu na kumsogelea Roma kwa mbele.
“Naomba angalau nione macho yako”Aliongea na Roma aliitikia kwa kichwa na kisha mwanadada huyu alimmulika kisha akabonyeza maratatu ile pentorch kwa kila jicho.
“Hii ni teknolojia mpya ya kuscan Nevu(nerve) ambayo nimeitengeneza , inaweza kunisaidia kujua kwa sasa hali ya ugonwa wako nitaenda kuzichambua picha nilizozipiga hapa” Aliongea na kisha aliingiza mkono kwenye mfuko wa koti na kutoa mkebe mwingine na kumpatia Roma.
“Humo ndani kuna dawa mpya ambazo nimefanikiwa kuzitengeneza , kama utahisi tatizo lako kukurudia jaribu kumeza , tukikutana kwa mara nyingine nitakupima na kujua kama zinafanya kazi kwa ufanisi”
“Asante sana Clark kwa kunijali , unaonekana ulikuwa ukitembea na dawa zangu muda wote kwenye koti lako kwa kuamini tunaweza kukutana”Roma alionekana kuguswa na matendo ya mrembo huyu.
“I just Could `nt help my Self Pluto , this is how I relieve my worries , I told my self we will meet again even by chance and here we are”(Sikuweza kujisadia mwenyewe Pluto , hii ndio ilikuwa namna nilivyokuwa nikipunguza wasiwasi wangu , nilikuwa nikijiambia ninaweza kukutana na wewe kwa bahati mbaya na leo imetokea)
“Clark you are good woman whom I had ever know in my life and every act of your kindness has a lot of meaning to me ,Thank you So much and goodbye”(Clark umekuwa mwanamke mwema kwangu sana ambaye nimewahi kukutana nae kwenye Maisha yangu na kila tendo la kikarimu unalofanya linamaana kubwa sana kwangu , Asante sana na kwaheri)
Aliongea Roma na kisha akaondoka na kumuacha mwanadada huyu akiangalia kivuli chake kinachotokomea kwenye macho yake na alijikuta akipeleka mkono kwenye macho yake na kufuta machozi ambayo hakujua yameanza kumtoka , huzuni aliokuwa nayo huyu mwanadada ni kama vile hatomuona tena Roma , haikueleweka ni hisia gani za huyu mwanadada anazo juu ya Roma.
*****
Mzee Alex alionekana kuwa ni mwenye hasira sana , alikuwa akitweta huku akitoa jasho , hakuamini dili kama hilo kampuni yake imeshindwa kulipata , hakuelewa ni kitu gani abuu anakifanya huko Japani mpaka kukosa dili kubwa kama hilo , aliapia kwa majina yote ya ukoo wake Abuu akirudi lazima amtandike risasi.
Alimfikiria Abuu kama toto jinga ambalo halikupaswa kupewa nafasi kubwa katika uongozi wa kampuni , kiasi cha kwamba aliamini huenda angempa mtoto wake mkubwa wa kike nafasi hio huenda angeleta mabadiliko makubwa.
“Abubakari ni mjinga sana , kashindwaje kusaini mkataba mnono kama ule na kumuachia Edna , anajua ni kiasi gani gepu ambalo lipo kwasasa baada ya kampuni yetu kukosa hilo dili na Edna kulipata ,, sh**t huyu mtoto nikimuacha hai labda sio mimi Alex , labda asirudi na anabahati hata kazima simu ningemtukana mpaka matusi ambayo hayajavumbuliwa bado”
Alijiongelesha maneno yasio na mpangilio kwa sauti huku akigonga stering ya gari wakati likiendelea kuwa katika mwendo, na wakati huu alikuwa akipita Kongowe na kuchanja mbuga na ndani ya madakika kadhaa tu alikuwa ashafika sehemu aliokusudia na kukata kushoto na Range yake kuingia kwenye barabara iliokuwa na rami lakini iliokuwa imependezeshwa na miti midogo ya miarobaini iliopandwa kwa mstari pembezoni mwa barabara na kufanya eneo hili lipendeze.
Baada ya kutembea umbali wa mita chache tu alikutana na kizuizi cha geti na kusimammisha gari na alitoka askari aliekuwa ameshikilia SMG na baada ya kumuona ni mzee Alex alitingisha kichwa chake kwa heshima na kumruhusu.
Naam hapa ndio anapoishi mheshimiwa mstaafu Kigombola , sehemu ambayo ilikuwa ikifahamika kwa jina la Village G , ni sehemu ambayo ilijaa ufahari kuanzia mazingira mpaka nyumba.
Mheshimiwa huyu alionekana alipenda muundo wa jengo la ikulu ya Dar kwani , hapa ndani palikuwa pakifanana san ana ni kama injinia aliejenga hapa ndani alikopi tu muundo na kujenga ,hivyo hii sehemu ni sahihi kusema ni kopi ya ikulu, mheshimiwa kigombola alionekana kupenda ‘vibe’ la ikulu.
Baada ya Mzee alex kuegesha gari alitoka moja kwa moja , huku siraha yake ikiwa kiunoni bila ya kuonekana.
Baada ya kuingia kwenye sebule kubwa iliokuwa ndani ya jengo hili , sebule maalumu kwa ajili ya maongezi ya mheshimiwa Kigombola na wageni wake ,Mzee Alex alijikuta akishangaa watu waliokuwa hapo ndani na ghafla tu akachomoa Bastora yake na kuikoki.
“Baba….Babababa .. naomba unisamehe .. babba najua nimeboronga.. lakini naomba unisameh…aaa”Alikuwa ni Abuu aliekurupuka mara baada ya kumuona baba yake mlezi, haikueleweka alikuwa amefika saa ngapi nchini na hapo ndani.
Kila mtu alishangazwa na kitendo cha mzee Alex kutoa siraha , waliokuwa hapa ndani walikuwa ni Abu , Mheshimiwa Kigombola ,Elvice Temba , mzee Temba mwenyewe ambaye alikuwa ni Mkuu wa mkoa wa Dodoma , alikuwepo pia Meya wa jiji la Dodoma mzee Abubakari Juma lakini pia kiongozi mkuu wa kundi la Black Mamba .
“Alex hebu punguza jazba… weka siraha chini tupo hapa kwa ajili ya kujenga sio kubomoa , acha kuonesha udhaifu mbele ya kila mtu”
Aliongea mheshimiwa Kigombola kwa hasira na muda ule ule tu Aliingia kwa kitaalamu kabisa mlinzi wa Kigombola wa kike na kubetua siraha na ikadodokea mikononi kwake na kumpiga Roba Alex.
“Scorpion , unaweza kumuachia”
Aliongea Kigombola na Scorpion aliekuwa amempiga Roba mzee Alex alimuachia , lakini ni kama Alex alifunguliwa kwani alimkimbilia Abu na kuanza kumpiga mangumi na Abu ambaye alikuwa amepiga magoti alijikuta akidondoka chini , lakini mzee Alex hakuacha aliandelea kusindilia mateke , ngumi , Scorpion alitaka kuingilia lakini Mzee kigombola alimpa ishara asifanye chochote.
Abuu alipigika na mpaka damu zikaanza kumtoka ndipo mzee Alex alipomuachia huku Abuu akilia kama mtoto.
“Mzee Alex kama hasira zako zimepungua unaweza ukaketi tukaongea tuyajenge sasa , sio muda wa malumbano sasa , mwenyewe sijapenda yalitokea huko Japani , lakini hata kama ni wewe usingeweza kumdhibiti Roma.”
Aliongea Kigombola na mzee Alex alionekana kupoa kidogo na muda huo huo aliingia mhudumu na kumpa glasi ya maji na akayanywa yote kwa pupa na kisha akasogelea sofa na kukaa.
Ilionesha Abu alikuwa ashahadithia kila kitu kilichotokea huko Japani mpaka kujikojolea kwake na sasa Kigombola alikuwa akimpasha habari kwa ufupi ya kile walichoambiwa na Abu.
“Niseme tu hata mimi naelewa Roma sio mtu wa kawaida , nimejaribu hata mimi kufukunyua kupata taarifa zinazomuhusu Roma lakini sikufanikiwa , badala ya kupata taarifa inayoonesha , alikuwa akiishi nchini Marekani kabla ya kuja hapa Tanzania na inasemekana nchini Marekani alikuwa akilelewa na moja ya matajiri wakubwa , jimbo la Michigani , Tajiri mmoja anefahamika kwa jina la Robert Eglon”Aliongea Kigombola.
“Hata kama sio wa kawaida , tunashindwaje kumuua mtu mmoja watu wote sisi na nguvu yote tulionayo , tunaachaje mtu mmoja aharibu kila kitu tulichokijenga kwa miaka”Aliongea Mzee Alex na Mstaafu kama kawaida yake aliachia tabasamu.
“Alex kwenye vita ili uwe na uhakika wa kushinda mbinu ya kwanza ni kujua adui yako anauwezo wa namna gani , huwezi kwenda kichwa kichwa utashindwa , na sisi kusema Roma sio wa kawaida ni swala la kuutambua uwezo wake , lakini haimaanishi tumeshindwa”
Aliongea na kisha alimimina maji kwenye glasi na kunywa kidogo na akageuka na kuwaangalia kila mmoja hata Abuu ambaye alikuwa akimwangalia baba yake kwa woga.
“Mpango mzima wa Yamakuza mpaka sasa tuseme umefeli kwa asilimia mia moja na tumezidiwa akili , lakini haimaanishi kwamba tumeshindwa , Roma ni kama nzi kwetu na cha kufanya ni kuitega na viganja viwili na kisha kuimaliza”
Kila mmmoja alimwangalia mzee wa mipango bwana mstaafu kwa kumtaka endelea kuongea Zaidi.
“Najua wote mnaelewa The Doni alikuwa ni mtu ambaye siku zote ni mwenye kutaka upatikanaji wa ‘Safe Root’ katika biashara zetu na niwaambie tu , hilo swala lazima lifanikiwe na hakuna njia nyingine ,Vexto ni kama zao la mkulima aliepanda mbegu njiani na hakuna budi kwa wapita njia kukanyaga na kutengeneza njia”
“Kwa hio mhesimiwa nini kifanyike?”
“Nadhani kila kitu kipo kwenye mipango Bakari , kwani mpango B wenu mliopanga ulikuwaje?”
“Mpango B ilikuwa ni kumua Roma na Edna siku ya kusanyiko la wafanyabiashara”
“Nadhani tuendelee na mpango huo huo cha kufanya tu ni kwamba mpango huu tunatakiwa kuongezea nguvu ili uwe na asilimia kubwa za mafanikio” Kila mmoja alishangaa lakini mheshimiwa alitabasamu na kisha akamgeukia mlinzi wake.
“Mwambie aingie”
Mlango ulifunguliwa na hapohapo akaingia bwana ambaye aliwafanya kila mtu kugeuza macho na kushangaa.
Make kwa kutulia nitaleta muendelezo saa nne kamili usiku , kama huwezi kusubiria lala utaukuta asubuhi………
Comments