“Edna simu yako inaita”Aliongea Blandina na kumfanya Edna kusimama huku akieguka na kumwambgalia mama mkwe wake wa mchongo.
Aliekuwa akipiga ni Roma kwani jina lilisomeka hivyo kwenye skrini juu n ahata Blandina aliliona na hakujua ni kwanini Roma alikuwa akipiga simu.
Edna aliichukua na baada ya kuona jina ni Roma alijikuta akitamani kukata , lakini aligundua kuwa Mama yake Roma anamwangalia , hivyo hakuwa na jinsi na kupokea.
“Unasemaje?”
“Em.. Babe wife natumaini unafurahia kampani ya watto kuliko mimi mumo”Aliongea Roma upande wa pili.
“Ongea nipo kwenye haraka”Aliongea Edna huku akipandisha kisirani.
“Kuna jambo Bi Wema alisahau kukuambia asubuhi , hivyo kaniomba nikueleze , alishatafuta kampuni ambayo itahusika na kutuhamisha”Aliongea Roma na kumfanya Edna akumbuke kwamba siku kadhaa nyuma alijadiliana na Bi Wema juu ya kuhamia Osterbay. Kwenye nyumba yake kubwa.
“Nilisahau kabisa… wewe unaonaje?”Aliongea Edna huku akishusha sauti chini.
“Kwanini unaiuliza hivyo, mimi nimekupatia taarifa hivyo”
“Lakini pia una maamuzi kwanini kila kitu lazima nikitolee maamuzi mimi , nafasi yako ni ipi?”Aliongea Edna huku akianza kukosa utulivu.
“ Edna nini kinaendelea huko kituoni mbona unaongea kama haupo sawa?”Edna alifikiria kidogo na kisha akamgeukia Blandina kama vile anasoma jambo kutoka kwake.
“Kama kampuni ya uhamishaji ishafika mnaweza kuendelea na vitu muhimu vya kuhama navyo , kuhusu chumba changu vitu viachwe kama vilivyo mpaka nitakaporudi”Aliongea
“Okey nitamueleza”Aliongea Roma na kisha simu ikakatwa .
“Mama nilisahau siku ya leo tulikuwa na mpango wa kuhamia Osterba kwenye nyumba kubwa”Aliongea Edna akimwangalia Blandina.
“Ooh!... Edna tunapaswa kurudi na kuangalia utaratibu wa uhamishaji wa vitu” Edna alifikiria maneno ya Blandina na akaona ana pointi ya msingi , lakini bado moyo wake ulikuwa ukitaka kumuona Lanlan.
“Edna yule mtoto sijui kakufanya nini , ila kwa sasa atakuwa na wazazi wake,,, najua unapenda Watoto sana na natamani siku uje upate wa kwako utakuwa mama mzuri”Aliongea Blandina na kumfanya Edna kushangaa kidogo ukweli wazo la kuzaa bado halijawahi kujia akililini na muda huo ni kama limeingia upya.
“Kweli , lanlan atakuwa na wazazi wake kwasasa , sipaswi Kwenda nyumbani kwao”Aliwaza Edna na kisha akakubaliana na Blandina warejee nyumbani kwa ajili ya kusimamia uhamaji wao kwenye nyumba yao ya zamani.
Dakika arobaini na tano ziliwatosha kabisa kufika nyumbani na gari kubwa la kubeba mizigo lilikuwa ndani ya nyumba yao na wafanyakazi wa kampuni ya uhamishaji walikuwa wakiendelea na kazi.
Edna alirtoa maelekezo ya baadhi ya vitu vya kawaida kuacha hapo ndani kwa mfano vifaa vva kielectronics na baadhi ya samani nah io ni kutokana nyumba ya kule Osterbay ilikuwa na kila kitu.
Roma aliekuwa akisaidiana na wafanyakazi kubeba baadhi ya vitu muhimu, alishindwa kuelewahali aliokuwa nayo Edna , ni kama kulikuwa na kitu ambacho alikihisi wakati Edna anaingia hapo ndani ambacho hakuwa nacho tokea aonane nae kwa mara ya kwanza.
“Edna.!!”Aliita Roma baada ya kufungua mlango na kuingia ndani ya chumba cha Edna taratibu na Edna hakuongea chochote baada ya kuingia Zaidi ya kujiweka bize na anachokifanya , Edna alikuwa akipangilia baadhi ya vitu vya kuhama navyo.
“Edna nini kimetokea mlikotoka , nahisi haupo sawa kama ulivyoondoka asubuhi”Aliongea Roma lakini Edna alikuwa akiendelea na anachokifanya huku akiwa amempa mgongo Roma na alionekana kuchangua baadhi ya vitu kwenye kabati lake pasipo mpangilio maalumu ni kama mtu ammbaye alikuwa akitafuta kitu muhimu pasipo kukipata na Roma aliona jambo hilo na kuishia kutabasamu , kuna kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kutoka kwa Edna ambacho alikuwa akikihisi kutoka kwake , lica ya kumwangalia Edna kwa macho yake na kuona mwili wake hauna shida lakini kuna mabadiliko makubwa kutoka kwa Edna ni kama vile mtu anapokaribia eneo la hatari zile hisia zinazomjaa mtu ndivyo ilivyokuwa kwa Edna wakati anaingia hapo ndani akiwa na Mama yake.
Roma baada ya kuona ajibiwi alikata hsauri ya kumsogelea na kumkumbatia kwa nyuma na kumfanya Edna asimame wima huku akitulia kama mtu anefikiria hatua ya kuchukua kwa tukio ambalo kafanyiwa.
Roma alifahamu Edna angeleta shida kwa kumkumbatia kwa nyuma , lakini majibu yake yalikuwa nje ya mategemeo yake , kwani aligundua Edna Zaidi ya kuleta ukinzani alianza kulia kwa kwikwi na kumfanya Kushangaa, mbaya ni kwamba sasa staili ya namna Edna anavyolia ni tofauti na aliokuwa ameizoea , Edna alikuwa akilia kwa kwikwi huku akiwa ameshikilia moyo wake ni kama mtu ambaye amepoteza kitu kikubwa kwenye Maisha yake.
Roma ilibidi amuache Edna aendelee kulia atakavyo , alijua moja kulia ni sehemu ya mtu kutoa sumu moyoni na ndio maana hakutaka kumzuia Edna kutoa kilio, lakini licha ya kwmaba alikuwa amemuacha Edna kulia , lakini moyo wake ulikuwa ukiuma ajabu, hakupenda kumuona Edna analia na pia alijiambia Edna ni mwanamke ambaye siku zote anajua ni imara katika kuziendesha hisia zake na ndio maana hakuwa mtu wa kuwaza sana , lakini kitendo cha Edna kulia waziwazi mbele yake, lakini pia mabadiliko ya Edna aliokuwa nayo vilimfanya kuwa na wasiwasi na kuwa na uchungu kwa wakati mmoja.
Roma ilibidi amsogelee Edna alierudi kukaa kitandani na kisha kumkumbatia na kumruhusu Edna kulia kwenye kifua chake.
“Edna niambie ni nini kimetokea kituoni leo?”Aliuliza Roma baada ya Edna kunyamaza huku akijifuta machozi na kusimama na kuanza kuweka nguo zake kitandani.
“Hakuna kilihotokea”Aliongea Edna huku akirudiwa na hali yake, Roma alijiambia kama Edna ndani yake kulikuwa na pepo , pasi hhilo pepo ni la aina yake kwani lilikuwa likimuenbdesh Edna kwa namna ambavyo sio ya kawaida.
Roma alijiuliza inakuwaje mtu dakika kadhaa nyuma alikuwa akilia kama mtoto , lakini sasa hivi anaonekana kama vile sio yeye na ukauzu wake kurudi kama kawaida, Roma kwa jinsi alivyomuona Edna aliamini kabisa hapo hakuna maongezi tena ya kuendelea kwani Edna asingeongea chochote.
“Unamaanisha kweli hakuna kilichotokea au unanikalia kimya”Aliuliza Roma.
“Roma.. nishasema hakuna kilichotokea”Aliongea Edna huku akiendelea na kazi yake ya kuanza kupangua nguo baadhi na kuziweka kitandani .
“Kama hakuna kilichotokea kwanini ulikuwa ukilia kama mtoto dakika moja iliopita?”Aliongea Roma na kumfanya Edna kusimama na kumgeukia Roma na kumwangalia usoni , ni kama alikuwa akaitafuta jibu la kumpatia.
“Sijui.. nilijikuta natamani kulia na sababu sina”Aliongea Edna kinyonge na kisha akageukia kabati na kuendelea.
Upande wa Roma alitamani kucheka , yaani alishindwa kabisa kumuelewa Edna na alijiambia sijui ni lini ataweza kumuelewa maana alioan muda mwingine Edna hakuwa mtu wa kawaida , alijiuliza inakuwaje mtu kulia pale anapojiskika pasipo kuwa na sababu maalumu.
Roma alimwangalia Edna kwa dakika kama nne huku Edna akijifanya hajali uwepo wake na baada ya hapo aliamua kupiga hatua kutoka nje.
“Romaa..!!”Aliita Edna kabl aya Roma kufunga mlango na Roma aligeuka na kumwangalia.
“Juzi niliwaambia Daudi na Wendy wakutafute juu ya maswala ya kampuni , ila sijapata mrejesho wa kile kinachoendelea”Aliongea Edna na Roma alitabasamu.
“Boss unataka ripoti hio sasa hivi?”Aliuliza Roma kiutani , lakini Edna aliendelea kuwana mwonekano wake uleule na kisha aktingisha kichwa.
“Unahisi siwezi kuongoza vyema kampuni , kama ulikuwa huamini kama naweza kuongoza kwanini umenipatia niongeze”Aliongea Roma.
“Nimekuuliza kwa ajili ya kupata mipango yenu , sijawahi kufanya maamuzi ambayo nitajutia baadae , amini kwamba nayaamini maamuzi yangu” Aliongea Edna.na Roma alirudi nyuma na Kwenda kuketi kwenye kitanda.
“Njoo ukae hapa kwanza pembeni yangu”Aliongrea Roma hhuku akipa ishara Edna ya kusogea mpaka kitandani lakini Edna alijikuta kukosa maamuzi kwa dakika kadhaa, lakini mwishowe alisogea na kuketi kitandani.
Sasa kitendo cha Edna kuketi kitandani tu , alijikuta akifanyiwa shambulio ambaclo hakulitegemea kwani Roma alimbeba juu kama mtoto na kubwaga katikati ya kitanda , wakari Edna hajachuku hatua juu ya kipi cha kufanya , alijishutikia Roma yupo juu yako.
“Roma..Acha..”Aliongea Edna kwa kusitasita , kwani mpaka hapo alikuwa shajua Roma anataka kufanya nini.
Comments