Roma mara baada ya kubeba bunduki aliangalia kama ilikuwa na risasi na baada ya kuona zipo za kutosha alimgeukia Mika.
“Dogo unajua kutumia bunduki?”Aliuliza Roma na kumfanya Mika kutingisha kichwa kwamba alikuwa akijua kutumia na Roma alitegemea hilo kwani alikuwa akielewa kama Samweli Nguluma ambaye ni baba yake Benadetha alikuwa bosi wa kundi la kiharifu la ZoaZoa basi Mika asingekosa mafunzo muhimu ya namna hio.
…Tafadhari Ingia/Jisajili uweze kuendelea.
Comments