Reader Settings

Ukweli ni kwamba pengine Eliza  hakuwa akijua  tu  vizuri lakini  eneo hilo  lilianzishwa na  Mjerumani mmoja  aliefahamika kwa jina la Bruno , ilikuwa ni eneo ambalo  kazi yake kubwa ni kuvuna viungo vya binadamu na kuvisafirisha nje ya  nchi.

Baadae serikali baada ya kuingilia  ndio  ikabadilishwa kutoka kuwa  sehemu ya kuvuna viungo na kuwa kituo cha  wagonjwa   wenye magonjwa yasiowezekana kupona na msimamizi wa hilo eneo anaitwa Dokta Ivan  B Bridge ni mtanzania halisi kwa kuzaliwa  licha ya kuishi sana nje ya nchi  kabla ya kurudi tena , chimbuko lake  ni familia   za kikoloni zilizotawala Tanganyika   katika eneo hilo  na kujikita  katika  biashara ya kilimo cha Katani.

Lakini licha ya eneo hili kufahamika kama hospitali  na makazi ya Dokta Bridge lakini ndio sehemu ambayo biashara  ya kimagendo ya kuuza  viungo ilikuwa ikifanyika kwa usiri mkubwa mno, vijana wengi waliokuwa wakihitaji kuuza  figo zao  koneksheni ilikuwa ni kuja ndani ya hilo eneo.

Hoteli ya Troitsa ndio sehemu  ambayo  wauza viungo na wale wanaotaka kununua   hutumia kama makazi  mpaka kupata huduma na mara nyingi  wanaofikia ndani ya hoteli hio wanapata huduma bure kabisa kama ilivyokuwa kwa  Hamza.

Ni eneo lenye ulinzi mkali na asilimia kubwa ya wagonjwa wanaoingia hapo ni wale wanaojiweza ki uchumi ,  walikuwa wanaingia  mpaka wagonjwa  kutoka nje ya nchi kwa  kigezo cha  kupata huduma ya  tiba ya muda mrefu lakini ukweli in kupandikizwa viungo.

Ukiachana na hayo yote Profesa Bridge  ni mwanachama mwenye cheo kikubwa tu katika   shirika la Utatu  giza(Black Trinity)

Hamza  mara baada ya kutoka kwenye gari akiwa ameambatana na  Eliza  walisogea  kuingia ndani ya eneo hilo , lakini  kabla hawajapita  kwenye  kizuizi  walizingirwa na mabodigadi waliovalia nguo nyeusi na ilikuwa ni kama walikuwa wakimsubiria.

Hamza aliishia kutoa tabasamu  baada ya kuona ni kama alivyotarajia  na aliishia kumwangalia bwana  wa kizungu ambae alionekana  ndio kiongozi.

“You can’t be Van Bridge, right?”Aliongea Hamza akimaanisha bwana huyo  hawezi kuwa Van  Bridge.

“Master hana muda na nyie , ameniambia  mnipatie fedha , kiasi milioni mia sita , mkimaliza kulipa  baba yenu ataachiwa huru”Aliongea yule bwana kwa lugha ya kiswahili licha ya uzungu wake.

“Kwanini ni  milioni  mia sita  na sio Mia tatu?”

“Mkataba wa mkopo ndio unavyotaka,  milioni mia tatu  zilizoongezeka ni riba ya mkopo , baba yako alikubali kipengele za kulipa   asilimia hamsini ya  madini yatakayopatikana ,  lakini madini  hayakupatikana , Bosi ni muungwana  hakutaka kupiga hesabu kamili hivyo  ameweka milioni mia tatu  pekee ya Riba”Aliongea  yule bwana yule  na kumfanya Eliza  kuhisi kiungulia   cha  kifungua kinywa alichopata  asubuhi , zilikuwa hela nyingi mno ambazo hata kama angekopa asingeweza kulipa.

Upande wa Hamza hakushangaa sana ,  hilo ni swala ambalo alitegemea  kukutana nalo.

“Najua Van Bridge hajaniita  kwa kuniharakisha kwasababu ya  kuja  nimlipe hiko  kiasi , achana na usaili wako nataka kuonana na bosi  wako, maana sijaja hata na mia  hapa”Aliongea Hamza.

“Huwezi kupita hapa bila ya  hela , unakujaje mikono mitupu   kwa kujiamini namna hio, kama unataka kumuona  bosi  pita kwangu kwa nguvu tuone”Aliongea yule mzungu kwa kujiamini.

Baada ya kiongozi wao kuongea maneno hayo , wale mabidigadi wote walikaa mkao  wa tahadhari ya kushambulia , Hamza aliishia kumrudisha  Eliza nyuma huku akianza kuwasoma mmoja baada ya mwingine  kutoka pande zote.  Hakusubiri hata wao waanze kushambuia,   akiwa  ni kama anamzunguka Eliza  alimshambulia bodigadi aliekuwa karibu yake na teke moja tu alidondoka chini  kama mzigo.

Yule bwana wa kizungu alijikuta akishangaa maana   ni kitu ambacho hakukitegemea , alikuwa ameshamdharau Hamza kwa muonekano wake, lakini hata hivyo hakutaka kumwangalia Hamza anamshambulia bodigadi wake mwingine , hivyo mara baada ya kuona nafasi azimu alisogea kwa spidi  huku akiwa amekunja ngumi yake na kutaka kumpiga  nayo Hamza tumboni.

Hamza  ilikuwa ni kama amemuwekea tumbo  vizuri ili ampige  , lakini kabla hata hajamfikia mkono wake  wa  kushoto ulimdaka na kisha  kupindisha kiganja cha  mkono.

“Arghhhhhhhhhhh”

Yule bwana wa kizungu alijikuta akitoa  yowe la  hali ya juu mno , mkono wake ulishikwa na maumivu makali mpaka ukafa ganzi.

“Unaonekana   una mafunzo ya  nishati za mbingu na ardhi kwa kutumia njia ya kufanya mapenzi , lakini kitu ambacho hamjawahi kuelewa hio mbinu  haina matokeo  mazuri kwa mtu ambae ndio anaanza  mafunzo , unahitaji msingi  wenyewe wa mafunzo  kabla ya kuvuna nishati, la sivyo  utaishia kuongeza mvuto wa kingono na  nguvu za mapambano huna”Aliongea Hamza.

“Who  the hell  are you?”Yule Mzungu alijikuta akipagawa mara baada ya kusikiliza maneno ya Hamza.

“Si wote mshalisikia jina langu ,au mnataka nianze upya kujitambulisha , niambie ni wapi alipo  Ivan  la sivyo nitaendeleza”Aliongea  Hamza  kwa jeuri.

“Master yupo  kwenye chumba cha upasuaji?”

“Upasuaji gani unafanyika hapa ndani?”Aliuliza Hamza huku akiwa na mshangao   huku upande wa Eliza akishikwa na hofu kwa kuamini pengine ni baba yake anaefanyiwa upasuaji wa kuondolewa viungo vya mwili.

“Ni  mkuu wetu ndio anaefanyiwa  upasuaji  na washirika wote wapo hapa wanasubiri”Aliongea.

“Kuna mkuu wenu?”

“Kama  hakuna mkuu unadhani hili eneo  linaendeshwa na nani, namaanisha mtoto  wa bosi  Bridge tunamwita Mkuu”Aliongea.

“Kama washirika wote wapo hapa , je ni kwasababu  operesheni ni ngumu na ya hatari  au kuna kipi  kingine?”

“Ndio  ni ya hatari , ni upasuaji wa moyo , halafu kwanini maswali mengi?”

“Upasuaji wa moyo?”Hamza alijikuta akishangaa huku akijiambia pengine hilo eneo halikuwa la kawaida kama alivyodhani.

“Hebu nipeleke  na mimi nikajionee”Aliongea  huku akishikwa na msisimko wa kuona kinachoendelea.

“Hata kama uwezo wako wa kimapigano ni mkubwa kuliko  wangu haimaanishi unaweza kuingia  na kusumbua madaktari ambao wapo kazini  na ukaachwa  hivi hivi”Aliongea.

“Umenielewa vibaya mkuu , mimi situmii nguvu kuingia ,  kama ni upasuaji wa moyo  basi mimi ni daktari bingwa  wa huo upasuaji, haitakuwa  tatizo  pengine naweza kusaidia”

“Nini!, wewe ni  mtaalamu wa upasuaji wa moyo?”Aliuliza kwa mshagao lakini kabla hata Hamza  hajajibu,  simu ya yule bwana iliita.

“Mruhusu Dokta Hamza aingie” Ndio alivyosikia na kuzidi kutokwa na macho ya mshangao.

Eliza alitamani  kutokuingia lakini kutokana na hofu ya baba yake kutolewa viungo  aliamua kuingia na Hamza.

Baada ya wote wawili  kuingia kwenye lift  na kushushwa chini kwenye  vyumba  Hamza aijikuta akishangaa  baada ya kuona  mazingira ndani ya  hospitali hio , ilikuwa ni eneo ambalo  lina kila  kifaa  cha teknolojia ya  hali ya juu , ilikuwa ni  sahihi kusema ni taasisi  ya daraja  la kwanza ya  kitabibu.

Sehemu iliokuwa ni kama ukumbi , kulikuwa na kusanyiko kubwa la watu  waliokaa kwenye   viti  huku macho yao yakiangalia  runinga kubwa iliokuwa ikionyesha  kinachoendelea, moja wapo ya watu hao alikuwa ni Dokta  Bridge  mwenyewe , watu wote walionekana kuwa na ukwasi wa pesa kutokana na sura zao na mavazi yao huku wakiwa wamezungukwa na kundi la mabodigadi.

“Nini kinaendelea?”Aliuliza bwana mmoja aliekuwa na muonekano wa kizungu , alikuwa mzee hivi  na nywee zake zilikuwa nyeupe.

“Dokta Hamza  amefika”Aliongea  yule bodigadi mzungu  na kumfanya yule  mzungu kukunja sura kama amekula pilipili.

“Nani kasema Hamza ni dokta , inakuwaje  mwanafunzi wa  chuo cha  uchumi   na dereva ndani ya kampuni kuwa  Daktari , umeanza lini kunitania Lamberk?”Aliongea kwa hasira.

“Lakini bosi  wewe ndio umesema  ni Daktari  ni mruhusu”Aliongea   kwa wasiwasi kujitetea na bwana yule wala hakujali na macho yake yalimgeukia Hamza.

“Dogo ukiambiwa uje sehemu unafanya safari bila ya kujifikiria, huna msimamo binafsi  na nani kakuambia  uje na mwanamke?”Aliongea yule bwana  tena kwa lugha ya kiswahili.

“Huyu  ni binti wa baba  uliemteka  na mpenzi wangu acha  porojo?”Aliongea Hamza.

“Mimi Dokta  Bridge ni raia mwema ndani ya  nchi hii , siwezi kuteka mtu nniombe radhi kwa kunisingiizia”Aliongea.

“Kama  hujamteka umefanya nini? ,  nyie ndio mliemuingiza kwenye mtego ili   aingie kwenye madeni ,  mmefanya hayo yote kwasababu ipi?”.

“Tunafanya vitu kwasababu nyingi , ikiwemo  kujilipa fidia  kwa wadeni wetu ambao wameshindwa kulipa kiasi cha pesa ila hatujawahi kuteka mtu”Aliongea.

“Unamaanisha kuondoa viungo  vyao vya mwili?”Aliuliza Eliza.

“Binti  kuwa makini  na unachoongea , hakuna  kitu kama hicho   hapa ndani , ila baba yako akitaka kutuuzia figo na  mwenye kuhitaji  akajitokeza litakuwa ni dili  zuri”Aliongea.

Hamza alijiambia huyo jamaa sio mzungu kabisa , kuishi ndani ya Tanzania kumemfanya kuwa mswahili.

“Najua sababu ulioniitia hapa  ni kwa ajili ya kukusaidia upasuaji wa  mtoto  wako , sijui umezipatia  wapi taarifa za mimi kuwa  daktari wakati ni  siri yangu , lakini naweza kukusaidia kama upo tayari  kutimiza masharti yangu”Aliongea Hamza.

“Well!, japo  ni kweli nimesikia taarifa za  wewe kuwa daktari  , ila siwezi kukuamini na kukupatia mtoto wangu kwa ajili ya  kumpasua,haiwezekani kwa kijana kama wewe  ambae huna cheo na sikujui vizuri  uwe Daktari,hata Leseni unayo?”Aliongea.

“Kama unaamini  siwezi kuwa daktari hizi hila zote zilikuwa za  nini?”

“Hakuna hila yoyote , taarifa za siri zimenifikia na nikaambiwa wewe ni daktari, lakini  sijaweza kuamini wala hakuna uthibitisho wa wewe kuwa daktari..”Aliongea kufikiria kituo na akaishia njiani na kumwangalia Eliza.

“Binti  baba yako yupo kwenye mtatizo kwasababu  yako , nikikuangalia  naona kila sababu kwanini  ulikuwa  ni shabaha ya Gabusha  kama  Spiritual host , lakini  inasikitisha mpango wake umefeli  baada ya kuonja umauti?”Aliongea  na kauli ile ilimshangaza  Eliza.

“Mzee Gabusha amefariki!!?”

“Anakaribia kufariki”Aliongea.

“Unamaanisha nini kukaribia kufariki?” Aliuliza Hamza awamu hio.

“Hii ni sehemu ya kulaza wagonjwa  ambao wamekufa ubongo”Aliongea na Hamza alijikuta akimwangalia Eliza kama kwamba hawakuwa wakiamini.

“Baada ya kusikia  una uwezo wa kufanya upasuaji  wa  moyo  nimekataa kuamini  lakini  sikutaka kudharau pia ,  Binti nimenunua deni la baba  yako  kwasababu  una mpenzi aneonekana kuwa na ka’uwezo,  ni aidha unilipe au yeye anilipe ndio baba yako aachiwe huru  au alipe yeye mwenyewe kwa kutoa figo zote mbili”

“Figo  zote mbili!?”Aliuliza Eliza kwa mshangao.

“Nani wa kukubali kuingia hasara kwa figo ambazo zimeharibiwa na pombe , binti  baba yako hana kiungo kizuri  kwenye mwili wake kutulipa vyote vimechakaa”Aliongea  na angalau kauli ile ilimfanya Eliza kupatwa na ahueni baada ya kuona baba yake yupo hai.

“Kama umeniita kwa  kunidhania mimi daktari   basi nipo tayari kulipa  deni  lote kwa kumfanyia mtoto wako  upasuaji  wa daraja la kwanza, kama upo tayari  kutii masharti nipo tayari  kuona medical history na surgery plan  kisha nitatoa  maoni yangu”Aliongea Hamza.

“Dokta  anaefanya upasuaji ni bingwa niliemtoa Italy ,  Dokta Antonio Salazer  si tu  ana ujuzi wa upasuaji lakini  vilevile amefanikiwa kufanya aina nyingi za upasuaji wa moyo, nimekuita hapa kwa dharula lakini hata kama unaweza kusaidia  ushachelewa  maana  upasuaji ushaanza”Aliongea Dokta Bridge.

Ukweli Hamza hakujua kwanini  mzee huyu kaamua kumfanyia mtoto wake  upasuaji  ndani ya hilo eneo ,  alikuwa na hela za kutosha za kumpeleka  nje ya nchi kwenye hospitali kubwa , jibu  moja tu la  makisio yake ni kwamba pengine  mtoto wake ni mhalifu na popote atakapoenda atakamatwa, ila kwasababu alikuja kumaliza swala la Eliza  alitaka kufanya namna yoyote ile kulipa deni lake.

“Dokta Salazer anaweza  mtaalamu  , lakini operesheni anayoendelea nayo sio nyepesi , kama  kweli   unamwamini kumponyesha  mwanao  kwa asilimia mia moja  usingefanya hila  za kununua deni  ili kufanya hila za kunileta hapa  na  pili msingekuwa mmekakamaa sura kwa namna hii”Aliongea Hamza huku akiangalia  runinga inayoonyesha upasuaji unaoendelea.

Dokta Bridge  hakupingana na maneno ya Hamza , hata yeye ni dokta   wa upasuaji , licha ya kubobea kwenye upasuaji wa kawaida  lakini kama dokta alikuwa akijua kinachoendelea, ndio maana  hata alipoletewa Intellijensia  na ushirika  wake wa Black Trinity juu ya Hamza kuwa mtaalamu wa kitabibu hakuidharau.

Hamza  upande wake hakushangaa sana taarifa za  yeye kujua   kufanya upasuaji wa moyo kumfikia   Dokta Ivan Bridge , ukweli ni kwamba  chata za fuvu alizoziona ndani ya  eneo hilo tokea anaingia alijua fika  hii hospitali inaendeshwa na  Black Trinity na kama ni hivyo  ni rahisi kwa taarifa zake kuvuja kupitia koneksheni za nje ya nchi.

Baada ya dokta Bridge  kufikiria kwa muda alitoa maagiizo ya  Hamza kupewa taarifa za kimatibabu za  mtoto wake  Christian, Hamza mara baada ya kupitia pitia ikiwemo picha za  CT Scan  macho yake yalionekana  kama mtu anaefikiria jambo  kwa kina.

“Kwa ripoti hii hakuna kitakachofanikiwa”Aliongea Hamza.

“Unasemaje wewe , nini hakiwezi kufanikiwa” Dokta Bridge alimaka.

“Huyo  dokta wako unaemuita  Profesa Salazer  ametumia  njia rahisi sana ya kubadilisha Aortic Valve na kuweka bandia,  lakini hata kama akifanikiwa  katika hili  Christian hali yake itakuwa mbaya zaidi  na anaweza kupoteza maisha  siku chache baada ya upasuaji”Aliongea Hamza , ukweli ni kwamba haikueleweka  Hamza ni dokta kweli au anataka  kujipatia sifa  kwa kuhatarisha maisha ya mgonjwa.

Lakini watu wote waliokuwa ndani ya hilo eneo ni kama hawakumwelewa, hata Eliza  hakuelewa na hakuongea  chochote  licha ya kuwa na mshangao wa kutotaka kuamini Hamza ni daktari, katika mawazo yake Hamza asingeweza kuwa dokta kwa umri  wake aliokuwa nao , maana madaktari wa moyo walikuwa wakisoma zaidi ya miaka kumi na tano mpaka kuwa bingwa ,  udaktari wa aina hio sio swala pekee la kuwa na akili nyingi bali ni swala la kuwa na uzoefu.

“Dokta Bridge , kama unataka mtoto wako  kupona  basi ni vyema kama  utafanya maamuzi  haraka na  upasuaji kusitishwa  na mimi kuendelea nao”

“Unaongea kichekesho gani , wewe ni  nani mpaka kwa maneno yako  tu  tumsitishe Dokta Salazer kuendelea na upasuaj, unajua nimelipa bilioni ngapi na koneksheni  kubwa kiasi gani kumshawishi  Dokta Salazer kuja kufanya upasuaji wa siri hapa Tanzania?”Aliongea huku awamu hio akifoka.

“Since I dared to say that , I  naturally have my   own  reasons , if  you don’t  believe me  , you can let  me confront  that professor  and see what he’ll say”Aliongea Hamza  akimaanisha kwamba kwasababu  ana ujasiri wa kusema hivyo basi ana sababu zake  na kama haamini ampe nafasi ya  kuongea na  Profesa anaefanya upasuaji aone ataongea nini.

*****

Masaa nane baadae  jina la Hamza lilibadilika  moja kwa moja , kila mtu alikuwa akimwita Dokta  Hamza Mzee , Eliza  hata yeye  alishangazwa  na uwezo wa Hamza katika wakati wote alioshuhudia akifanya upasuaji  na kuelekeza manesi na watu wa ganzi nini cha kufanya.

Ukweli  ni kwamba Dokta Bridge hakumwamini kabisa Hamza kwenye maswala ya upasuaji na hakutaka  kumruhusu  Dokta Salazer  amwachie Hamza , hivyo alimwambia  Hamza aangalie upasuaji unavyoendelea na atoe ushauri  kwa Dokta Salazer  ikionekana amekosea.

Lakini sasa   upande wa Dokta Salazer ambae   aliongea na Hamza kabla ya kuendelea na upasuaji alikasirika sana , kwake alichokuwa akifanya Hamza alikuchukulia kama tusi kwa utaalamu wake  aliojijengea kwa muda mrefu ,  alikuwa ni daktari bingwa na sio mtoto kama alivyokuwa akionekana  Hamza.

Lakini  Hamza upande wake hakutaka kuonekana  mtoto , aliongea kwa kutoa sababu  kwanini  mpango wa upasuaji anaoendelea nao hautofanikiwa,  lakini licha ya hivyo dokta huyo  alipandisha mabega  na kuamua kutumia  uwezo wake wote kutaka kumuonyesha Hamza kwamba yeye ni mzoefu na hajabahatisha kupata cheo cha  uprofesa , lakini masaa sita mbele hali ya mgonjwa ilibadilika ghafla na moyo  uliacha kudunda kiasi cha  kuanza  kuhangaika kuurudisha hai kwa kutumia electrical  plate kwa ajili ya kuushitua na  hata kuufanyia masaji  kwa mkono.

Kitendo kile kilimfanya  Dokta Salazer  kuachia  nafasi yake kwa Hamza kwa maagizo kutoka kwa Dokta Bridge ,  Hamza alikuwa amekwisha kujiandaa muda mrefu  kuvaa Scrub  na hata kujisafisha  hivyo baada ya kuachiwa uwanja alionyesha maajabu  ambayo yalimuacha mdomo wazi. Hamza alifanya upasuaji  kama vile alikuwa na uzoefu wa miaka hamsini.

Dokta Salazer akili yake haikutaka   kuamini  kwa umri  aliokuwa nao Hamza ameweza kusoma  masomo ya  udaktari kuhitimu  na kisha kujijengea uzoefu.

Hamza hakujali alikuwa akiangaliwa kwa macho ya mshangao, kwa spidi yake ya upasuaji , wala hakujali  Eliza ambae alikuwa kwenye mshituko akiwa haamini  ni Hamza aliekuwa akicheza na mikasi ndani ya  chumba cha upasauji ,  mchakato ambao  ulipaswa kufanyika kwa masaa  saba Hamza aliufanya kwa masaaa  matatu na nusu  pekee.

Mpaka anakwenda kumaliza  Profesa Salazer alijiktua akimwangalia Hamza kwa macho yaliojaa maswali, hakuwa na mshangao  lakini alikuwa na maswali, ni kama vile kuna kitu ambacho alikuwa akijaribu kukitafuta kutoka kwa Hamza.

“Hapana, haiwezekani   uzushi niliowahi kusikia ukawa kweli, huo muonekano unaendana  na mwili wake haiwezekani akawa na miaka mingi  tofauti na mwonekano wake”Alijiwazia Profesa  Salazer huku akimwangalia Hamza kama kiumbe cha ajabu.

Kwa mtu  ambae angeweza kujua mawazo aliokuwa nayo Dokta Salazer basi  pengine angeonekana  amepandwa na ukichaa, lakini  kwa upande wake licha ya upasuaji huo kuisha  hakutaka kukubali kirahisi  na mpango mpya  wa kufuatilia  kile alichokuwa akiwaza  ulianza  kwanzia dakika hio hio.

Ilikuwa ngumu kwa Dokta ambae alikuwa akiaminiwa  na  nchi  nzima  ya Italy  kushindwa  na mtu aliechanganya rangi kama Hamza ambae hana  kitu  kisichokuwa cha kawaida cha kutisha.

Upande  wa Hamza hakujua kama  kuonyesha ujuzi wake ambao hautabiriki,ulikuwa umeibua kitu kingine katika kichwa cha Muitali Dokta Antonnio Salazer Slytherin.

*******

Asubuhi  siku iliofuata  Eliza na  Hamza walianza safari ya kurudi Dar Es salaam, isitoshe wote walikuwa na kazi za kufanya kwa siku hio  na isingekuwa vizuri kuchelewa.

Kuhusu baba yake Eliza aliachiwa huru na  Dokta Bridge alikubali kufuta deni kutokana  na kile  Hamza alichofanya.

Hamza alipata nafasi ya kujitambulisha kwa baba yake  Eliza  na mzee huyo mara baada ya kusikia Hamza ndio  kasababisha  kuachiwa huru  alimshukuru sana.

Eliza  hatimae alijihisi kuwa huru kwa mara ya kwanza na amani kumrudia, ijapokuwa  haikuwa vizuri kufurahia  matatizo ya binadamu mwenzake  lakini bila ya kupenda taarifa za  Mzee Gabusha kuwa mgonjwa  mahututi aliekufa ubongo kutokana na kupata ajali  zilimpa amani.

Saa tatu asubuhi muda ambao Hamza alikuwa akitoka kwenye treni ya mwendokasi akifikiria kuchukua taksi kumpeleka  kwenye kampuni , simu yake iliita na  alivyoangalia aliekuwa akipiga ni  Shangazi.

“Hamza upo wapi?”Ndio kitu cha kwanza alichoweza kusikia Hamza huku sauti ya Shangazi ikionyesha kuwa na utofauti.

“Nipo nje ya stendi ya  treni ya mwendokasi Posta  nataka nielekee kazini,nini  kimetokea shangazi?”

“Madam.. ametutoka” Sauti  ya Shangazi ilionyesha alikuwa akishindana na majjonzi.

Hamza alishikwa na mshituko  kwa sekunde kadhaa  licha ya kwamba ni kitu ambacho alitarajia.

“Regina anafahamu?”

“Ndio maana nimekupigia , nimeshindwa kumpata kwa simu  na nyumbani hayupo, nilijua upo nae”Aliongea  Shangazi na kauli ile ilimpa mshituko Hamza na kujua lazima kuna kitu kilichomtokea Regina.

Previoua Next