FOR YOU 2
A Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA KUMI NA TATU
★★★★★★★★★★★★★★★★★
Taarifa za kuuawa kwa Oscar ziliwafikia viongozi wale wafisadi na waovu, yaani Raisi Paul Mdeme, Jenerali Jacob Rweyemamu, Luteni Jenerali Weisiko, na wale wengine kwenye muungano wao wenye kufanya na kuficha maovu. Raisi Mdeme alikasirishwa kwa kadiri kubwa na kuwajulisha wawili hao kuwa nafasi kama hiyo ilitakiwa kuwa yenye matokeo mazuri, yaani Oscar akamatwe akiwa hai ili waweze kumbana vyema kusema wenzake wako wapi. Mdeme alichoambiwa ni kwamba, wakati walipofanikiwa tu kumkamata Oscar, wenzake walitokea na kumuua ili asije kuwafichua, kisha wakatokomea. Kwa hiyo Raisi huyu akawaambia wakuu hawa wa kijeshi wahakikishe watu wao wanafanya mambo kwa umakini zaidi ili kupata matokeo aliyotaka.
Lakini Mdeme alifichwa ukweli muhimu na Jenerali Jacob pamoja na Weisiko. Kumbuka wawili hawa walikubaliana kwamba hawangeruhusu yeyote kati ya watu kutoka kundi la Mess Makers akamatwe na watu ambao hawakujua siri zao (watu kama Luteni Michael na timu yake), ijapokuwa Raisi Mdeme yeye alichukulia mambo kijuujuu tu na kulazimisha watumie njia hiyo kuwakamata (yaani timu ya Luteni Michael na ACP Nora), kwa hiyo Jenerali Jacob na Luteni Jenerali Weisiko waliamua kwamba wangeiweka "silaha" fulani muhimu ya Weisiko kuifatilia timu ya Luteni Michael, ili wakiwakaribia tu Mess Makers, "silaha" hiyo iwe ya kwanza kuwashika na kuwanyonya ukweli, la sivyo iwaue kabla ya Luteni Michael na wengine kuupata.
Silaha hiyo, ndiyo yule mtu asiyefahamika ambaye alimuua Oscar usiku ule, pamoja na wanajeshi wale watatu wa timu ya Luteni Michael.
Kwa hiyo, "silaha" hiyo, au "silaha" huyo, alirudi kwa Weisiko na kumwambia hakufanikiwa kumkamata Oscar kwa wakati, kwa hiyo akamuua. Baada ya Weisiko kuwa amemjulisha Jenerali Jacob juu ya hilo, akampongeza kwa kazi hiyo na kumwambia aendelee kuwa chonjo nao kwa sababu bado Luteni Michael na timu yake wangeendelea na msako huo, hivyo "silaha" angepaswa kuwa karibu endapo wangefanikiwa kuwapata Mess Makers ili awepo kufanya yake.
Jenerali Jacob na Weisiko wakaendelea kuwa na ukaribu wao ambao tokea zamani uliwapa nguvu, huku Raisi Mdeme akidhani bado wanafuata tu njia yake kwa utiifu, kumbe ni wanafiki wakunjufu.
★★★
Maandalizi kwa ajili ya msiba wa wanajeshi wale watatu, Mishashi, Vedastus na Omari, yalikamilika na kufanyika siku mbili baada ya kuuawa kwao. Wangepatiwa heshima na utambuzi mkubwa nchini kwa kuwa walionekana kama wajitoaji muhimu kwa nchi yao mpaka kufikia kifo kwenye vita hii iliyokuwa ikiendelea baina ya serikali na Mess Makers. Wanafamilia, marafiki, viongozi mbalimbali wa usalama wa taifa pamoja na makamu wa Raisi wangekuwepo hapo, na vyombo vya habari vilirusha kipindi maalumu cha kuwaaga "wazalendo" hao.
Luteni Michael alikuwa mwenye hasira sana kutokana na jambo lililowapata watu wa timu yake, na aliona ni kama msiba huu ulikuwa ni matangazo tu yasiyokuwa na maana yoyote kwa sababu aliamini njia sahihi ya kuwaenzi watu wake hao ilikuwa ni kuwakamata Mess Makers. Alikuwa anataka kuwaua yeye mwenyewe, lakini pia alielewa kazi yake ilimtaka kuwakamata wakiwa hai kwanza. Ijapokuwa wengine wangekwenda msibani, yeye alikuwa akifanya utafiti peke yake wa matukio ya usiku ule ili abaini mambo haraka, na hivyo kuweza kuwalipizia kisasi watu wa timu yake.
Maneno mengi sana yalisemwa kuhusu jinsi ambavyo Mess Makers wameendelea kuua watu wasio na hatia na uhakika wa kuwakamata. Picha ya Oscar ilitumiwa kama onyesho la mafanikio katika kulikaribia kundi la Mess Makers, kwamba muda si mrefu wote waliokuwa pamoja naye wangekamatwa, kisha aidha kufungwa au kupewa hukumu ya kifo kutokana na mabaya waliyoiletea nchi.
Baada ya pindi maalumu za msiba kuisha, ACP Nora alijiunga pamoja na Mario, Hussein, Alex, na Bobby, kwenda kwa Luteni Michael ili kuendelea na utafiti. Ilikuwa bado ni kwenye jengo lao lile lile, nao wakaanza kujadiliana naye kuhusu hatua ambazo zingefuata. Nora tayari alikuwa ameyarudisha mafaili yale yenye taarifa za watu waliojeruhiwa kwenye bomu kwa daktari Shani, naye alimshukuru kwa hilo na kumpa pole ya msiba wa rafiki zake. Luteni Michael alionekana wazi kuwa amevunjika moyo ijapokuwa hakukata tamaa. Wengine walijitahidi kufuata maagizo yake na kuangalia kila njia mpya ya kubaini lolote kuhusu Mess Makers, lakini wakashindwa kupata lolote lenye kuwasaidia.
Kwa hasira nyingi, Luteni Michael alianza kupiga vitu kwa nguvu na kurusha maboksi yenye vifaa mbalimbali chini. Alihisi ni kama sasa wasingeweza kuwapata watu hao maana walijificha kwa njia iliyokuwa ngumu sana kufichua. Akawaambia wanajeshi wake pamoja na Nora waondoke tu na kwenda kupumzisha akili na mwili mpaka muda fulani ambao ungefaa siku ya kesho ili wajadili mambo kwa njia nzuri zaidi. Hakuwaambia hakuwa sawa kihisia, ila wote walielewa hiyo ndiyo iliyokuwa sababu.
Wanajeshi wa timu yake wakaondoka tu, na hapo akabaki Luteni Michael na Nora pekee.
"ACP... nafikiri umenisikia niliposema mnaweza kwenda. Mbona umebaki?" Luteni Michael akauliza huku akisoma jambo fulani kwenye makaratasi.
"Siyo makosa yako," Nora akamwambia kwa sauti yenye kujali.
"Nini?"
"Kilichowapata... siyo makosa yako," Nora akasema.
Luteni Michael akamtazama kiufupi, kisha akasema, "Nenda karukeruke kidogo popote ujuapo ili ukirudi ufanye kazi kwa njia ambayo itasaidia makosa mengine yasitokee. Ondoka... kapumzike ni usiku sasa."
Nora akamwangalia tu kwa huruma kiasi. Alielewa mwanaume huyo alikuwa kwenye hisia kali za hatia ijapokuwa alijitahidi kuonyesha yuko imara. Kwa kuelewa kwamba alichohitaji ilikuwa ni kuachwa peke yake, akaridhia tu kwamba kumwacha kwanza ilikuwa jambo la busara.
"Okay. Nikirudi bila shaka nitakuwa nimepata jambo lingine la kufanyia kazi. Usiku mwema," Nora akasema, kisha akaanza kuondoka.
Luteni Michael akamtazama tu mpaka alipotoka ndani ya jengo, naye akaketi kiuchovu na kufunika uso wake kimasikitiko. Alijisikia vibaya kutokana na yote yaliyotokea, lakini hata zaidi alijihisi vibaya kwa kumsemesha Nora kwa njia ambayo hakuona inafaa.
Kufikia wakati huu alikuwa amejenga upendezi mwingi kumwelekea mwanamke huyo ijapokuwa hakuonyesha wazi jambo hilo, na sasa akawa anafikiria huenda ingempa faraja kwa kadiri fulani kama angefunguka kwake. Akanyanyuka na kwenda mpaka nje kwenye gari lake, akiwa ameamua kumfuata Nora kule kule kwenye chumba chake cha hoteli ili aongee naye. Hakujua itikio la mwanamke huyu lingekuwaje, kwa hiyo alijiweka tayari kwa lolote na kuiridhisha nafsi yake kuwa angekubali matokeo; mazuri au mabaya.
Aliendesha gari lake mpaka maeneo ilipokuwepo hoteli alikopanga Nora, lakini aliishia mbali kidogo kuifikia baada ya kukuta kundi la watu nje hapo wakionekana kama wamezunguka tukio fulani. Akashuka na kwenda pale ili kujua ni nini kilikuwa kinaendelea, naye akalikuta gari la Nora likiwa limeegeshwa upande huo na mlango wa mbele ukiwa wazi. Walinzi wawili wa jengo la hoteli hiyo walikuwa wakizuia mtu yeyote asiliguse gari hilo mpaka polisi wafike, naye Luteni Michael akawakaribia na kuwauliza nini kilikuwa kimetokea.
Walimweleza kwamba wakati ACP Nora alipokuwa tu amefika hapo, lilikuja gari fulani kama hiace lenye rangi nyeusi, na wanaume kadhaa wakashuka na kumkamata Nora kisha kumwingiza ndani yake kwa lazima, na kutokomea kusikojulikana. Luteni Michael aliwauliza kiukali walikuwa wanafanya nini mpaka wakaruhusu mtu anatekwa kirahisi sana, nao wakamwambia walikuwa kwenye kazi zao hivyo hawakuweza kutenda kwa uharaka kwa sababu watu hao walishtukiza sana.
Baadhi ya walioshuhudia jambo hilo walikuwa wanasema Nora alishuka, kisha wanaume hao wakaja haraka na kuanza kumvuta kwa nguvu lakini akawa akijitahidi kujinasua, ndiyo wakampiga na kumfanya apoteze fahamu, kisha wakamwingiza na kuondoka naye. Luteni Michael alikasirika sana, huku hofu ikimpanda kwa wakati huo huo. Akauliza ulikuwa umepita muda mrefu kadiri gani tokea jambo hilo lilipofanyika, na washuhuda wakasema zilikuwa zimepita kama dakika 25 hivi.
Upesi Luteni Michael akampigia Bobby na kumjulisha yaliyotokea, naye akamwambia atumie utaalamu wake kufatilia Nora alikopelekwa kisha amwongoze ili aende huko. Bobby akakubali na kusema angewaambia na wengine ili wachangamke kwenda kumuunga mkono na kumpatia dada wa watu msaada. Mambo yalikuwa yanazidi kwenda vibaya upande wa Luteni Michael aisee. Alikuwa tu ametoka kuwapoteza watu muhimu sana ambao alifanya nao kazi kwa miaka mingi, na sasa ikiwa angempoteza mwanamke aliyekuwa ameanza kumpenda, asingejisamehe kamwe.
Akaondoa gari kwa kasi sana kuelekea upande ambao Nora angekuwepo.
★★★
Ikiwa ni saa nne ya saa tano usiku sasa, Nora aliamka akihisi maumivu makali kichwani kwake. Alihisi pia kama yuko mwendoni, na kwa haraka akatambua alikuwa ndani ya gari. Alipoanza kuangalia ndani hapo, akatambua alikuwa katikati ya wanaume kadhaa walioketi siti za kando huku wakiongea mambo yasiyoeleweka kwake. Alihisi kizunguzungu kikali pia, akiwa kama ametoka kunywa pombe iliyomlewesha kupita maelezo.
Gari lilisimama hatimaye, naye Nora akahisi aliposhikwa na kuanza kutolewa nje. Maumivu kichwani yalikuwa makali, lakini akajitahidi kukisawazisha kidogo na kukaza meno yake ili atafute njia ya kutoroka. Wanaume wawili waliokuwa wamempa egamio ili atembee walikuwa wakisema kwamba wenyewe ndiyo wangeanza kwanza, tena kwa matundu yote mawili kwa wakati mmoja!
Nora akatambua kwamba hawa watu walikuwa na nia ya kumbaka, lakini kutokana na jinsi walivyokuwa wamemkamata ilionyesha walikuwa wamejipanga sana, hivyo labda nia yao nyingine baada ya kumfanyia ubaya huo ilikuwa ni kumuua. Wazo la kwamba huenda walikuwa ni Mess Makers ndiyo wanafanya hivi ili kulipa kisasi kwa ajili ya kifo cha mwenzao lilimwingia, naye akaona ilikuwa lazima atoroke haraka kwa sababu maisha yake yalikuwa hatarini.
Kwa kasi, akajinasua na kuwapiga wanaume hao wawili sehemu zao za siri na kuanza kujitahidi kukimbia. Wale wengine walikuwa wametangulia mbele kidogo, hivyo wakaanza kumkimbiza haraka na kufanikiwa kumshika. Alikuwa anajitahidi kurusha ngumi na mateke ili kujinasua kwa uwezo wake wote, lakini mmoja wa wanaume hao akampiga ngumi kwa nguvu sana tumboni na kumfanya Nora alegee mno. Alihisi kuishiwa nguvu, akaanguka akiwa analia kwa maumivu. Wanaume hao wakaanza kucheka na kuwatania wenzao waliopigwa na Nora, kisha wakamnyanyua mwanamke huyu juu na kuanza kumpeleka ndani ya jengo lililokuwa hapo.
Nora alijitahidi sana kujikaza kutokana na maumivu aliyohisi kichwani na tumboni, na kwa haraka akagundua kwamba hapo alikuwa ametekwa na wanaume saba. Walimwingiza ndani ya jengo hili ambalo lilikuwa ni ghorofa linalofanyiwa ujenzi, likiwa limefunikwa kwa neti ndefu za kijani kulizunguka kutokea juu mpaka chini kwa nje, na mbao za kupandia juu za mafundi zilikuwepo bado. Walimpeleka mpaka kwenye ghorofa ya nne, kukiwa na giza, lakini mwanga hafifu wa taa za kutokea jijini ukifanya vitu vionekane kwa mbali. Pembeni mwa jengo hili ulikuwa ni mnara mrefu wa mtandao wa Vodacom, hivyo kufikia ghorofa ya nne ya jengo hili ilikuwa ni kama wamefikia nusu ya mnara huo.
Wanaume wawili waliokuwa wamembeba Nora, wakamshusha na kumweka tu chini, kisha wakarudi nyuma kusimama na wenzao huku wakimwangalia kwa hila. Nora akawa akijivuta-vuta chini hapo kwa kurudi nyuma, akiwa na hofu kwa kadiri fulani. Mmoja wao akamsogelea na kuchuchumaa karibu yake, kisha akamshika kwenye goti la mguu, naye Nora akaikunja miguu yake na kujirudisha nyuma tena.
"Usigope mrembo... sisi hatutakuumiza. Tunataka tu kucheza," mwanaume huyo akasema.
"Mnataka nini? Nani amewatuma? Nyie ni Mess Makers?" Nora akauliza kwa sauti tetemeshi.
"Ndiyo... sisi ni Mess Makers..."
Mwanaume huyo akasema hivyo na kufanya wenzake wacheke.
"Wewe mtoto mzuri namna hii unafanya nini polisi? Hizo kazi ungewaachia wale wanawake wanene tu ndiyo huwa zinawafaa... wewe ungekuja kwangu tu..."
"Nisikilize. Mimi ni askari. Unajua mtapatwa na mambo mabaya mkinifanyia ujinga. Naomba mniachie..." Nora akasema kwa ujasiri.
"Unataka tukuachie? Sawa. Tutakuachia. Lakini lazima kwanza tucheze..."
Mwanaume huyo akamwambia hivyo na kumshika sehemu ya paja. Nora alipojirudi nyuma, akagusa kitu alichotambua kuwa ni mbao, naye akatulia kidogo.
"Hapa tuko wengi, na hauna ujanja. Ikiwa wewe ni mtu mwenye akili kama wanavyokutangaza, utajiachia kwetu tufanye yetu. Baada ya hapo labda ndiyo tutakuachia," mwanaume huyo akamwambia.
"Kweli?" Nora akauliza.
Wanaume wale wengine wakacheka.
"Ndiyo, kweli kabisa..."
"Kwa hiyo... mnataka... niwape... nyie wote?" Nora akauliza.
"Vyovyote utakavyopenda mrembo..."
"Lakini mko wengi," Nora akasema.
Wote wakacheka sana.
"Basi tutafanya mmoja baada ya mwingine..."
"Lakini... kama ndiyo hicho mlichokuwa tu mnataka... si mngechukua slay queen huko, kwa nini mimi?" Nora akauliza kijanja.
"Sikia. Wewe hapa ulikuwa ni kufa tu. Lakini sisi tunakuonea huruma. Acha maswali, anza kuvua nguo. La sivyo tutakutupa kutokea hapa mpaka chini, umeelewa?"
Nora sasa akawa ametambua kuwa hawa walikuwa wametumwa na mtu fulani kumfanyia ubaya, siyo kwamba labda wao ndiyo walikuwa wana nia mbaya naye moja kwa moja.
"Nani amewatuma?" Nora akauliza.
"Hujanisikia? Nimekwambia..."
"Okay, okay, nimeelewa. Naombeni tu nwelewe kwamba nina maumivu maana mmenipiga kichwani na tumboni, kwa hiyo inabidi nijiandae," Nora akasema.
"Dah, hivi huyu demu yuko serious kweli?" mmoja wa wale wanaume akauliza.
Yule mwanaume aliyekuwa karibu na Nora akamgeukia mwenzake ili atoe jibu, na hapo hapo Nora akavuta ubao ule na kumtandika nao sehemu ya mgongoni. Mwanaume huyo akatoa sauti ya maumivu kidogo na kuangukia pembeni, naye Nora akajitahidi kusimama huku akiwa ameushika ubao ule. Wale sita wengine wakaanza kumzunguka polepole huku yeye akirudi kinyume-nyume, akiwaonyeshea ubao kuwa yeyote akimsogelea atampiga.
"Bado una kiburi kumbe?" mmoja akasema.
"Kaeni mbali nami. Nitawaua wote," Nora akasema kwa ujasiri.
"Basi anza na mimi..." mwingine akasema na kumfata kwa kasi.
Nora akampiga na ubao huo kwa nguvu begani, na mwingine alipomsogelea akampiga tumboni. Hapo hapo mwingine akawa amemshika kwa nguvu, nao wakaanza kurudi ovyo ovyo nyuma kwa sababu ya Nora kujaribu kujinasua. Mwanaume huyo akamsukuma kwa nguvu mpaka sehemu ya ukutani na kufanya Nora ajibamize uso wake kwa nguvu, naye akaanguka chini huku wanaume hao wakimcheka.
"Tunapenda sana wanawake wanaojua kupambana..." mmoja wao akasema.
Yule mwanaume aliyekuwa amepigwa kwa ubao mara ya kwanza akawasukuma wenzake pembeni ili awe wa kwanza kumtendea Nora vibaya kimwili, na wenzake wakawa wamemzingira Nora ili asiponyoke. Mwanaume huyo akatoa bastola kutoka nyuma ya kiuno chake na kumwonyeshea Nora, kisha akampa mwenzake na kutoa ishara kwa wengine kwamba wamshikilie Nora ili amwingie kwa nguvu kimwili.
Wanaume watano wakamfata Nora, wakamshika na kumlaza chini kwa nguvu, wawili wakiwa wameishika mikono yake na wengine kuisambaza miguu yake. Mmoja wao alikuwa akiivuta suruali yake Nora ili kuitoa yote, huku mwanamke huyu akipiga kelele za kuomba msaada na machozi yakimtoka. Yule aliyekabidhiwa bastola akatoa kitambaa na kwenda kumfunika mdomo kwa nguvu, kisha akakifunga nyuma ya shingo yake. Nora alikuwa akilia kwa hisia sana, na hatimaye wanaume wale wakafanikiwa kuitoa suruali yake yote, wakimwacha na chupi nyeupe tu.
"Wow! Mtoto msafi wewe! Yaani unanukia kila kona siyo kama yale manyanya ya traffic yanayonuka mijasho tu," mwanaume huyo akasema huku akifungua suruali yake, na wenzake wakawa wanacheka.
Mwanaume mmoja akataka kuitoa na chupi ya Nora, lakini huyu aliyetaka kuanza kumwingia akamzuia.
"Nataka niitoe mwenyewe, wewe shika mwili huo asifurukute," mwanaume huyo akasema.
Nora akawa analia tu huku anatikisa kichwa kumwonyesha mwanaume huyo kwamba asifanye hivyo, naye jamaa akawa amemaliza kuitoa suruali yake na kuvua boxer pia. Akawa anaitingisha-tingisha kichokozi mashine yake iliyosimama kumwelekea Nora, na wenzake wakawa wanacheka.
"Ila bro, faster. Hatuna muda mwingi wa kupoteza," mmoja wa wale wanaume akamwambia.
Jamaa akaanza kumkaribia Nora ili afanye yake, pale kishindo fulani kilipotokea sehemu ya nje upande ambao ulikuwa na mbao za mafundi za kupanda juu. Wote waliangalia upande huo, lakini ni upande ambao walikuwa wameupa visogo ndiyo akatokea mtu fulani aliyeingia kwa kasi sana na kupita katikati yao mpaka sehemu ya pembeni, akijiviringisha chini na kunyanyuka juu; akiwa amesimama kwa kuwapa mgongo.
Wote walishtushwa na hilo, lakini kilichofuata kuwashtua hata zaidi ni sauti ya kilio cha maumivu kutoka kwa yule jamaa aliyetaka kumwingia Nora kinguvu. Walipomwangalia, wakakuta hana uume! Yaani ulikuwa umekatwa kabisa na kubakiza damu tu zilizoruka-ruka kama maji kwenye bomba lililopasuka. Mtu huyo aliyeingia hapo ghafla alikuwa amepita na uume wa jamaa kwa kutumia kisu kwa kasi aliyoingia nayo, na wanaume wale wengine wakamwachia Nora na kubaki kumwangalia mwenzao akilia kwa maumivu sana huku akigaagaa chini.
Nora alijivuta nyuma na kuegamia ukuta, akimwangalia mtu huyo aliyekuwa amesimama huko mbele. Alionekana kuvaa nguo nyeusi mwili mzima na kificha uso kichwani kilichoacha sehemu ndogo tu ya mdomo wake. Kwa haraka akawa amemtambua mtu huyo, kwamba ndiye yule ambaye alikuja na wenzake kumwokoa Kevin Dass usiku ule walipofanikiwa kumkamata kule Mwanza. Wale jamaa wengine wakajiweka tayari kimapambano, huku yule aliyekuwa amekabidhiwa bastola na huyu aliyekatwa uume akiitoa na kumnyooshea mgeni aliyeingia.
"Unasubiri nini? Mpige risasi!"
Mmoja wao akasema hivyo kwa sauti, na hapo hapo jamaa akaanza kufyatua risasi kuelekea sehemu za mgongo na hata miguu ya mtu huyo. Alipiga risasi kama 9 hivi, kisha bastola ikawa tupu. Wanaume wote walibaki kushangaa tu mtu huyo akiwa amesimama tuli wakati alikuwa ametoka kumiminiwa risasi mwilini, lakini Nora alielewa wazi kwamba nguo aliyovaa ilizizuia risasi hizo. Kisha mtu huyo ambaye hakufahamika kwa yeyote ndani hapo, akakitupa kisu alichokuwa amekishika, naye akajisawazisha na kuwatazama kwa utayari.
Wanaume wale wakaambiana kwa kuamrishana kuwa wamfate na kummaliza kwa mikono yao wenyewe, kwa kuwa alikuwa peke yake, hivyo ikaonekana kwamba wangemshinda nguvu. Kichwa kichwa tu wakaanza kumfata kwa kasi ili wamshambulie, lakini akawakwepa kwa mitindo ya sarakasi na kuingia katikati yao, kisha kutokea mpaka sehemu ambayo Nora alikuwa amejiegesha. Wanaume wale waligeuka nyuma, na mmoja akamwahi mtu huyo ili ampige, lakini akaikunja-kunja mikono yake na kuivuta kwa nguvu sana pande mbili tofauti, kitu kilichofanya aivunje-vunje mifupa yake kuanzia mikononi mpaka mabegani. Jamaa akatoa kilio cha maumivu kwa kulemazwa mikono sasa, na mtu huyo akamsukuma pembeni kama mzigo wa uchafu.
Wengine wawili wakamrukia, lakini mtu huyo alikuwa na njia fulani ya kukwepa ambayo ilimstaajabisha sana Nora. Akavipigisha vichwa vyao kwa nguvu sana uso kwa uso na kufanya wavunjane pua, na wakati huo huo mwingine aliyemkaribia akamtandika teke shingoni kwa kuruka sarakasi ya nyuma, na alipotua akaisambaza miguu yake chini kwa msamba na kuizungusha ili amkate mtama jamaa mwingine.
Aliwachangamkia kwa kasi sana wanaume hao na kuwapiga kwa kuwachanganya mno, na mmoja wao akakiokota kisu kile ambacho mtu huyo alikitupa chini, kisha akamfata ili amchome lakini akaambulia kuzungushiwa mkono wake yeye mwenyewe na kujichoma mdomoni. Wengine hawakuwa hata na muda wa kushangaa, na tayari mtu huyo akawa amemchana sehemu ya kitovu mwanaume mwingine na kufanya utumbo wake mwingi umwagike chini.
Nora alihofishwa kwa kiasi kikubwa na mauaji hayo yaliyotokea mbele yake. Wanaume wawili wakamkamata mtu huyo na kumng'ang'ania kwa nguvu, kisha yule aliyebaki akaanza kumfata ili amwangamize, lakini mtu huyu akainyanyua miguu yake juu na kudunda kwenye kichwa cha jamaa aliyekuwa anamfata na kujibinulia nyuma ya wale waliokuwa wamemshikilia, nao wakajitoa kwake kwa kukosa mhimili mzuri.
Walipojisawazisha tu, mmoja akashtukia anapigwa ngumi ya tumboni, lakini maumivu yalikuwa ni makali sana kwa sababu mkono wa mtu huyo uliompiga ulikuwa bado na kisu kile, kwa hiyo kiliingizwa mpaka ndani ya tumbo lake kama vile kupigilia msumari wote ndani ya ukuta. Akaanguka chini akiwa amejishika tumbo bila kutoa sauti yoyote kwa kuhisi maumivu makali yaliyofanya koo yake ikaze, na yule wa pembeni akamrukia mtu huyu ili ampige kichwani kwa uchuma wa bastola ile tupu aliyoiokota chini, lakini mtu huyu akamkwepa na hapo hapo kukishika kichwa chake na taya kwa kuizungushia mikono yake kinyume, halafu akaivuta mikono kwa nguvu na kufanya shingo ya jamaa inyongwe kwa njia iliyofanya uso wake ugeukie mpaka mgongoni!
Mwanaume huyo akadondoka chini na kuanza kushtuka-shtuka mwilini sana, naye Nora akawa akisikia jinsi mtu huyo aliyemnyonga jamaa alivyopumua kwa nguvu.
Kisha mtu huyu akamwangalia yule jamaa mwingine aliyebaki, ambaye alikuwa kasimama tu akionekana kuogopa. Akaanza kurudi nyuma na kugeuka ili akimbilie sehemu iliyokuwa kwa ajili ya mlango ili atoroke, lakini mtu huyu akaokota bastola ile na kumponda kwa nguvu sana nyuma ya kichwa chake, kitu kilichofanya jamaa aweweseke na kujigonga ukutani. Mtu huyo akamfata pale chini, na bila kukawia akamkanyaga nyuma ya shingo na kuikandamiza kwa nguvu sana mpaka ulimi wote wa mwanaume huyo ukatoka nje ya mdomo wake!
Nora alikuwa ameghafilika haswa. Alipatwa na mshtuko mkubwa sana kiasi kwamba alikuwa ametulia tuli tu kama vile hayuko hapo. Mtu huyo akageukia upande wa Nora, naye Nora akatambua kwamba alikuwa anawaangalia wanaume wale waliolala pale chini. Kati ya wanaume wote saba, ni wawili tu ndiyo bado walikuwa hai; yule aliyekatwa uume, na yule ambaye alivunjwa mikono mapema kabisa.
Mtu huyo akaanza kutembea kumwelekea yule aliyemvuja mikono, naye jamaa alipoona anafuatwa, aliingiwa na nguvu fulani mpya iliyomfanya anyanyuke hivyo hivyo huku mikono yake ikiwa imelegea kama mikono ya mashati ya Brother-K, naye akawa anarudi kinyume-nyume kwa kuogopa sana. Mtu huyo akawa anamfata taratibu tu, akijua kwamba woga wa mwanaume huyo ulimaanisha kifo chake mwenyewe kwa sababu alikuwa anarudi nyuma bila kutambua kwamba alielekea sehemu yenye uwazi mwishoni mwa chumba hicho, na kufikia hapo mwishoni jamaa akaanguka mpaka kule chini bila hata kusukumwa!
Hiyo ikamwacha mzee wa uume-mkato pale chini, akiwa anaugulia maumivu tu huku damu nyingi ikiwa imemtoka, na mtu huyo akamfata mpaka hapo na kuchuchumaa karibu yake. Jamaa akaomba apelekwe hospitali eti, akisema yeye hana makosa kabisa. Mtu huyu akatoa kitu fulani kutoka kwenye nguo aliyovaa, kisha akamziba pua jamaa kwa vidole na kumwekea kitu hicho mdomoni mwake. Akaiachia pua yake, naye jamaa akaanza kutetemeka sana huku akiwa kama anataka kukohoa lakini anashindwa. Ilikuwa ni sumu ndogo tu kama kidonge ambayo ilienda kukatakata ogani ndani ya mwili wa jamaa, kifo cha taratibu chenye maumivu ambacho angekisikilizia vizuri kabisa.
Mtu huyo akasimama na kuanza kumfata Nora mpaka alipokaa. Nora alikuwa hata hajatoa kitambaa kile ambacho wale wanaume walitumia kuufunga mdomo wake ijapokuwa mikono yake haikuwa imefungwa. Yaani ni kama nguvu zilikuwa zimemwishia kutokana na yote yaliyokuwa yamefanyika kufikia sasa, naye akabaki kumwangalia tu mtu huyo kama anasubiri zamu yake ya kuuawa ifuate. Mtu huyu akachuchumaa karibu na Nora, akionekana kama anamwangalia.
Kwa ukaribu huo, Nora aliweza kuiona vyema sehemu ya usoni ya mask aliyoivaa, ikiwa kama nguo fulani ngumu sana yenye kitu kama vioo vya miwani nyeusi (tinted), na ni sehemu ya mdomo wake tu ndiyo iliyokuwa wazi, lakini kuanzia kidevuni kuelekea chini palifunikwa vyema kama mwili wake wote. Mdomo wa mtu huyu ulipakwa rangi nyeusi, hivyo haingekuwa rahisi kuukariri, lakini kama ni kitu kimoja alichotambua Nora ni kwamba mtu huyu alikuwa mweupe. Ulikuwa weupe wa pembeni kuzunguka midomo yake, ulioonekana vizuri gizani hapo na kumfanya Nora adhani huenda ni mzungu, lakini kihalisi, ilikuwa ni Lexi.
Kishindo alichokuwa ameingia nacho hapo kilikuwa ni balaa!
Alipomtazama Nora, aliona jinsi alivyoogopa ingawa alijikaza sana kuonyesha ujasiri wake, naye akamsogelea usoni na kupeleka mikono yake karibu na uso wake. Nora aligeuzia shingo pembeni akifumba macho yake kwa nguvu sana kwa kudhani angeumizwa, lakini Lexi akakishika kitambaa kilichomfunga mdomoni na kukifungua kutokea nyuma ya shingo yake. Alipohisi kitambaa kimetolewa, Nora akageuka na kumwangalia mtu huyu ambaye hangeweza kutambua ni nani. Lexi akaifuata suruali ambayo alijua ni ya Nora, kisha akamrushia mapajani mwake.
Nora alishindwa kuelewa nini kilikuwa kinaendelea. Alijua wazi kuwa mtu huyo mbele yake ni mmoja wa watu waliojiita Mess Makers, na bila shaka ni huyu huyu ndiye aliyempiga risasi nne mara ya kwanza kule Mwanza lakini akamwacha tu. Leo tena, kwa kufikiri labda wanaume wale saba waliomteka waliagizwa na Mess Makers ili wafanye hayo, isingepatana na akili kwamba mmoja wao angeamua kuwaua wote ili tena amwokoe yeye. Kama siyo Mess Makers waliowatuma watu hao, basi angekuwa ni nani? Na kwa nini mmoja wao ahatarishe uhai wake ili tu kumsaidia yeye? Mambo mengi yalikuwa yanachanganya sana akili yake.
Baada ya kuwa amemrushia nguo hiyo, Lexi akaanza kuelekea sehemu ya mlangoni taratibu, lakini Nora akamwita.
"Hey... subiri..."
Lexi akasimama kwanza. Kisha akamgeukia na kumwangalia alipoketi pale chini, naye Nora akajitahidi kusimama huku bado akihisi maumivu mengi kichwani kwake. Akawa anamwangalia mtu huyo mbele yake huku akipumua kwa njia ya uchovu fulani hivi.
"We... we' ni nani?"
Nora akauliza swali hilo, bila kutambua kwamba jibu tayari alilijua.
Lexi akaendelea tu kumwangalia, nao wote wakasikia sauti za gari zikifika nje ya jengo hilo. Nora kwa haraka alijua bila shaka hao walikuwa aidha ni maaskari au Luteni Michael, naye akabaki kumtazama tu mtu aliyekuwa amesimama mbele yake kama vile hajawasikia wanaokuja. Hatua za haraka za kupanda ngazi zilisikika kutokea chini, naye Lexi akaacha kumwangalia Nora na kuanza kuelekea sehemu ile ya wazi kuelekea mbao za mafundi za kupanda. Akaruka na kuanza kupanda moja akienda juu, huku Nora akiachwa na maswali mengi kichwani.
Kutokea nje ya mwingilio wa chumba hicho, sauti ya Luteni Michael ilisikika ikisema kwamba kwa wale waliokuwa ndani hapo, wajisalimishe kwa kuwa walikuwa wamewazingira. Nora akajikaza na kuita kwa sauti, kisha kuwaambia waingie ili kumsaidia haraka. Alitangulia kuingia Luteni Michael, naye alipigwa na butwaa baada ya kuiona miili ya wanaume wale pale chini. Wakaingia wanajeshi wa timu yake pia, Alex, Mario, Hussein na Bobby, na wao vile vile wakashangazwa na waliyoona.
Luteni Michael akamwangalia Nora na kumwona akiwa bila suruali kwa chini, naye akamfata pale upesi na kumuuliza nini kilitokea. Nora akamwambia kichwa kilimuuma sana na tumbo pia, hivyo akamwomba amsaidie kuelekea hospitali kwanza na mambo mengine angemweleza baadaye. Luteni Michael akatii na upesi kumbeba Nora mikononi mwake, kisha akawaamuru Bobby na Alex wabaki na kuchunguza mambo hapo, halafu wawatafute mapolisi ili waje washughulike na masalio.
Luteni Michael akiwa amembeba Nora, akifuatwa na Mario pamoja na Hussein, wakaanza kuelekea chini upesi ili kumwahisha ACP hospitalini.
★★
Lexi alikuwa amepanda kuelekea juu mpaka ghorofa ya sita, kisha akapita ndani ya jengo na kurukia upande wa pili wa mbao za mafundi, na kuanza kushuka kuelekea chini wakati ule ambao Luteni Michael ndiyo alikuwa amefika ndani ya chumba kile alichomwacha Nora. Akafanikiwa kurukia upande mwingine wa ukuta uliozungukia jengo hilo, naye akawa katikati ya kokoto nyingi zilizozagaa chini hapo na kujibanza ukutani ili ashushe pumzi kidogo. Lakini alipotazama mnara ule wa Vodacom, akaona kitu fulani kule juu kilichovuta umakini wake. Akajitoa kwenye ukuta huo na kusimama vizuri zaidi ili aangalie kitu hicho, naye akatambua ilikuwa ni mtu.
Kulikuwa na mtu juu ya mnara huo, akiwa amening'inia kwa njia fulani ya kizembe, lakini Lexi akatambua kwamba alikuwa amejishikiza vizuri, na alikuwa anamwangalia. Hakuuona uso wake, lakini kwa haraka Lexi akajua mtu huyo ndiyo yule aliyetokea siku ile ghafla na kumuua Oscar, yaani silaha ya Luteni Jenerali Weisiko. Aliona kwamba sasa huyu mtu hatari sana alikuwa anamfatilia aidha Nora au yeye, lakini sanasana Nora kwa sababu kwa yeye Lexi haingekuwa rahisi kujua njia zake. Alitamani kumfata hapo hapo juu, lakini akafikiria hali zilizowazunguka wakati huu, hivyo akaamua kuachana naye tu na kujiahidi kwamba wangekutana tu tena, na kwa wakati huo hangemwacha salama.
Lexi akaondoka sehemu hiyo upesi kuelekea upande mwingine, na "silaha" huyo wa Weisiko akajisawazisha vizuri hapo juu na kumsindikiza tu Lexi kwa macho, akiwa ameona vizuri sana kila kitu kilichotokea kwenye jengo lile tokea Nora alipoletwa na wanaume wale mpaka Lexi alipowaua, naye akashuka kutoka juu ya mnara huo kwa kamba ndefu na kutokomea kusikojulikana.
★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★
Comments