FOR YOU 2
A Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA KUMI NA SABA
★★★★★★★★★★★★★★★★
Nora akatembea taratibu na kuchuchumaa chini, akaushika uso wa Lexi na kumwangalia kwa huruma.
"Lexi..." Nora akaita kwa sauti yenye huzuni.
"Niko sawa mheshimiwa... niko sawa," Lexi akajibu huku anatoa tabasamu hafifu.
Nora akainamisha uso wake na kufumba macho. Hivi siyo jinsi alivyotarajia siku yake iende hata kidogo. Alitarajia iwe siku ya kuituliza akili yake, lakini mambo yaliyokuwa yametokea ndiyo yakaivuruga kabisa. Akashusha pumzi, kisha akasimama na kumwangalia Luteni Michael kwa mkazo.
"Nora..."
"Toka," Nora akamkatisha.
"Nora nisikilize, huyu..."
"Mario, Hussein, nawaomba wote mwondoke. Now," Nora akawaambia.
"Lakini Nora, naomba tu uni...."
Luteni Michael alikuwa akimsogelea karibu zaidi wakati alipokuwa anasema hivyo, lakini Nora akaanza kumtandika makofi mengi sana usoni. Akampiga kwa goti sehemu yake ya siri, naye Luteni Michael akaugulia maumivu na kukaza kichwa, lakini akajitahidi asitoe sauti. Nora akamwongezea goti lingine hapo hapo tena, naye Michael akadondoka chini.
Alipomtazama, kweli Luteni Michael aliona Nora alikuwa amekasirika sana. Alikuwa anapumua kwa hasira nyingi mno, huku amekunja ngumi kwa nguvu. Mario na Hussein wakamfata Luteni Michael pale chini na kumnyanyua taratibu ili wamsaidie kumwondoa hapo. Luteni Michael alipomwangalia Lexi kwa ufupi, Lexi akampandishia nyusi kichokozi huku anatabasamu, na hilo likamkasirisha sana Michael.
Wanajeshi hawa watatu wakaondoka hapo hatimaye, naye Nora akaufunga mlango na kumsaidia Lexi kuelekea kitandani. Baada ya Lexi kukaa, Nora akatafuta kitu chochote hapo ndani cha kumponya Lexi sehemu alizoumia, kisha akakaa karibu yake na kuanza kumchua usoni taratibu. Akauliza ikiwa kuna sehemu zingine za mwili zilizohitaji tiba, lakini Lexi akakanusha kwa kusema aliumia tu hapo usoni na shingoni. Lexi alipomtazama Nora, aligundua kwamba mwanamke huyo alikuwa anajitahidi kuficha hisia zake nyingi, naye akamwambia inatosha; angekuwa sawa.
Nora alipoacha kumpaka dawa, akatazama tu pembeni na kuanza kulia sana. Alilia huku akiwa amefunika uso wake kwa viganja vyake, na kiukweli jambo hili lilimhuzunisha sana Lexi. Akamshika begani na kumvuta usawa wake, naye Nora akalalia kifuani kwa Lexi huku akijitahidi kujikaza. Wakaendelea tu kukaa namna hiyo hiyo kwa robo saa zaidi, kisha Nora akakaa sawa na kujifuta machozi yaliyobaki. Akamwangalia Lexi, ambaye alimpa tabasamu na kumbonyeza shavuni kichokozi, naye Nora akatabasamu pia.
"Nisamehe Lexi... yaani..."
Lexi akavishika viganja vya Nora kwa pamoja.
"Usijali. Jamaa amefanya tu jinsi moyo wake ulivyomtuma, wala haikuwa na shida sana," Lexi akasema.
"Hapana. Ilikuwa ni tatizo kubwa sana ambalo siwezi nikalifumbia macho. Luteni Michael amevuka mipaka. Ni lazima apewe somo," Nora akasema.
"Utamfanya nini sasa huyo sokwe?" Lexi akauliza kiutani.
"Ahahah... nitajua tu. Ona alivyokuumiza jamani..." Nora akasema huku akiushika mdomo wa Lexi.
Wakatazamana kwa hisia sana, naye Nora akaufata mdomo wa Lexi na kumbusu. Ilikuwa busu ya taratibu tu, kisha Nora akaanza kumpapasa Lexi mgongoni huku akiendelea kumpa denda laini. Lexi alianza kuhisi jambo hilo lingeelekea sehemu ambayo hakuwa akiitaka kwa wakati huu, hasa akijua wazi kwamba mwanamke huyu alikuwa adui yake kwa njia isiyo ya moja kwa moja, hivyo akajitoa mdomoni mwake na kujifanya kama vile sehemu fulani ya mwili wake inauma.
"Vipi Lexi?" Nora akauliza kwa kujali.
"Niko sawa. Kuna sehemu tu hapa shingoni... inauma," akasema Lexi.
"Oh, okay. Basi... aam... ngoja niagize chakula... walete, wewe lala hapa," Nora akamwambia.
Lexi akajivuta taratibu na kujilaza kitandani, huku Nora akimtengenezea mto ili aegamie. Nora akazichezea taratibu nywele za Lexi huku wanapeana tabasamu, kisha akaelekea sehemu iliyokuwa na simu ya mezani na kuomba chakula. Lexi alibaki hapo akimwangalia kwa makini sana. Alikuwa anawaza ingekuwaje siku ambayo dada huyo mwenye moyo mzuri angegundua kwamba mtu aliyeanza kumwamini ndiye aliyekuwa mbaya wake. Alikuwa hata anawaza hivi wakati huu kwa sababu kiukweli alianza kumjali sana Nora, kitu ambacho hakikutakiwa kutokea, lakini tayari ikawa hivyo.
Baada ya Nora kuita vyakula kwa ajili yao, akarudi kitandani na kulala karibu na Lexi, wakiwa wanatazamana tu machoni. Aliyapenda sana macho ya Lexi, naye akawa anatembeza kidole chake taratibu kwenye uso wake. Akamwomba kwa kusema hata wakimaliza kula, Lexi aendelee kukaa naye hapo hapo mpaka kesho, yaani alale pamoja naye usiku huo. Lexi akatikisa kichwa kukubali, naye Nora akafurahi na kumbusu kidogo kichwani, na wawili hawa wakaendelea kulala hapo wakisubiri chakula kiletwe.
★★
Luteni Michael, Mario na Hussein walirejea kule kwenye timu yake baada ya kutoka kwa ACP Nora. Bado mwanaume alikuwa na hasira sana, naye aliwaamuru Mario na Hussein wasiseme lolote kuhusu kilichotokea huko hotelini la sivyo wangemtambua. Alipofika tu jengoni kule akawauliza wengine walikuwa wamepata nini kuhusiana na Lexi. Hakupata jibu haraka, kwa kuwa wote walimwangalia kimaswali. Pua yake ilivimba kiasi kutokana na Lexi kumtandika kwa kichwa usoni, hivyo walikuwa wanajiuliza alipatwa na nini. Akawaambia waache kushangaa na waanze kumpa taarifa alizohitaji.
Manengo akamweleza kwamba mwanamke yule anakwenda kwa jina la Lexi Sona, na ni mgeni nchini humu kutokea Ghana. Akamweleza kwamba ameingia nchini kihalali kabisa, na aliishi Pemba kwa muda fulani akifanya kazi kama msimamizi wa biashara ya magari kwenye garage fulani ndogo mpaka alipokuja huku. Luteni Michael akauliza mambo mengi sana ambayo yangemhusisha Lexi na Mess Makers, lakini kiukweli, kwa sababu wanajeshi hawa hawakuwa wamefatilia mambo kwa kina sana, hawakuweza kuona kitu chochote kilichodokeza kwamba alihusiana nao.
Kwa hasira, Luteni Michael akapiga meza kwa ngumi yake, kisha akawaambia wenzake wangeweza kwenda kupumzika lakini kesho asubuhi na mapema wawe hapo kuendelea na kazi. Akaondoka upesi akionekana kuwa mwenye ghadhabu, na wengine wakaanza kuwauliza Mario na Hussein nini kilitokea huko walikoenda. Lakini wanaume hao wakawaambia hiyo ilikuwa ni siri yao, kwamba eti ni "top secret," kwa hiyo wengine hawakupaswa kujua lolote isipokuwa wao tu. Alex, Mario na Hussein wakawaaga wengine pia na kusema wangeonana kesho, huku Hussein akimpandishia nyusi kichokozi Aliyah. Ikabidi Mario amvute mkono ili waondoke hapo, kwa kuwa walikaa pamoja na Alex kwenye nyumba fulani ndogo ya kulipia.
Wakati wakiwa wanaelekea nje, Tariq akaangaliana na Aliyah, na bila mtu mwingine kuona akamtikisia kichwa mara moja kwa ishara ya kumwambia afanye jambo fulani, naye Aliyah akaanza kuelekea nje upesi. Aliwahi kabla Hussein na wenzake hawajaingia kwenye gari, naye akamwita na kumsimamisha. Hussein akaachia tabasamu la furaha akijua mtoto alikuwa amemwelewa, kisha Aliyah akafika karibu yake na kumwambia angependa wakatembee pamoja kabla hajaenda kupumzika. Hussein akatae? Akazirusha funguo za gari usoni kwa Mario na kumwambia yeye na Alex watangulie tu, huku Mario akimtazama kwa kukerwa.
★★
Aliyah alimwongoza Hussein hadi kwenye chumba alichokuwa anakaa. Kilikuwa kwenye nyumba iliyo ya ghorofa, kukiwa na wapangaji kadhaa sehemu hiyo, na yeye Aliyah alikuwa kwenye ghorofa ya tatu. Kufikia wakati walipofika kwenye mwisho wa ngazi kuelekea chumba chake, Hussein alikuwa amepiga naye story nyingi zenye kufurahisha, na Aliyah kiukweli alipendezwa naye sana. Hussein aliongea mno na kila muda ambao mada moja ingeisha angetokeza nyingine yenye kufurahisha hata zaidi. Alijitahidi sana kumfurahisha Aliyah, akijua leo angekwenda kupewa bonge la keki.
Walipoingia tu ndani, Aliyah akaenda moja kwa moja kwenye fridge ndogo ya vinywaji. Kwa kujua kile ambacho kingefuata, Hussein akaamua tu kukaa kimya na kumtazama.
"Unataka bia?" Aliyah akauliza.
"Ningependa juice tafadhali," akajibu Hussein kikejeli.
"Kaa sasa," Aliyah akamwamrisha.
Hussein akaketi kwenye sofa. Alikuwa ameshaanza kuizoea tabia fulani ya Aliyah ya kujifanya kama kibosile. Aliyah alikuwa mrefu wa kadiri, mweupe, na mwenye umbo zuri la kike. Hata kama angevaa nguo za kijeshi isingezuia sehemu za mapaja yake na kalio kuonekana vizuri jinsi zilivyoshiba, na ni kati ya mambo yaliyomvutia zaidi Hussein kumhusu mwanamke huyu.
"Hapa palivyokaa inawezekana kuna njemba imejificha huko ndani. Inabidi niwe chonjo," Hussein akatania.
Aliyah akaanza kumfata huku akicheka, kisha akampatia juice yake. Yeye alikuwa ameshika chupa ndogo ya bia, kisha akainywa nusu chupa huku akiwa amesimama mbele yake. Hussein akawa anamwangalia kwa umakini, akipendezwa na jinsi mabuti yake ya kijeshi yalivyomfanya aonekane kama jemedari wa kiume. Aliyah akaiweka mezani bia yake, kisha bila kupoteza muda akapiga magoti katikati ya mapaja ya jamaa na kuanza kuvuta suruali yake kwa njia iliyomwambia Hussein anyanyuke kidogo ili afanikiwe kuitoa.
Njia ya Aliyah ya kwenda moja kwa moja kwenye pointi ilimvutia sana jamaa, naye akatii na kujinyanyua kidogo, kisha Aliyah akaitoa suruali yote na boxer mpaka jamaa akawa mtupu huku chini. Akaikamata mashine yake iliyokuwa imevimba tayari na kuitumbukiza mdomoni mwake, akimnyonya vizuri na taratibu sana.
"*****... nilihitaji sana hii kitu," akasema Hussein kwa kuhisi raha.
Aliyah alikuwa anampa zawadi hii ya kumkaribisha kwake, akimnyonya kwa njia ambayo hangesahau.
Akaitoa mashine yake jamaa mdomoni muda mrefu vya kutosha kusema, "Mkeo huwa hakupi namna hii kwani?" kisha akaendelea kumnyonya.
Ilimchukua Hussein sekunde chache kusawazisha akilini alichosema Aliyah kutokana na kupagawishwa haswa.
"Mimi sijaoa... nina marafiki tu wa vitambo. Walikuwa wanahh...hitaji penzi... kwa hiyo nikawa nawasaidia... ila hii show yako hawajaifikia..."
Aliyah akacheka kidogo na kusema, "Hapa bado!"
Akaendelea kumnyonya mpaka miguno ya mwanaume ikaanza kusikika. Kisha Aliyah akaitoa mdomoni kwa ufupi na kuanza kuipekechea mkononi. Hussein akatabasamu.
Aliyah akamuuliza jamaa kwa maringo, "Luteni Michael naona kama huwa mnamwogopa sana. Ni kwa nini?"
"Tunamheshimu, siyo kumwogopa. Hata nyie pia, siyo?" akajibu Hussein huku amefumba macho.
"Yeah... Nilipomwona wakati mmerudi nikadhani amegongwa na treni usoni!" Aliyah akasema.
"Ahahah... hamna. Kapigwa. Tena kapigwa na mwanamke hahah..." Hussein akafunguka.
"Yule yule Lexi?"
"Yeah. Alikuwa anataka kumkamata, ila demu akamletea nyodo ndiyo akaanza kumshushia kipondo. Lakini na kenyewe kalimuonja... ahahah... na ACP akamkunja," Hussein akasema.
Aliyah akarudia zoezi lake na kuanza kuinyonya tena mashine ya Hussein. Ustadi ulikuwa mwingi kutoka kwa meanamke huyo mpaka jamaa akawa amemwaga vitu vyake kwa raha mustarehe!
Walitulia kama dakika moja, kisha Aliyah akanyanyuka na kukirudia kinywaji chake. Akamwambia Hussein anaenda chooni mara moja, naye akamwacha hapo jamaa amekaa kwenye sofa akiwa amejiachia kama anasubiri kuchunwa ngozi kwenye sehemu zake za siri. Lakini hakujua kwamba hii ilikuwa ni njia fulani ya kupata ukweli kutoka kwake kuhusu kilichotokea muda ule walipoondoka na Luteni Michael. Aliyah aliingia sehemu ya bafuni na kumpigia simu Tariq, akimweleza yale ambayo Hussein alikuwa amesema. Tariq akampongeza kwa kazi nzuri na kumwambia aendelee kumzuzua tu namna hiyo hiyo kwa leo.
Aliyah akarudi mpaka pale alipoketi Hussein na kukuta jamaa akipasafisha vizuri. Akatabasamu, kwa kuwa alipenda sana njia fulani yenye ucheshi ya kufanya mambo aliyokuwa nayo mwanaume huyo. Akaanza kuvua nguo zake zote na kubaki akiwa mtupu kabisa, kisha akaanza kumfata Hussein ambaye hakuwa amemwona bado. Alipofika nyuma yake, Hussein akageuka na kukutana na mwili mweupe wa mwanamke huyu. Akaachia tabasamu la mbali, naye Aliyah akamsukuma kwenye sofa.
Kisha mwanamke huyo akapanda juu yake akiwa amepiga magoti, naye Hussein akaishusha tena suruali yake mpaka usawa wa magoti. Aliyah akakaa juu ya mashine ya jamaa taratibu na kutoa pumzi ya juu akihisi raha. Kisha akaanza kupanda na kushuka, akijisugua vizuri katikati ya mstimu wa mwanaume huyo machachari huku Hussein akiyanyonya matiti yake makubwa. Wakaendelea kupeana mahaba kwenye sofa mpaka walipopitiwa na usingizi na kulala pamoja usiku huo.
★★
Upande wa Tariq, taarifa aliyokuwa amepewa na Aliyah ilitakiwa kufika kwa Kanali Oswald Deule. Kati ya wanajeshi wale watano walioongezwa kwenye timu ya Luteni Michael, ni hawa wawili ndiyo ambao walikuwa wamewekwa kujua mambo yote yanayoendelea ambayo Luteni Michael hangemweka wazi Kanali, ili wamwambie yeye. Kwa hiyo Tariq akamjulisha Kanali Oswald kuwa Luteni Michael alitaka sana kumkamata mwanamke fulani lakini akaambulia kuabishwa tu na ACP Nora, ikionekana alikuwa anapoteza tu muda wake kwa sababu alikuwa na hisia za kimapenzi kumwelekea mtoto wa huyo wa Jenerali Jacob.
Kanali Oswald akamshukuru Tariq kwa kumjuza kuhusu hilo na kumwambia asiache kumpa ripoti za mambo yoyote yatakayofanyika, na baada ya hapo wakaagana.
★★★
Asubuhi na mapema ya siku iliyofuata, Nora aliamka na kukuta Lexi akiwa bado amelala pembeni yake. Aliachia tabasamu la hisia nzuri sana, akihisi ni kama kuna jambo fulani kuhusu uhusiano wake na Lexi ambalo lilikuwa geni sana kwake, na hiyo ilimfanya ajihisi tofauti sana. Hakuwahi kukaa kufikiria kwamba siku moja na yeye angewahi kujaribu mahusiano na mwanamke, ijapokuwa kihalisi Lexi hakuwa "mwanamke."
Akaanza kumtekenya usoni kwa kupitisha kucha yake usawa wa midomo yake, kama anaichora, na ghafla kinywa cha Lexi kikafunguka na meno yake kuking'ata kidole cha Nora, lakini kwa wepesi. Hii ilimshtua Nora kidogo, ambaye alifikiri Lexi alikuwa bado kasinzia, lakini kwa kutambua alikuwa anamtania kichokozi, akaanza kucheka huku amefumba mdomo.
Lexi akakiachia kidole cha Nora, kisha akafumbua macho na kumwangalia machoni.
"Good morning," Nora akamwambia.
"Same to you," Lexi akasema.
"Unahisije? Bado maumivu yapo?" Nora akauliza.
"Kwa mbali shingoni, lakini najua itapoa," Lexi akajibu.
"Pole. Nahitaji kwenda kuoga. Kuna sehemu natakiwa niwahi,'' Nora akamwambia.
"Wapi?"
"Ni ofisi mpya nitakayotumia sasa. Nitafatwa na mtu fulani, ananipeleka kunionyesha, ila najua lazima tu atawahi mno, kwa hiyo... best be ready..."
"Aaaa... angalau utakuwa mbali na yule sokwe..."
Nora akacheka kidogo na kusema, "Yeah... angalau."
"Okay. Me bado nahisi usingizi. Wewe kapambane na bafu, halafu mimi nitaendelea na uchunguzi wangu hapa hapa kitandani," Lexi akasema na kufumba macho tena.
"Ahahahah... haya bwana," Nora akasema.
Kisha akambusu kwenye paji lake la uso, halafu akatoka kitandani na kuelekea kuoga.
★★
Baada ya kumaliza kujiandaa, Nora alimwangalia Lexi na kuona bado amelala. Akahisi labda kwa sababu ya jambo lililompata jana alihitaji kupumzika sana, hivyo akamwachia ujumbe kwenye simu yake kuwa angewasiliana naye au wangeonana baadaye. Akamfunika vizuri kwa shuka, kisha akaelekea nje ambapo tayari mtu aliyetakiwa kumpeleka ofisini kwake alikuwa akimsubiri.
Lakini muda wote huo Lexi alikuwa anajifanya kasinzia tu, hivyo baada ya Nora kuondoka, akanyanyuka na kwenda kujimwagia pia. Akavaa nguo zake haraka na kuondoka hapo upesi mpaka kwenye gari lake. Alikuwa akificha kifaa kile cha mawasiliano maalum na Torres kwenye gari lake, hivyo akakitoa na kuangalia kama Torres alimtafuta tena. Akakuta ametafutwa mara kadhaa jana na asubuhi hii, hivyo akampigia yeye ili kujua yaliyoendelea upande wake.
Torres alimjulisha kuwa kuna jambo la muhimu sana ambalo alitaka kuzungumza na kundi lao lote, hivyo Lexi angetakiwa kwenda kule kwenye nyumba yao ya maficho, a.k.a "chini." Lexi akamwambia huenda ingekuwa ngumu hasa ukitegemea hali aliyokuwa nayo na Kendrick na pia ACP Nora, lakini Torres akasisitiza sana kuwa jambo lililoendelea lilikuwa muhimu kuliko tofauti zao, na alimhitaji sana ili kupanga mambo mengi vizuri. Lexi akatafakari kwa sekunde chache, kisha akamwambia angekwenda huko upesi. Torres akafurahi sana na kusema wote walikuwepo kule tayari, hivyo angemsubiri kwa hamu ili "kikao" chao kianze.
Baada ya kumalizana na Torres, Lexi akaliondoa gari lake hapo na kuanza kuelekea kule kwenye hoteli aliyokaa. Alikuwa anamuwaza Valentina, akikumbuka kuwa alitakiwa kumtafuta kwa simu ili labda wakutane leo, lakini kwa sababu ya mambo kuingiliana haingewezekana. Hivyo akaamua kuacha kumtafuta mpaka wakati mwingine. Akawaza jambo la kumwambia Nora kuhusu yeye kutokuweza kuwa naye baadae, naye akaendelea na safari yake.
★★
ACP Nora alifikishwa mpaka kwenye jengo ambalo ofisi yake mpya ya utafiti ingekuwa. Lilikuwa ni Kituo maalum cha Usalama wa Taifa (Defense Agency), nalo lilikuwa na ghorofa 9 kuelekea juu. Lilijengwa hasa kwa vioo sehemu za nje, na eneo lote kulizunguka lilikuwa safi na lililotunzwa vizuri. Akapelekwa mpaka sehemu za ndani, akipishana na watu wengi walioendelea na kazi zao mbalimbali, kisha wakachukua lifti na kupandisha mpaka ghorofa ya mwisho. Huko ndiko kungekuwa na ofisi yake.
Afisa aliyemleta hapo alimwambia kwamba Msimamizi Mkuu wa kitengo cha Huduma za Ulinzi nchini (Ministry of Defence) alikuwa akimsubiria. Nora akauliza kwa nini, naye akaambiwa alikuwa tu anatakiwa kumpokea kwenye ujio wake hapo. Yote haya hayakumpendeza sana Nora, lakini kwa wakati huu aliona ni bora kuwa huku kuliko kuwa karibu na Luteni Michael baada ya kitendo alichomfanyia Lexi.
Walipofika kwenye ofisi ya Msimamizi huyo mkuu, Nora akatabasamu kwa furaha. Alimfahamu, lakini hakujua ikiwa alipatiwa cheo hicho tayari. Huyu alikuwa ni mwanamama Emiliana Ngoyi, yule yule wa tokea kipindi kile cha Demba Group. Alipoingia ofisini kwake, Emiliana akampokea kwa kumbatio, akiwa ndani ya suti ya kike yenye rangi ya blue-bahari, huku Nora yeye akiwa amevaa suti nyeusi ya kike. Wakajuliana hali zao, kisha Emiliana akaanza kumwelezea mambo mengi ya kitengo chao, ingawa kwa kadiri kubwa Nora alifahamu.
Ofisi ambayo Nora angepewa ilikuwa kwa njia fulani kama ofisi ya mpelelezi mkuu, ijapokuwa Nora hangechukua cheo hicho kwa sababu angekuwa hapo kwa muda tu. Katika maongezi yao, Emiliana alimjulisha Nora kwamba leo alitakiwa kwenda pia kwenye mahojiano maalum ambayo yangefanywa kuhusiana na Salim Khan, kwa kuwa huenda naye angeshiriki kuuliza maswali na hata kupata mambo mengi kutoka huko. Nora akakubali mwaliko huo.
Baada ya kumaliza maongezi yao, Emiliana akamsindikiza sasa Nora mpaka kwenye ofisi yake mpya. Alipokelewa na mwanamke aliyekuwa mweupe kiasi, akiwa amevalia miwani machoni, naye akajitambulisha kwa jina la Halima Said. Angekuwa ndiyo msaidizi wake Nora kwenye masuala ya kutuma jumbe, kupokea jumbe, yaani chochote kile ambacho Nora angehitaji kwa muda wote ambao angekuwa hapo. Nora akamshukuru sana Emiliana kwa kila jambo, kisha akaelekea ndani ya ofisi yake kuanza kazi.
Ilikuwa ofisi yenye mpangilio mzuri sana, naye Nora akaenda kwenye meza iliyokuwepo na kuketi kwenye kiti cha kiofisi. Kulikuwa na kompyuta hapo pia, lakini yeye akaitoa laptop yake na kuiwasha. Moja kwa moja alianza kumsoma tena Oscar Amari. Taarifa zote kuhusiana na maisha yake nchini humu zilikuwa fupi, ikionyeshwa tu kwamba alitokea Ghana kama mfanyabiashara na kukaa huku kwa miaka zaidi ya mitatu. Alijaribu kuunganisha vidokezo mbalimbali vyenye uhusiano kati ya Oscar na Kevin Dass, lakini kiukweli hakupata lolote.
Alikuwa na wasiwasi kuhusu hawa watu kwa sababu ikiwa Oscar aliweza mpaka kutoka kimapenzi na mdogo wake, basi wangeweza kuwa sehemu yoyote ile na kufanya lolote walilotaka. Ingawa alijua kuna siri nyingi zilifichika kutoka kwenye serikali yake mwenyewe, alitaka sana kuwafichua Mess Makers upesi ili matatizo haya yote yaishe haraka.
★★
Baada ya muda fulani, ujumbe kwenye simu yake Nora uliingia kutoka kwa Lexi. Akitabasamu kwa furaha, akachukua simu kuusoma, lakini akakuta Lexi amemwandikia kuwa amepatwa na dharura fulani ambayo ingempeleka nje ya mkoa, hivyo baadaye hawangeweza kuonana. Ingawa hii haikuwa taarifa nzuri kwake, Nora akampa tu pole na kusema haikuwa na shida, na kumwambia amjulishe wakati ambao angerudi.
Halima aliingia ofisini humo akiwa amemletea Nora kiamsha kinywa. Nora akauliza kama yeye pia alikuwa anapata chai, lakini Halima akasema yeye angepata baadaye. Nora akamwambia hapana; afate chai, aje wapate kiamsha kinywa kwa pamoja ofisini humo. Halima alikuwa mwenye kusita kiasi hasa kwa sababu hakutarajia "boss" wake mpya amtendee namna hiyo, lakini Nora akamsisitizia afanye hivyo upesi la sivyo asingekula chakula alichomletea.
Basi dada huyo akatii, na baada ya muda mfupi akaingia ofisini hapo ili kupata chai pamoja na Nora. Kulikuwa na sehemu yenye meza ndogo ya kioo na masofa mawili, hivyo wote wakaketi hapo na kuanza mlo. Nora alipiga story nyingi na mwanamke huyu, akipata kujua maisha yake kwa ujumla, amefanya kazi hapo kwa muda gani, na ikiwa ameolewa na ana watoto. Halima aliongea kistaarabu sana, na upesi Nora akapendezwa naye.
Katika maongezi yao wakiwa wanaendelea kupata chai, simu ya Nora iliita mara kadhaa, lakini alikuwa anaitolea sauti na kuipuuza kwa sababu mpigaji alikuwa ni Luteni Michael. Bado alikuwa na hasira naye, kwa sababu mwanzoni alimwona kama mwanaume anayeweza kuwa rafiki mzuri, lakini kwa kitu alichomfanyia Lexi ndani kwake hangeweza kusahau. Halima akamwambia Nora kwamba na yeye angependa kwenda kwenye mkutano wa leo ambao ungefanywa na Salim Khan, lakini hangeweza kwa sababu za kiofisi. Nora akamwambia asijali, kwa sababu angefanya mpango ili waende wote. Baada ya kumaliza msosi, Nora akarudi mezani kwake ili kuendelea na mambo mengine.
Haikupita muda mrefu sana, naye Halima akaingia ofisini humo tena akiwa ameshika faili moja. Akamwambia kuwa limeletwa na mwanajeshi mmoja hapo, na Nora alipolitazama akatambua lilitumwa kwake na Luteni Michael. Akamshukuru Halima na kumwambia aende. Halima akatoka hapo kurudi kwenye meza yake nje. Faili hilo lilikuwa na karatasi zenye taarifa fulani muhimu. Lakini alipolifungua tu, mbele hapo akaona kikaratasi chenye maneno "I'M SORRY NORA. I HOPE WE CAN TALK SOON," naye Nora akakibandua na kukikunja-kunja kisha kukirusha pembeni kwenye kopo la uchafu.
Alipoanza kupitia mafaili hayo, akaona zilikuwa ni baadhi ya taarifa kumhusu Lexi. Akatikisa kichwa chake kwa kusikitika, kwa sababu aliona ni kama bado Luteni Michael alizidi kumchokonoa pabaya. Akasoma tu mambo mengi yaliyoandikwa hapo, na ijapokuwa kuna vitu ambavyo Lexi hakuwahi kumwambia kumhusu vilivyokuwa hapo, Nora hakuiona hiyo kama sababu ya kumshuku. Akalifunga tu na kuliweka pembeni, naye akainamisha uso wake kwa kuuweka kwenye viganja vyake alivyokunja. Alikuwa akiwaza sana kwa nini Michael aliendelea kulazimisha mno aamini jambo ambalo hakutaka kuamini. Akanyanyua tu uso wake na kuamua kupotezea, kisha akaishika laptop yake ili kuendelea na mambo mengine.
Lakini, akatulia kwanza baada ya jambo fulani kuingia kwenye akili yake. Akalichukua faili hilo tena, naye akasoma kwa makini zaidi. Ilikuwa bado haijaingia akilini mwake kuwa alisoma Lexi alitokea Ghana na kuja huku, vilevile na Oscar pia. Hii ikawasha kitu fulani kwenye akili yake. Akaanza kuwaza tena vipi kama jambo hilo lilimaanisha wawili hawa walikuwa na uhusiano wa aina fulani? Ingawa hakutaka kuamini hilo, kitu hiki kikaanza kuisumbua akili yake.
Alianza kutafakari jinsi ambavyo yeye na Lexi walikutana, mpaka kufikia leo ilikuwa ni kama aliingia kwenye maisha yake kwa wakati ambao ulikuwa SAHIHI kabisa kwake. Vipi kama kweli alikuwa mmoja wao? Akawa anatikisa kichwa chake kama kukataa kwamba hilo halingewezekana. Ila alipoanza kukumbukia maneno ya Luteni Michael, kwamba siku ile walipompata tu Oscar, Lexi aliingia ndani ya jengo lile la utafiti na ndipo mambo yao yakaharibika, mashaka yake yakaongezeka. Akachukua simu yake na kujaribu kumpigia Lexi, lakini hakupatikana.
Wasiwasi ukamwingia mwanamke huyu, mwingi sana. Akaendelea kukaa humo ofisini tu akitafakari mambo mengi sana kuhusu Lexi, akitumaini jambo hili lisingekuwa la kweli kumhusu.
★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★
Comments