Reader Settings

FOR YOU 3

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★

 SEHEMU YA NNE

★★★★★★★★★★★


Alfajiri na mapema tu, tayari Luteni Jenerali Weisiko alikuwa amefika kwenye nyumba ya "binti yake" baada ya kupewa taarifa kwamba alikuwa ametekwa. Alifika akiwa na hasira kali siyo mchezo, akiwa pamoja na walinzi wake maalum, na walinzi wale wa nyumba ya Azra walikuwa wamepigishwa magoti ndani ya geti la nyumba hiyo kama vile wanafunzi waliochelewa kuhesabu namba shuleni. Weisiko alitaka kujua ilikuwa vipi "mtoto wake" akatekwa wakati walinzi hao walikuwepo muda wote, nao wakamweleza kwamba waliomchukua walitumia nyaya za umeme kuingia na kutoka, na kwamba walikaribia kuwakamata lakini wakawaponyoka kimuujiza.

Weisiko hakuwa aina ya mtu aliyeamini miujiza, ila kama ni muujiza aliotaka utokee ilikuwa ni "Mary" wake kurudi hapo haraka iwezekanavyo. Akawauliza watu hao walitoroka vipi eneo hilo, nao walinzi wakamwambia walitumia gari ambalo baada ya kulifuatilia walikuta limelipuka, bila kuwa na miili yoyote ndani. Weisiko alichanganyikiwa sana. Silaha yake muhimu zaidi ilikuwa imeibiwa, lakini kilichomfanya ahuzunike hata zaidi ilikuwa ni ile hisia kama vile amempoteza mtoto wake kwa mara nyingine tena. Akawauliza walinzi hao ikiwa wangeweza kuwatambua watu waliomteka binti yake, lakini wakakanusha.

Kwa jazba kali sana, akachukua bastola kutoka kwa mmoja wa walinzi wake yeye na kuanza kuvifyatua vichwa vyote vya walinzi wale sita kwa risasi! Wote wakaanguka chini wakiwa wamepoteza maisha yao, naye Weisiko akaendelea kuimiminia miili yao risasi huku akipiga makelele kwa hasira mpaka bastola ikawa tupu. Akawaambia walinzi wake washughulikie miili hiyo, kisha yeye akaenda pembeni na kumpigia simu Jenerali Jacob. Akamweleza yaliyokuwa yametokea, naye Jacob akakasirika sana.

Moja kwa moja wote wakawa wamefikia mkataa kwamba ni Mess Makers ndiyo waliomteka "Mary," kama jinsi walivyomwita Azra. Jenerali Jacob akamwambia Weisiko wangepaswa kufanya juu chini kufahamu ni jinsi gani Mess Makers walijua mahali ambapo "Mary" angekuwepo, na labda kwa njia hiyo wangeweza kuwapata pia. Weisiko alihofia sana kwamba huenda watu hao wangemdhuru "binti yake," kwa hiyo akaapa kuwapata wote mapema na kuwaua, kwa sababu kumgusa Azra ilikuwa ni kama wamemgusa yeye moja kwa moja.

Lakini hakujua kwamba kama tu ilivyokuwa ngumu kwa serikali yote ya nchi kuwapata wahuni wale, ingekuwa tata hata zaidi kwake. Akaondoka tu kwenye nyumba hiyo akiwa na hasira kali huku akiwaza afanye nini ili kumpata "Mary" wake.


★★★


Mess Makers wakawa wamemfikisha Azra kule "chini" kwenye nyumba yao ya maficho kwenye mida ya asubuhi, wakipokelewa vyema na Torres. Mpaka wakati wanafika Azra hakuwa amerejesha fahamu bado, na wakati huu mikono yake ilikuwa imefungwa pamoja na miguu kama tahadhari tu.

Walimwingiza kwenye chumba fulani kidogo kilichokuwa kimejengewa kule kule chini ya handaki lile pana, ambacho kilikuwa ni aina ya chumba chenye kusaidia kupasha miili joto kwa muda mfupi (steam room, siyo sauna). Kutokana na jinsi mwili wa Azra ulivyoshikwa na baridi baada ya safari ndefu ya usiku kutoka kule kwenye nyumba yake, lilikuwa wazo la Torres kumweka ndani hapo ili mwili wake upate joto la taratibu kadiri ambavyo fahamu zake zingekuwa zinarejea.

Kevin kama kawaida yake bado alikuwa akisema kwa msimamo wake kwamba wazo la kumpeleka mwanamke huyo hapo akiwa hai halikuwa zuri, na badala yake walitakiwa kumpa kifo tu kama vile alivyomfanyia Oscar. Mwanaume huyu alikuwa ameshaanza kumkera sana Lexi, lakini Lexi alikuwa imara vya kutosha kumpuuzia tu kwa sababu aliielekeza zaidi akili yake kwa mdogo wake.

Victor akaondoka pamoja na Kevin ili kuziondoa kero za jamaa hapo, na wengine wakamkalisha Azra vizuri tu kwenye kiti na kumfungulia kamba baada ya Lexi kusema wafanye hivyo. LaKeisha akasema angekwenda kujimwagia baada ya usiku wenye kuchosha, akimwomba Torres waondoke pamoja kwenda kujisafisha pamoja kwa kuwa Azra hangechukua dakika nyingi kuamka, ili pia kumwacha Lexi na mdogo wake peke yao. Wakamsihi Lexi awe mwangalifu naye, kisha wakaondoka sehemu hiyo.

Lexi alikuwa anamwangalia Azra sana huku anatafakari mambo mengi, na baada ya sekunde kadhaa kupita, yeye pia akavuta kiti kidogo na kuketi. Akaendelea kumwangalia mpaka alipoanza kugeuza shingo yake taratibu, lakini ghafla akashtuka na kudondokea chini, akijaribu kujiweka katika hali ya kujihami. Lexi akasimama na kuanza kumwambia asiogope kwa sababu alikuwa sehemu salama, lakini Azra akachukua kile kiti na kujaribu kumponda nacho, naye Lexi akakikwepa.

"Calm down! Listen to me! I'm not gonna hurt you. I'm not (Tuliza hisia! Nisikilize. Sitakuumiza. Sitakuumiza)," Lexi akasema kwa kumtuliza.

Azra akawa anarudi nyuma nyuma huku anapumua kwa nguvu, na akiwa anamwangalia Lexi kwa hasira.

"I'm sorry. I'm sorry I attacked you. But it was the only way to bring you with me (samahani... samahani kwa kukushambulia.. lakini ndiyo ilikuwa njia pekee ya kukuleta pamoja nami)," Lexi akamwambia.

Azra akawa anamtazama tu kama hamwelewi.

"Look... I know this is all messed up... and a lot is going on even I don't understand, but one thing I know for sure... is that you're my sister. I know you probably don't know me... but I know you. I do. Let's just... I just want us to talk. Please (ona... najua mambo yote haya ni mvurugo.. na mengi yanaendelea hata mimi mwenyewe sielewi, lakini kitu nachojua kwa uhakika ni kwamba wewe ni dada yangu. Najua labda hunifahamu.. lakini mimi nakujua. Nakujua. Tu.. nataka tu tuzungumze.. tafadhali)," Lexi akamwomba.

"Who the hell are you? (Wewe ni nani?)" Azra akauliza.

Hapo ndiyo alikuwa amemwongelesha Lexi kwa mara ya kwanza, na Lexi kuisikia sauti yake kulifanya afarijike sana moyoni. Bado ilikuwa jinsi ile ile alivyoikumbuka kabisa.

"My name is Lexi. Well... its my new name. You used to know me as... Sandra (naitwa Lexi.. ni jina langu jipya.. wewe ulikuwa ukinijua kama Sandra)," Lexi akamwambia.

Aliona ampe utambulisho wa yeye kuwa Sandra kwa sababu suala la kubadilishana mwili na pacha wake lingemchanganya kwa wakati huu.

"I'm your sister (mimi ni dada yako)," Lexi akamwambia.

"I don't have a sister (sina dada)," Azra akamwambia kwa mkazo.

"Azra... we're siblings. We're... from the same womb. I don't know what happened to you, but everything I'm telling you is the truth. Azra our parents we're killed right in front of us.... our parents died that night... that horrifying night of our entire lives... that changed everything about who we've become now. It was never supposed to be like this.... (Azra sisi ni ndugu. Tumetoka tumbo moja. Sijui ni nini kilikupata lakini kila kitu nachokwambia ni kweli. Azra wazazi wetu waliuliwa mbele ya macho yetu.. usiku ule walikufa.. usiku ule wenye kuogopesha sana katika maisha yetu uliobadilisha kila jambo kuhusu watu ambao tumekuwa sasa.. Haikupaswa kamwe kuwa namna hii)" Lexi akawa anazungumza kwa hisia.

"What the hell are you talking about? (Unaongelea nini?)" Azra akauliza.

"I need you... to look deep down in you even if you don't remember... I know your heart knows its the truth. What those people did to you... might have erased all of your memories about our family. Azra... I am your family. I mean come on, we even look alike, don't you see? We share the same blood (Nakuhitaji ujichunguze ndani yako kabisa.. hata kama haukumbuki.. ninajua moyo wako unajua nayokwambia ni kweli. Mambo ambayo watu hao wamekufanyia huenda ndiyo yamesababisha upoteze kumbukumbu kuhusu familia yetu. Hebu tazama, yaani mimi na wewe tunafanana kabisa, au huoni? Sisi ni wa damu moja..)," Lexi akasema.

Alikuwa akiongea hivyo huku akipiga hatua chache kumfata Azra.

"Stay back! (Tulia huko huko!)" Azra akamwonya.

"Azra..."

"I'm not! Don't call me that! (Mimi siyo! Usiniite hivyo!)" Azra akamwambia kiukali.

"Its your name! You're my sister, you're Azra (ndiyo jina lako.. we ni dada yangu, we ni Azra)," Lexi akasisitiza.

"No, no, I'm not. Whoever you are, or whatever game you think you're playing with me its not gonna work. I will kill you, do you understand me? (Hapana, hapana, mimi siyo. Sijali wewe ni nani au ni mchezo gani unafikiri unanichezea, lakini hautafanikiwa. Nitakuua, unanielewa?" Azra akaonya.

"Really? You'd kill me? (kweli? utaniua?)" Lexi akauliza.

"Without a blink (bila kukonyeza)," Azra akajibu.

"Then why didn't you? (mbona haukufanya hivyo basi?)" Lexi akauliza.

Azra akabaki kimya.

"The other night when I found out it was you... you had a knife on my neck.... why didn't you do it? (Usiku ule nilipojua ni wewe.. uliweka kisu kwenye shingo yangu.. kwa nini haukufanya hivyo?)" Lexi akauliza.

"Ahah... you really just love acting don't you? (unapenda sana kuigiza, siyo?)" Azra akauliza.

"Azra, I'm your sister. If I wanted to harm you, I would have. My only goal coming after you was to avenge my friend's death, but when I found out it was you.... I thought you were dead. I thought all of you were. Everything is a shock to me the same as it may apply to you, but I'm telling you the truth. You gotta believe me. Azra... (Azra mimi ni dada yako. Kama ningekuwa nataka kukudhuru ningekuwa nimefanya hivyo. Lengo langu kukufata mwanzoni lilikuwa ni kulipiza kisasi kwa kifo cha rafiki yangu lakini nilipojua ni wewe... nilidhani ulikuwa umekufa. Nilidhani nyote mlikuwa mmekufa. Kila jambo limenipa mshtuko kama jinsi inavyoweza kuwa kwako pia.. lakini nayokwambia ni kweli. Unapaswa kuniamini. Azra...)" Lexi akaishia tu hivyo.

Machozi yalikuwa yamejaa kwenye macho yake kwa sababu ya hisia nyingi sana za huzuni. Azra alikuwa anamwangalia kwa kutomwamini bado, na jambo moja lililokuwa akilini mwake ilikuwa ni kutoroka sehemu hiyo waliyokuwepo haraka iwezekanavyo.

"Azra look... I can show you some of the things that... may help you see that what I'm saying is true... if you'll let me (Azra ona.. ninaweza kukuonyesha baadhi ya mambo ambayo yanaweza kukusaidia uone kwamba nayosema ni kweli.. ikiwa utaniruhusu)," Lexi akamwambia.

"Like... what? (kama nini?)" Azra akauliza.

"I'll ask my friend to... get some old photos of us. You used to love to take many photos of us and post them on Facebook back then... (nitamwomba rafiki yangu atafute baadhi ya picha zetu za zamani. Ulikuwa ukipenda sana kuchukua picha zetu nyingi na kuzirusha Facebook kipindi hicho..)" Lexi akasema.

"I don't know what you're saying (sijui unachokionhelea)," Azra akamwambia.

"Its true. I can prove it to you (ni kweli.. ninaweza kukuthibitishia)," Lexi akamhakikishia.

"And then what? I become... Azra... your beloved sister? Everything'll just change... your gang'll just forget I killed one of you? That I'll switch sides, join you, and live happily ever after? (Halafu baada ya hapo? ndiyo nitakuwa.. Azra.. mdogo wako kipenzi? Kila kitu kitabadilika tu.. genge lako litasahau kwamba niliua mmoja wenu? Halafu nitakuja upande wenu, tuishi maisha ya raha mustarehe milele?)" Azra akauliza.

Lexi akabaki kumtazama kwa hisia.

"Ahah... there's no such thing as that. What you're saying, even if it was true, won't change anything. I'm not your sister. I'm not... Azra. I don't want you to prove anything to me. What we've become now has to stay as it is... enemies. You and I, we're enemies. That's the only relationship we got (hakuna kitu kama hicho. Unachokisema hata kama kingekuwa ni kweli, hakitabadili lolote. Mimi siyo dada yako. Mimi siyo Azra. Sitaki uthibitishe lolote kwangu. Tulicho kwa sasa kitapaswa kubaki hivyo hivyo.. maadui. Wewe na mimi ni maadui. Ndiyo uhusiano uliopo baina yetu)," Azra akamwambia.

Lexi akadondosha chozi la huzuni. 

Azra akakunja ngumi na kujiweka katika hali ya pambano. "I'm getting out of here. Alive or dead (ninatoka hapa.. nikiwa mzima au nikiwa nimekufa)," akamwambia.

Lexi akainamisha uso wake chini kwa huzuni. Alitambua kiukweli huyu aliyekuwa mbele yake hakuwa na chembe yoyote ya hisia kumwelekea. Jinsi watu wabaya walivyokuwa wamembadili mdogo wake ilimuumiza sana, na ijapokuwa ilivunja moyo, Lexi hangekata tamaa. Kwa sababu ni Azra pekee kati ya watu wote wa familia yake ndiyo alikuwa amebaki, naye hangekuwa radhi kumpoteza kwa mara nyingine tena. Azra alikuwa amejiweka tayari kuanzisha mapigano na Lexi ili atoroke hapo, lakini Lexi akawa amesimama tu huku anamwangalia kwa hisia.

Ile tu Azra alipotaka kumfata, kengele ndogo ya chumba hiki ikaanza kutoa sauti, na kwa haraka Lexi akatambua kwamba hiyo ilikuwa ni wonyesho kwamba mlango wa chumba ulitaka kufunga. Yaani kutokea alipokuwa amesimama, mlango wa humo haukufungwa, na hiyo ilikuwa ni kwa sababu hakukuwa na mtu mwingine kwa nje. Ikiwa ungejifunga wakiwa ndani bado, basi wangechemshwa wazima wazima kwa kuwa hawangeweza kuufungua wakiwa kwa ndani.

Sehemu ya kibonyezeo cha kuufunga na kuufungua kilikuwa kwa nje, kwa hiyo Lexi akatoka kwa kasi sana kuwahi kabla haujajifunga. Ulikuwa wa chuma na ulifunga kama milango ya lifti ifanyavyo lakini kwa upande mmoja, naye akawahi ulipokuwa karibu kabisa kujifunga na kuuingiza mwili wake katikati, akikanyaga kwa mguu sehemu iliyobaki ili kuacha nafasi kidogo. Hii ilimuumiza sana, lakini akajikaza na kujikakamaza kutokana na msukumo wa mlango.

"Azra... get out!" Lexi akasema huku amekaza meno.

Azra alitenda upesi na kukimbia mpaka hapo, kisha kwa wepesi wake akajitelezesha chini ya uwazi mdogo aliouacha Lexi na kutokea upande wa nje wa chumba hicho. Akanyanyuka na kumwangalia Lexi, ambaye alihitaji msaada wa kuvutwa kwa nguvu, lakini Azra akamsogelea na kumsukumia ndani!

Mlango ukajifunga, Lexi akiwa ameangukia ndani kule, naye Azra alipoangalia kifaa kile kinachoonyesha kiasi cha joto, akaona kiko mwisho kabisa. Akashindwa kuelewa iliwezekanaje mtambo huo kujiweka namna hiyo wenyewe tu, lakini akaamua kuacha hivyo hivyo ili mwanamke aliye ndani aive vizuri. Alimwona Lexi kupitia kioo kidogo sana cha mlango huo akisimama na kumtazama tu kwa hisia, naye Azra akampuuzia na kuanza kuondoka hapo kwa uangalifu. Hangeweza kutambua kwa urahisi mwanzoni kwamba alikuwa chini ya ardhi, kwa sababu palikuwa na mwonekano kama wa nyumba ya kawaida, lakini kadiri alivyosonga akatambua alikuwa chini ya ardhi. Akaziona sehemu za ngazi kuelekea juu, naye akazipanda ili aondoke upesi.

Lexi alihisi kuchanganyikiwa. Alihofia mengi sana kuhusu Azra, lakini pia hali yake ndani hapo. Joto lilizidi kuwa kali na kama angeendelea kukaa humo kwa dakika zaidi ya 15 basi angekufa kwa kukauka. Hakuwa na kifaa cha mawasiliano hapo, na hata kama angepiga kelele wenzake wasingesikia, na alijua wasingekuja huku chini kwa sababu ya yeye kuhitaji muda wa kibinafsi na mdogo wake ambao sasa ulikuwa umevurugika. Ambacho kingekuwa msaada ni ikiwa Azra angefika huko juu na kukutana na mmoja wao, ambaye labda ndiyo angekuja kumsaidia, ila tena na hapo akawa anahofu sana kwa sababu huenda Azra angewaumiza wenzake vibaya mno. Ikaonekana kama ni muujiza tu ndiyo ungepaswa kutokea la sivyo hakuna jambo lolote ambalo lingekwenda vizuri.

Torres ndiyo alikuwa ametoka tu kuoga na kumwacha LaKeisha bafuni kwa sababu walikuwa wanaoga pamoja, na sasa akiwa kwenye sehemu ya chumba chake anajipangusa maji kutoka kwenye nywele zake, akaona jambo fulani lililomshtua sana. Kutokea aliposimama kulikuwa na dirisha pana la milango ya vioo, na kwa hapo aliweza kuona jambo hilo ambalo alijua halingekuwa zuri hata kidogo ikiwa lingefika ndani.

"Holy shit!"

Torres akatamka maneno hayo na kwa kasi akatoka kwenye chumba hicho akiwa ndani ya taulo tu. Alikimbilia upande ule wa kule chini ili kwenda kumwambia Lexi alichoona, lakini njia aliyotumia kufika huko ilikuwa tofauti na ile ambayo Azra aliitumia baada ya kufanikiwa kutoka kule chini. Kwa hiyo wakapishana kidogo tu, naye Azra alimwona Torres, hivyo akajibanza na kumwacha apitilize kwenda huko. Kwa kuwa alitambua angekwenda kwa Lexi, akaona awahi kutafuta njia ya kutokea nje, naye akatoka haraka na kuanza kuelekea sehemu za mbele ya nyumba hii.

Torres alifika kule chini upesi na kukuta taa nyekundu ya chumba kile cha joto ikiwaka. Akashangaa kidogo, naye akasogea karibu zaidi na kumwona Lexi akiwa kwa ndani huku ameinama, akionekana kukosa hewa. Upesi Torres akaizima na kuufungua mlango, kisha akaingia ndani hapo na kumshika Lexi.

"Lexi..." Torres akaita.

"Torres... Azra... she's gone... (Azra amekimbia)" Lexi akasema kivivu.

"Lexi... Zelda's out! (Lexi.. Zelda ametoka nje!)" Torres akasema.

Lexi akamwangalia kwa mshangao, kisha akajitoa mikononi mwake na kuanza kukimbilia nje. Alijitahidi kuwahi kwa kuwa alijua ikiwa angechelewa, basi shida ambayo ingetokea asingeweza kuirekebisha.

Azra ndiyo alikuwa amefika tu usawa wa sehemu yenye eneo pana kidogo lililoelekea mpaka kwenye milango ya kuingilia kwenye nyumba hii, pale aliposimama na kutoa macho kwa mshangao baada ya kushtushwa na kile alichokiona. Milango ilikuwa wazi, na kwenye mwingilio wa hapo alisimama mnyama mwenye kufanana na simbamarara (tiger), lakini ngozi yake ilikuwa nyeupe kiasi yenye madoa meusi yaliyoonekana kwa mbali kutokea mgongoni mpaka miguuni. Mwili wa mnyama huyu haukuwa mnene wala mwembamba sana, akionekana kama duma mweupe. Huyo ndiyo alikuwa Zelda!

Azra alikuwa amesimama, akimwangalia kwa hofu iliyokuwa imeanza kumpanda, naye Zelda akawa anamtazama kwa macho makali. Umbali mfupi ambao Azra alisimama kutoka kwa mnyama huyu ulimwambia kwamba hata akijaribu kufanya nini, asingeweza kushindana na kasi ya mnyama huyo, hivyo ilikuwa ni kifo tu. Ni kama Zelda alikuwa anasubiri mtu huyu mbele yake afanye jambo fulani, lakini Azra akajitahidi kutulia tu kwanza kwa sababu alijua hata akitenda chochote haingekuwa na faida kwake. Woga ule wa msichana wa kawaida ulikuwa umemwingia, ikionekana kama hakuwa na njia ya kuepuka janga hilo mbele yake.

"Zelda!"

Sauti ya Lexi ikasikika kutokea upande mwingine wa sehemu hiyo, akiwa tu ndiyo amefika hapo. Azra akamwangalia, naye akamwona na Torres akiwa nyuma ya Lexi kwa njia ya kujificha, huku Lexi akipiga hatua taratibu kuja mbele. Azra akatambua sasa kwamba Zelda alikuwa ni huyu mnyama, na aliyemfuga ni huyo mwanamke aliyekuwa anasisitiza wao ni ndugu.

"Zelda... look at me. Look at me girl... look at me..."

Lexi akawa anajaribu kumsemesha Zelda ili asimkazie fikra Azra, naye Zelda akamwangalia Lexi. Victor alikuwa anatokea chumbani kwake kule juu huku akitafuna nyama ya kwenye paja la kuku, na baada ya Torres kumwona akamwonyesha kwa ishara kuwa arudi upesi. Ijapokuwa hakuelewa, akarudi na kuchungulia kutokea huko huko kuona yaliyokuwa yakiendelea, naye akashtuka sana.

"That's it... that's it... look at me. That's a good girl..." Lexi akaendelea kumsemesha Zelda huku akipiga hatua za taratibu kumwelekea.

Azra, kwa kufikiria sasa angeweza kujitoa hapo, akapiga hatua mbili nyuma, naye Zelda akamwangalia.

"No! Azra... don't... move!"

Lexi akamsemesha Azra kwa sauti yenye tahadhari kubwa sana kumzuia asijongee, na pumzi za Azra zikaongeza uzito kwa kuwa sasa Zelda alimwangalia kwa ile njia ambayo alijua ni ya mauaji.

"Zelda... look here, look here... she's my sister... don't you dare...."

Lexi alipokuwa anaendelea kumsemesha hivyo, LaKeisha akawa amefika hapo, karibu na Torres, na baada ya kuona hayo, akaanza kumsogelea Lexi pia taratibu.

"Lexi... ametokaje huyo?" LaKeisha akauliza.

Lexi alipokuwa anaendelea kukaribia zaidi upande wa Zelda, hofu ikamjaa baada ya kuona jinsi Zelda alivyochezesha mkia wake na kuonyesha utayari wa kumshambulia Azra kwa kunguruma kidogo.

"Shit!"

Lexi akapiga kelele hivyo na kujirusha kwa kasi yote baada ya Zelda kujifyatua na kumfata Azra kwa kasi. Lexi alijirusha upande aliosimama Azra, ambaye alikuwa ameanguka chini kwa hofu kubwa iliyompata, naye Lexi akakutana hewani na Zelda, hivyo akampamia na kuanguka naye sakafuni na kufanikiwa kumshikilia shingoni.

"Keish!"

Lexi akapiga kelele namna hiyo, naye Azra akashtukia anashikwa mkono wake na Lakeisha, ambaye alianza kumvuta ili waelekee chumbani upesi pamoja na Torres. Lexi akajitahidi kumng'ang'ania Zelda ili kumzuia asimuumize mtu, lakini Zelda akamshinda nguvu na kwa hasira kumkwarua sehemu ya juu ya kiganja chake. Lexi akahisi maumivu sana na kumwachia, naye Zelda akaanza kuelekea kule mbele kuifata nyama yake.

"Anawafata! Pigeni lock!"

Lexi akawaonya wengine namna hiyo kwa sauti ya juu kutokea alipokaa. Torres, Lakeisha na Azra waliingia kwenye chumba kile ambacho Mess Makers walikuwa na kawaida ya kufanya mikutano kwa pamoja na kukifunga kwa ndani. Kilikuwa na milango ya vioo, hivyo ni wakati tu wamerudi nyuma ndipo wakamwona Zelda akifika hapo na kutishia kupita lakini akajigonga. Azra alikuwa anapumua kwa hofu sana, huku Torres nusu adondoshe taulo! LaKeisha akasogea mpaka karibu na mlango huo na kuanza kumfokea Zelda, akimwambia aondoke haraka sana. Mnyama huyu alikuwa anamwangalia tu kwa njia ya hasira, naye akaanza kuzunguka kuzunguka hapo kwa dakika kadhaa, kisha akaondoka.

Kwa hapo, ni Lexi na Lakeisha pekee ndiyo ambao Zelda alikuwa amewazoea, na mtu mwingine aliyemzoea alikuwa ni Kendrick, kwa sababu kwa muda ambao Lexi alimchukua na kumfuga, ni watatu hawa tu ndiyo ambao alikua akiwa karibu nao miaka michache nyuma. Kwa hiyo wengine angewaona kama maadui, na ndiyo sababu muda mwingi alifungiwa kwenye nyumba yake ndogo mpaka aidha ya watatu hao washughulike naye. Mara zote ambazo wengine wangeambiwa kumsafisha, haikumaanisha walimkaribia na kumsafisha yeye Zelda, bali kusafisha sehemu aliyokaa kwa kutumia njia za uangalifu.

Baada ya Zelda kuwa ameondoka hapo, LaKeisha akamgeukia Torres na Azra, ambao walikuwa wanatazamana kwa njia yenye kuonyesha uajabu fulani hasa kutokana na hali ya Torres ya kuwa kifua wazi na kuvaa taulo tu, naye Torres akaelekea upande mwingine wa chumba hicho na kuketi.

"Are you okay? (uko sawa?)" Lakeisha akamuuliza Azra.

Lakini binti akabaki tu kumtazama.

"Don't worry. Your sister will take care of that. Just stay here (usijali.. dada yako atashughulika na hilo. Wewe kaa tu hapa)," LaKeisha akasema.

Kisha akatoka hapo mlangoni na kumfata Torres. Torres akamwambia LaKeisha aende kuangalia kama Lexi alihitaji msaada, lakini LaKeisha akagoma kwa kusema Lexi angemalizana na Zelda mwenyewe. Kihalisi alikuwa hataki tu kumwacha Torres peke yake na Azra huku akiwa bila nguo, kwa kuhofia labda eti kuna vitu vingetokea baina yao. Wivu huo.

Ilikuwa ni ajabu sana kwa Azra kwa sababu hakuelewa nia ya watu hawa kufanya mambo yote haya ilikuwa ni nini. Bado alihisi ni kama anafanyiwa mchezo, lakini akifikiria jinsi ambavyo mwanamke yule alijitoa kuokoa uhai wake, akili yake ikazidi kuchanganywa sana. Akakaa tu kwenye kiti kimoja humo, ikiwa ni kama ameshasahau kuwa dakika kadhaa nyuma lengo lake lilikuwa ni kutoroka hapo, naye akatulia tu akitafakari mambo mengi.

Zelda aliporudi kule alikomwacha Lexi, alimkuta akiwa amejiegamiza kwenye ukuta huku ameshika kiganja chake kusitiri maumivu. Pamoja na huyu kuwa mnyama, lakini alielewa kwamba mtu huyo aliyempenda alikuwa akiumia, naye akamsogelea mpaka karibu na kuanza kufanya kama jinsi paka huwa wanafanya wanapokuwa na mtu waliyemzoea. Akawa anasugua-sugua kichwa chake kwenye shingo ya Lexi, lakini Lexi alionyesha wazi kwamba alikuwa amekasirika kwa kuwa hata hakumwangalia.

"I told you to stop. Why didn't you listen to me? (nilikwambia uache.. kwa nini hukunisikiliza?)"

Lexi akamuuliza hivyo kwa sauti ya chini. Lakini mnyama huyu alikuwa anamwangalia tu, naye akaketi pembeni yake kwa njia ya kujilaza akimuegamia. Lexi alikuwa na hasira, lakini hakuwa na hasira na Zelda, bali baada ya kuwa ametafakari mambo yote yaliyotokea na kujua chanzo chake ni nini, ndiyo ikamfanya ahisi hasira kali sana. Lakini kwanza, angehitaji kumshawishi mnyama wake arudi kwenye nyumba yake ndogo kule nje ili aje kushughulika na mambo mengine. Kutokea vyumbani, sauti ya Victor ikasikika ikiuliza kama mambo yalikuwa shwari, naye Torres akasema atulie mpaka Lexi aseme jambo fulani.

Lexi akajinyanyua taratibu, naye Zelda vile vile akasimama. Akaelekea pamoja naye mpaka sehemu ya jikoni na kutoa mfuko wenye nyama iliyochomwa na kuhifadhiwa, kisha akaanza kuelekea nje pamoja naye mpaka kwenye nyumba yake ndogo. Akamfungulia, na upesi Zelda akaanza kula. Lexi akamwangalia sana mnyama wake, akijua hakuwa na makosa katika haya yote, ila aliyekuwa na makosa alikuwa ndani. Akamwacha na kuufunga mlango wa hapo kisha kurejea kule ndani. Alipokuwa akielekea kwenye chumba ambacho Torres na wengine walikuwa, akapaaza sauti kwa Victor kumjulisha kwamba mambo yalikuwa sawa, naye akafika kwenye chumba kile.

LaKeisha akamfata na kuuangalia mkono wake uliokuwa umeumia, naye akatoka haraka kwenda kufata boksi la huduma ya kwanza. Torres akasema angekwenda kuvaa nguo na kurejea, hivyo hapo akabaki mtu na "dada yake." Wakawa wanaangaliana sana, naye Lexi akamsogelea karibu zaidi. Wakati huu Azra hakujiweka tayari kwa pambano, kwa kuwa kufikia hapa aliona kweli Lexi hakuwa na nia mbaya naye.

"Are you okay?" Lexi akamuuliza.

Azra akaangalia tu pembeni.

"I'm sorry. That won't happen again (samahani.. hiyo haitatokea tena)," Lexi akamwambia.

"So you set loose your pet lion and put on a show in order to win my trust? (kwa hiyo ukamwachia simba wako wa kufugwa na kufanya hayo maigizo ili kunifanya nikuamini?)" Azra akauliza kimtego.

"Look bitch... (Ona malaya wewe...)" 

LaKeisha akawa amefika na kuanzisha maneno.

"This woman here just bust her ass to save yours, and that's how you thank her? (huyu mwanamke hapa ameumia ili kukuokoa wewe, halafu hivyo ndiyo unavyomshukuru?)"

"Keish..." Lexi akajaribu kumzuia.

"Keish nini? Unajaribu kumsaidia halafu anazingua kifala tu? You should have just let Zelda eat her! (..ungemwacha tu Zelda amtafune!)" LaKeisha akasema kwa kuudhika.

Azra akawa anamwangalia kwa hisia kali.

"Okay inatosha. Siyo makosa yake, you know that," Lexi akamwambia Lakeisha.

"Whatever," LaKeisha akasema.

Akauchukua mkono wa Lexi ili aanze kuupaka dawa. Lexi akamtazama mdogo wake kwa hisia sana, huku Azra akimwangalia kwa njia ya kufikirisha kwamba hakujali.

"Look... a lot is going on that I haven't figured out yet. But that's not going to stop me from doing what I know to be right... make up to you. I wanna make up for all that time that we've spent apart. I want to show you what we were... and what we can become... together. I want you to stop thinking of yourself as nothing but a weapon. I don't think of you as a weapon. You're not a weapon. You're my sister Azra. And I'm never ever gonna give up on you... ever," Lexi akamwambia kwa hisia.

Alikuwa akisema ingawa kuna mambo mengi yaliyoendelea ambayo hata yeye hakuelewa, hangeacha kufanya jambo lililo sahihi na muhimu zaidi, yaani kumwonyesha upendo aliostahili na alioukosa kwa muda mrefu kwa sababu ya kutengana kwao. Akamhakikishia kwamba yeye hamwoni kama silaha, hivyo naye alipaswa kuacha kujiona kama silaha tu. Hangemkatia tamaa kamwe, kwa sababu alikuwa ni mdogo wake kiukweli.

Azra akaanza kulengwa na machozi, lakini akageukia upande mwingine ili kutoonyesha hisia zake. Hata akawa anajiuliza alikuwa amepatwa na nini. LaKeisha akaangaliana na Lexi, naye akampa tabasamu hafifu la kumtia moyo.

"What happened here? (nini kimetokea hapa?)"

Wote wakasikia swali hilo kutokea nyuma, na baada ya kugeuka wakakuta ni Victor pamoja na Kevin. Ni Kevin ndiye aliyekuwa ameuliza hivyo.

"Zelda ndiyo amekufanya hivyo? Dada yako amekuletea majanga huyo," Victor akamwambia Lexi.

"Na wewe ulikuwa wapi?" LaKeisha akamuuliza Kevin.

"Chumbani... nimelala. Hizo vurugu zote zilikuwa za nini?" Kevin akauliza.

"Zelda kaingia ndani. Una bahati haukutoka la sivyo angetafuna scones zako hahahahah..." Victor akatania.

Lexi akawa anamtazama Kevin kwa mkazo sana.

"Ni sawa kumwachia huyo mdogo wako namna hiyo? Ameshaiona na nyumba hii, na sura zetu, sasa nini kitafuata?" Kevin akauliza.

Wakati huu LaKeisha akawa amemaliza kuufunga mkono wa Lexi kwa bendeji, naye Torres akaingia hapo tena.

"Kufikia hapo inamaanisha Lexi anamwamini vya kutosha kutotusaliti, si ndiyo?" Torres akaongea.

"Kwa jinsi mambo yalivyo, sidhani kama kumwamini inahusu. Ni suala la yeye kutotusaliti. Lexi, huyu ni mdogo wako sawa, lakini kwa hii miaka yote ambayo imepita hajakuwa pamoja nawe. Ameishi maisha tofauti, na anafanya kazi na maadui. Anaweza hata kuigiza kwamba atakuwa upande wetu halafu akatugeuka. Umeshawaza kuhusu hilo?" LaKeisha akamuuliza.

Lexi akamtazama Azra, ambaye sasa alikuwa anamwangalia pia.

"Ndiyo. Nimeshawaza kuhusu hilo. Nitafanya kila kitu ndani ya uwezo wangu kumfanya anikumbuke," Lexi akasema.

"Lexi... amejaribu kukuua mara kadhaa, hata leo. Una hakika gani hatafanya kitu kibaya kwako au kwetu? Huyu siyo mtu uliyekua naye, ni mtu tofauti sasa. Amefundishwa kulenga tu shabaha, na siyo kuingiza hisia. Utambadilisha vipi?" Torres akauliza.

Lexi akamsogelea karibu zaidi Azra.

"Sitambadilisha. Atabadilika yeye mwenyewe. I know her. I believe in her," Lexi akawaambia huku anamtazama Azra.

Azra akawa anamtazama pia kwa hisia.

"Yaani kama siyo yeye, basi ni huyo simba wako ndiyo atakuja kutumaliza. Lexi dada yangu naheshimu sana mambo yako, lakini kiukweli unapotea, sitakuficha," Kevin akaongea.

"LaKeisha, take her to your room (mpeleke chumbani kwako)," Lexi akasema.

"What?!" LaKeisha akauliza kimshangao.

"Tunamfunga au hivyo hivyo tu?" akauliza Victor.

Lexi akamwangalia mdogo wake kwa umakini, kisha akasema, "Hakuna haja ya kumfunga. She needs to be free (anahitaji kuwa huru)."

Azra akaangalia chini tu.

"Free? Ahahahah... boss atapenda sana hii. Yaani nawaambia kesho kesho-kutwa sisi wote tutakuwa mikononi mwa Jacob kwa sababu ya huu upuuzi," Kevin akasema.

Torres akamsogelea Lexi karibu na kumuuliza, "Are you sure? (una uhakika?)"

Lexi akatikisa kichwa kukubali. Alionyesha kwamba anamwamini Azra, kwamba ingawa yeye bado alionyesha ugumu wa kuamini yale aliyoambiwa, lakini moyo wake ulijua ni ya kweli. Aliamini kabisa kwamba Azra alimwelewa, na hapa alikuwa anafanya kama kipimo cha imani yake kwa mdogo wake. LaKeisha akamwambia Azra amfuate ili ampeleke kwenye chumba kimoja hapo, na baada ya Azra kumtazama Lexi kwa kifupi, akawapita wote na kumfata LaKeisha taratibu.

"Yaani ni katoto tu, lakini mambo kanayofanya! Hivi ana miaka mingapi?" akasema Victor.

"Atakuwa kwenye 22 sasa, si ndiyo?" Torres akauliza.

Lexi akatikisa kichwa kukubali.

"Mtakuja kujijambia katakapowafanya myeyushwe. Sasa hivi mnaniona mjinga, lakini mtakuja kuona," akasema Kevin.

"Ah, we' kijana, yaani huachi tu!" Victor akasema kwa kukerwa.

Lexi akashusha pumzi, kisha akamfata Kevin na kumtandika kofi zito usoni!

Torres na Victor wakashangaa kiasi, na wakati tu Kevin alipomwangalia Lexi kwa hasira, Lexi akampiga ngumi mbili za kasi usoni, kisha akamtandika teke la tumbo, na hapo hapo kumnyanyua kwa nguvu sana na kumrusha mezani! Kevin alidondokea mpaka kwenye viti na kusababisha vishindo vilivyosikika mpaka kwa Lakeisha na Azra walipokuwa wamefika tu huko juu, naye LaKeisha akamwambia Azra waendelee tu kwenda kwa sababu hakukuwa na shida.

Kevin akajinyanyua akiwa amechanganywa sana na Lexi, hata Torres na Victor wakawa wanamuuliza anafanya nini, lakini akamfata tena Kevin na kuanza kumtandika hapa na pale kwa hasira sana, na kwa kiburi Kevin akawa anarusha ngumi pia. Akampiga moja usoni, na kwa hasira Lexi akamtandika kwa mtindo wa haraka uliosabahisha amuumize Kevin sehemu ya nyonga. Jamaa akaanza kujivuta chini hapo akishindwa kunyanyuka, hivyo ikabidi Victor aende kumsaidia. LaKeisha akawa amerejea na kukuta hilo zari, naye akauliza nini kilikuwa kinaendelea bila kupewa jibu. Torres akamshika Lexi na kumuuliza alikuwa ana tatizo gani, naye Lexi akauvuta mkono wake kwa hasira kutoka kwake na kumsogelea Kevin usoni.

"Najua ni wewe ndiyo uliyeifunga steam room. Najua ni wewe ndiye uliyemfungulia Zelda. Kevin ninakuonya. Ukija rudia kufanya jambo lolote lile kumwelekea Azra, au hata kusema tu, hautapaswa kuwaza tena kuhusu sisi kuyeyushwa. Kwa sababu nitahakikisha wewe ndiyo unayeyuka... milele," Lexi akamwambia kwa mkazo.

Wote wakawa wanamwangalia kimaswali sana, naye akaondoka hapo akiwa ameudhika haswa. Victor akamwachia Kevin kwa njia ya kumsukuma kidogo, naye akamwangalia huku anatikisa kichwa kwa kusikitika. Wote wakaondoka na kumwacha jamaa humo akiwa anaugulia maumivu kwenye kiuno chake, lakini pia akihisi aibu na hasira kwa sababu ya kile alichofanya kutofanikiwa na kuumbuliwa.

Lengo lake siku hii lilikuwa ni kuwamaliza dada wawili bila yeye kujulikana, lakini tena mpango wake ukakwama. Alidhani hakuna mtu ambaye angetambua ilikuwa ni yeye ndiyo alifanya yale, lakini sasa akatambua kwamba alikosea sana. Kuanzia wakati huu kiwango cha kumwamini kutoka kwa wengine kingepungua, naye alijua kuna siku tu ambayo watu hawa wangeamua kumalizana naye, hivyo kwa jinsi akili yake ilivyokuwa mbovu, akaanza kufikiria tena cha kufanya ili kuwakomoa.

Hakuna yeyote aliyekuwa ametambua kuwa wakati LaKeisha aliporejea huku, Azra alikuja pia na kuona kilichotokea. Alimwona Lexi alipomwongelesha Kevin maneno yale, naye upesi alirudi kwenye chumba kile alichopewa na kujifungia. Alikaa akiwaza mambo mengi sana. Bado akili yake ilimwambia alipaswa kujihami mno, hasa kutokana na mafunzo yake ya kutomwamini yeyote yule, lakini kuna hali fulani ndani ya moyo wake iliyokuwa ikimsukuma kuamini kwamba Lexi alikuwa ni mtu mzuri kwake.

Sasa alichobaki akijiuliza kilikuwa ni kitu kimoja; angefanya nini kuhusu haya yote?


★★★★★★★★★★

 ITAENDELEA

★★★★★★★★★★

Previoua Next