Reader Settings

Karibu  na jiji la Paris kulikuwa  na jumba kubwa  ambalo lilikuwa limejaa kijani kibichi , lililojengwa kwa  mtindo wa baroque, usanifu wake ulikuwa mkubwa sana na  kila  kitu kilikuwa kikijielezea.

Mwanaume  wa kizungu alionekana akipata kifungua kinywa  nje ya kibaraza  kilichozungukwa na nguzo nyeupe.

“Master! Bi Somerset amewasili” Mwanaume alievalia nguo za kinadhifu za  uhudumu wa nyumba aliongea kwa lugha ya kifaransa.

Yule mwanaume mara baada ya kusikia kauli hio ,  aliishia kutingisha kichwa chake bila ya kubadili muonekano wake huku akijifuta midomo na kitambaa.

“Mkaribishe ndani”

Haikuchukua muda mrefu  baada ya mhudumu kuondoka ,  mwanamke mrembo sana wa kizungu alievalia gauni   jeupe aliingia.

“Haha.. congratulations  to Miss Silyvie , the new president of the Set Association”

Mwanaume yule mara baada ya kumuona mwanamke huyo mrembo akiingia uso wake ulibadilika na kuweka tabasamu la ucheshi huku akimpatia pongezi Silvia.

Silvia aliekuwa na tabasamu usoni , aliishia kunyoosha mkono wake na  kusalimiana na yule mwanaume.

“Mr Leibson , kama  isingekuwa wewe kuwahonga  wafanyakazi wote wa Set , mambo yasingeenda vizuri kama hivi”

Mwanaume huyo mzungu alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa wa siraha , Leibson ambae alikutana na Hamza siku chache nyuma  katika  Alice’s Party.

“Nilishawahi kusema ,  kwenye huu ulimwengu hakuna kitu ambacho hela haiwezi kununua. Haijalishi ni  mtazamo gani unao , haijalishi  una msimamo namna gani , kila kitu ni upuuzi mbele ya hela , ili mradi  pesa  iwe mbele  kila kitu kinaweza kutekelezeka”Aliongea Leibsoni huku akicheka  kwa  kujikweza.

“Ndio sasa ninaamini , hakika  Mr Leibson   una busara sana upande huu”Mara baada ya kucheka kidogo alimpa ishara Silvia kukaa  na yeye mwenyewe alichukua jukumu la kummiminia chai.

“Madam Silvie , sasa umeshakuwa raisi  wa Set, unapaswa kuanza kutimiza ahadi  na  kumzingatia rafiki  yangu”Aliongea  kwa sauti iliojaa zaidi ya maana.

“Bila shaka nakumbuka vyema. Soko lote la siraha la  Black Market ya Sharia  litakuwa chini  yako , Mr Leibson..”

“Miss Silvie  mimi sina ukosefu wa hela , kwangu hela ni namba tu . Ninachotaka ni muda wa kuzifurahia hela zangu”

“Najua” Aliongea Silvia na tabasamu “Unachohitaji ni maisha marefu, hivyo unaitaka dawa ya  kifo, si ndio?”

“Nataka kuendelea kuwaona wewe na mwalimu wako Mr Black . Nataka kujifunza namna ya kuishi milele  na ili mradi  nitaweza kutunza mwonekano wangu , nipo tayari hata kukugawia  nusu ya utajiri wangu”

“Oh! Nusu ya utajiri wako ,  ni hela nyingi sana , naweza kununua nchi kadhaa Africa”

“Mh! Familia yetu imekuwa ikiendesha biashara ya uuzaji wa siraha  kwa zaidi ya miaka mia moja sasa. Nusu ya  utajiri wetu unatosha kununua  nusu ya bara lote la Africa”Aliongea Leibsoni kwa kujivunia.

“Wewe ni tajiri mno , ila  haujikwezi , ndio maana  Gwiji kama Skellidoni  unaweza kumuendesha utakavyo , Mr Leibson..”

“Haha.. Skellidoni mwenyewe wakati alipokuwa mdogo , alikuwa na  binti  yake ambae ni mchawi. Alidhani hakuna anaefahamu , lakini angewezaje kuuficha ukweli nisijue? Nikaona kama nitaweza kumtawala binti yake nitakavyo   si  yeye  pia atasikiliza kila ninachomuambia? Sio yeye tu , ili mradi  nikifanikiwa kuishi maisha marefu , kama nipo tayari naweza  kuwafanya na magwiji wengine wote kuwa chini yangu , Hela  na siraha za kutosha zinaweza kunifanya kuutawala  ulimwengu wote”Aliongea Leibson na kisha alisimama na  kupanua mikono yake.

“Kitu pekee  ambacho siwezi kutawala  ni uhai wangu , lakini lazima niishi muda mrefu”

Tabasamu ambalo halikuwa tabasamu , lilionekana katika uso wa Silvia

“Inasikitisha , Awamu hii Mr Leibson , hujaweza kumtawala ikatosheleza..”

“Unamaanisha nini?”Aliuliza  huku akishangaa.

“Lucifer ashanifahamu tayari. Mchezo  kati yangu na Skellidoni  ulishatambuliwa na  Lucifer , hivyo ni sawa na kusema watu wengine  muda si mrefu  wataweza kuanza kunishuku”

“Usiwe na wasiwasi , Lucifer anaweza kuwa na nguvu lakini  Skellidoni aliniambia yeye mwenyewe jana usiku , ana  mbinu ya kuweza kumuua Lucifer. Nina uhakika muda si mrefu nitapokea taarifa za kufurahisha kutoka kwa Skellidoni”

“Mh ni hivyo?” Silivia aliguna na kucheka kikauzu “Lakini mpelelezi wangu  ameniambia Lucifer ,  namaanisha Skellidoni ameuliwa na Lucifer” Leibsoni mara baada ya kusikia hivyo aligeuka kwa mshangao.

“Nini!? Inawezekanaje?”

“Kwamba hauniamini? Unaweza kutuma mtu kwenda kuchunguza kama ni kweli  na sio kusubiri taarifa nzuri , kwasababu Skellidoni hawezi kukuletea hizo  taarifa tena”

Leibsoni haraka haraka alituma  mhudumu  kwenda kuchunguza na hazikuchukuwa hata  dakika kumi taarifa iliweza kurudi  na kuambiwa Hamza yupo hai na Skellidoni hafahamiki alipo.

Mara baada ya kusikia taarifa hizo , Leibson hasira zilimvaa na kupiga kofi meza na kupasua pasua vikombe.

“Mr Leibsoni kama unataka kuonana na mwalimu wangu , hakuna shida  lakini  vigezo vinapaswa  kuzingatiwa  na  ni wewe  kulimaliza hili suala vizuri  ili  mwalimu wangu kukuruhusu kuonana nae”Aliongea na kisha alisimama.

“Lucifer ana kila sababu ya kutufanya tufeli. Anatisha  zaidi kuliko miaka mitano iliopita. Kama tusipommaliza , hata kama tukianzisha mipango yetu , tunachokaribisha ni vita nyingine takafifu. Ni matumaini yangu wewe na watu wa  jamii yenu ya muungano  wa siri  mnalizungumza hili  na kujua ni namna gani mtaweza kummaliza. Ni yeye pia ambae amefelisha mpango wa kutengeneza dawa ya kifo  mwanzo , au  nakosea?”Aliongea na kumfanya Leibsoni kung’ata meno kwa hasira na  kisha akaongea kwa sauti nzito.

“Najua , huyu Lucifer , nimemchukulia poa sana ,ila dawa yake inakuja”

Silvia  hakuongea neno  na alitembea kimadaha kutoka ndani ya aneo hilo  na ile anapita eneo la bustani  aliweza kukutana na  msichana mnene kiasi, mwenye nywele zake za dhahabu  na macho ya bluu , alikuwa ni binti  wa  Leibsoni aliefahamika kwa jina la Barbara.

Dakika ambayo Barbara alisogeleana karibu na  Silvia , macho yao yalikutana na palepale  midomo yao ilicheza na kuonyesheana tabasamu lisilo la kawaida.

*****

Hamza aliendesha gari moja kwa moja mpaka hospitalini , Mganga mkuu na mkurugenzi wa hospitali  alikusanya kundi la  watumishi wa  hospitali hio na kuwasubiria  nje  kuwapokea.

Hamza hakujali sana  mapokezi hayo na aliishia tu kutoa maelekezo  haraka , kwamba mke wake apatiwe  wodi ya daraja la juu kabisa  na kisha afanyiwe vipimo  vya mwili mzima.

Mpaka inatimia mchana ,  vipimo vilionyesha hali ya Regina ilikuwa sawa  kabisa. Huku madaktari wakienda mbali na kusema alikuwa na  afya  tena zaidi ya afya nzuri na  ni kwamba tu  muda huo  kapoteza fahamu kwasababu ya uchomvu , hivyo wangempa dripu  za virutubisho na kumsubiri aamke mwenyewe.

Hamza alitaka kuendelea kukaa hapo wodini , lakini Nyakasura alipanga kuondoka Ufaransa kurudi Tanzania na ndege ya  saa tisa , hivyo alitaka  kabla ya kuondoka kujua ni kwa namna gani   Hamza aliweza kumdhibiti Skellidoni , mathalani kujua mbinu yake aliotumia.

Kwasababu Nyakasura alimuokoa,  Hamza hakuwa na pingamizi na kumfanya aone, maelezo hayo yalimjumuisha na Rhoda pia.

Hamza hata hivyo hakuwa mtu wa kuficha uwezo wake . Aliamini uwezo wa mtu unategemeana na juhudi zake mwenyewe  na kipaji na kwa hao ambao hawawezi kuweka juhudi kwenye kujifunza , hata kama waambiwe siri zote za  ulimwengu juu ya kumfanya binadamu kiumbe hatari  itakuwa ni ngumu kwao kufanikiwa.

Wawili hao walisogea mpaka eneo lililojitenga  nyuma ya hospitali kando kando ya ziwa la kutengenza . Hakuna aliesogea kuwasumbua  hata baada ya wakati wa chakula  cha mchana.

Hamza alimuomba Black Fog kisu chake  na kisha alitoa maelezo mepesi sana  juu ya uelewa wake mpya juu ya mapigano.

“Ukweli ni kwamba mbinu za nje zimejitosheleza zenyewe kumfanya mtu kuwa na nguvu , kama ilivyo mbinu za ndani . Lakini mahitajio ya mbinu za nje  yanachanganya  sana tofauti na  ule uwezo ambao mtu anazaliwa  nao , ndio  maana watu wanaongeza uwezo wao taratibu taratibu kwa  kukusanya  nguvu ya kiroho na kunyonya nishati ya  mazingira…”

“Mwenyewe nilidhani   ni hali ya  kushangaza sana , kwani mpaka kufikia umri huu nimejifunza mbinu zaidi ya elfu tatu za kumfanya bidanamu kuwa na uwezo wa ziada. Lakini mara baada ya kukutana na shambulizi ambalo lilinifanya  mwili wangu kujihisi  kuwa  dhaifu kiasi kwamba ni kama nimerudishwa katika kipindi nilichokuwa na miaka mitano  ndio nimekuja kugundua , haijalishi utajifunza vipi lakini nguvu unayoingiza ndani ya mwili kutoka nje  ina kikomo chake, tofauti ya ile unayotoa ndani kwenda nje”Aliwaangalia na walionekana kushangaa tu.

“Hamuwezi kunielewa  ninachoongea,  angalieni  namna ambavyo  nitatumia hii siraha  na ndio mtaona”Aliongea Hamza.

Na mara baada ya meneno hayo , Hamza alijituliza na kugandisha macho yake  katika ziwa.

Hamza alikusanya mawazo yake na kuwa kitu kimoja  na kisha  akayabadilisha kuwa nia  na makusudi ya kimatokeo. Kadri alivyokuwa akikusanya  mawazo yake  ndio namna ambavyo misuli yake ilionekana  kumuitikia  vyema na palepale  kwa wepesi  zaidi na  kwa  umakini  mkubwa aliinua ile siraha akiwa ameipa presha kubwa  na  kuipigiza juu ya  maji ya ziwa lile.

Kilichoonekana kilishangaza ,  ziwa lile ilikuwa ni kama  vile ghafla tu kumetokea ukuta  ambao ulitenganisha maji ya ziwa sehemu mbili  na kutengeneza mwinuko mkubwa wa maji.

Ziwa hilo la kutengenezwa lilikuwa na kina cha mita tatu kwenda chini , lakini kupitia kisu kidogo tu  Hamza aliyakata maji na kutengeneza njia ambayo mpaka matope chini yake yaliweza kuonekana. Tukio hilo liliwafanya Nyakasura  na  Rhoda kushangaa mno.

Hawakuweza kuhisi nguvu yoyote  ya kinishati  wala nguvu ya kiroho kutoka kwa  mwili wa Hamza  na shambulizi lake.

“What the hell! Umewezaje kufanya hivi?” Nyakasura alimaka.

“Kila  tunachoweza kukifikia kuna sababu  ndani yake , hili ndio fumbo kubwa  kwetu binadamu tunalopaswa kufumbua,  lakini ukweli mchache  ndio pekee ambao naweza kuelezea kwa  maneno”

Black Fog  yeye pia aliona  haiwezekani kabisa  na alijikuta akichukua kile kisu kutoka kwa Hamza na kukikagua kwa mshangao mkubwa.

“Bro naomba na mimi nijaribu”

Hamza hakuwa na pingamizi lolote na kumuacha   Black Fog kuigiza kile alichofanya.

Lakini kadri ambavyo Rhoda alifanya kama alivyofanya  Hamza hakukuwa na matokeo  ya aina yoyote kabisa na aliishia kupoteza kisu chake ndani ya ziwa.

“Hii inashangaza , nimetumia mbinu sawa kabisa na wewe , lakini kwanini  hakuna kinachotokea?”Aliongea Black Fog akionekana kuchukia.

“Labda utakuwa dhaifu sana?”Aliongea Nyakasura.

“Ndio kusiwe hata na mtikisiko wa maji?”

Unapaswa kuelewa  Hamza kabla hajagusa maji hayo , misuli yake ilikuwa ikionekana kile anachofanya , ni kama  alikuwa akielezea kila kiungo cha mwili wake ni tukio gani anakwenda kufanya.

“Inaonekana uelewa wangu ni mdogo mno , hii mbinu hata kama unifundishe  kwa muda mrefu , sidhani kama nitaweza kuijua”

“Nilishawahi kusikia kuhusu manuio ya kisiraha, lakini inasemekana lazima  moyo wako uwe umejazwa na imani  ya kiroho ,  lakini  kwanini  wewe unafanya  kwa nia pekee bila ya imani? Kama umeweza kugawanya maji ya ziwa basi lazima kutakuwa na  nishati ambayo umetoa  , ila hio nishati sio  ya mbingu   na ardhi wala  haitokani na  nguvu ya kiroho , kama sio hivyo  ni nini?”

Hamza hata yeye mara baada ya kusikia swali la Nyakasura , alikumbwa na hali ya kuchanganyikiwa  , ukweli  aliamini alichofanya ni  nia tu ambayo aliiweka katika  siraha alioshika mkononi , lakini ni kama kulikuwa na  maelezo yalikosekana.

Hamza alijiuliza au  bila kuelewa ametumia aina ya nishati  nyingine ambayo hakuwahi kuifahamu?.

Wakati Hamza akjifikiria ,  sauti ya mwanamke ilisikika na mara baada ya kugeuka waligundua ni dokta .

“Mr Hamza , mke wako  ameamka” Aliongea Dokta.

Hamza mara baada ya kusikia ripoti hio , hakuwa hata na muda wa kufikiria kitu kingine na alikimbia kuelekea wodini.

Nyakasura na Rhoda pia walitaka kujua hali ya Regina ipoje baada ya kuamka hivyo walifuata nyuma.

Mara baada ya kufika kwenye wodi ya VIP , dirisha  lilikuwa limefunguliwa  na kuruhusu mwanga wa jua kuingia ndani  na chumba kilikuwa angavu sana.

Regina ni kweli alikuwa ameamka na alikuwa amekaa  huku nywele zake zikiwa zimeogeshwa  na kuvalishwa gauni la hospitalini na kumfanya aonekane msafi zaidi na wa kuvutia.

‘Wife!”

Hamza  aliita huku akimwangalia mwanamke huyo aliekuwa  ameamka  kwa furaha.

Regina aliishia kugeuza sura yake  na kumwangalia Hamza , Rhoda na Nyakasura na mara baada ya  sekunde sita kupita alionekana  kuwa katika hali ya kushangaa.

“Wewe , umeniita mimi?”

Tabasamu la Hamza lilikakamaa , huku mapigo yake ya moyo yakiongezeka kwa kasi  na aliishia kujilazimisha kutabasamu.

“Mke wangu nini tatizo , acha utani basi  ni mimi”

“Wewe ni nani kwani! Kwanini  unaniita mkeo?” Regina alionekana kukunja sura huku akionyesha hali ya kumshangaa Hamza . alikuwa pia hana furaha huku uso wake ukijaa ukauzu.

“Jamanii , Inamaana aliumia sana  na kumfanya ubongo wake kuathirika  mpaka kumpelekea kupoteza kumbukumbu?!”Aliongea Nyakasura kwa mshangao.

“Hapana , haiwezekani , Sister Regina ni mimi Rhoda , hunikumbuki?”Aliongea Rhoda  kwa wasiwasi.

“Sikujui ,  hapa ni wapi na kwanini  nipo hospitalini?”

Mapigo ya moyo ya Hamza yalikuwa yakidunda kwa hali ya ajabu mno , ile furaha aliokuwa nayo ilipotea ghafla, aliishia tu kujituliza ili kuonekana kawaida na kutokumchanganya Regina zaidi.

“Wife , mimi ni mume  wako , usiwe na wasiwasi , umepoteza tu kumbukumbu zako  lakini  nitakuaminisha  haraka iwezekanavyo mimi  na wewe ni mume na mke , unaweza kuniamini”

“Mimi! , ni lini nimeolewa? Wewe ni nani na  una kusudi gani kwangu?”Regina aliongea kwa kufoka.

Hamza aliishia kukunja sura na kisha alitoka kitandani na kutoka nje na kumwangalia  dokta.

“Wewe si ndio uliesema , mke wangu yupo sawa?”

Dokta  bingwa huyo alikuwa akitokwa na jasho  sio kawaida. Mara baada ya  kusikia  tafsiri , ndio sasa anajua Regina alikuwa amepoteza kumbukumbu  zake  na haraka sana alijielezea.

“Hamza .. Mr Hamza  nitaongea na  watu kuandaa haraka  vipimo  yakinifu  vya ubongo’Aliongea.

Previoua Next