Reader Settings

Deepstate.

Kwa  mtazamo wa Yasin , alijua  Hamza angenywea kutokana na ukubwa wake , lakini matokeo yake ilikuwa ni tofauti. Hamza alionekana  kutokumjali kabisa wala kuwa na hofu.

Yulia kusikia  kauli ya Hamza aliganda kwa sekunde kadhaa , lakini palepale alijikuta akicheka chini chini , katika moyo wake alionekana kuridhishwa   na  Hamza.

“Babe  huna haja ya kuwa na haraka , tuna muda wa kutosha wa kuwa pamoja kwenye ulimwengu huu , ni kwamba tu  mdogo wangu Yasin  amekuja kunipa zawadi ya farasi  na  wewe ndio  umetokea, unaonaje nikiijaribu kwanza?”

“Unajua kupanda Farasi?”

“Ndio najua , nisingejua  kungekuwa na haja ya mimi kujenga banda la farasi nyuma ya hoteli kubwa kama hii , si ingekuwa ni upotevu tu wa pesa?”

Muda huo  Bertha aliekuwa  bize  kuongea na  mwanaume , huku akionekana kumvalisha scarf shingoni alisikika;

“Bosi , nimesikia ukisema  naweza kupanda  mimi  au nimesikia vibaya?”

“Wewe mpenzi wangu amekuja ,  kaa mbali?”Aliongea Yulia.

“Hata mimi  kaa mbali , unadhani  mpenzi wako tu ndio mwanaume , mpenzi wangu  Ayubu pia  yupo hapa  na ni handsome kuliko huyo Hamza wako”Aliongea Bertha huku akijipiga kifua.

“Unaongea nini mpenzi , acha ukorofi basi”Yule mwanaume mtanashati aliekuwa  na  Bertha alimtuliza na kisha  palepale akasimama na kumsogelea Hamza  kwa kujiamini na kumpatia mkono.

“Hello Bro ,  jina langu naitwa Afande Ayubu Masana , kutoka Kambi ya moto. Mara nyingi nakuwa safarini na bosi  Yasin  na ndio mara yangu ya kwanza kukuona.  Mpenzi wangu ana tabia ya ukorofi   naomba radhi kwa ajili yake  na ni furaha kwangu kukutana na wewe”

“Hakuna shaka ,  hakika kweli  ni  mtanashati kunizidi mimi” Aliongea Hamza kwa  dhati kabisa na kumfanya  Ayubu kucheka kidogo na kisha akamsogelea bosi wake.

“Bosi Yasin , ngoja nikailete ile farasi , sidhani kama Kocha ataiweza kuiongoza”

“Sawa Ayubu”

“Ayubu unaondokaje bila  kuniiaga wakati nimekupa zawadi?”Aliongea Bertha huku akimkonyeza.

Ayubu ambae alikuwa akitembea alisimama na kumkonyeza Bertha na  kisha mrembo huyo alisogea  na  walipeana light kiss na kuachiana. Hamza aliekuwa akiangalia wenza hao, mwili wake ulimsisimka  na  kujiambia kweli mapenzi ni upofu.

“Darling , uletewe kinywaji?”Aliongea  Yulia akipokea  glasi ya mvinyo kutoka kwa mhudumu.

“Sipendi kunywa chochote leo”

“Kwanini?”

“Basi tu sijisikii”

“Sister  huyu farasi ninaekupatia kama zawadi , ni wa kipekee sana , kwa kumwangalia tu lazima umpende”Aliingilia Yasin.

“Nina farasi wengi wazuri hapa ,  yupo Holly , Bari na Thera. Nadhani haujapanga kunipatia  farasi  chotara. Banda langu halina nafasi kwa  machotara?”Aliongea Yulia.

“Haha!  Farasi ninaekupatia kama zawadi  ni wa damu  safi kabisa , labda nielezee hivi , kama nisingeweka oda kwa muda mrefu  tokea mwaka jana  huko Asia nisingeweza kuinunua hata kwa msaada wa marafiki zangu”Aliongea  Yasini.

Yulia mara baada ya kusikia hivyo , alijikuta macho yake yakichanua  kwa mshangao huku usiriasi  ukiongezeka.

“Kama umeagiza kwa muda mrefu  hivyo  , bado tu unataka kunipatia mimi?”

“Una kila thamani ya kuwa dada yangu , ndio maana nataka kukupatia kitu ambacho  hela haiwezi kununua kwa wepesi , kama ulishawahi kusikia Ferghana Horse , ndio zawadi yangu kwako”Aliongea  Yasini huku akipiga makofi mengi, wakati huo   Yulia akiwa katika hali ya mshangao.

Moja ya hobi ya Yulia tofauti na watu wengi , ilikuwa ni  farasi , alikuwa akipenda farasi kuliko magari ya kifahari  na hio ilimfanya  kufuatilia aina nyingi ya farasi duniani  na uwezo wao. Hivyo jina la Farasi  aina ya Ferghana halikuwa geni kwake.

“Umelipia shilingi ngapi mpaka kuipata! Nasikia  farasi wa  aina hio hawazidi elfu tatu  duniani?”Aliongea Yulia.

“Hela ni suala dogo sana kwangu . Ijapokuwa  mdogo wako sio tajiri kama wewe , lakini sikosi ya kukununulia zawadi ya Christmas”Aliongea Yasin kwa majivuno.

“Umekuja na bahati leo. Mimi ni mpenzi sana wa farasi  na  ni kwa muda mrefu sana nimekuwa nikizifuga , lakini  sijawahi  kupata damu ya farasi aina ya Ferghana kabisa. Kwanza unajua kupanda farasi?”Aliongea Yulia akimwangalia Hamza.

“Ndio”

“Haha safi sana , unaweza kuendesha utakavyo baadae”Akiongea Yasin

Wakati wakiongea sauti  kali ya farasi iliweza kusikika kutoka mbali.Dakika mbili hazikuwa nyingi  ilionekana gari  ikisogelea eneo hilo  ndani yake ikiwa imebeba Farasi aliekuwa akizunguka zunguka kwa kurudi  nyuma na kwenda mbele.

Yulia mara baada ya kuona farasi ile , macho yake yalichanua akiwa na muonekano kama vile haamini.

“Kama nilivyozisikia sifa za  Ferghana , umbo lake , rangi yake , kila kitu ni kizuri”

Hamza aliishia kumwangalia mwanamke huyo  na  hakika aliweza kuona Yulia alikuwa ni mpenzi mkubwa wa farasi.

Ukisikia pure breed or pure blooded horse  maana yake ni  farasi ambae damu yake ni safi ,  hana mchananganyiko wowote wa damu  kutoka kwenye asili ya chimbuko la uzao wake.  Sasa aina ya farasi hao   ni ghali mno , kuna hadi farasi waliokuwa wakiuzwa kwa mabilioni ya hela  na  ni kwa watu matajiri  pekee kama  Yulia  wanaweza kumiliki aina  ya farasi hao , farasi wa damu safi  ni ghali kuliko  magari mengi ya kifahari.

Mara baada ya  gari ile kusimama ,  walitoka wachina wawili kutoka mbele ya gari   wakiambatana na Ayubu na kusogea upande wa nyuma  na kufungua mlango , sekunde ambayo mlango ulifunguliwa farasi ile iliruka na kutoka  na kwa ustadi wa hali ya juu kabisa kijeshi , Afande Ayubu aliirukia  na kuishika  hatamu zake. Lakini sasa  ile farasi ilionekana kukataa  kumtii  na kuanza kuzunguka ikionekana inataka kumrusha chini Ayubu.

Ayubu  pia alikuwa na nishati za mbingu na ardhi ,  alikuwa akikaribiana na  Bertha , lakini licha ya hivyo aliogopa kuituliza ile fatasi na nishati za mbingu na ardhi kwa kuogopa kuidhuru, hivyo alishuka tu chini na kisha akaishikilia kamba na kuisogeza mbele ya Yulia.

Muda ambao  Ayubu alisogeza farasi hio mbele ya kundi hilo la watu , alikuwa amejaa jasho la kutosha usoni na Bertha haraka haraka alimpatia  kitambaa kujifuta , huku wale wachina wakisalimiana na Yasin.

“Hii farasi bado tu haijatiishwa?”Aliongea Yulia  huku akikunja sura.

“Haha..  hio ni farasi  poli , nimeipata kwa tabu sana ndio maana nimeamua kukupatia makusudi.  Sister , Hamza , mnaonaje mkiijaribisha kuipanda?”Aliongea Yasin huku   akiangaliana na wale wachina na kucheka , ilikuwa ni  wazi   kulikuwa na nia mbaya kwenye macho yake.

“Yasin , unataka kuniua , yaani Ayubu ambae  ana mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi  imemshusha chini  kwa nguvu  bila hata kuiongoza , ni ngumu kuiitiisha farasi kwa muda mfupi,  halafu unataka nijaribu?.”

“Sister kama  ujasiri  huna basi potezea , sitaki ujidhalilishe  kwa kudondoshwa chini kama kifusi.  Hamza vipi wewe  , unaogopa  pia kujaribu?”Aliongea

“Hapana , naweza kuipanda”Aliongea Hamza na kumfanya Yasin kuzubaa kidogo  na kisha akacheka.

“Oh! Nimekumbuka sasa hivi nimeambiwa wewe ni mpiganaji hatari sana, lakini huwezi kutumia nguvu  kuilazimisha ikutii , maana  unaweza kuijeruhi  na itakuwa usumbufu  tena”

“Siwezi kutumia nguvu  na  hii farasi haiwezi kuumia”Aliongea

Yasin aliishia kuongea na wale  wachina kwa namna ya kuwatafsiria  na walionekana kuwa na mashaka na Hamza na  upande wa Yulia alionekana  kushangaa.

“Babe , kuna haja ya kujaribu sasa hivi , hii farasi ndio kali kuliko zote duniani , inachukua muda mrefu sana mpaka kumtii  mtu ..”Aliongea Yulia akiwa na shauku.

Hamza alimshika Yulia kiuno kwa kumvutia kwake  na kisha alimwangalia kwa  tabasamu la ujasiri.

“Unataka kuipanda na mimi?”

Mkao wao ulikuwa   sio wa kawaida , kwa namna sura zilivyokaribiana , Yulia aliweza kuona ni kwa namna gani Hamza alikuwa akijiamini.Mara baada ya kusita kidogo , Yulia aliona ngoja amuamini  ili kuona kama kweli anao uwezo wa kutiisha farasi hatari duniani kama Ferghana.

“Nitakusikiliza , unapaswa tu kunilinda nisiumie”Aliongea Yulia huku akiweka mwonekano wa msichana mdogo.

Mara baada ya Yasin kusikia wawili hao wanakwenda kupanda hio farasi , alijikuta akisota ndani kwa ndani , lakini kwa nje aliwapigia makofi.

“Safi sana , Hamza hakika  una ujasiri. Ndio maana  mwanamke kama dada yangu ameweza kukupenda. Ayubu mpatie  hatamu  Hamza”

Ayubu bila kusita alifanya kama bosi wake alivyosema na kumpatia  Hamza kamba za farasi ile. Lakini Hamza hakujisumbua hata kupokea  kamba zile na  badala yake alimbeba Yulia.

“Naendesha farasi haina haja ya hizo kamba”Aliongea na kauli yake ilimshangaza Yulia na wengine.

“Una uhakika , hii farasi ni kali kama simba!?”Aliongea Ayubu.

Hamza alicheka  kidogo na kisha  akiwa ameshikilia Yulia , hatua moja tu alikuwa asharuka na kwenda kutua kwenye  mgongo wa farasi ile nyekundu.

Ayubu haraka haraka aliachia zile kamba  na kuiachia huru  , huku akirudi nyuma na kukaa mkao wa kumlinda bosi wake.

Farasi ile   mara baada ya kuhisi  kuna mtu katua kwenye mgongo wake , ilionyesha makeke yake kwa mara nyingine kutaka kumshusha Hamza na Yulia  chini. Hata hivyo Hamza hakukasirika  , aliendelea  kukaa juu yake huku akiiangalia  kwa macho makali  yenye  nguvu ya  mkandamizo.

Msisimko wa kimkandamizo ambao Hamza alikuwa akiupeleka kwa farasi  ile  ni mambo aliokuwa ameyafanya kwa kipindi chote cha kuzaliwa kwake ,  alikuwa akivuta kumbukumbu za matukio ya hatari alioyafanya , iwe kwenye vita au kwenye misheni na  kadri alivyokuwa akiikodolea ile farasi macho ni kama alikuwa  akionyesha   nini maana ya kuwa  mtu hatari na ile farasi  ilionekana kuona kitu katika macho ya Hamza na kushikwa na hofu.

Wanyama wako sensitive  zaidi  kuliko binadamu , hususani  mbele ya  watu waliofunikwa na vivuli vya dhambi. Wanyama wanakuwa sensitive kwasababu  ulinzi  wao binafsi upo katika hisia zao na sio kwenye macho.

Hamza mara baada ya kuvua  helmeti  la  upole alilokuwa amevaa  na kuuvika ule uhalisia wake aliokuwa nao miaka kadhaa iliopita , farasi  hio yenye kiburi  hatimae ilimchukulia kama kiumbe hatari zaidi.

“Chii.. chii!!”

Ile farasi iliishia kukoroma kidogo  tu  na kisha  ilishusha  kwato zake chini  bila ya kusogea.

Yasin , Ayubu , Bertha na wale wachina walionekana kutoa macho , huku wakihisi ubaridi kwenye  migongo yao wakati  Hamza akirukia farasi ile , ila kilichowaacha na butwaa ni mara baada ya kuona ile farasi ikitulia .

Hamza aliipiga tumboni ile farasi na miguu yake kwa pamoja na  palepale ilianza kutembea  kwenda mbele kwa adabu  kabisa. Hamza aligeuka kulia na ile farasi pia ilifanya hivyo hivyo.

Yulia mwanzoni alihisi ni ajabu , lakini mara baada ya  kuhisi mabadiliko ya  muonekano wa Hamza , alionekana kuelewa kilichotokea na alijikuta akishindwa kujizuia na kumwangalia Hamza.

“Wewe ni hatari mno ,  ni watu wangapi umeua?”Aliongea Yulia na muda ule Hamza alirudi katika hali ya kawaida  na kisha alimuweka Yulia vizuri mbele yake.

“Mswali gani hayo , unaweza kweli kuwa na mtu kama mimi?”Aliongea Hamza.

“Ngumu kusema sasa hivi , unajuaje , pengine naweza kukupenda  na kuanza kukufauta kama mbwa au kifaranga”

“Unayajua hata mapenzi yalivyo?”Aliongea  na Yulia alisogeza mdomo wake karibu na sikio la Hamza na kumnong’oneza.

“Wewe ndio unapaswa kujiuliza , je  katika moyo wako ulishawahi  kujali kuhusu hisia zangu  mpenzi?  Najua  tokea mwanzo  ulivyochukua hatua ya kunisogelea , hukutegemea mapenzi ya dhati kutoka kwangu , bali ni kwasababu nina kitu unachotaka. Nakuona kama kaa nyamizi anaetafuta gamba , baada ya kupata na kuona halimtoshi  au muda wowote anapoona zuri zaidi  anaachana na  la mwanzo na kuchukua jipya. Kama mimi ni gamba ambalo unahitaji kwa muda ,  kuna haja ya kujali hisia zangu kwako?”

Hamza aliishia kuangalia macho ya mwanamke  huyo mrembo  na kupepesa kwa sekunde , hakujua   ni namna gani anapaswa kujibu. Hio ni kwasababu  ni kweli kabisa  mahusiano yao yalianzia kisiwani  Chole , lakini licha ya siku ile hakuwahi kufikiria mahusiano yao  kwa  uzito kabisa . Kama isingekuwa  Yulia  kumtega na Herbert na kisha kumkasirisha na kupelekea  kupatwa na majanga   na kisha kulipa kwa kufanya nae mapenzi  hakufikiria sana , lakini mara baada ya Bertha kuumia na kuona  Yulia akiwa na wasiwasi , Hamza aliona pengine ipo nafasi ya kumponyesha mwanamke huyo na kumfanya awe na hisia kama  watu wengine.

Muda huo sasa Hamza hakujua hisia zake kwa Yulia ni za namna gani , ni za mapenzi au za kutaka kujaribu kumfanya  mwanamke huyo kuwa na hisia.

Yulia mara baada ya kuona Hamza amenyamaza pasipo kujibu , aliishia tu kucheka na kisha aligeuza uso wake na kumwangalia mdogo wake Yasin.

“Shukrani  kwako  mdogo wangu , hii farasi inaleta hisia tofauti sana. Mimi dada yako nimepokea zawadi hii”

Yasin aliishia kulazimisha tabasamu huku akioneysha ishara kwamba  sio kitu.

Hamza aliendesha farasi na kwenda mbali zaidi na   kundi hilo la watu na muda ule  ndio  Yulia alipata uhuru wa kuongea.

“Ulisema utanisaidia kuimiliki familia ya Wanyika na nguvu yake yote , ni kweli?”

Hamza alikuwa akifikiria kuhusu maneno mengine ambayo Yulia aliongea  na mara baada ya kusikia kauli hio  alijikuta akishindwa kujizuia na kutoa pumzi nyingi.

“Unataka kuongea nini?”

“Yasin ndio mshindani wangu mkuu , ingawa nimefanya vitu vichache vizuri kwa nchi ,  ndani ya  ukoo wangu , nilichofanya  ni kwa ajili ya  nafsi yangu mwenyewe  na sio kwa  manufaa ya familia nzima. Upande wa Yasin amekuwa kidete kwenye kupanua biashara za familia katika masoko ya kimataifa. Na  ndugu wengi  waliopo kwenye bodi wanampa sapoti kubwa”

“Nataka unisaidie kumuua Yasini ,  hakikisha unafanya  kisiri siri na hakuna mtu atakaejua kama nahusika , ukifanikisha , utakuwa umenisaidia jambo kubwa sana”Aliongea Yulia akiwa siriasi.

“Hata kama ni mtoto wa mjomba , lakini bado ni binamu yako   kwa damu kabisa  si ndio, hajakufanyia hila yoyote  kwanini unataka  kumuua?”Aliongea Hamza.

“Katika kupambania madaraka ndani ya familia , hakuna undugu. Mimi wazazi wangu wote wamekwisha fariki na  ndani ya familia nipo mimi kama mimi , kama bado nataka kusimama  lazima niwe kiongozi”

“Kwanini unataka kuwa kiongozi wa familia  ya Wanyika , kwa akili zako  hata kama  sio kiongozi wa ukoo  bado unaweza kuwa na nafasi kubwa katika idara ya sayansi na teknolojia ndani ya nchi ya Tanzania na hio inaweza kuwa  nguvu yako tosha na nchi ndio ingekulinda na hakuna mtu yoyote angekugusa hata awe mwanafamilia”

“Kichwa kikubwa ila ubongo mdogo”Aliongea Yulia  akisonya.

“Hey ! Usidhani kwasababu  ni mpenzi wangu siwezi kukushikisha adabu, ukiendelea kuongea mbovu  nitakupiga makofi ya makalioni “

“Nimesema hivyo sio kukutusi , bali kwasababu hufikirii mbali katika mtazamo wangu , hivi ushawahi kujua nipo katika hatari kubwa kiasi gani?”

“Unamaanisha nini?”

“Unadhani mimi kujihusisha  na Earth Axis  ndio  tiketi yangu ya kujikinga na hatari?. Ngoja nikuambie tu   tunaweza tukawa nyuma katika maendeleo ya sayansi  na  teknolojia , lakini  haiwezi kuwa ngumu kwa  nchi kutafuta mtu mwingine kuifanyia  utafiti na kutafsiri taarifa zake , tupo nyuma kimaendeleo tu ila hatupo nyuma kiakili , kama mimi nimepatikana basi wengine wanaweza kupatikana pia. Sio kwamba hawawezi  ni kwasababu tu  ni kwamba  mimi tayari  washanipa kazi na wanataka kulinda taarifa   ndio maana hawawezi kuruhusu kila mtu kujaribu. Hata kama nikifa leo  au kesho  watatafuta mtu kama mimi mwingine tu ,  wanaweza wasimpate  mrithi wangu kesho , kesho kutwa au miaka mitano ijayo lakini  mwisho wa siku lazima atapatikana tu. Nchi yetu sasa hivi tumetoka katika   kuiendesha kwa manufaa yetu binafsi na tumeimarika kifikra kuangalia ni kipi ambacho nchi inafaidika  na  viongozi kupitia Malibu wamejengewa  mtazamo huo , hivyo  mtu yoyote  kwasasa  mbele ya maslahi ya taifa  ni nyenzo tu ambayo inaweza  kuachwa ikipoteza faida au nyenzo nzuri zaidi ikitokea. Mimi natumika tu  hapa kwasababu ya akili yangu  na kadri ninavyoendelea kutumika ndio thamani yangu inavyozidi kupungua. Unadhani  watanifanya nini kama wakishaona  hawanihitaji tena  huku uwepo wangu ni tishio kwa usalama wa nchi?”

Hamza mara baada ya kusikia maelezo hayo moyo wake ulitetemeka .

“Unamaanisha  wewe ni kama bomu?”

“Inaweza isiwe hivyo lakini  sio mbali  na unachomaanisha. Kwangu mimi kuna njia mbili tu naweza kuzichagua. Ya kwanza ni kuwa kiongozi wa familia ,  nikiwa kiongozi maana yake nakuwa  mkuu wa Deepstate ambae naiongoza nchi nyuma ya pazia , pili kukubali kuendelea kufanya kazi   kwa ajili ya serikali na  kukosa uhuru wangu na kuishi maisha yangu yote kama mfungwa  licha ya mfannikio makubwa nitakayofanya”

Hamza alijikuta akivuta pumzi  nyingi  iliochanganyika na harufu ya bahari,  kwa namna Yulia alivyoongea   ni kama sasa  ameweza kugundua mambo sio mepesi kama alivyokuwa akichukulia.

Ilikuwa kweli kabisa , kipaji ni kama  upanga ukatao kuwili, kipaji na nguvu ya kimadaraka  ndio  huonekana. Kama Yulia hatoweza kuwa kiongozi wa familia , basi   kampuni ya Prima itachukuliwa na  mtu mwingine. Isitoshe  Prima haikuwa kampuni ya Yulia bali ni kampuni ya Familia na alipewa uongozi kwa ajili ya kulinda kile anachokifanya nyuma ya pazia katika kufasiri siri za Earth Axis.

Sasa kama Yulia atapoteza nafasi yake  kama mwenyekiti wa  kampuni  maana yake atabakiwa kuwa na cheo tu cha  mkuu wa idara ya utafiti  na mwanajeshi. Kwa maana hio Yulia hatoonekana uraiani tena na  maisha yake yote yatakuwa  katika taasisi  akitii maagizo ya nchi  kwa utiifu kama  sheria za kijeshi zinavyomtaka na akikengeuka anazimwa haraka.

“Kama siwezi kuwa kiongozi wa ukoo , basi sitokuwa na natasi tena ya kusimama  ndani ya nchi hii na kujilinda  , mimi mwenyewe na uhuru wangu. Yasin anajua  nguvu yangu na akishapata nafasi hawezi kunivumilia na ikifikia muda huo  kitu pekee nitakachoweza fanya ni kuuza  uhuru wangu na kuacha nchi ndio inilinde. Naweza kusema nitoroke  na hela nilizokuwa nazo nikaishi mbali , lakini hakuna ambae ataniacha  niwe salama watanitafuta  na kuniua popote pale”Aliongea Yulia .

Hamza aliishia kumwangalia mwanamke huyo kwa  macho yasioelezeka  akionekana kuwaza pia  na  kisha alitingisha kichwa kwa ishara ya kukataa.

“Sitokusaidia kumuua mdogo wako”

“Kwanini , si ulisema unakwenda kunifanya kiongozi?”

“Kwasababu nikifanya hivyo , hautokuja kuelewa hisia za  ubinadamu zilivyo”Aliongea Hamza.

“Naona bado unaniamini sana ,  kwahio unadhani  nitatoa chozi nikishapatwa na hisia za kibinadamu,  inasikitisha kwasababu pengine muda huo nikiwa na hisia nitakuwa nishapoteza uhuru wangu  tayari”

“Haiwezekani , siwezi kuruhusu itokee”Aliongea Hamza.

“Kivipi! Utaweza kupigana  na nchi kwa ajili yangu ? Haha..acha hizo bwana , usiniambie unao uwezo huo au upo tayari? Mbele yako  unachopendelea zaidi ni mwonekno  wangu ,  pengine miaka  kumi au ishirini ijayo  nitakuwa nimepoteza mvuto na ukaniacha halafu nitafanya nini?”Aliongea kwa kejeli.

“Yulia kwanzia sasa unapaswa kuzingatia jambo moja tu”Aliongea Hamza kwa usiriasi.

“Jambo gani?”

“Nifanye nikupende”Aliongea Hamza akishikilia moyo wake  na kauli ile ilimgandisha Yulia  maana ni kama hakutegemea angeongea hivyo.

“Ili mradi  utakuwa  mwanamke ambae nakupenda kweli , hata  kama  itanipasa kuwa adui wa dunia  kwa ajili yako , siwezi kusita na hakuna wa kunizuia”

Yulia aliishia kumwangalia  Hamza uso wake  wa kimashambulizi  na alijikuta akimeza  mate mengi , alishikwa na hali ya ukimya na kutokujua  aongee nini. Walikuja kushitukia farasi imegeuka na kuwarudisha walipotoka.

“Inashangaza sana!”Aliongea  Yasin  huku akipiga makofi.

“Hii ndio mara yangu ya kwanza kuona mbinu ya namna hii ya kutiisha farasi”Aliendelea kuongea huku wale wachina pia wakitingisha kichwa.

“Sijawahi kufundisha farasi , ila  nilichokifanya ni kuipa  woga. Farasi ni moja ya wanyama wenye akili sana  na wanajua  ni  wakati gani wa  kuhisi woga. Ukweli ipo hivyo hivyo hata kwa   binadamu. Muda mwingine binadamu anaweza kujihisi  sio muoga , ila ukweli  ni muoga  ila  ujinga tu umemjaa”Aliongea Hamza na kauli yake ilimfanya   Yasin  kucheka.

“Kweli kabisa, watu wanapaswa kuheshimu moyo unachowaambia. Ni kama nilivyotarajia kwa  Bro Hamza mtu jasiri aliefanikisha  hata kumuua  mtoto wa  Mzee Kijazi” Kauli hio ilimkumbusha Hamza alivyomuua Herbert Kijazi na kumuacha Himidu kushughulikia kutuliza familia ya marehemu.Ila hata hivyo hakutaka kufikiria sana na alimgeukia Yulia.

“Twende sehemu iliotulia na nitakutambulisha kwa huyu Bro niliekuja nae”

Yulia  alikuwa ashamuona Zade kwa muda mrefu  akiingia katika eneo hilo na Hamza. Ila kwasababu Hamza hakuongea chochote hakutaka kuuliza.

“Sawa , Yasin  mdogo wangu sitokupa kampuni kwasasa , unaweza kumchukua Bertha tu  muondoke nae kwasasa”Aliongea Yulia na kisha aligeuka na  kuwapa ishara Hamza na Zade kumfuata.

Bertha kusikia kauli hio , alipatwa na furaha kwa kuona ndio muda sahihi wa  kutoka out na mpenzi wake.

Kuhusu Yasin , alimwangalia  Hamza na  Yulia wakiondoka  na uso wake ulizidi kujawa na ukauzu na muda ule simu yake ilianza kuita na aliitoa na kuangalia   jina la mpigaji   na kutoa tabasamu mara moja.

“Kanali Dastani, wakati sahihi  kabisa!!”Aliongea huku akiwa na  tabasamu   la kejeli akiendelea kuwaangalia Hamza na Yulia wakitokomea huku simu ikiwa sikioni.

Hamza alifuatishana na  Yulia mpaka  ndani ya ofisi  lakini kabla  hajaongea chochote , Yulia alimgeukia Hamza.

“Nielezee kwanza , ni taarifa  gani za kitafiti za Saidi ulizonipatia?” Hamza mara baada ya kusikia swali hilo alishangaa.

“Nini kimetokea kwenye hizo taarifa kwani?”

Previoua Next