Reader Settings

SEHEMU YA 223.

Black hole

Hamza muda ule  alikumbuka biashara ya vyungu , ambayo ilikuwa ikifanywa na Alex ,  ukweli ni kama suala hilo alilipotezea kwa muda, ni suala ambalo pia lilimgusa rafiki yake Amir , lakini ni kwa muda hakuwasiliana nae tokea  mara ya mwisho  kuachana  Karambezi.

Hamza  aliangalia yule  mrembo wa haja  akipatiwa mzigo wake kwenye boksi na kisha  kutoa kadi ya benki na  kulipa.

“Unaangalia nini?”Alikuwa ni Regina aliegeuka na kugundua Hamza alikuwa akiangalia upande  mmoja.

“Hakuna tu wife” Aliongea Hamza na kisha akarudi kwenye uhalisia

“Wife mbona  hiko kinywaji kifungashio chake kina mwonekano mbaya sana , kwanini ununue?”

“Mimi naona kinavutia”Aliongea   Regina na palepale alikumbuka na Hamza anapaswa kunywa, “ Unataka kuchukua  radha ipi?”

“Ila sio kwenye hicho  kikombe cha kizombi”Aliongea Hamza akicheka.

“Nani kakulazimisha , wewe chagua   kinywaji tofauti unachopenda , hiki nitatumia mwenyewe”Aliongea Regina ,  alionekana kuwa katika mudi nzuri mno , uso wake ulijawa na tabasamu  na kumfanya awe mrembo kama malaika.

Licha ya hivyo  vinywaji hivyo hakukuwa na  radha ya strawberry  zaidi ya kuwa soda. Hamza upande wake  alichukua Coca.

Wawili hao  waliingia ndani ya ukumbi na kuongozwa moja kwa moja mpaka katika siti za wapenzi . Ilionekana  filamu ilikuwa imeshaanza muda mrefu tu. Tofauti  na matarajio  siku hio watu hawakuwa wengi sana, pengine ni kwasababu ya sherehe za christmas watafutaji wengi ambao ni  wapenda filamu wamesafiri .

Walikaa na kuendelea na filamu ambayo ilishakwisha kuanza, Hamza  alimwangalia Regina  ambae alikuwa akinywa kinywaji chake taratibu pembeni yake  na palepale aliinua mkono wake na kupitisha kwenye mabega yake.

Regina alitingishika kidogo lakini  alielewa ishara ya  Hamza  na palepale aliegamia  kwenye bega lake.

Wawili hao hawakuongea neno wakati wakiendelea kuangalia filamu  inavyoendelea . Taratibu Regina alijihisi  kuchoka  kukaa staili moja na alisogea karibu  na kuegamiza kichwa kwenye kifua cha Hamza.

Hamza aliweza kunusa marashi  mazuri kutoka katika nywele za Regina na alishindwa kujizuia na kupeleka mkono na kuanza kuzigusa , zilikuwa laini mno na za kuteleza.

Hamza aliishia kuinamisha kichwa chake na kubusu kichwa cha Regina  bila ya kuwa na nia nyingine , ilikuwa ni busu  la kuonyesha  mapenzi.

Regina aliinua kichwa chake , hakujua  Hamza alikuwa akimaanisha nini kubusu kichwa chake hivyo alimwangalia kwa macho yaliokuwa na kuchanganyikiwa kidogo.

Mara baada ya kuona sura hio ya kipole ,Hamza alishindwa kujizuia na kutaka kumchokoza , hivyo alimshika kidevu na kisha aliinamisha kichwa na kumbusu  lipsi zake.

Regina aliishia kutoa mguno tu  huku akimpiga Hamza  kwenye  mapaja yake  lakini mwishowe aliacha kuleta ukinzani.

Busu hilo lilidumu angalau kwa dakika kumi , wawili hao walikuwa hata wamesahau walikuwa kwenye ukumbi wa sinema , mpaka pale Hamza alivyoshika shati la  Regina.

“No!”

Regina alijikuta akimaka wakati akifungua macho yake na kukumbuka  walikuwa  ndani ya ukumbi  wa sinema.

Hali hio ilimfanya  Hamza kujisikia vibaya kidogo .Hio ni kutokana Regina alipiga makelele kwa nguvu  kiasi kwamba  mpaka  watu waligeukia   upande wao.  Regina aliishia kushikwa na aibu za kike na ilikuwa bahati tu  eneo  walilokuwepo  lilikuwa limejitenga na siti za kawaida na kufanya watu wasione kinachoendelea, lakini walikuwa wakionekana na kusikika.

“I'm sorry, my love is so strong … … you understand.”Aliongea Hamza  akiwaomba radhi wazungu waliokuwa karibu yao. Asilimia kubwa ya watu waliopo ndani ya ukumbi huo ni wenza , hivyo walikuwa wanaelewa.

“Bro , be steady!”Aliongea mzungu akimpa  Hamza ishara ya mkono akimwambia kuwa ngangari.

Kutokana na aibu iliojaa utamu , Regina alijikuta akijitenga mbali na Hamza kidogo na kukumbatia  nguo zake kama vile alikuwa akiogopa kuibiwa.

“Wife kuhusu hili  , sisi ni wanandoa tuliopita mambo mengi , kugusana  kidogo tu sio tatizo”Aliongea Hamza.

“Hapana! Hukunichumbia , hukufanya harusi na mimi , vipi kama nikipata mtoto? Nitashindwa hata kuangalia watu usoni”Aliongea Regina akiwa siriasi.

Hamza  kidogo tu acheke kwa nguvu sana ,  aliona Regina alifikiria mbali sana , mpaka kudhani  angepata mtoto kwa kuguswa tu?.

“Nimekugusa tu , sio kama ungepata mimba bwana”

“Busu tu linatosha , ukienda mbali sikuongeleshi tena”Aliongea Regina akiwa siriasi na kumfanya Hamza apotezee  kwa kuupoza  moyo wake na kisha kuendelea kuangalia filamu.

Ingawa walikuwa wamepitwa na matukio mengi , Hamza na  Regina hawakuwa wajinga hivyo walianza kuelewa.

“Unadhani  ni kweli watu wanaweza kutabiri  matukio yajayo?” Regina alishindwa kujiuliza mara baada ya kuona  mwanamke  sterring akionekana kujua nini kitatokea  katika miaka ijayo.

“Nadhani inawezekana , isitoshe  maarifa tuliokuwa nayo kwasasa ni  hafifu mno, lakini hata sasa kinadharia inawezekana kupindisha muda  na anga, inawezekana hata kuwa nje ya muda  na nafasi , hivyo  sidhani inaweza kuwa ngumu kutabiri”Aliongea Hamza.

“Kuwa nje ya muda na nafasi  unamaanisha kusafiri mbele ya muda? Inawezekana vipi  kusafiri?”

“Hujawahi kusikia natharia ya  uhusiano wa vitu(theory of relativity)? Nadharia hii  inaeleza kwamba wakati kitu chenye uzito  mkubwa kinapokandamizwa  na kuwa kwenye nafasi ndogo sana , kani mvutano  huwa kubwa kiasi kwamba  hupindisha muundo wa anga  na muda(Spacetime). Mvutano huu  unakuwa mkali kiasi kwamba hata  mwanga hauwezi  kutoroka  na eneo hilo ndio hujulikana kama shimo jeusi(Black Hole). Sasa wanasayansi wanaamini uwepo wa Black Hole unaweza kutengeneza uwezekano wa kusafiri  mbele  ya muda”

“Ni kweli! Unamaanisha kwamba kadri kitu kitakavyokuwa na mass kubwa , ndio  kinasababisha  athari kubwa kwa ulimwengu  na ikifikia hatua flani  muda na  anga  huathirika?”

“Ni kama hivyo mke wangu , hebu chukulia mfano huu , chukulia anga lote juu ni kama kitambaa  kilichotandazwa ,  ukiweka kitu  chenye uzito juu ya hiki kitambaa kinabonyea  kwa kuchukua nafasi na kutengeneza mlima  wa shimo  si ndio? Sasa kama kuna vitu  vidogo  ambavyo havikuwa na uzito mkubwa na sasa umeweka kitu chenye uzito ,vitu hivyo vyote vitaangukia au kusogelea  katika eneo  ambalo  kipo kile kitu kizito. Hii ndio sababu, nyota ina uzito mkubwa na ndio maana  kila nyota  kuna sayari zinazunguka . Ukiwa na uzito mkubwa maana yake  lazima uathiri wengine …”

Hamza wakati akiongea hivyo  ghafla tu  aliingiwa na  kitu kama mwanga kwenye akili yake na  kuacha kuongea mara moja. Alionekana kupata  jambo jipya katika akili  yake ambalo hakuwahi kulifikiria ,  jambo muhimu zaidi katika mafunzo yake.

Regina alikuwa akisikiliza kwa furaha kubwa , na ndio muda huo alijua mume wake alikuwa na maarifa mengi.

“Kwanini unayajua hayo yote? Si ulikuwa mpiganaji tu?”Aliuliza Regina.

Hamza hata hivyo hakuwa katika  mudi ya kusikiliza maswali ya Regina. Muda huo aliweza kuhisi  pengine ameweza kujua  tatizo liko wapi , alijikuta akipatwa na msisimko  na kutamani kuruka  kwenye siri yake.

“Wife nisubiri naja,  naenda nje mara moja”

Hamza aliongea  wakati akiwa amesimama tayari ,  Regina alionekana kushangaa kwasbabu sinema haikuwa imeisha bado na anandoka.

“Wewe , unaenda wapi?”

“Kufanya majaribio”Aliongea Hamza huku akipotea.

Kufanya majaribio ! Regina alikuwa katika hali ya mshangao baada ya kushindwa kuelewa Hamza anamaanisha nini. Hata hivyo hakuwa na furaha , alishia kushika kikombe cha kizombi na kuking’ata kwa nguvu.

“Mshenzi wewe Hamza , mara yangu ya kwanza kuja kuangalia  sinema na wewe unanitelekeza” Regina alilaani sana katika moyo wake ,  lakini  hakujua  Hamza alikuwa ameenda wapi , hivyo  aliishia tu kubakia hapo na kuendelea kuangalia filamu.

Muda huo huo , Hamza alikuwa ametoka nje  kabisa ya ukumbi na  ndani ya  dakika kadhaa tu alikuwa  juu kabisa ya jengo la  Dosam Tower ambalo lilikuwa mkabala kabisa  na  ukumbi wa   kuangalia  Sinema.

Jengo  hilo lilikuwa refu sana kwenda hewani kuliko majengo yote  yanayozunguka katika eneo hilo  na Hamza mara baada ya kukanyaga juu yake aliweza kupigwa na upepo mwingi.

Mara baada ya kusimama juu yake aliweza kuangalia upande wa chini uliokuwa umefunikwa na taa nyingi  za umeme  , na Hamza  aliingia katika tafakari nzito.

“Quality as an invisible energy(Ubora kama nishati isionekakan) Au inamaanisha…”

Hamza alijikuta akiacha kuongea na palepale aliweka   mkono wake katika staili ya mashambulizi , kama vile ameshikilia siraha. Alifumba macho  yake  na kisha akautuliza moyo wake , katika  akili yake . alizikumbuka hisia  ambazo zilimtokea wakati  akitumia mashambulizi ya kunuia kumuua Skellidoni.

Mwanzoni Hamza alielewa kwamba  nguvu za nje ni nguvu za nje tu , siraha ni siraha na mbinu za mapigano ni mbinu za mapigano. Lakini Hamza hakuelewa kwanini yeye ambae hakuwa na nishati yoyote ya  mbingu na ardhi  anaweza kuzalisha nishati  kubwa yenye nguvu isioonekana.

Kimantiki ni kwamba , hata kama angekuwa na uwezo mkubwa wa kiimani  au  kuwa na uwezo wa kucheza na elementi za upepo , asingeweza kutengeneza nguvu ile. Lakini muda  ambao alikuwa akimwelezea  Regina  kuhusu ukubwa wa uzito wa kitu  na athari zake kwa ulimwengu , Hamza aliweza kuelewa tatizo lilikuwa wapi.

Hamza alifumbua macho yake , yalikuwa kama siraha , mwili wake ulipiga hatua mbele  na  kwa  kuzungusha tu  alifyatua siraha yake mbele.

BOOM!

Ghafla tu bango kubwa  la mtandao , lililokuwa   juu ya ghorofa , mita ishirini  kutoka katika jengo alilosimama , lilitoboka  kwa nguvu kubwa mno. Hamza aliangalia   bango lile ambalo  lilionekana kushikwa na  cheche za  umeme  na alijikuta akipatwa na msisimko  ambao  ulifanya mwili wake wote kumtetemeka.

“Ndio!  Ni ubora , its Quality! Hahahaha…” Hamza alijikuta akiongea huku akicheka kwa nguvu kama vile alikuwa amegeuka na kuwa kichaa.

Uzito uliokuwa ukizungumziwa hapo , haukuwa  uzito wa  mtu   lakini ulikuwa ni uzito wa kila seli ndani ya mwili wake  na kila  chembe  iliomilikuwa  na Hamza baada ya miaka mingi ya mafunzo makali.

Nguvu ya ndani   ni  imani  na nguvu  hivyo huvunwa taratibu taratibu  mpaka kufikia katika  viwango vya juu sana , inasemwa kwamba kupitia nguvu ya ndani mtu anao uwezo wa  kufanya kila jambo  hata  kuhamisha  milima  na kuutupia baharini , kupitia  nguvu ya ndani anao uwezo hata wa kuita mvua na upepo na hata kuukomesha.

Kama kila kitu ni asili , kwanini wavunaji  wasitumie  nishati za nje  kutawala nishati ya ulimwengu? Kwanini wasigeuke na kuwa malaika ? Jibu ni hapana nguvu ya nje haitoshi , ni nguvu ya ndani pekee ambayo  inavunwa hatua kwa hatua  ndio inayofanya nishati ya mtu kuwa bora zaidi kuliko ile inayopatikana nje.

Si  ni malengo ya  kila mvuna nishati kuboresha mwili wake  na kuwa na nguvu? Lakini bila shaka  siraha  ambayo inaweza kuogopesha ulimwengu ni mwili wangu binafsi.

Hamza alikumbuka  siku ile , wakati akiwa  mbele ya ziwa la kutengeneza hospitalini , hakugusa kabisa maji  lakini alitoa nguvu isiokuwa ya kawaida  na sababu  ambayo Black Fog alivyoraibu hakuna kilichotokea ni kwasababu mwili wake haukuwa umepitia mafunzo ya kutosha na kuumiliki mwili wake kisawa sawa. Isitoshe pia Black Fog  alikuwa akijifunza kuvuna nishati za  nje hivyo  nguvu zake za ndani zilikuwa  dhaifu zaidi.

Hamza muda huo alijua sio tu nia ya kisiraha ambayo iliweza kutoa majawabu yale , bali ni kwasababu mwili wake umeingia katika hatua nyingine kabisa  ambayo  inampa ubora  ambao unamfanya  baadhi ya nishati za ulimwengu  kujigandisha kwake  mwenyewe bila kujua.

Uwezo wa Hamza ni kama sumaku, namna  ambavyo inavuta vitu  na kuvinasa  ni kwasababu ya nguvu yake , hivyo mwili wa Hamza ni kama umekuwa bora na kuwa sumaku ambayo inaweza kunasa  nishati isiokawaida ya ulimwengu wa asili , hivyo  ndio maana mwili wake umekuwa  bora , haukuwa bora kwa  nguvu ya ndani pekee , lakini kwa mafunzo aliopitia kwa muda mrefu na kufanya  aumiliki  mwili wake kisawa sawa. Kwa lugha nyepesi ni kwamba  mafunzo  yamemfanya  kuumiliki mwili wake kwa asilimia mia moja. Hamza anaamini  kwamba  licha ya miili yetu kuwa  yetu , lakini  asilimia kubwa haipo chini ya umiliki wetu bali  ipo chini ya umiliki wa asili.

Lakini namna ambavyo Hamza ananasa nguvu hizo zisizo za kawaida , bado hakuelewa , alijiuliza je kuna  sheria  ya kifizikia ambayo bado haijawahi kufahamika kuhusu  ulimwengu  au  kuna sababu  nyingine ya kuweza kuwa na uwezo huo?.

Hata hivyo Hamza alikuwa na uhakika  na jambo moja tu , hakuwa  amechagua njia mbaya katika mafunzo.

Ingawa hakuwa na nishati yoyote katika mili wake , kama nishati ya mbingu na ardhi , kupitia kuuelewa vyema mwili wake, kuumiliki kwa asilimia mia moja  na kuimarisha  imani yake , mwili wake umekuwa mzito  na wa tofauti na kuanza kuathiri  nguvu iliojificha ya ulimwengu.

Nishati ya mbingu na ardhi ilikuwa ikiisha ikitumika sana na mtu , lakini ukifananisha na  nguvu yake yeye , ilikuwa haina kikomo. Kwa lugha nyepesi  wavuna nishati wanaomba asili iwapatie nguvu  ilihali Hamza yeye  anaamini  sisi binadamu ndio tunapaswa kuimiliki asili   na kuiamrisha ifanye mambo  yenye nguvu , kuumiliki mwili maana yake ni hatua ya kwanza ya  kujitoa  katika minyororo ya asili  na kuifanya ikutumikie.

 Hamza muda huo alihisi ni kama alikuwa na nishati ya mbingu na ardhi bila kuomba umiliki , hivyo kupata fursa wa kutumia bila  kumuishia tofauti na  wavuna nishati wa kawaida ambao  lazima wavune nishati nyingi ya asili na kisha ndio waitoe kufanya matendo yenye nguvu. Hamza hakuhitaji kuvuna,  alikuwa  akitumia.  Moja ya sababu ambayo ilimfanya tokea mwanzo kuachana na   mafunzo ya kuvuna nishati ni kwasababu  hata ajitahidi vipi kupanda levo kuna ukomo akifikia hawezi kwenda mbele.

Yule aliesema unaweza kuhamisha mlima na kutupia baharini  , kumbe  ilikuwa ni kitu kinachowezekana na  siri ilikuwa kwenye kuumiliki mwili  wangu kwa asilimia mia moja  na kuwa bora zaidi kuliko asili.

Muda huo Hamza akiwa na furaha , ghafla alihisi kuna kitu hakipo sawa , ni kama akili yake ilirudi na kumwambia si alifika hapo akiwa ametangulizana na  Regina. Kwanini ghafla tu yupo juu ya jengo anatafakari.

“Shit! Nimemsahau  kumbe nilimwacha  ndani peke yake”

Hamza palepale haraka  sana alishuka chini  na kukimbilia ukumbini, mara baada ya kufika  , filamu ilikuwa imeisha  tayari. Bila kujua Hamza alikuwa ametumia zaidi ya lisaa akifikiria.

Hamza aliweza kumuona Regina akiwa amesimama nje  na sura iliovimba  na alimwangalia na macho makali sana. Hamza mara baada ya kuona ukauzu huo alijikuta akijilegeza tu  na  kwa  aibu aliishia kutabasamu  huku akimsogelea na kutaka kumsaidia kubeba mkoba wake.

“Wife , kulikuwa…”

“Hebu niache , usichukue  mkoba wangu” Regina alikoroma na kisha palepale alielekea upande wa maliwato.

Hamza aliishia kushika  paji la uso wake tu , alijua amekosea hivyo hakuwa na namna zaidi ya kusubiri  hapo nje.

Dakika chache Regina alitoka , hakumjali Hamza na badala yake alimpita na kutembea kuelekea upande wa maegesho ya magari. Hamza aliishia kumfuata nyuma nyuma huku akijaribu kumuongolesha.

“Mke wangu najua nimekukosea. Nilipatwa na  ufunuo mpya kuhuisu  mafunzo yangu  na nilikuwa na  shauku kubwa ndio maana , nakuahidi haitojirudia siku nyingine …” Regina kimya.

“Wife , acha basi kunichunia. Nifanye nini  ili unisamehe?”

Regina aliendelea kuwa kimya  na  kuendelea na safari ya kuelekea eneo la maegesho  ya magari. Hamza alijiambia katika moyo wake sio mbaya sana , zamani  kama angemkasirisha hivyo  asingeruhusiwa hata kupanda nae gari  moja.

Hamza mara baada ya kuondosha gari ,  kimya kilitawala na hakujua  ni neno gani  aongee kulegeza hali.

“Sina furaha..” Ilikuwa ni sauti ya Regina mara baada ya kimya kirefu  na Hamza mara baada ya kumsikia , alijua njia ipo.

“Wife najua huna furaha kwasababu  yangu , nimekukosea , ngoja nikupeleke sehemu nzuri ukale chakula kitamu ,  nakupenda sana mke wangu , usiwe na hasira basi   vinginevyo moyo wangu utavunjika vipande vipande”

“Wewe kibudu, nani  akuamini .. sijali chochote kama unanipeleka kula au nini , sitokusumbua kwa wiki nzima”

“Nitakupeleka mahali , kwenda kula  mishikaki , kuna sehemu naijua wanaichoma  vizuri sana’

Regina mara baada ya kusikia hivyo , aliishia kutingisha  kichwa tu. Hajawahi kula  mishikaki  zaidi ya kuona tu ikichomwa hivyo alijawa na matarajio.

Dakika chache tu Hamza aliweza kufika  katika  mgahawa mmoja ambao  ni maarufu kwa kuchoma mishikaki mitamu na saladi. Eneo lilikuwa na watu wengi  sana , lakini  huduma ilikuwa safi  sana  na Hamza alichangamka na kuagiza  mishikaki na kila kitu kinachopatikana  kwa ajili ya  Regina kuonja.

Mara baada ya kuletewa oda yao na   harufu tamu ya nyama  za kuchoma kufikia pua zake , Regina hamu iliongezeka  , isitoshe hakula sana chakula cha usiku , hivyo hata  kule kununa kulipotea mara moja.

“Wife nimesahau kuagizwa vinywaji , utapendelea nini , huna  haja ya kuendesha  gari hivyo unaweza kunywa  kidogo” Hamza aliongea huku moyoni akijiambia nikifanikiwa kumlewesha huyu mrembo , pengine naweza   kupata faida.

Regina mara baada ya kusikia neno kinywaji , palepale  alikumbuka kuna kitu amesahau

“Aaa! Kinywaji changu cha kizombi jamani!” Hamza mara baada ya kusikia hivyo alikumbuka ni kinywaji kile   kilichowekwa kwenye  kikombe kilichokuwa na chata la zombi na hakujua acheke  ama alie kwa muda huo.

“Wife nilikuona ukiingia nacho toilet , ulisahau kutoka nacho”

“Ndio! Wewe mjinga kwanini hukunikumbusha? Unadhani elfu kumi na tano ni ndogo?”

“Wife unatumia zaidi  ya mamilioni ya hela kununua magari , unaumia kupoteza kikombe cha elfu kumi na tano?”

“Ile nilipenda chata lake la kizombi”Aliongea  Regina kinyonge.

“Kula kwanza huu mshikaji , nyama yake imenona kweli , itakufanya  usahau kabisa  kuhusu kinywaji chako cha Zombi , usiposahau utanunua tu , si karibu na  kazini pale?”

“Ah! Sasa na wewe kwanini unanichagulia hio yenye mafuta mengi” Hamza  mara baada ya chaguo lake kukataliwa aliishia kuweka chini.

“Usinichagulie , nitachukua mwenyewe ninayoona nzuri”Aliongea Regina na kisha alianza kuchagua unaomfaa  na kuchanganya na saladi na kutafuna.

“Wife kakipande  kadogo hivyo , saladi kibao ,  si uharibifu tu unaofanya?”

“Nimependa hivyo , wewe  kinachokusumbua nini ,  kama unahisi  nafanya  uharibfu basi kula mwenyewe , sitaki tena” Mara baada ya kuongea hivyo palepale alibeba mkoba wake na kugeuka kutaka kuondoka.

Hamza aliishia kujishangaa na kujiulizza imekuwaje amemkasirisha tena! Mbona ni kama ameongea kawaida tu  au ni hasira ndio zinamwendesha.

“Mke wangu kaa basi  na wewe , sitoongea tena”Aliongea Hamza huku akisimama na kujaribu kumkarisha chini.

“Nina hasira , halafu umesema mwenyewe unataka kuomba msamaha , lakini unanifanya nisiwe na furaha  tena..”

Hamza aliiishia kujiambia wanawake bwana , ni kama watoto , lakini hata hivyo  alijituliza.

“Wife unataka nifanye nini ili  kurudisha furaha yako?”

“Nenda ukumbini  ukaniletee kikombe changu  cha kizombi”

“Ah! Yaani turudi hadi kule , dakika   ishirini kwenda na   ishirini kurudi si   tutakesha barabarani kwa ajili tu ya  kikombe cha plastic”

“Kama hutaki potezea , kula nyama zako mwenyewe”Aliongea Regina huku akionekana hakutaka kuendelea kubaki  hapo. Hamza aliishia kung’ata meno kwa nguvu kujituliza.

“Basi sawa mke wangu ,  nisubiri  muda mfupi tu nitaenda kukuletea”Aliongea Hamza huku  akisimama  na Regina mara baada ya kuona kweli Hamza anataka kwenda alimshika mkono.

“Umekuwa mjinga? Unataka kweli kwenda , si kutakuwa kumefungwa  sasa hivi?”

“Lakini si umesema unakitaka hicho kikombe?”Aliongea Hamza kinyonge na kumfanya Regina kumwangalia usoni  na palepale mwonekano wake ulilainika.

“Nilikuwa nakuchezea   akili tu , sina hasira tena , usiende  bwana”

“Wife , hivi ni sentensi gani ambayo ni  ya kweli kutoka kwako? Unanifanya niogope unajua?”Aliongea Hamza.

“Wewe ndio mtawala mkuu wa ulimwengu wa giza, Lucifer mwenyewe , kwanini  unaniogopa kiasi hicho. Huoni kama nakusumbua bila sababu?”

Hamza hata yeye  alishajisahau kama ana hiko cheo na ni kama amekumbushwa na kuishia kujisikitikia tu.

“Sio kama nakugopa , nilitaka kukuona ukiwa na furaha kasababu nakupenda”

“Mh! Unahisi  nakutosheleza kwa kuwa hivi?”Aliuliza Regina na Hamza alitaka kutingisha kichwa  lakini alijua atajifunga na kubadilisha mara moja.

“Vyovyote vile mke wangu , mimi  nakupenda  sana na najali furaha yako”

“Hebu malizia  huko hio mishikaki, inapoa”Aliongea Regina ambae mudi yake ilionekana kurudi  upya  na kumtaka Hamza kukaa chini na kuendelea kula mishikaki.

Hamza alirudi zake chini na kisha  alichukua  mshikaki na ile anataka kupeleka mdomoni  aligundua Regina alikuwa akimwangalia.

“Wife kula na wewe ,  hizo zenye mafuta niachie mimi , chagua inayokufaa”Aliongea.

“Hamza , kwanini hukasiriki wala kunigombeza?”

“Eh!”Hamza alishindwa kuelewa ni swali gani hilo linamtoka huyo mwanamke.

“Kila muda mimi ndio nakasirika  na  wewe unakubali tu makasiriko yangu , kwanini   huonyeshi kukasirika wala kunigombeza  kwa kukasirika bila sababu za msingi , hujawahi kuwaza kunishikisha adabu?”Aliuliza Regina  akiwa na shauku.

“Kwanini  nikushishikishe adabu? Si kawaida  kwa  mke  kubembelezwa , isitoshe hujaniambia nifanye kitu kibaya , hivyo  nafanya tu kile unachotaka”

Regina mara baada ya kusikia hivyo , aliishia tu  kutoa tabasamu lililompendezesha.

“Licha ya kuwa na wanawake wengi lakini bado unanijali . Labda ni kwasababu  unajua kuna baadhi ya vitu   naweza kuvumilia”

“Ndio hivyo ,  kama  nina mwanamke nje  na familia yangu kunichukia , siwezi kuwachukia, kwasababu mimi ndio  mwenye makosa”Aliongea Hamza.

“Mh! Unakiri kabisa waziwazi , una wanawake nje. Kuna  haja ya kuongelea hilo suala  hapa ,ona sasa umenikasirisha  tena, kwanini uwazungumzie  wanawake wako muda kama huu?”

“Wife , lakini wewe ndio umeanzisha ..?”

“Sitaki kujali mimi. Nipe na mimi nyama , nichakulie isio na mafuta na pilipiuli nyingi na ilioungua kiasi”

“Sawa sawa , ngoja nikuchagulie nzuri utakayopenda”

Usiku huo  Hamza alifaidika na vingi ,  licha ya kwamba alihisi ni kama akili yake ni kama  inazungushwa kwa kuteswa na Regina  lakini licha ya hivyo aliweza kupata ufunuo muhimu sana  juu ya mafunzo yake na  kuwa na uelewa mpya.

Previoua Next