Reader Settings

Siku iliofuata , Hamza alivyofika kazini , aliweza kumuona Rhoda akiwa amefika na amevalia  suti safi na kuonekana kama  mtaaluma flani hivi.

Linda mara baada ya kupewa taarifa Hamza amehamishwa na nafasi yake kuchukuliwa na mwanamke mwingine , alijikuta akipatwa na presha kubwa na mwonekano wake ulizidi kuwa siriasi.

Hamza alimkabidhi  Rhoda  ofisi yake huku akimpa maelekezo ya kutokugombana na  Linda   na kufuata wajibu wake kama bodigadi.

Mara baada ya hapo Hamza alikusanya vitu vyake na kuelekea katika idara ya  usalama na ulinzi ,  alipewa nafasi ya kuwa meneja msaidizi ,  ijapokuwa   bosi wake alikuwa ni Anna  ambae alirithi nafasi ya Yonesi , lakini  Hamza alikuwa   ni kama bosi  tu.

Wafanyakazi wengi wa makao makuu walikuwa wakijua  Hamza ndio mtu  ambae alikuwa   na msaada  mkubwa  pembeni ya Regina , kwani tokea ajiunge na kampuni mambo mengi yalikuwa yakienda sawa  kabisa.

Mara baada ya kupita katika ofisi kubwa ya   idara ya  ulinzi ,  hakuweza kuona  wale walinzi wa kike  kwasababu  asilimia kubwa wengi wao  walikuwa  aidha  katika floor nyingine kuhakikisha usalama na wengine  walikuwa wakikagua  kampuni Tanzu.

Unachopaswa kuelewa  Idara zote za makao makuu zilikuwa zikisimamia kampuni zote  tanzu. Hivyo   kufanya kazi makao makuu ni kama kuwa bosi  kwa  kampuni nyingine.  Hivyo wafanyakazi wa  makao makuu walikuwa mabosi moja kwa moja ndio  maana  idara ya ulinzi ilipewa floor yao kabisa inayojitegemea.

Hamza mara baada ya kuingia katika ofisi ya Anna ,  pua zake zilinasa harufu ya marashi  ilioambatana na ile  inayotolewa na AC. Yalikuwa marashi yaliokuwa yakiashiria utu uzima.

Mapambo ndani ya ofisi hio yalikuwa  mengi sana , kulikuwa na kila  aina ya  vitu vya kuchonga  vya kila aina  na pia kulikuwa na picha nyingi ambazo zilikuwa ni za Anna alizopiga katika kila  inchi  aliowahi kufika.

Mara baada ya kumuona Hamza akiingia , mrembo Anna  uso wake wa duara  ulionyesha tabasamu pana.Alikuwa na nywele ndefu alizozifunga kwa nyuma  na kibanio  na ngozi yake ilikuwa  imetakata zaidi kuliko alivyokuwa  ninja.

Licha ya   ubaridi wa AC , Anna alikuwa amevalia  shati la mikono  mirefu ya kitambaa cha  mtelezo , ukweli ni kwamba   kutokana na amani ambayo alikuwa nayo  kipindi hicho imefanya  kubadilika sana , Anna alikuwa amenenepa  na kufanya  eneo la kifua chake kuwa  zito sana.

Hamza alikuwa na habari zote , tokea Anna aanze kufanya kazi ndani ya hio kampuni  ,  wanaume wengi  nje na ndani ya kampuni walikuwa wakijaribu  bahati zao kumtaka  Anna kimapenzi , wengine walifanya kwa siri na wengine  waziwazi. Lakini hata hivyo aliona  walikuwa na kila haki , Anna alikuwa amebarikiwa rangi nyeusi ya kuvutia sana , ukijumlisha na lipsi zake na meno yake yalivyokuwa meupe  ilitosha kutetemesha mioyo ya wanaume wengi.

Hamza kuchunguza uzuri wa mwanamke huyo uamna ulivyoongezeka , alijikuta akishindwa kujizuia  na kukumbuka   mchezo waliofanya.

“Karibu kwenye idara yetu , Meneja Msaidizi , Mr Hamza”Aliongea Anna huku  akisimama na kumkonyeza Hamza kimadaha huku wakiwa wameshikana mikono.

Hamza aliishia kuushika mkono wa mwanamke  huyo na hakuwa na haraka ya kuuachia.

“Anna kwanzia sasa nitakuwa  chini yako , naamini tutafanya kazi nzuri pamoja”

“Hebu acha zako ,    upo hapa kwasababu bosi  anataka  kukuchunga.  Nathubutu  vipi kufanya kazi nzuri na wewe?”Aliongea Anna huku akimwangalia   na macho ya kurembua.

Hamza aliishia  tu  kuvuta pumzi ya hewa ya baridi  na  kujiambia  mbona sauti  ya huyu mwanamke ni tofauti na mwonekano wake , alionekana kuwa siriasi huku usoni akimchokoza.

“Vipi  hali ya kazi   ndani ya kampuni kwa ujumla , ndugu zako vipi?”Aliongea Hamza kwa wasiwasi kidogo.

Anna hakuwa na haraka ya kujibu  na aliishia tu kumwangalia Hamza usoni kwa sekunde kadhaa  huku bado wakiwa wameshikana mikono.

“Kabla hatujaendelea kuongea , Meneja Hamza unaonaje tukiachiana mikono kwanza?”

Hamza alijifanyisha  ndio alikuwa anajua wameshikana mikono na kucheka  kwa nguvu  na ile anataka  kuondoa  mkono , Anna alimtekenya Hamza kwenye kiganja chake  na kuifanya akili ya Hamza kuchafuka , huku akijiambia huyu jini ananitafutia matatizo.

Kitendo cha kumwangalia Anna , aliona kabisa  kulikuwa na  nguvu kubwa inayotumika kuzuia hisia.

“Nimezisikia habari , umekuwa maarufu sana  ndani ya kampuni kwa muda mfupi ,  vibosile wengi wa kampuni wanakufukuzia , lakini hakuna alieweza kung’oa jimbo”

“Wanaume wengi  wa hili jiji wamekaa   kistaarabu sana  na mimi sijazoea ustaarabu  wa  kugandana, nimi nataka ile  mambo  heavy” Aliongea  Anna na kisha  alirudi kwenye kiti chake na kutoa  sigara na  kuiwasaha  na kuvuta moshi huku akipiga nne na kufanya mapaja yake kutuna yalionona kutuna.

Hamza aliishia kuangalia mapaja ya mwanamke huyo yalivyo tuna na kujikuta akimeza mate mengi.

“Kama ni hivyo basi itakuwa ngumu sana kwako , kwa kambini huko sawa, ila show za kibabe huwezi kuzipata kwa hawa wazee wa viyoyozi”

“Show za kibabe , sio kitu ninachokitafuta , ninachotaka ni mwanaume   muungwana na anaejua , ukweli   kwenye moyo wangu nahitaji mwanaume  mwenye njaa kama mbwa mwitu . Mfano mwanaume  wa haiba ya Meneja Hamza  na kadhalika ..”

Hamza mara baada ya kusikia  kauli hio ya  pua , moto uliokuwa umejificha chini ya  kiwiliwili cha chini  uliamka  na kubaunsi  na kutamani kuchukua hatua. Lakini  mara baada ya  kufikiria namna alivyomkasirisha  Regina siku ile alipotoka kwa Anna , alijikuta ni kama anamwagiwa  ndoo ya maji ya baridi na  bwana yule alinywea haraka.

Dunia ina wanawake wengi sana wazuri , kama atashindwa kujizuia kwa Anna basi  atakuwa amepoteza  juhudi zake za miaka kumi au   kadhaa hivi. Aliona apotezee , isitoshe alikuwa ndani ya kampuni na  angalau  mahali hapo anapaswa kumuonyeshea mke wake heshima.

“Anna kwasababu unajua kabisa unachokitaka , hio  ni hatua nzuri , nadhani  haina haja ya kukataa  wanaume ,  wape muda na weka hisia zako wazi , sidhani kama utakosa   na pengine unaweza kupenda kabisa. Unajua  katika maisha haina haja ya kuleta mikanganyiko mingi, zingatia ninachokisema ,  itakuwa vizuri ukiwa  na familia yako”

Anna aliishia kumwangalia Hamza kwa mshangao  na kisha palepale alitoa moshi mwingi wa sigara.

“Inaonekana  nimekuchukulia poa  uwezo wako  wa   kujizuia. Au nimekuwa mzee na ucheshi wangu umepungua?”

“Haha.. ukweli ni kwamba kama ningekunywa pombe kidogo  , nisingeweza kuhimili. Usiudharau kabisa ucheshi wako , ili mradi utafungua mlango , wanaume wanaokufukuzia wataongezeka maradufu na nina uhakika hautokosa anekufaa”

“Lakini  haijalishi ni wanaume wangapi watanifukuzia , hakutokuwepo mwanaume kama  Hamza”

Hamza alihisi mtekenyo kwenye moyo wake  kama vile alikuwa akiogopa kuendelea kukaa hapo na Anna ataongea kitu ambacho kitamkuna,  hivyo haraka aliona aondoke.

“Nitaenda   kusalimiana na wengine ili watambue uwepo wangu. Halafu huyo kwenye picha ni Yonesi?”

“Ndio, Vipi una taariza  zake zozote?”Aliuliza Anna na Hamza aliishia tu kutingisha kichwa   kukataa , ilionekana  sio yeye tu anaemkumbuka bali  hata  marafiki zake wa jeshi.

Hamza aliishia kutoka nje na kufanya  ofisi hio  kuwa na utulivu kwa mara nyingine.

Anna aliishia kuvuta sigara na kutupa kipisi kwenye  dustibin na kisha alichukua mkonga wa simu na kubonyeza bonyeza na palepale simu iliunganishwa.

“Limeendaje?” Sauti upande wa pili ilikuwa ni ya Regina.,

“Bosi! Hamza amefanikiwa kufuzu jaribio. Ameenda mbali na kunishauri  nitafute mwanaume wa kuanzisha nae familia”

“Ndivyo hivyo. Kazi nzuri , endelea kumchunguza”

“Sawa , nitawachunga na   wadogo zangu  pia  na kutowaruhusu kumsogelea  Hamza”Aliongea Anna.

“Anna , wewe una busara sana. Unapaswa kujua nimekuomba ufanye hivi   kwasababu  yako na  dada zako.  Ili mradi mume wangu ataendelea kuwa chini ya idara yako na hasababishi matatizo , sitowafanyia chochote”

“Usiwe na wasiwasi  Bosi Regina , najua chakufanya”Aliongea Anna  kwa upole na kisha akakata simu.

Muda huo Hamza aliekuwa  ametoka nje ya ofisi , hakujua alikuwa  kwenye mtego wa Regina na  ameweza kuukwepa. Ukweli ni kwamba hata kama afahamu kuhusu hilo asingeweza kufanya chochote , isitoshe alishalala na Anna . Hivyo hata kama  asingependa majaribio hayo , angeishia tu kukubali majaliwa yake.

Anna pia alikuwa akielewa , alijua fika  hata kama alikuwa akimtamani Hamza , lakini bado ni mume wa mtu.  Na huyo mtu mwenyewe ndio huyo anaempa mshahara wa kuweza kulipia kodi na mahitaji mengine ya kuishi maisha mazuri yeye na ndugu zake, hivyo  asingeenda kinyume. Ndio maana aliamua kukubali kufanya jaribio hilo  licha ya kwamba hakupenda. Ni kwa bahati   walifanya  siri   na Hamza hakujua na mpango ulifanikiwa kwa amani.

Hamza alienda katika ofisi ambayo Yonesi alikuwa akitumia , lakini ndio hivyo hakuwepo.  Hakujua ni wapi Yonesi alipo  na alikuwa akifanya nini.

Mara baada ya kuweka vizuri vitu vyake , aliwasha  tarakishi  na kama kawaida alipanga kuiset vizuri ili isionekane  na mitandao ya kampuni , lakini ni muda ule watu waliingia katika ofisi yake.

“Bro!”

Mwanaume alieita alikuwa ni Aroni  na nyuma yake alikuwa ameongozana na sura ambazo hakuzifahamu.

“Tumepata taarifa umehamishiwa kwenye idara yetu kama meneja msaidizi na hatukupata usingizi kabisa. Sikutarajia utakuja kweli , kwa uwepo wako hapa,  idara yetu  itakuja kuwa  levo nyingine kabisa”

“Vipi  kwanza , naona watu wapya?”

“Ndio kampuni inazidi kutanuka na majukumu kuwa mengi na hakukuwa na  walinzi wengi wa kiume , hivyo bosi Anna kaniambia nilifanyie kazi , ndio wameanza hivyo nawazunguza zungusha. Wale wengine wapo likizo   ya christmass”

Hamza pia alijua biashara  za Regina zilikuwa zikikua kwa kasi mno  na kulikuwa na maeneo mengi yalihitaji ulinzi , hivyo aliishia tu kutingisha kichwa kwa kuelewa.

Mara baadda ya kupiga soga na  Aroni na  wenzake , na kisha kwenda kupata chakula pamoja. Hamza aliona hayo ndio maisha  sasa. Hakukuwa na kazi  nyingi alizopangiwa kwa siku hio, hivyo alijitengenezea kinywaji na kwenda kucheza na tarakishi yake.

Baadhi ya marafiki zake  Eliza  na   wengine aliokuwa na ukaribu nao walimtania sana siku hio  na kumfanya kufurahi.

Muda wa kuondoka Hamza alikumbuka alikuwa na miadi  na Irene  kuonana  eneo walilopanga kukutana , lakini ni muda huo huo  alipokea simu kutoka kwake.

“Wewe mtoto , ndio najiandaa kwenda eneo letu la miadi , ushafika?”

“Hamza , nimepata ajali”

“Ajali ! Vipi , umeumia?”

“Hapana , nilikuwa nikirudisha gari nyuma ili kuliegesha ila  nikagonga nguzo ya taa. Sijui hata cha kufanya hapa?”Aliongea na Hamza alipatwa na ahueni.

“Uko wapi?”

“Nipo Haille sellasie , mkabala na jengo la  Conn supermarket”

“Nitumie link ya eneo ulipo , nakuja hapo sasa hivi”Aliongea Hamza na kukata simu.

Previoua Next