Reader Settings

Mbwa wa kijerumani

Hamza  mara baaada ya kaungalia  uelekeo aliotumiwa na Irene hakuona haja ya kutumia gari na  badala yake aliona achukue taksi ndio ingeweza kumuwahisha haraka.

Mara baada  ya kufika  ni kweli ni kama ambavyo

Irene aliongea ,  kwani aliweza kuona gari aina ya Porsche ikiwa imeengeshwa  mshazari  karibu na  nguzo ya taa  huku  mlango upande wa siti ya mbele ukiwa umebonyea kwa kuingia ndani.

Nguzo ya taa yenyewe ilikuwa imepinda , ilionekana iligongwa kwa nguvu sana na gari hio.

Hamza aliishia tu kusikitika na kujiuliza ni uendeshaji gani wa gari  wa namna hio?.

Pembeni ya Irene kulikuwa na  wasichana wawili   watu wazima hivi na wanaume kama  wawili , na walionekana wote walikuwa wakizungumzia ajali hio iliotokea.

Irene mara baada ya kumuona Hamza alijikuta akimkimbilia haraka kama mtoto mdogo na kwenda kumkumbatia.

“Hamza..!”

Alijikuta akianza kujidekeza  kwenye  mikono ya Hamza.

“Nini kinaendelea hapa , mbona  huu ugongaji sio wa kawaida ?”

“Nilitaka kurudisha gari nyuma niliegeshe , ila nilisahau kumbe sikuweka gia ya nyuma na ile nakanyaga pedeli gari ikaenda mbele  na kugonga nguzo”

Hamza mara baada ya kusikia kauli hio , hakujua acheke ama alie.

“Ndio maana nasema bado hujaiva kwenye uendeshaji gari ila  king’amg’anizi tu”

“Lakini naogopa  mwenzio hili gari sio ya kwangu , kuna dada nilibadilishana nae , akiona gari yake nzuri hivi nimeiharibu sijui atanifanyanyaje. Hamza please nisaidie”Aliongea Irene kwa kupasha viganja moto.

Hamza kweli kwa kuangalia gari hio , aligundua ilikuwa ni zile gari za hela nyingi , na hata yeye pia alishangaa mwanzoni kuiona , kwa uelewa wake  mahesabu ya  haraka haraka ya gari  hio yangegharimu zaidi ya  milioni mia nne za  kitanzania.

Lakini hata  hivyo  haikumpa shida  , maana  option zote mbili alikuwa akiweza kufanya ,  aidha kuitengeneza na kuirudisha katika mwonekano wake wa kawaida  kama bima haitoshelezi au   kununua  nyingine. “Nitakusaidia , haina haja ya kuwa hivyo”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu.

Irene mara baada ya kusikia , Hamza angewezxa kumsaidia , alijikuta akishkwa na furaha.

“Hamza nilidhani utanifokea kabla ya kunisaidia . Kwa ujinga wangu naenda  kukugharimu kiasi kikubwa cha pesa . Asante sana , naahidi nitakulipa kwa namna yoyote unayotaka”

Hamza aliishia kutabasamu kwa uchungu  na kujiambia kwahio ashakuwa danga tayari.

“Hawa  watu ni wakina nani?” Aliuliza Hamza akinyooshea kidole wasichana watatu na wanaume  waliokuwa wamesimama kando ya gari ya  Irene.

“Hawa dada walikuwa wakipita , huyu baba ni  mlinzi ndani ya supermarket. Walikuja baada ya kuona  nimegonga  nguzo , kulikuwa na wengine wameondoka kabla ya kutokea”

“Hey! dada huyo ni  mpenzi wako?”Aliuliza  dada  aliekuwa katika mavazi ya kiofisi.

Hamza mara baada ya kusikia  Irene akiulizwa  juu ya yeye kuwa Boyfriend ni kama hakupenda. “Ndio dada, unamuonaje ni  handsome eh!”

Irene ni kama alikuwa ameamka katika   hofu ya kugonga gari na sasa alikuwa  akitaka kutamba na Hamza.

“Haha ! Kwa bahati mbaya sio  aina  ya chakula changu , kama  mpenzi wangu anesikia nimegonga gari  angenifokea mpaka basi. Lakini naona mpenzi wako hajakufokea zaidi ya kukumbatia na kukutuliza , Hakika una bahati”

Irene kusikia hivyo alijikuta akisikia sana raha , huku akimwangalia Hamza na macho ya kuridhika na  yaliojaa mahaba.

Hamza  muda huo alijua  nini anachomaanisha, lakini ukweli ni kwamba hata kama ingekuwa ni mwanamke mwingine ambae angekuwa katika ajali  asingewaza sana kuhusu gharama za gari zaidi ya kumsaidia kwanza kama alivyofanya kwa Irene.

Kwake yeye kufokea  mwanamke na kumpiga ni kitu ambacho anaamini sio  kwa ajili ya wanaume kufanya.

“Wewe Irene hebu  acha kucheka , vipi  ulishawasiliana  na watu wa Bima?”

“Ndio nimetumia namba za kwenye gari  na anasema anakuja”

Mara baada ya watu kutawanyika ,  fundi kutoka Bima alifika  na kisha alianza kukagua na aliangalia kitambulisho  cha gari na  kuona kweli ilikuwa kwenye mfumo wao wa Bima.

“Huu  mlango unapaswa kubadilishwa  kabisa , hivyo itahitajika kuutoa  kabisa. Hii ni ajali kubwa sana ,  mnapaswa  kwanza kuwataarifu polisi waje wakague na kuwapatia ripoti ya uthibitisho”

“Ah! Si itakuwa hela nyingi sasa?”

“Ni kama milioni arobaini hivi kutokana na gari yenyewe “

“Nini! Mbona ghali hivyo?”

“Hii gari ipo chini ya bima  ya kampuni yetu , kwanza unapaswa kuwasiliana na mmiliki wa gari na kisha hakikisheni mnapata uthibitisho kutoka polisi  na ndio kampuni itaweza kufidia kila kitu”Aliongea  na kisha alitoa maelekezo machache kidogo na kupanda pikipiki yake na kuondoka .

Hamza upande wake aliishia kukuna kichwa,alijiuliza kwanza ni nani ambae amempatia Irene gari ya kifahari namna hio kuendesha?.

Hata hivyo hakutaka kuwaza sana na palepale   muda mfupi tu polsii wa barabarani walifika  na mara baada ya kuona  Irene ameharibu nguzo , walimwambia kwanza anapaswa kulipia  nguzo na kisha aende polisi kuchukua ripoti.

Irene ilikuwa mara yake ya kwanza kukutana na utaratibu wa hatua nyingi namna hio  na kichwa kilianza kumuuma, ni kwa bahati tu  Hamza alikuwepo.

Hamza aliangalia gari hio na aliona bado ilikuwa  ikiendesheka.

“Haina haja ya kwenda kucheza leo, nitakupeleka sehemu ukale kwanza  na kesho nitakusaidia kufuata  taratibu  na kupata ripoti”Aliongea.

“Utanisaidia kweli?”

“Unatakja kufanya mwenyewe?”

Irene kusikia hivyo alimkumbatia Hamza na kumbusu shavuni , bila ya kujali barabara hio ilikuwa na watu waliokuwa wakipita.

“Hamza unanijali mno. Nina furaha kubwa kuwa na  boyfriend kama wewe”Aliongea Irene na kumfanya Hamza kuishia kucheka tu.

“Sijui kwanini , ila nashindwa tu kukukasirikia, hebu twende kwanza ukale”

“Hehe , si kwasababu unanipenda sana ndio maana”

Hamza aliishia kujiuliza au ni kwe,i ametokea kumpenda huyo msichana ndio maana hakasirishwi na  matendo yake.

Mbona kama namchukulia tu kama mdogo wangu?.

Hamza alimchukua  Irene kwenda kula na baada ya  chakula alimpeleka nyumbani kwao. Licha ya kwamba gari ilikuwa imeharibika ubavuni , lakini iliendesheka vizuri tu.

Mara baada ya kufika Masaki  anapoishi Irene na kuingiza gari ndani ya geti,mlango ulifunguliwa  na mwanamke alieonekana kujipenda na alishangaa baada ya kuona  gari ya Irene ilikuwa imepondeka na kumfanya kuwa na wasiwasi. “Nini kimetokea! Irene kwanini gari yako imehariibika , ulipata ajali?”

Ile anasogelea ile gari kwa kuizunguka  ndio muda ule Hamza alishuka kutoka kwenye gari. Mwanamke yule mara baada ya kumuona Hamza alikunja ndita.,  huku macho yake yakionyesha hali ya mshangao.

Hamza hakuwa mgeni na sura ya mwanamke huyo , hio ni kwasababu kipindi alichokuwa akija kumfundisha  Irene alishawahi kuona picha yake , alikuwa ni   bibi yake Irene upande wa baba . Ilionekana baada ya  baba yake Irene kuachana na  mke wake alimwita   mama yake kuishi na mjukuu wake.

“Shikamoo Madam! Nimefurahi kukuona kwa mara ya kwanza”Aliongea Hamza.

Irene upande wake haraka haraka alikimbia na kwenda kumshikilia  mkono bibi yake  huku akianza kumbembeleza.

“Bibi  naomba usije kumwambia baba , akijua nimepata ajali hatoniruhusu tena kuendesha gari. Bibi  nakuomba  tafadhari”

Lakini sasa bibi huyo hakuonekana kumjali kabisa Irene na badala yake macho yake yalikuwa kwa Hamza , akimwangalia kwa namna ya wasiwasi.

“Irene , kwanini umekuja na huyu mwanaume” Irene alishangazwa na swali lile.

“Bibi Hamza ni tafiki yangu , alikuwa ndio mwalimu wangu mama alienitafutia”Aliongea  

Hamza mwanzoni alishikwa na wasiwasi kidogo kwa kudhania Irene angesema yeye ni mpenzi wake. Hakutegemea  Irene angeficha  anavyomchukulia.

Ilionekana msichana huyo  sio kwamba hakuwa akiogopa , bali alikuwa akimhofia mno  bibi yake.

“Rafiki! Kwanzia leo huruhusiwi kukutana nae tena , huruhusiwi kuwa na urafiki na mtu kama huyu?”Aliongea huyo mwanamke  wa makadirio ya miaka sabini kwa usiriasi mkubwa.

“Bibi! Kwanini ? Sisi ni matafiki tu, kwanini siruhusiwi kuwa nae  kama rafiki”Aliongea Irene.

“Unasema unataka sababu? Wewe hujui huyu ni mume wa mtu? Wewe ni msichana na yeye ni mwanaume , kwanini  kuwe na urafiki kati yenu. Ukiendelea kuwa hivi  unadhani ni  mwanaume gani wa maana  kutoka familia nzuri  atakutaka kukuoa hapo baadae?”

Hamza alifikiria  maneno hayo na kuona alichoongea bibi  huyo  kilikuwa na mantiki. Lakini kwa wakati mmoja  kwasababu ya  kulindwa kuja kuolewa na familia nzuri  kuzuiwa kutokuwa na marafiki si sawa .

Lakini hata hivyo kuna kitu  ambacho Hamza alikigundua , pengine mwanzoni hakukijua , alionekana bibi huyu alikuwa na ukaribu zaidi na  familia ya  Regina mpaka kumjua mara moja tu kuwa alikuwa ameoa. Alikumbuka   Regina alimfahamu  Irene tokea akiwa mdogo kwasababu ya  ujirani   , hata kwa Prisila pia.Lakini  muitikio wa bibi huyo  kwa kuonekana na  Irene haukuwa wa kawaida, alionekana kama mtu mwenye hofu.

“Bibi Hapana! Hamza ni mtu muhimu sana kwangu . Mimi sitokusikiliza’

“Ninaenda kuongea na baba yako kuhusu hili na yeye ndio atadili na wewe! Tumekuharibu sana kwa kukudekeza. Angalia sasa marafiki uliokuwa nao?”

Aliongea na kisha bibi yule alimwangalia Hamza  kwa macho mabaya.

‘Inakuwaje  mwanaume umeoa  , halafu unacheza na  mjukuu wangu  kama hivi. Hebu ondoka na usije kumsogelea tena. Kwa  ajili ya  Irene ngoja niishie hapa. Siku nyingine nikikuona na  mujukuu wangu sitosita kumpigia simu bosi Regina”

“Kumpigia simu! Bibi mimi najuana na Regina  na tulishwahi kula chakula pamoja. Siwezi kuogopa hata ukimwambia”Aliongea Irene kwa ubishi.

“Nini! Wewe ..  umekutana na Regina ? Ni kwa muda gani tokea ukutane nae?”

“Nimekutana nae na  ananifahamu tokea nikiwa mdogo”

“Alikwambia nini   na kwanini mkutane   kwa ajili ya chakula?”Aliuliza  bibi kwa  wasiwasi na hali ya mchecheto kidogo.

“Bibi kwanini upo hivyo leo? Najuana na Hamza ndio  maana nimekuja kufahamiana na Sister Regina. Kwani kuna tatizo mpaka kutaka kujua ni lini nimekutana nae?”

Bibi yake Irene alikuwa na sura  yenye hali ya kupaniki na mara baada ya kufikiria kwa sekunde kadhaa  aliongea;

“Nakuonya kwanzia sasa , hupaswi kusogelea ndoa ya watu . Ukiendelea nitakufungia na hutoenda shule na hata chuo tutakupeleka nje ya nchi’

“Bibi....!!’

Irene kusikia hivyo machozi nayo hayakuwa mbali na kuishia kumwangalia bibi yake kwa hasira pekee. Hakutegemea bibi yake angemwadhibu kwa staili hio , kisa tu kuwa na ukaribu na Hamza.

“Bibi umeenda sana mbali , si kila siku unasema unanipenda sana. Wewe hunipendi tena na nakuchukia”

Mara baada ya kuongea aliikimbilia nje ya geti. “Wewe Irene unaenda wapi? Sijamaliza rudi hapa” Aliongea huku akionekana kuzidi kuwa na wasiwasi.

Hamza aliishia tu kupumua kwa nguvu  na hakuongea chochote kwasababu  hakujua  uadui wa  bibi yake  Irene na yeye umetokea wapi.

“Bibi  ngoja nikamlete”Aliongea  Hamza na kisha  alikimbilia nje kwenda kumleta Irene  kabla hajaenda mbali.

“Irene hebu acha kukimbia”Aliongea Hamza wakati akimshika mkono Irene na kumfanya asimame na  kumkumbatia Hamza.  

“Hamza kwanini bibi anakuchukia sana?”

“Acha kwanza kulia. Wewe huoni hili sio kawaida ?”

“Sio kawaida?!” Aliuliza kwa mshangao kidogo huku akimwangalia Hamza.

“Ndio! Bibi yako anaonekana  kufahamiana na familia ya   mke wangu  na kwa mwonekano wake wa leo ni kama kuna kitu ambacho kilitokea baina ya familia hizi mbili”

Hamza aliona hata kama  ameoa , kumleta Irene nyumbani na kujitambulisha kama rafiki yake  , haikuwa sababu ya kutosha kwa bibi yule kuonyesha  hali ya kumchukia  katika macho yake na kupaniki kwa wakati mmoja.

“Kuna kitu kilichotokea? Itakuwa ni kitu gani?”

“Hata mimi sijui . Ila hisia zangu zinaniambia kuna kitu kinaendelea”

“Hata mimi nashangaa. Sio mara yangu ya kwanza kumtambuslisha bibi marafiki zangu,  na bibi ndio anaenipenda sana  na kunijali kuliko hata ya mama. Nimeshangaa leo  ni mara yake ya kwanza kunikasirikia namna ile kisa wewe”Aliongea Irene.

“Basi kutakuwa na sababu , kwanini bibi yako amekuwa hivi. Hivyo hebu acha kulia na kisha urudi nyumbani . unadhani kama bibi yako hakupendi ana mjukuu gani mwingine wa kumpenda? Nenda nyumbani na hakikisha haubishani na bibi yako , muache atulie kwanza. Tukishapata  sababu  kwanini amekasirika sana ndio  tutajua namna ya kudili na tatizo”

“Hamza naona kabisa mwanzo ulikuwa una sita sita , ila sasa hivi unanichukulia kabisa kama  mpenzi wako. Angalia unavyonishika sura yangu?””

Hamza palepale alishituka , kumbe alikuwa akionyesha  mahaba  kwa  Irene bila ya kujijua.

“Hehe huna haja ya kuwa na hofu , nilijua tu msichana mrembo  kama mimi huwezi kuacha kunipenda”AliongeaIrene huku akimkumbatia Hamza.

Hamza aliishia tu kulaumu tamaa zake , ukweli hakujua  ni tamaa au nini .

Baada ya dakika chache za kumtuliza Irene hatimae alimrudisha nyumbani na kisha  alitumia usafiri wa  bolt kurudi nyumbani. Hamza kabla hajakaribia nyumbani , alikumbuka , hakuwa amenumnunulia Regina zawadi yoyote , hivyo  aliomba kushushwa na kisha moja kwa moja alienda  katika moja ya mgahawa   na kuchukua  kahawa ya maziwa ya kawaida na ya soya.

Mara baada ya kufika nyumbani , Shangazi alikuwa  amekaa kwenye masofa living room na alikuwa akingalia Tv, alikuwa deep  katika tamthilia hio kiasi kwamba alikuwa hadi akifuta machozi.

Mara baada ya kumuona Hamza amerudi, na kumuona akiwa na machozi alishikwa  na aibu kidogo  na kujibaraguza .

“Hamza , mbona leo umerudi mapema sana?” “Nimerudi  baada ya chakula. Vipi Regina amesharudi ?”

“Ndio , baada ya kula ameenda kwenye chumba chake kwa ajili ya kuendelea na kazi”

Hamza aliishia kutabasamu  na kisha

alizipandisha  ngazi kuelekea katika chumba cha Regina na kugonga mlango , lakini aliishia katikati  mara baada ya kumsikia Regina alikuwa akiongea na simu , hivyo aliingia moja  kwa moja.

Regina alikuwa  bize mno , mbele yake kulikuwa na furushi la makaratasi , huku akionekana alikuwa akipokea maelekezo   kupitia simu kuelewa baadhi ya vipengele. Na mara baada ya kumuona Hamza akiingia aliishia tu kumwangalia na  kumalizia kuongea na simu. “Vipi  naona leo umerudi mapema ?”

“Ndio mke wangu. Nimekuletea kahawa ya aina mbili ,  kikombe cha kulia ni kahawa ya  maziwa  na ya kushoto kwangu ni ya   soya, vipi unataka ipi  hapa?”Aliongea  Hamza akiwa na tabasamu.

******

“Vipi mbona unaonekana kuwa na furaha  sana?” Ilikuwa ni sauti ya Kanali Dastani kwenda kwa mwanamke alievalia  nguo ya kulalia ya kitambaa cha  hariri  , katika  moja ya hoteli ya kifaharai iliokuwa  katikati ya jiji .

Mwanamke huyo alionekana alikuwa akiongea na simu  na  ilikuwa ni kama amepokea taarifa nzuri .

“Nilikuambia ilikuwa chaguo zuri kumtumia Irene”Aliongea  huku akisogea kimadaha  na kwenda kukaa kitandani .

“Unamaanisha nini?”

“Sikutegemea. Ila inaonekana  mpango wetu umeenda haraka  zaidi  kuliko nilivyotarajia. Nimepokea simu Irene kaiharibu gari  yangu”Aliongea.

“Tresha  nina  wasiwasi na matendo yako , ya kwanza ilikuwa Alex na sasa  unataka kuwa karibu na huyu Hamza. Sioni faida yoyote”

“Dastani shida inayokusumbua naijua, unasumbuliwa na wivu , unadhani kwasababu Yulia  katokea kumpenda huyu Hamza , hata mimi  nitahadaika na kutoka nje ya mipango ya kazi. Kama ndio unachowaza kuwa na amani. Isitoshe  hii  ndio nakusaidia wewe. Sidhani unaweza kufanikisha mpango wa Yasin bila msaada wangu”Aliongea huku akiwa  na hali ya kujivunia kwenye uso  wake.

“Unafikiria mbali. Ninachotaka mimi ni umakini juu ya  mipango yetu ,  unaona kilichomtokea mzee Mgweno. Sasa hivi  Malibu macho  yote yanamchunguza kwa  kushirikiana na Sinagogu. Kosa kidogo tu na sisi tutaingia kwenye rada  za jeshi”

“Pole yake  Aunt Rehema . Namsikitikia   kwa kile kilichomkuta ma kumuunganisha Mgweno”Aliongea.

“Licha ya Rehema kuwa na msaada mkubwa na kukufikisha hapo   ulipo , lakini sioni  huzuni  kabisa katika macho yako”Aliongea Dastani huku akiwa na kejeli kwenye uso wake.

“Unataka nitoe kilio , ndio  uione huzuni katika macho yangu , sikatai  Rehema ndio alienifanyia  koneksheni mpaka kufahamiana na wakubwa , lakini hio haiondoi ukweli kwamba nimefika hapa kwa juhudi  zangu , ndio maana mimi nipo hai , lakini yeye  alishatangulia mbele za haki”

“Tukiachana na hayo , vipi kwanza hili suala la

Alex. Una uhakika hajui chochote?”

“Nishakwambia hajui chochote , ndio maana nimemwachia  huru. Alex anatumika tu , lakini suala la  malighafi zinazowekwa katika vyungu hahusiki kabisa , yeye ni msambazaji na vyungu anavyopelekea  wateja vinatengenezwa sehemu nyingine kabisa. Mwanzoni nilidhani  ni suala lenye muunganiko  wa moja kwa moja  na watu wa Binamu , lakini sivyo. Kuna uwezekano Jasusi Alonzo ni  Decoy”

“Decoy! Unamaanisha  nini?”

“Wakati ulipokuwa  Ufaransa  nilikuwa nikifuatilia hili suala kwa umakini mkubwa . Alonzo anapokea maagizo  chini ya watu wa kanisa la Wabrazili , lakini katika moja ya kumfuatilia , nimegudua pia  yupo chini ya Taasisi ya Haliz Foundation”

“Haliz Foundation  na kanisa la Wabrazili! Unataka kusema nini?”Aliongea  Kanali huku akihisi  kama kuna kitu kinakuja kwenye akili yake.

“Kuna uwezekano   wa muunganiko   kati ya taasisi ya Haliz Foundtation na vyungu , lakini vilevile kuna uwezekano wa  Haliz kuwa na mahusiano ya karibu na makanisa ya Wabtazili  na kama ni hivyo basi moja kwa moja Kanisa la Wabrazil lipo chini ya  wasinagogu  

“Na kama  kanisa la Wabrazil lipo chini ya Wasinagogu maana yake , Wabtazil wanajua moja kwa moja suala la vyungu lipo vipi  na  Alonzo kuonekana kama analifuatilia hili suala  ni kama chambo tu  kufunika kile kinachoendelea”Alimalizia kanali.

‘Ndio maana nikasema Alonzo anaweza kuwa Decoy Agent. Hili ni suala ambalo hatuna uhakika nalo kwasasa  kutokana na mkanganyiko wa matukuo yaliotukia hivi karibuni . Ingekuwa rahisi kwetu kama  Rehema angerudi  Tanzania . Sasa hivi lipo juu yako Dastani kulitafutia ufumbuzi”Aliongea  Tresha.

“Ufumbuzi! Unamaanisha  unataka niwe mrithi wa nafasi ya  Rehema?”

“Unadhani isipokuwa wewe , atakuwa nani? Kama huwezi kufanya mwenyewe wasiliana  na umoja wako wa  Black Trinity  waamshe  jasusi wao ndani ya kitengo, Sidhani  kama wanakosa Sleep Agent  ndani ya Malibu”

“Hapana , siwezi kuwasiliana na umoja kwasasa. Ni mapema  mno, kwasasa ulinzi ni  mkubwa sana ndani ya kitengo na kila  mwanachama anafuatiliwa”Aliongea  na Tresha alimwangalia usoni kwa sekunde kadhaa na kisha akapotezea.

‘Vipi kuhusu faili umefanikiwa , Au safari ya  Ufaransa  imekuwa bure?”

“Upo mwanga tu , mbinu yangu niliotumia  imelipa kwa kiasi  flani , lakini sina wasiwasi kwasasa.  Nishapata  shabaha nyingine’

“Shabaha  nyingine! Unamaanisha nani?”

“Mdogo wake Dina , kutoka upande wa  familia ya babu yake. Inaonekana bado  ana kinyongo  na Dina kuwa kiongozi na sio yeye. Ninavyosema sasa hivi  wapo  hapa Tanzania. Ni mimi tu kupanga mipango yangu ya namna ya kumuingia

, ni rahisi kupata hili faili.”

“Ukifanikiwa nina uhakika utajiweka katika nafashi muhimu sana ndani ya circle ya  Eliasi.

Kulia yupo  Yasin , kushoto yupo Eliasi. Tukifanikiwa kumwangusha  Yulia na kumpandisha Yasin . Mipango yetu yote itanyooka”

“Kwa Yulia sio kirahisi  sana. Uwepo wa Hamza  ndio changamoto. Licha ya hila nyingi kuchezwa afie Ufaransa  lakini imekuwa tofauti. Yule mtu ni hatari sana”

“Hamza niachie mimi. Udhaifu wake upo kwa  wanawake na hao hao watakuwa anguko lake”Aliongea Tresha huku akisimama na kujizungusha zungusha kwenye kioo.

Previoua Next