Reader Settings

“Kama umesema kila kikombe kina kahawa , kuna utofauti gani. Halafu mbona sijawahi kuona hivyo  vifungashio?”

“Ndio habari ya mjini kwasasa  hivi mke wangu, ni kahawa iliotengenezwa hapa hapa nchini , lakini kutokana na upekee wake ndio  maana  inauzwa kwenye migahawa mingi   ambayo ni francaised.Nashangaa mwanamke kama wewe huna habari , wakati ndani ya kampuni  wafanyakazi wengi wameshikilia mkononi” “Kwahio unasema mimi ni mshamba au?” “Hapana, ninachomaanisha ni kwamba mke wangu wewe ni wa matawi sana , ndio maana ni ngumu kujua  biadhaa mpya za aina hii”Aliongea Hamza kujitetea.

“Nitajaribu kila kimoja , kujua radha yake ilivyo”Aliongea Regina huku akichukua mrija kutoka katika vikombe vyote  na kuanza kufyonza kidogo katika kila kimoja.,

“Nataka hiki chenye maziwa ya  soya, unaweza  kunywa hiko kingine”Aliongea Regina huku akishangazwa na utamu wa kinywaji hicho.

Hamza mara baada  ya kuona namna ambavyo mwanamke huyo alivyokuwa  na furaha  akinywa kinywaji alichomletea alijihisi joto kwenye moyo wake  na kujiambia   alifanya vizuri kupiga stori kidogo na marafiki zake  Eliza. Ndio waliompa  taarifa juu ya  utamu wa kinywaji hicho, namna kinavyoshangamsha akili na radha yake.

Regina aligundua , Hamza alikuwa akimwangalia muda wote  na kumfanya uso wake kushikwa na joto kidogo.

“Mbona unaniangalia kiasi hicho?”

“Ni kwasababu mke wangu anaonekana kuwa mzuri sana. Si kinai kukuangalia”Aliongea Hamza  huku akicheka.

“Na hizo sifa unazonipa hata sikuamini tena. Leo nimetoka vijipele kwenye uso wangu, naonekana mbaya”

“Wapi! Mbona hata sivioni?” Hamza kweli hakuweza kuona hivyo vipele Regina anavyoongelea.

“Na huo upofu wako , utaonaje?”Aliongea Regina huku akitingisha kichwa chake kwa kumsikitikia.

“Vipi , si ulisema unatoka na  Irene ? Mtoko wenu umeendaje?”

Hamza alifikiria kwa sekunde kadhaa  na aliona sio mbaya kama atamwambia Regina kilichotokea.

Regina mara baada ya kusikia Irene alipata ajali alipatwa na wasiwasi kidogo  na kuuliza kama alikuwa sawa   na mara baada ya kusikia ni gari pekee lililopata  shida aliona  kumbe sio suala kubwa.

“Wife  hujawahi  kukutana na  bibi yake Irene. Inaonekana anakufahamu vizuri tu  na  kunifahamu hata mimi na wewe tuna mahusiano”

“Sijawahi  kukutana nae wala kumsikia na hata bibi na  shangazi  sijawahi kusikia wakimzungumzia , labda  hawakuongea chochote. Ila itakuwa kulikuwa na mahusiano. Ninachojua tu ni Mama yake Irene aliekuwa ni jirani yetu  na mara nyingi alikuwa  akiishi na ndugu  wa upande wa kwao”

“Basi itakuwa  kuna  kitu tu  hatujui , ila kimetokea  zamani kidogo , isitoshe wote ni wazee “Aliongea  Hamza.

“Kwanini unajali sana. Kama  una shauku sana kwanini usimuulize Shangazi?”Aliongea Regina.

Hamza alifikiria kidogo , ila aliona haina haja ya kumuuliza shangazi , hivyo aliamua kupotezea.

“Wife sitaki kuendelea kukusumbua. Endelea kuwa bize”Aliongea Hamza , hakutaka  kuonekana kuwa siriasi na suala hilo na kumfanya Regina ahisi  tatizo.

“Nisindikize kwenda kwenye  Harambee na Mnada kesho. Kama una nafasi”Aliongea Regina.

Hamza alionekana kushangaa. Alikuwa tayari alishasikia kuhusu mnada huo kutoka kwa Yulia  na  ndio sasa Regina anamwambia.

Sasa kwasababu mke wake amekwisha kuongea na kumwalika , hakuona sababu ya kukataa. “Sawa , kesho nitajianda vizuri kwa ajili ya kukusindikiza na kuhakikisha unajivunia kwenda na mimi  mke wangu”Aliongera  Hamza akiwa na tabasamu.

“Eh! The Manificient King of hell  will accompany me to  a small charity  auction , I’ am flattered”Aliongea Regina kwa kingereza huku akimwangalia  Hamza na mwonekano wa kichokozi.

Hamza aliishia kutoa  pumzi ya kufarijika mara baada ya kumuona Regina  yupo kwenye mudi ya kumtania  , na aliona ni vizuri.

“Wife nimekuita ‘ Mke au Wife ‘ Kwa muda mrefu , kwanini sijawahi  kukusikia ukiniita’ Hubby?” Hamza aliona achukulie  fursa mudi nzuri ya Regina.

“Kwanini unalazimisha nikuite hivyo , kwani haitoshi tu mimi kukuita kwa jina lako. Mbona wenza wengi tu wanaitana kwa majina yao?” “Lakini natamani kusikia ukiniita hata mara moja

, sio lazima  kila saa  japo mara moja moja”

“Nataka nifanye kazi , unaweza  kuondoka sasa”Aliongea Regina huku akikaa katika mkao wa ubize .

Hamza  hakuwa na  jinsi , aliona bado mwanamke huyo hakuwa  karibu sana na yeye  kimwili , hivyo aliona ngoja asubiri , wakati utafika tu .

*****

Siku iliofuata  Hamza aliishia tu kuzunguka ndani ya kampuni  na ilipotimu   muda wa jioni  jioni , Regina alimpigia simu.

“Wife mbona kama muda wa kwenda kwenye harambee bado?”Aliuliza Hamza mara baada ya kuona bado ni mapema.

“Kuna sehemu nataka unisindikize kwenda kwanza , tukitoka huko tutaelekea moja kwa moja kwenye mnada”

“Tunaenda kukagua  biashara zako?”

“Hapana”

Kipindi hicho , Black Fog  alikuwa  msaidizi  rasmi wa karibu  wa Regina na  ndio aliehusika mara nyingi kutoka  na Regina  kukagua biashara zake.

“Kuna sehemu   binafsi naenda  na nadhani itakuwa vizuri tukienda pamoja”Aliongea Regina.

Ijapokuwa Hamza alikuwa katika hali ya kushgaa , lakini bado alikubali na kushuka  kwenye maegesho ya magari  na kuwasha gari na kumsubiri Regina .

Haikuchukua muda Regina   alishuka kutoka  ofisini kwake akiwa ameshikilia mifuko. Hamza mara  tu  baada ya kuona mifuko hio , alijua ni wapi Regina anaelekea.

Mara baada ya wawili hao kuingia kwenye gari ,

Hamza aliendesha gari moja kwa moja mpaka  yalipo makazi  ya famili ya Regina ya zamani. Maneo ya Msasani.

Regina alipanga kumpatia  Lamla zawadi ambazo alitoka nazo Paris , ijapokuwa alikuwa amesahau kwa muda , ila baada ya kukumbuka n i kipindi cha sikukuu , aliona ndio apeleke.

Mara baada ya kufika , kulikuwa na mabadiliko kiasi , kutokana na kuwepo mtu anaeishi ndani ya jumba hilo kubwa  , angalu halikuwa na hali ya upweke  sana.

Tokea  Lamla  arudi ndani ya nyumba hio ,

Regina aliwasiliana na TDS( Taita Domestic Service) Kuacha kuendelea na huduma yao.Hivyo kila kitu kilikuwa chini ya Lamla.

Lamla alizoea kuishi maisha ya kifahari tokea akiwa mdogo , lakini mara baada ya kupitia  magumu , alionekana  mdogo mdogo kuanza kuyakubali maisha yake mapya.

Wawili hao mara baada ya kushuka kwenye gari , waliweza kumuona Lamla akitoka  nje  akiwa ameshikilia boksi kubwa la glasi au kioo.

Alikuwa amevalia Aproni na  ndala miguuni. Nywele zake alikuwa amezifunga  kwa kurudisha nyuma. Kama vile alikuwa bize kufanya  kazi za nyumbani.

Katika lile boksi la glasi , kulikuwa na Kasa aliekuwa amelala kivivu ndani yake.

Mara baada ya kumuona Hamza na Regina ,  Lamla alionekana kuganda kidogo , alionekana kuwa na wasiwasi , lakini  kulikuwa na hali ya furaha kwenye macho yake.

“Regina , Hamza ,  karibuni”Aliongea  

Regina  mara baada ya  kuona kasa yule mdogo  alionekana kushangaa.

“Unamlea huyo  Kasa?”

“Ndio! Naboreka kuwa mwenyewe , sijawahi kufuga kitu chochote hapo kabla , lakini mara baada ya kusikia Kasa  ni mwepesi kufuga  na anaweza kuniondolea upweke . ndio  maana nikamnunua kwa  baba mmoja aliekuwa akiwasambaza. Nimeambiwa niwe namtoa  juani kila siku ili  mgogo wake kumulikwa na jua”

Regina mara baada ya kusikia , hivyo alijikuta akigeuka na kukagua mazingiraya nyumba na aliweza kuona mimea mingi ikiwa  imepandwa. “Hayo maua wewe ndio umepanda?”

“Ndio, sipo sana bize ndio maana nikaona pia nipande pande maua”Aliongea na kumfanya Regina kutabasamu.

‘Vipi , umegundua sasa  kazi nyingi ni ngumu kuliko ulivyokuwa ukifikiria?”

“Ni kweli! Sasa hivi kadri  ninavyofikiria , najiona kweli sikuwa mtu mzuri”Aliongea huku uso wake ukiwa umejaa  huzuni.

Regina alichukua ile mifuko chini na kisha alimpa ishara Lamla kupokea.

“Nimekuletea hizi. Nilienda Paris nikaona sio mbaya nikikuletea zawadi. Kuhusu mifuko mingine miwili niliokuja nayo , haijapata mtu , nimeona nikuletee pia”

Hamza mara baada ya kusikia maneno ya Regina kidogo tu atoe kicheko, Yaani Regina kanunua mikoba yote hio kwa ajili yake , halafu muda huo anaigeuza kama vile  ni kweli imekosa  mtu.Alimfikiria Regina ila hakupata picha kamili.

Lamla hakuwa mjinga , mara baada ya kuoina mifuko hio ya Zawadi , alijikuta akipanua mdomo kwa mshangao  na sekunde chache mbele macho yake yaligeuka na kuwa mekundu.

“Regina kweli umeniletea hizi zawadi kwa ajili yangu?”

“Ndio , kama hutozipenda unaweza kuzitupa tu, isitoshe sina pakuziweka”Aliongea  Regina bila ya hisia nyingi .

“Nazipenda , nina uhakika nitazipenda”Aliongea  Lamla huku akitingisha kichwa  kwa  hamasa kubwa na kupokea.

“Karibuni ndani ,  mpate hata kinywaji chochote , sio vizuri kusimama nje wakati hapa ni nyumbani”Aliongea.

“Asante , ila kwasasa hapana , kuna sehemu tunawahi”Aliongea Regina.

Mara baada ya kumsikia   Regina akiongea hivyo ,  Lamla alishikwa na hali ya kusikitika kidogo , lakini aliificha na kicheko .

“Basi hata siku nyingine , najua mpo bize , siku ukipata  nafasi njoo  nitakuandalia chochote”

Regina aligeuka  na kujiandaa kuingia ndani ya gari , lakini kabla hata hajapiga hatua , Lamla aliita .

“Regina!”

“Ndio , kuna  unachotaka kuongea?”Aliuliza Regina bila kugeuka na muda huo  alionekana Lamla akijing’ata ng’ata.

“Najua ninachoweza kusema sasa hivi kinaweza kisiwe na maana , lakini bado nataka kukuambia , Samahani”

Regina mara baada ya kusikia kauli hio, alitetemeka kidogo.

“Ulishaniambia  hivyo mara ya mwisho”Aliongea Regina.

“Ndio. Lakini  nataka kuongea kitu  chochote kwako leo . Asante sana , nakushukuru sana. Najua hakuna kitu naweza kukufanyia katika haya maisha , lakini  kama pepo ipo  natamani kuja kuwa  mama kwako. Moja ya kitu ninachojutia mpaka sasa , ni  tokea siku niliokuona sijawahi kukujali   kabisa.”

Regina aliishia kukunja ngumi kidogo na kisha kuiachia na akavuta pumzi nyingi na kuzishusha.

“Siku ya Christmass , njoo Kigamboni  nyumbni , nadhani haitokuwa vizuri kumhangaisha shangazi kuja mpaka huku”Aliongea  

Lamla alijikuta akishangaa , kama vile alikuwa amesikia vibaya  na kujikuta akiuliza kama Regina anamaanisha.

‘Ni kweli naweza kuja?”

“Usifikirie vibaya , sitaki tu kumuona  shangazi akichoka kuja mpaka huku. Pia itakuwa vizuri kama utakuwepo na kumsaidia saidia”Aliongea Regina.

“Naelewa , hata usiwe na wasiwasi , hakika nitakuija na kumsaidia  na maandalizi”Aliongea Lamla huku akiitikia kwa furaha.

Mpakla  hapo Regina hakuingia kwenye gari haraka  na Lamla hakujua  nini cha kuongea , kila mmoja alionekana kuwa katika hali ya kutafakari.

Hamza aliishia kunyamaza kwa sekunde kadhaa na kisha aliishia kusugua pua yake akihisi hali ya hewa kidogo imekuwa nzito.

Alijikuta akiangaza macho yake na kumshangaa yule kasa aliekuwa kwenye boksi akipigwa na jua.

“Huyu mbona ni kasa mweusi?!”

Lamla alijikuta akikurupushwa kutoka kwenye mawazo mara baada ya kusikkia  sauti ya Hamza.

“Kuna shida  kwani ? Mimi  nilikutana na mzee wakati nikitoka sokoni ndio akaniambia anamuuza , nilivyoona ni mzuri nikamnunua”

“Kuna  shida kwani   akiwa mweusi?”aliuliza Regina.

“Huyu ni Kobe mweusi , ni jamii ya kobe ambao ni adimu sana. Nadhani huyo baba aliekuuzia  alimpata kwenye mabonde ya maji  ndani ndani huko porini , ila aina hii ya  Kasa  wanalindwa mno  kutokana  na kuadimika kwake”Aliongea Hamza.

Regina alishindwa kujizuia na kumwangalia huyo  kasa , alionekana kulala kivivu vivu na macho yake ya rangi ya kijani , ukweli ni kwamba alionekana  kuwa wa kijani ambae anaelekewa kuwa mweusi .

“Kwahio unataka kusema nini? Kwamba ampeleke katika idara ya hifadhi wanyama au”Aliuliza Regina.

“Haina haja , kwasababu unamlea basi endelea  kumlea”Aliongea Hamza na kisha kumwangalia  Lamla kwa macho ya udadisi.

“Kama unataka kuwa mama bora ,  sio mbaya kuanza kulea kobe”Aliongea na kumfanya Lamla kuwa na macho yaliojaa  shukrani. “Asante  sana, nitafanya hivyo”

Hamza na Regina waliingia kwenye gari yao na kisha walianza safari ya kuelekea  kwenye  Harambee na mnada.

Wakiwa njiani , Hamza  alishindwa kujizuia kumwangalia  Regina  mara kwa mara  na kuwa na  tabasamu.

Regina alikuwa akimwona  kila saa  na alikuwa kimya , ila alishindwa kuvumilia mara baada ya kuona Hamza anazidi.

“Unamwangalia nani na kutabasamu?”

“Hamna tu , ni kwamba  nashindwa kujizuia na kuona  mke wangu anazidi  kupendeza kila   saa ninavyomwangalia, hivyo nashindwa kujishikilia na kukuangalia mara kwa mara”

“Mh! Lazima utakuwa unanikejeli ndani kwa ndani?”

“Kwanini nikukejeli?”Hamza alishangaa. “Unaijua sababu  mwenyewe ya kunikejeli , huna haja ya kujifanyisha”

“Wife m ukweli ni kwamba   hata  sijali kama umemsamehe  Lamla au unaendelea  kumchukia , ila  ukweli  nimetokea kukubali moyo wako , kama ingekuwa ni mimi, nisingeweza kufanya hivyo”Aliongea Hamza.

“Kweli!” Aliuliza Regina huku akionyesha hali ya  mshangao kiasi katika macho yake.

“Unadhani naweza kukudanganya. Nimekuwa mbwa?”

“Wewe ni  jibwa kabisa”

“Basi wewe ni kajimbwa kadogo”

“Mimi sio mbwa. Shenzi!”

“Haha, mke wangu unavyonukia ni kama  vile vimbwa vya kijerumani” Regina kusikia hivyo  alijikuta akikasirika  na kugeuza kichwa chake pembeni.

“Sitaki kuongea na wewe tena”

Ilikuwa utani tu , hivyo Hamza asingeendelea kumwambia alikuwa mbwa.

Hamza mara baada ya kuishi na mwanamke huyo kwa muda mrefu kidogo , aligundua alikuwa akijali sana mwonekano wake , hivyo hakufurahishwa na utani wa kuambiwa alikuwa mbwa wa kijerumani.

Mara baada ya kufika  katika jengo ambalo mnada na harambee ya kusaidia watu,wawili hao walishuka nje ya gari  na  waliweza kuona kulikuwa na magari mengi zaidi ya mia yaliokuwa ni ya kifahari. Kusanyiko hilo la Harambee lilionyesha ukubwa wake  kwa namna lilivyokusanya watu wazito ndani ya jiji la Dar.

Eneo la nje la kuingilai kulikuwa  kumepambwa sana, asilimia kubwa ya mapambo yalikuwa ni yale ya kukaribisha mwaka mpya.

Kwasababu ilikuwa  ni Harambee  na Mnada watu wengi walivalia kawaida.

Mwonekno wa Regina ulivutia watu wengi. Wasifu wa mwanamke mrembo na tajiri  , ilikuwa ni moja ya sifa kubwa iliombeba Regina.

Watu walijaribu kumsogelea  Regina kuongea nae , lakini  kama kawaida ya Regina  hakujisumbua kuendeleza maongezi muda mrefu zaiid ya salamu pekee tema ile ya kujivuta.

Lakini hata kama Regina alionekana kuwapotezea watu hao , hakuna ambae angekasirika , isitoshe ukauzu wa Regina ndio ulifanya watu wengi kutamani  kupata fursa ya kumsogelea na angalu kuongea nae  kwa muda mrefu na kwenda kujisifia.

Hamza alishindwa kujizuia na kujihisi  kujivunia katika moyo wake , katika macho ya wengine , mwanamke kauzu kama huyo ambae ni ngumu hata kuanzisha nae maongezi , alikuwa ndio mke wake. Ingawa  nafasi yake kama mume kwa Regina haikuwa imefahamika kwa watu wengi lakini Hamza alijihisi kidume kweli.

Ile wawili hao  wanakaribia kuingia katika mlango wa ukumbi  , kundi dogo la watu lilionekana na  kumvutia Hamza macho.

Alikuwa ni mwanaume na mwanamke wazee hivyi ambao wameongozana na  watoto wadogo  na walionekana ndio wanafika.

Previoua Next