Reader Settings

Mchoro wa kesho yetu

Alikuwa ni  Mama Wadeni  wa kituo cha kulele watoto  cha Morogoro ,Foot Academy, aliekuwa ameongozana na kundi la watoto. Pembeni yake kulikuwa na mwanaume  mzee. Hamza alimjua ni moja ya wazee waliokuwa wakisaidia ndani ya  kituo hicho. Hakumuona Mzee Hizza.

“Madam Wadeni!” Aliita Hamza kwa mshangao mara baada ya  kumuona.

“Hamza! Kumbe na nyie mmekuja! Nilikuwa nikijiuliza kama ningewaona  , ila  matarajio yangu yamekuwa sahihi”Aliongea mwanamama huyo akiwa na mwonekano wa  furaha huku akimwangalia Regina.

Upande wa Regina muda huo alikuwa akimwangalia msichana mdogo kibonge  aliekuwa bize kulamba ice cream. Na msichana yule mdogo mara baada ya  kumuona Regina alimtolea  ulimi  kwa ishara ya kumchokoza.

“Dada Mbahili”Aliongea  yule msichana , walifahamiana na Regina  kituoni alipoenda  na  Hamza na  matukio yaliotokea ndio yalimfanya Regina kuonekana na msichana huyo kama dada mbahili.

Regina alichanua  macho yake na ile anataka  kubishana na huyo msichana aligundua alikuwa   eneo la  wazi  na watu wengi walikuwa wakiwaangalia, hivyo aliishia  kujifanyisha hakumsikia.

“Madam Wadeni , na nyie mmealikwa”Aliuliza  Regina.

“Katibu wa Viwanda  ndio katualika mara baada ya kuona michoro ya watoto. Amesema itaongeza uzito  juu ya mchoro tuliowakilisha kupigwa mnada kama watoto  watashiriki  pia.Ndio maana  nimekuja nao. Isitoshe huu  ni mkutano wa mabosi, hivyo nimeona sio mbaya kama watakuwepo  hapa kutoa shukrani zao”

“Mhmh! Mbona sijawahi kusikia huu utaratibu, nani  kasema uwalete?”Aliongea Regina akiwa amekunja sura.Kawaida  licha ya  vitu mbalimbali kuletwa kupigwa  mnada lakini watoto hawakushiriki kabisa zaidi ya viongozi wawakilishi pekee .

Lakini muda huo mwanaume  mwenye kitambi  mrefu  kidogo alievalia suti  nyeusi ya Armani alisogea akiwa na uso uliopambwa na tabasamu.

“Katibu  Gondwe , wewe ndio  umemwalika

Madam Waden na watoto kuhudhuria?”

“Kumbe bosi Regina unafahamiana  na Waden wa Foot Academy! Ndio  ni mimi niliewaalika”Alikubali bila shaka yoyote na kisha alimgeukia  Wadeni.

“Wewe ndio ndio Madam  Hizza! Mimi ni Khatibu  Gondwe , ndio niliekutumia  mwaliko”Aliongea Katibu akipeana mikono na  Madam Wadeni huku akiwaangalia watoto kwa namna ya kuwahesabu.

“Mbona umekuja na watoto wachache sana?”

“Oh! Ndio , nimeona  itapunguza  usumbufu  kudili nao wote , maana wengi ni  watundu sana”  Waziri kusikia vile alionekana kutoridhika.

“Wadeni  upo siriasi kwelim niliposema uje  na watoto   nilimaanisha wengi hata kituo kizima. Kwanini kuwe na usumbufu. Hata hivyo sio mbaya , muda ushaenda sana hatuwezi kubadilisha”Aliongea  na kisha palepale aligeuka  na kuanza kuita baadhi ya watu ambao alionekana kutangulizana nao.

“Mzee Dochi , Mzee Filimbi sogeeni sasa ni muda wa kupata picha ya pamoja  na watoto”

Wafanyabiashara kadhaa walisogea waliokuwa  wakisalimiana na Regina mara baada ya kumuona.

Mara baada ya hapo  waliita watu  na  kuwachukua wale watoto na kwenda kuwasimamisha katika mabango waliokuwa wameandaa . Mabango hayo yalikuwa na majina yao kama vile walikuwa wakihofia wasipoandika majina kuna mtu anaweza kutowatambua.

“Huyu Gondwe ni nani?”Aliuliza Hamza  ambae hakuwa na uso mzuri kabisa.

Ilikuwa ni wazi kabisa watu hao  wanawatumia hao watoto  kujitafutia sifa na sio kwamba wapo na moyo wa dhati wa kuwasaidia.

Hamza  aliwachukulia Madam  Wadeni , Mzee

Hizza na  watoto wa kituo cha Morogoro kama familia yake , hivyo  ilikuwa  kawaida kutokuwa na furaha kwa kuona tukio hilo.

Mara baada ya kuona sura ya  Hamza, Regina alijua tu lazima atakuwa amekasirika.

“Ni katibu mkuu  wa wizara ya biashara na viwanda. Ni mfanya biashara mkubwa wa  kuzalisha chuma”Aliongea Regina.

“Najua utakuwa umekasirika , lakini  hakuna haja ya kulikuza hili suala  kwani haitokuwa nzuri kwa watoto”

Hamza macho yake yalisinyaa , kama isingekuwa  hakutaka kumtia wasiwasi Madam ,  angeshafanya  jambo mpaka muda huo.

Mara baada ya  watoto hao kupangwa vizuri mbele ya mabango , wafanyabiahsa wale walisogea wakiwa na matabasamu  ya kutosha osoni na picha zikaanza kupigwa na waandishi wa habari ambao walionekana kabisa walikuwa wameandaliwa kwa kazi hio.

“Bosi Regina., unaonaje ukiungana na sisi. Haina haja ya kuwa na bango la kukutambulisha.  Sura yako ni utambulisho tosha”Aliongea Gondwe.

“Haina haja”Aliongea  Regina akitingisha kichwa.

Ukweli  ukaribisho huo ulikuwa wa kinafiki tu  na Gondwe na wenzake hawakutaka Regina ashiriki, kwasababnu walijua   Regina akiwa sehemu ya picha  hawatoonekana tena.

Muda huo sauti ya maringo  na   hatua za kimapozi zilisikika.

“Mbona kuna shamra shamra  sana hapa?”

Alikuwa amevalia  gauni refu lenye pasua la saizi na kikoti cha  manyoya kilichomkaa vyema mwilini na kumfanya aonekane kama malkia.

Uvaaji wake uliop[itiliza ulivutia watu wengi , hata Regina  ambae alikuwa na mwonekano  wa kuvutia kidogo , alifunikwa na vazi hilo.

“Oh ! Bosi Yulia  naona umefika na wewe muda mwafaka. Unaonaje ukiungana na sisi na kupiga  picha  kadhaa?”Aliongea Gondwe.

“Katibu Gondwe ,  huyo msichana  mbele yako anavutia mno , naweza kumkumbatia”Aliongea Yulia.

Walipokuwa wamesimama katikati ya wanaume  hawakuwa na furaha , sasa baada ya kumuona Yulia macho yao yalichanua.

“Dada Mkubwa wewe ni  mrembo sana”Aliongea kifurushi.

Yulia kusikia hivyo alifurahi  na kuinama chini na kumkumbatia.

“Kweli! Na wewe pia  ni mrembo mno. Niambie jina lako ni nani?”

“Naitwa Esma Bando”

“Esma Bando! Jina  limekukaa vizuri mno ,  ulivyonenepa kama kakifurushi”Aliongea Yulia huku akicheka.

“Ni Bando  sio  kifurushi”Aliongea Esma.

“Okey ! Esma  Bando. Mimi dada yako mkubwa nitakupeleka kula vitu vitamu baada ya hapa”Aliongea Yulia akionyesha ukarimu.

“Sawa dada mkubwa”

“Waheshimiwa , huyu  mtoto ni mdogo sana. Mimi naondoka nae”Aliongea Yulia.

Gondwe na  wenzake walijifanyisha  kutokumuelewa na kuendelea kutabasamu  na kumuacha Yulia aondoke na  Esma  Bando .

Yulia akiwa amembeba  Bando, alienda mpaka mbele ya Regina na Hamza, na kwa macho ya  kichokozi alimwangalia Hamza.

“Naona umekuja nae? Nilijua hatokuambia” Hamza aliishia kutoa tabasamu la uchungu, ,ingekuwa vizuri kama asingeongea chochote.

Regina  alimwangalia Hamza  na  mwonekano wa  maswali  ila hakuongea chochote.

“Esma kati ya mimi na huyu  dada , nani mzuri?”Aliongea  Yulia,

 Esma alimwangalia Regina kwa macho yasiokuwa na hisia , haikueleweka Regina alimfanya nin Bando mpaka  kumchukia.

“Dada Mkubwa wewe ni mrembo mno , kuliko huyu  Dada mbahili”

“Wewe...” Regina mara baada ya kusikia hivyo, alijikuta akipandwa na hasira ,  na alichukia kuona hawezi  kushindana na mtoto mdogo.

“Dada Mbahili! Regina umewafanya  nini hawa watoto kiasi cha kuwafanya wasikupende ? Watoto  hawana dhambi , hawawezi kudanganya.

Ila sio mbaya nadhani awamu hii nimekushinda” Yulia mara baada ya kuongea hivyo aliondoka na  Bando kuelekea upande wa  vioski.

“Namchukia huyu mwanaharamu”Aliongea Regina huku akipiga miguu yake chini.

Hamza alihisi kichwa chake kikianza kumuuma. Ilionekana mbele ya  Yulia , Regina alionekana bado mdogo.

“Mbona na wewe huongei.  Ni kweli yeye ni mrembo  kuliko mimi?”Aliuliza Regina kwa hasira akimwangalia Hamza.

“Inawezekana vipi! Hakuna mwanamke  kwenye dunia hii mrembo kumzidi mke wangu”

Regina licha ya kusikia kauli hio , alishindwa kuimeza hasira yake.

“Kama ningejua bora nisingekuja. Nimekasirika sana kumuona huyu mwanamke”Aliongea.

Muda huo Katibu Gondwe alimaliza kupiga picha na watoto wa  kituo cha FOOT  na  hawakuwa wamealika  hao tu wa Morogogo bali walikuwa wameita watoto wengine ambao pia  walipiga nao picha.

Hamza kuona hayo yote ,  moyo wake ulijisikia vibaya. Lakini asingeweza kufanya chochote kutokana na mazingira yalivyo.

Mara baada ya  Wadeni kumaliza , aliwachukua watoto na kumsogelea Hamza.

“Nini kimekutokea , mbona sura yako imekuwa mbaya hivyo ?”Aliuliza Madam.

“Hakuna tu”Alijibu Hamza kifupi.

“Mtoto mjinga. Unadhani sijui nini unafikiria. Lakini katika ulimwengu huu  kuna  vitu  ambavyo mtu hawezi kukataa  hata kama hapendi au  hafurahishwi navyo. Ila hayo  ni mambo ambayo unakubaliana nayo tu kwasababu  ni ya kupita, haijalishi mabosi wanatuchukuliaje , ila ili mradi tuna hela ndani ya kituo chetu   za kusaidia maisha ya watoto. Sioni  haja ya kufikiria sana ,  si ndio malengo ya  kituo ?”

Hamza na Regina mara baada ya kusikia maneno ya mwanamama huyo , walishangaa baada ya kuona  kwamba Madam Wadeni alikuwa akijua  unafiki wa  matajiri hao , ila aliamua tu kukubaliana nao kwa ajili ya watoto.

“Madam  ni  mara chache sana kuwakubali watu , ila kwako nimetokea kukubali sana”Aliongea Regina na tabasamu.

“Regina haina haja ya kuwa siriasi hivyo , mimi  na Hiza tayari ni wazee  na hatuna muda mwingi wa kuendelea kuwasaidia hawa watoto. Ikitokea fursa ya kuwasaidia , kitu pekee ni kufanya kila linalowezekana kufanikisha. Ijapokuwa malengo  yetu kwasasa ni kutafuta mtu ambae  anaweza kurithi nafasi zetu”

“Madam Wadeni , kwani  mna shida ya kiafya , nakumbuka hata mara ya mwisho Mzee Hizza alionekana kukonda sana  na hata wewe pia unaonekana kunyongea”Aliongea Hamza.

“Ukiwa mzee ni kawaida kukonda. Bado nina afya nzuri tu, hata usiwe na wasiwasi”Aliongea akijaribu kumthibitishia Hamza alikuwa na Afya nzuri.

“Sijui , ila sidhani kama  kutatokea viongozi wazuri wa kituo kama  wewe na Baba Hizza. Unaonaje tukisaidia , itakuwa vizuri mkipata mrithi mapema na kustaafu”Aliongea Regina.

Hata  Hamza alikuwa akifikiria hivyo hivyo , ila hakujua nani angefaa kuongoza  kwa kurithi nafasi za Wazee hao.

Regina alisalimiana na baadhi ya watu aliofahamiana nao kabl ya  tukio kuanza.

Muda mchache baadae Hamza na Regina walionyeshwa siti zao na kwenda kukaa mbele kabisa.

Haikuchukua muda mrefu pia , viongozi kadhaa  wa serikali walipanda juktwaani na kutoa hotuba fupi ambayo ilikuwa ndio kama ufunguzi wa tukio hilo la mnada na harambee.

Hatua ya kwanza ilikuwa ni mnada kwanza na kisha ndio harambee ingefuatia.

Na haraka haraka ili kuokoa muda , mtu wa kuongoza mnada alikaribishwa  na  rasmi mnada ukaanza.

Kitu cha kwanza kupigwa mnada , ni mchoro kutoka katika moja ya  kituo cha kulelea Yatima kilichopatikana Mkoani Tanga Wilaya ya Lushoto milimani.

Kulikuwa na kila aina ya vitu , iwe michoro , vifaa vya kuchomga na  vitu vingine vingi vya kisanii , lakini hata hivyo, vitu hivyo havikuwa na thamani sana, isitoshe ufundi uliotumika haukuwa ule mkubwa. Ila matajiri walivinunua kwa hela nyingi  zisizopungua  laki nne.

Ilivyofikia zamu ya  watoto wa kituo cha Foot , wakiongozwa na wadeni wao , waliweza kutoa karatasi kubwa kabisa iliokuwa imekunjwa kunjwa na mara baada ya kufunguliwa, kulionekana michoro ya aina nyingi katika karatasi hio ya pamoja . Moja ikiwa ni maua , michoro mingine ilikuwa majengo na nk. Ilionyesha dhahiri  watoto walishirikiana kuchora mchoro mmoja. Na kisha kuupatia jina la Mchoro wa Kesho yetu.

Mshereheshaji wakati wa kuutolea maelezo mchoro huo , alimpa nafasi  pia  Madam Wadeni kusimama , huku akisema  hela zote zitakazopatikana katika mchoro huo  zitaenda moja kwa moja katika kituo chake bila ya kupunguzwa hata kidogo.

“Bei ya kuanzia ya huu mchoro ni laki moja , kila mtu anapaswa kuongeza  elfu hamsini kila anapotaja bei”Aliongea.

“Nitauchukua kwa milioni kumi”Aliinua kibao  Katibu Gondwe.

Kununua mchoro huo kwa milioni kumi , licha ya kutokuwa na thamani , ilionekana kiasi kingi cha pesa. Na watu wengi walimpongeza kwa kupandisha bei  haraka  mpaka kufikia milioni kumi.

“Watoto ni  taifa la kesho , siwezi kuwasaidia watoto wote kwa hiki kiasi kidogo , kitu pekee ninachoweza kufanya ni kuonyesha  ukunjufu wangu wa moyo , hivyo msinipongeze sana , mimi Gondwe ni suala dogo sana hili kwangu”Aliongea  akiwa amesimama .

Kutokana na alichofanya , watu wengi waliona aibu kushindana nae , isitoshe walifahamu ndio aliewaalika  watoto wa kituo cha Foot kutoka mbali morogvoro huko , hivyo   alihitaji nafasi ya kujionyesha. Hivyo mabosi waliona haina haja ya kufanya mambo kuwa magumu kwake.

Isitoshe mchoro huo ulikuwa ni kama takataka tu baada ya kuununua , hata kama ungeuzwa kwa elfu kumi usingekuwa na thamani hio. Hivyo hakuna alieuhitaji.

Mara baada ya  Katibu Gondwe kuongea hivyo, palepale alitembea na kumsogelea Madam Wadeni na kupeana nae mkono huku akiwapa nafasi waandshi wa habari kupiga picha.

Madam Wadeni  hakuona shida , alionyesha ushirikiano na alienda mbali kutoa shukrani zake nyingi kwa niaba ya watoto.

Mara baada ya kuona tukio hilo na matendo yanayoendelea , Hamza alishindwa kabisa kuzikabili hasira  zake na kuishia kucheka kikauzu na kuongea  kwa sauti;

“Baada ya kupiga picha zote hizo , unatoa hela ndogo hivyo ?”

Ingawa sauti yake  haikuwa kubwa sana , lakini ilitosha watu wengi kuisikia ndani ya ukumbi huo  uliokuwa tulivu.

Isitoshe pia  mwanaume ambae ameambatana na Regina , alikuwa ni sehemu ya macho ya watu wengi na walitamani kujua ni nani haswa , lakini hawakuweza kuuliza.

Katibu mara baada ya kusikia kauli ya Hamza , mwonekano wake ulikakamaa na aliishia tu kutoa tabasamu kuficha hasira yake.

“Wewe ni mshirika wa Mkurugenzi Regina sio. Inaonekana una  maoni  mengi kuhusu mimi , naweza kujua  jina lako na cheo chako  kama hutojali”Aliongea.

“Mimi sio Mdoshi  kama wewe, kazi yangu ni ya ulinzi tu “Aliongea Hamza.

“Nini!” Mara baada ya kusikia Hamza alikuwa ni mlinzi tu halafu anajaribu  kuongea  ongea alijikuta  akikunja uso kwa hasira.

“Yaani mlinzi tu halafu unathubutu  kukejeli  ukarimu wangu ? Bosi Regina ni tabia gani hii ya mtu uliekuja nae?”

“Hujamuelewa tu alichomaanisha , anasema punguza ubahili”

“Wewe..” Katibu  ghafla tu alikosa usemi na kufanya watu waliosikia kauli hio kushindwa kujizuia na kuachia kicheko.

Regina alimwangalia Regina kwa sekunde kadhaa na  kisha aliinua kibao chake juu.

“Nitaununua kwa milioni mia moja”

“Haaa!!”

Wimbi kubwa la mmako lilisambaa  karibia ukumbi mzima , mara baada ya kusikia kauli ya Regina . Hata mwendesha mnada mwenyewe alijikuta akishangaaa  na kudhania , labda amesikia vibaya.

“Samahani! Mkurugenzi Regina , unamaanisha  milioni mia moja?”Aliuliza kupata uthibitisho.

“Ndio” Regina aliitikia.

Hamza aliishia kumwangalia mke wake na kujiambia huyu msichana  anaelewa kauli ya  mke anapaswa kumfuata mume. Kiasi hicho cha pesa kilikuwa kikubwa kulinganisha na milioni kumi aliotoa Katibu na kumkomesha kabisa.

Mwendesha mnada alijifikiria mwenyewe  na kujiambia kama mchoro huo unaweza kuuzwa kwa milioni mia moja , si jiwe la rangi tu kando ya barabara linaweza kugeuka  almasi na kuuzwa kwa bilioni?.

Waandishi wa habari waliokuwa ndani ya eneo hilo walimmulika Regina na picha  za kutosha  na hawakumjali tena Katibu  Gondwe. Kwenye vihwa vyao walikuwa wakijiambia , hio ni taarifa kubwa kesho kwenye vyombo vya habari.

Katibu Gondwe alikuwa na hasira kiasi kwamba uso wake  mweupe uligeuka kuwa mwekundu, ilikuwa ngumu kwake kutoa zaidi ya milioni mia kununua uchafu unaoitwa mchoro  kwa ajili ya kushindana na Regina.

“Milioni mia , kwa mara ya kwanza , milioni  mia kwa mara ya pili...”

Ile  watu walipodhani  , Regina anakwenda kuutwaa mchoro kwa  kiasi cha milioni mia moja , sauti nyingine kutoka nyuma ilisikika.

“Milioni mia mbili!”

Yulia  na sauti yake ya maringo aliongea . Hali ya msisimko   ilipaishwa zaidi na kauli ya Yulia Sio kwamba hakukuwa na matajiri  wakuweza kutoa kiasi hicho cha pesa ndani ya eneo hilo , kulikuwa na matajiri wakubwa tu kama  Tajiri Salim , Tajiri Bilali, Tajiri Rost na wengine. Licha ya kwamba wengi wao walikuwa wakitoa  misaada kwa  watu wenye uhitaji , lakini   ni wachache waliokuwa na moyo wa kutoa zaidi ya milioni mia mbili kwa pamoja.

Kingine hakuna ambae alikuwa tayari kushindana na mrembo  Regina ambae alikuwa ni  kama  malaika wa biashara ndani ya Tanzania? Waliona haina haja ya kushindana na mwanamke huyo.

Umati huo ulishindwa kujua nini kinaendelea , ukweli  ni kwamba Katibu  Gondwe  ambae  alipanga kuchukulia  mnada huo kama sehemu ya kujitangaza katika mbio zake za kuwania Ukurugenzi wa shirika la misaada dunani ukanda wa Afrika , hakujua  cha kuongea tena , kwani alifunikwa na akafunikwa tena.

Mwanzoni aliona ni sawa  kwa  mwanamke kauzu kama Regina kushindana nae maana alishazoea  kama mfanyabiashara , lakini  mpaka Yulia , Mwenyekiti  wa makampuni ya Prima

Wanyika. Nani wa kuthubutu kushindana nae , ilihali hata cheo chake kilitokana na koneksheni na familia hio .

Katibu huyo aliishia kutoa tabasamu la wasiwasi na kisha bila ya kupenda alijikalisha chini na kutulia. Ilionekana dhahiri hakutaka kuendelea kutaja bei.

Hamza upande wake alihisi kuna kitu hakipo sawa  na ilikuwa ni kweli , kwani mara baada ya kumwangalia  Regina , macho ya mwanamke huyo yalikuwa na hali ya ukauzu usiokuwa  wa kawaida.

Upande mwingine Yulia alikuwa akijisikia raha, alimwangalia Regina  na tabasamu la kejeli, lililojaa uchokozi.

“Milioni  mia tatu” Regina aliinua  kibao  kwa mara nyingine na kuongea.

Kwa mara nyingine  hadhira ilishikwa na mshituko. Mwendesha mnada kidogo tu azimie.

Katibu  Gondwe aliishia kutoa kitambaa tu na kujifuta jasho. Hakutaka kuongea neno na aliishia kujiuliza ni watu gani  hawa?.

Alikuwa akifikiria fikiria kutoa kiasi kikuibwa cha pesa , maana aliona kama angekosa mchoro huo , ingekuwa ngumu kwake kujitangaza na picha alizochukua.

“Milioni mia tatu kwa mara ya kwanza..”

Bila ya kusubiri mwendesha mnada kuongea kwa mara ya pili , Yulia  aliinua mkono wake tena.

“Bilioni moja”

Kwa namna ambavyo Yulia alitamka neno  , Bilioni moja ni kama alikuwa kwenye duka la mangi  na  ananunua  pakti ya sigara.

Matajiri wenye asili ya kihindi na kiarabu waliokuwa ndani ya eneo hilo , walijikuta pia wakishikwa na butwaa.

Bilioni moja. Kwao waliona ni kubwa sana na ingefanya  mambo mengi  ya kuendeleza biashara zao. Baadhi ya  wajasiriamali waliokuwa na mitaji chini ya bilioni moja sura ziliwashuka , ilikuwa hela nyingi sana.

“F*ck! Naota au , ni kweli Yulia  katangaza kutoa bilioni moja kwa ajili ya ule mchoro?”

“Kwenye  maisha yangu yote  ni bwana mdogo ndani ya suruali yangu anaeweza kutema bilioni moja pekee”

“Hahahah..”

Kundi hilo la watu waliishia kucheka na kushangaa. Lakini kwa wakati mmoja walimuone wivu  Wadeni  kwa kuwa na bahati namna hio kwenye usiku huo wa mnada.

Upande wa Madam Wadeni ,  alitaka kuzimia. Licha ya kwamba kituo chake  kishapokea msaada  mkubwa ,  lakini bilioni moja ilikuwa hela nyingi sana.

Hamza hakujali ni kiasi gani Yulia anatumia, jambo  kubwa hapo ni kwamba  Regina alikuwa akitaka kupasuka kwa  sababu ya  Yulia.

Regina aliishia kugeuza kichwa chake na kumangalia Yulia na kisha palepale alikunja ngumi na kuinua mkono wake juu.

“Bilioni kumi”

“Pwaah!”

Waliokuwa wakinywa vinywaji kidogo kidogo , walijikuta wakitema chini  kama vile vinywaji vimekuwa vichungu ghafla mara baada ya kusikia kauli ya Regina.

Eneo lote lilipatwa na hali ya ukimya ghafla , matajiri waliokuwa ndani ya eneo hilo , ghafla tu walijikuta   mikono yao  ikianza kuwatetemeka. Hawajawahi kuona  mnada kichaa wa namna hio ukitokea ndani ya  ardhi ya Tanzania.

Tena kwa  kununua mchoro ambao haukuwa na thamani yoyote , lakini ghafla tu unafikia  thamani ya bilioni kumi.

Yulia alijikuta akikunja sura , huku akimwangalia Regina na mshangao

“Bosi Regina  , usiwe na haraka , bilioni kumi ni hela nyingi sana..”

“Kweli kabisa , haina  haja ya kushindana na 

Yulia , utajiri wao ni wa kifamilia”

Baadhi ya  wajasiriamali waandamizi , waliokuwa na mahusiano mazuri na Regina walijaribu kumtuliza atengue kauli.

Previoua Next