Reader Settings

Bilioni  kumi waliona ni hela nyingi sana na , ni ngumu kwa Regina kuwa na  Cash ya kiasi chote hicho cha pesa , labda auze hisa za kampuni au kuuza vitu alivyokuwa akimiliki.

Kwa lugha nyepesi ni kwamba  kama Regina angetumia  bilioni kumi , maana yake  asingebakiwa na hela binafsi ,  zaidi ya hisa za kampuni  pekee ambazo ndio utajiri wake  hukadiriwa .

Ijapokuwa ni kiasi ambacho anaweza kupata ndani ya muda wa mwaka mmoja tu , lakini bado kilikuwa kiasi kikubwa cha pesa.

Hamza hata yeye aliona mwanamke huyo , alikuwa amekurupuka , ingawa alifurahi kuona  kituo kinakwenda kupata kiasi kikubwa cha pesa , ila hakutaka  mke wake kutumia  nusu ya  hela zake zote  kwasababu alikuwa na hasira  juu yake kwa kujihusisha na Yulia.

“Wife hakuna haja ya  kutoa kiasi chote hicho. Yulia anatumia hela za familia yake , ila wewe unatumia za kwako ulizopata kwa jasho”Aliongea Hamza.

Regina aliishia kumpotezea  Hamza na  alimwangalia  Yulia  akiwa kimya tu.

Vimulimuli vya kamera vilikuwa vikimmulika Regina mfulululizo. Muda huo hakuna aliethubutu kuondoa kamera katika  eneo  Regina alilokaa.

Mshereheshaji nae , hakuwa na haraka ya kutangaza , alivuta pumzi nyingi na kumsubiria  Yulia  kuongea.

Yulia aliishia kusinyaza macho yake kwa muda, na mara baada ya kufikiria kwa sekunde kadhaa aliishia kushusha kibao chake chini  huku akishusha pumzi.

Ingawa alikuwa na hela nyingi , lakini kama angetumia bilioni kumi , watu wa famili yake wasingekuwa na furaha nae. Hata kama ni  kifamilia , kiasi hicho cha pesa kilikuwa kikubwa mno.

Msherehesjaji mara baada ya kuona  hivyo , haraka sana alitangaza na kisha akagonga meza chini kuashiria mchoro umeuzwa.

Sauti nyingi za makofi zilisikika ukumbi mzima, licha baadhi ya watu kumuona Regina kama kichaa , lakini wengi walimpongeza kwa  ujasiri wake.

Watu wengi walitegemea  kwanzia kesho   na sherehe zote za christmass na mwaka mpya ,  tukio la Regina lingekuwa mada  ya moto itakayovuma.

Katibu  Gondwe aliishia kuufyata huku macho yakiwa yamtemtoka , licha ya  yeye pia kuwa mfanyabisahra , bilioni kumi ni  hela zake zote za uendesjaji katika biashara zake. Na ule mpango wa kutumia  picha  kujipa  promo ulifutika mara moja.

Baada ya  mchoro kununuliwa kwa bilioni kumi , mnada uliofuata ulipooza ghafla. Hata tukio la Harambee hela iliokusanywa haifukifia hata nusu ya kiasi ambacho Regina ametoa.

Mwisho wa Mnada na Harambee , mshereheshaji alikubali ombi la wengi na kumwalika Regina juu ya steji kwa ajili ya kutoa neno  ni kipi kimemsukuma mpaka kuamua kutoa kiasi chote hicho cha fedha?.

Hamza mwanzoni alijua mwanamke huyo asingekuwa tayari kupanda juu ya steji na kuongea , lakini ilikuwa nje ya matarajio yake  mara baada ya kumuona Regina akisimama na kuanza kuzipiga hatua kusogelea  steji.

Mwonekano wa Regina ulikuwa ni wa kikauzu na  wa utulivu wa hali ya juu  mara baada ya kupokea microphone.

“Najua...”Alianza, “Wengi wenu sasa hivi mnadhani labda nimekuwa kichaa  kwa kufanya kitu ambacho naweza kujutia”

Ukumbi wote ulikuwa kimya , huku wengi wakiongea chini , ilikuwa kweli , watu wengi walijua Regina anafanya kitu ambacho angejutia baada ya  kutoka hapo.

“Katibu Gondwe naomba nikuulize swali , ukiachana na  harakati zako za kisiasa, kama mfanyabiashara , umewezaje kupata hela zote ulizonazo?”

Watu wengi walishangaa , hawakutegemea Regina angemuuliza Katibu Gondwe swali lingine?.

Katibu Gondwe alikuwa kwenye mudi mbaya mno , kama sio Regina  yeye ndio angekuwa star wa usiku huo. Mara baada ya kusikia swali kutoka kwa adui   wa maendeleo yake aliishia kulazimisha tabasamu .

“Kama mjasirialmali nilijua ni nini wajibu wangu kwa jamii   na pili  uwezo ninao”

“Uongo!”

Regina alikataa waziwazi  jibu la Katibu  wa biashara na viwanda na kufanya  matajiri wengi waliokuwa ndani ya eneo hilo kumshangaa. Ni kama hawakutegemea kama Regina angekataa jibu waziwazi..

Katibu  Gondwe aliishia  kutoa tu mdomo , huku akiwa na hali ya  kukosa amani na kama mwanaume hakujua namna ya kurudisha  jibu.

Hamza aliishia kuangaza macho yake kulia na kushoto na alijikuta akishagaa mara baada ya kuona  uwezo wa mke wake kuongea mbele ya watu ulikuwa wa juu mno.  Aliona watu wengi walikuwa kimya wakitaka kusikia kile anachokwenda kuongea.

Mara baada ya  muda wa ukimya,kila mtu akiwa amemkazia macho  kwa umakini , Regina aliendelea ;

“Nimekataa jibu lake kwasababu sio yeye tu ambae anaweza kupata hela , kuna watu wengi hapa wanaweza kutengeneza pesa , ndio maana mpo wengi mliokaa hapa, kila utakae muuliza atakuwa na jibu hilo hilo , hakuna ambae atakataa, hana uwezo wa kutengerneza hela. Kuwa na uwezo wa kutengeneza hela , sio kwasababu  ya  uwajibikaji wenu kwa jamii , sababu ambayo inawafanya kuwa na uwezo wa kutengeneza kiasi kikubwa cha pesa ni kwasababu  mnajisikia  vizuri mkiwa na hela nyingi , hivyo mpo tayari kufanya chochote kuona mnahela nyingi, Kwenu hela ni kama madawa ya kulevya , hamna namna ya kujisikia vizuri  pasipo kuwa na hela za kutosha”

Watu wengi walimsikiliza kwa umakini , wengi walikubaliana nae na  wachache pia   ambao hawakukubaliana nae walikuwepo.

“Bosi Regina yupo sahihi , sio uwezo wetu unaotufanya  kuwa na pesa nyingi  pekee bali ni tamaa zetu ndio zinatusukuma   kutengeneza pesa nyingi , matajiri  wanapenda kuona akaunti za benki zikizidi kuongezeka  masifuri na  hakuna kiasi ambacho  wanaweza kusema hiki kinanitosha”Aliongea mmoja.

Aliamini matajiri kuwa na hela nyingi sio kwasababu ya uwezo  pekee  wa kuzitengeneza , bali  kutokana na hela kwao kuwa  sehemu ya furaha yao , wapo tayari kufanya lolote  hata kama  ni nje  ya uwezo wao kuona  wanaingiza hela.

Yanahitajika matamanio ya kuzipenda hela  sana ndio  kuweza kuzipata nyingi , kwani bila matamanio huwezi kwenda mbali kuzipata .

“Pengine wote  mnashangaa , kama nimeweza kutengeneza kiasi chote hiki cha pesa  kwa nguvu kubwa , kwanini  nitumie kiasi kikubwa mara moja kutoa msaada ? Sababu ni moja tu kwangu , hela kwasasa hazinifurahishi.

Watu wengi walikunja  sura , kama isingekuwa ni  Regina anaetamka maneno hayo , hakuna ambae angeendelea kusikiliza.

Nani asiefurahishwa na  hela? Hizo si kauli za masikini pekee ,kauli maarufu ya sizitaki mbichi hizi?.

“Ni wangapi kati yenu mnakumbuka mara yenu ya kwanza kuingiza kiasi kukubwa cha  fedha  ni hisia za aina gani mlizopata, ni furaha  gani  mliojisikia?”

Aliuliza Regina huku yeye mwenyewe akiwa amenyoosha mkono juu. Matajiri wengi waliokuwa ndani ya eneo hilo walinyoosha mikono yao juu , wakiwa na hali ya kumbukumbu za nyuma.

Kwao  kiasi kikubwa cha kwanza kutengeneza katika maisha yao ,  hisia waliozpata  ndio zilikuwa za aina yake.

“Mimi bado ni mchanga , lakini najua fika baada ya miongo kadhaa nitakuwa kama mabosi wengi mliopo hapa. Nitakuwa ni mwenye kukumbuka  siku nilioweza kuingiza kiasi kikubwa cha pesa  kwa mara ya kwanza. Hata hivyo je sasa hivi ni kama mwanzo , je mkiingiza kiasi kikubwa mnapatwa na hisia mlizopata wakati mkipata kiasi kikubwa cha pesa kwa mara ya kwanza? Jibu ni kwamba  hamuwezi. Sasa hivi  mnajua hata kama mpate hala nyingi hamuwezi kuwa na furaha wala kupata msisimko  mliokuwa nao  mlivyofanikiwa  kwa mara ya kwanza”

“Sisi  ni kama mashetani ambao  ili tuishi lazima tule hela bila kukoma , ndio maana kila kukicha tunawaza kukusanya  hela ambazo  tayari zishakosa thamani  kwetu. Na kadri tunavyokula hela ndio  njaa zinavozidi kutushika na kuona  labda  kiasi fulani kitanifanya kuwa na furaha , hivyo ngoja nijitahidi. Tunaishia kununua , Private jet , maboti ya kifahari , makasri   na  mengineyo  lakini licha ya hivyo  kila kitu  kinakuwa kawaida. Hatimae tunaanza kufa ganzi , tunapatwa na homa ya ajabu inayoitwa kutoridhika”

Matajiri wengi walikuwa na hali zisizoelezeka katika nyuso zao. Ilikuwa kweili , zamani kupata bilioni kuliwafanya kuwa na furaha , lakini  kipindi hicho kupata bilioni  haikuwafanya kuwa na furaha , walitaka   mabilioni  na hata wakipata hayo mabilioni wanajikuta hawaridhiki na watakaka zaidi na zaidi , mwisho wa siku sio  kutafuta hela tena bali ni  ugonjwa wa kutoridhika ndio unaowasumbua.

“Bosi Regina hizo ni athari za kuwa tajiri , kila jambo lina faida na hasara zake”Aliongea mmoja wa  wafanyabiashara.

“Kama unahisi hela ni ushetani , kwanini usitoe zote msaada kanisani au msikitini?” Aliuliza mwingine.

“Mnapaswa kuniuliza kwanini nimetoa bilioni kumi  kama msaada , jibu ni hili nasijisikia vizuri sana hapa. Kabla sijawaza kutoa  msaada wa bilioni kumi sikuwaza kabisa nitapata hisia kama ninazopitia sasa hivi , ni hisia zile zile nilizopata baada ya  kupata  kiasi kikubwa cha pesa kwa mara ya kwanza. Kutumia hela bila ya kufikiria  ni kiasi gani utapata , ni dawa  nzuri ya ugonjwa mliokuwa nao matajiri. Imenifanya sasa hivi nijue ni nini nakitaka  na sio pepo wa hela  anachokitaka kwangu. Kutoa ndio njia pekee ya kulimiliki pepo la njaa ya hela  na sio  pepo la  hela kukumiliki. Ninachokitaka mimi ni umiliki , sitaki hela nataka kuyamiliki  maisha yangu”

Regina mara baada ya kutamka kauli ya mwisho kwa nguvu , matajiri wengi walikumbwa na bumbuwazi. Wote walionekana kuathirika na maneno ya Regina kama vile alikuwa akiwahubiria.

“Vizuri! Umeongea vyema”

Haikujulikana ni nani alieongea wa kwanza , lakini ghafla tu watu waliunga mkono na makofi mengi yalisikika.

“Shenzi! Hata mimi pia ngoja nitoe kiasi  kikubwa cha pesa kujitia hasara ,   kufikiria tu kutoa  bilioni kadhaa nahisi mwili kunisisimka”Mmoja aliongea.

“Ndio kabisa , msisimko wake unaonekana kuwa  mzuri zaidi kuliko kununua boti ya kifahari” Matajiri wengi walionekana hisia zao kuamka , waliona   pengine wakitumia hela zao nyingi kutoa msaada wanaweza kuipata furaha ambao wameikosa kwa muda mrefu licha ya kununua vitu vingi vya kifahari.

Regina alishuka nje  ya steji ,   akipongezwa na makofi mengi sana mpaka alipoirudia siti yake.

“Wifey! Kwahio kumbe  uwezo wako wa kuongea  mbele ya watu ni mkubwa hivi.Nilijua huwezi kuongea  neno hata moja mbele ya kadamnasi ya watu”Aliongea Hamza.

“Kama sijui kuongea mbele ya watu , nawezaje kuwasiliana na wafanyakazi wangu. Usiniambie   kwenye vikao naenda tu kukaa kimya?”

Hamza  alikuwa akijua Regina alikuwa na  confidence ya kutosha kuongea mbele za watu , ni hivyo tu alikuwa akitafuta namna ya kumsifia.

“Lakini mke wangu , unapanga kweli kutumia bilioni  kumi kwa ajili ya kutoa msaada? Mbona ni kama hela nyingi sana , umemfanya hata Madam Wadeni kuchanganyikiwa”

Bila ya kusubiri Regina kujibu , Yulia alisogea.

Hamza alikuwa na wasiwasi ni  kauli gani mwanamke huyo anakwenda kuongea.

“Regina nimekubali kushindwa leo , hotuba yako iliokuwa ni yenye kugusa sana” “Asante”Alijiibu kavu.

Yulia  aliishia kumwangalia  Hamza na mwonekano wa  kichokozi.

“Kesho kutwa naelekea nyumbani kusherehekea  sikukuu ya Christmas na mwaka mpya.Unapaswa kutafuta muda wa kuonanakabla sijaondoka”Aliongea  

Hamza mara baada ya kusikia sentensi hio , miguu ilimlegea na alitamani kumpiga Yulia kibao cha makalioni. Kuongea hivyo  kama sio kumtafutia matatizo ni nini?.

Lakini Yulia alikuwa ashaondoka  baada ya kurusha bomu na kumuacha yeye na Regina pekee. Aliangaliwa na jicho sio la kawaida.

“Wife sio kama unavyodhania , ameongea vile kwa ajili ya kutaka tu kutugombanisha , usimsikilize kabisa”

“Unapaswa kumuwahi , amekuwambia anarudi nyumbani kwao?”Aliongea Regina  na kisha palepale alitembea kumsogelea Wadeni.

Madam Wadeni alikuwa bado katika hali ya kiwewe , Bilioni kumi  za haraka haraka   alijihisi ni kama  anaota hela zinamdondokea  kutoka juu angani.

“Mkurugenzi  Regina , nashindwa kujua ni kwa namna gani nikushukuru  kwa ukarimu wako. Natamani kupiga magoti na kushukuru  kwa niaba ya  watoto  na wafanyakazi wote wa kituo”

“Madam! Huna haja ya kuwa hivyo ,. Ni kama nilivyosema , nimetoa kiasi hiki  cha pesa kwa ajili yangu binafsi kujisikia furaha.Umefanya mambo mengi mzuri kulinganisha na mimi kwenye maisha yako”Aliongea Regina.

“Hili sio jambo dogo kabisa , ukweli nikwambie tu. Sijawahi kuwaza  tutakuja kupata kiasi kikubwa cha pesa namna hii kwa ajili ya kituo. Nashindwa hata kujua ni kwa namna gani tunakwenda kuzitumia. Isitoshe wewe na Hamza ni mume na mke naona ni kama  nachukua hela za familia”

“Madam kama unahisi kutuo hakihitaji  kiasi chote hicho cha pesa , zinaweza kugeuzwa za kitaasisi  ili kufikia watu wengi zaidi , nchi yetu  ina yatima kibao ambao wanahitaji misaada”

Madam   Wadeni mara baada ya kusikia kauli hio ya Regina , alijikuta akishangaa , kama vile alikuwa akifikiria  juu ya suala hilo.

“Madam hili ni wazo zuri kweli , unaweza kukaa chini na Mzee Hizza mkajadiliana. Kama kweli  mtaunda  Foundtadion, itawasaidia kuwekeza  hizi hela kibiashara na  kuziongeza zaidi na faida inayopatikana itaendelea kusaidia wenye mahitaji. Si ndio wife?”

Hamza  alitaka kumuunga mkoo Regina , ili kuwa na furaha , lakini ilikuwa ni kwa bahati mbaya mwanamke huyo alikuwa amekasirishwa na Yulia, hivyo aliaga na kuondoka bila ya  kujibu.

“Madam sisi tunakuacha , usifikirie sana kuhusu  ukubwa wa kiasi cha  pesa , hela inatatua shida nyingi. Kama kituo mnaweza kukaa chini na kufikiria  namna ya kuzitumia mtakavyooona inafaa”Aliongea Hamza na kumfanya Madam kutabasamu.

“Namuona Regina anaonekana kuwa na hasira. Ingawa  sio sahihi kujua nini  sababu , lakini  nakushauri kwenda kumbembeleza. Wanawake hawawezi kustahimili kubembelezwa na wanaume wanaowapenda”

Hamza alitingisha kichwa na kisha kumfuata Regina  nje.

Ile Hamza anafika nje , wakati  Regina akiwa amefikia gari na yeye pia , Regina aligeuka na kumwangalia kwa mshangao.

“Unaenda wapi?”

“Wife si tunaenda  nyumbani?”

“Nenda kamtafute Yulia, kwanini unataka kwenda nyumbani na mimi ?”Aliongea Regina bila ya kuonyesha furaha.

“Wife  alichoongea Yulia ilikuwa makusudi ya kukufanya uwe hivi ,  ukiendelea kuwa na hasira  utamfanya afurahi”

“Basi mpigie sasa hivi mbele yangu na umwambie huwezi kuonana nae tena  na akusahau”Aliongea Regina  akiwa na uso wa kikauzu.

Hamza mara baada ya kusikia kauli hio , mwili wake ulikakamaa  na kujiambia yote hayo yalikuwa makosa ya Yulia. Ukweli Regina hakuwa na haja ya kwenda mbali hivyo , lakini uchokozi wa Yulia wa siku hio , ulienda mbali sana. Lakini hata hivyo ingekuwa ngumu Hamza kusikiliza kauli ya Regina na kumpigia kweli  simu na kumwambia h awezi kuonana nae tena.

Muda huo huo Hamza akifikiria cha kuongea , simu yake ilianza kuita na haraka haraka aliitoa mfukoni na kuangalia nani anampigia  na  alikuta ni  Black Fog.

“Rhoda vipi! Kuna taitzo?”

“Bro Bazo  amezingirwa  na watu waliovalia Mask. Inaonekana kuna mtu amepanga kumteka Irene “Aliongea Black Fog.

Bazo ni moja ya maninja wa Baffodil ambao walipewa kazi ya kuml;inda  Irene kwa siri  na kwa umakini wa juu.

Kama lisingekuwa suala kubwa , Bazo asingechukua hatua ya kupiga simu na kuomba msaada. Hata pale  Irene alipopata  ajali, Bazo hakuchukua hatua kwasbabu halikuwa suala kubwa  sana. Labda tu Irene yupo katika hatari kubwa.

Nani anachokoza nyuki?

Previoua Next