Reader Settings

Msukule wa Utumwani.

Hamza mara baada ya kusikia taarifa hio, mapigo ya moyo yalienda kasi mno kwa kuhisi  tatizo ni kubwa.

“What position!”Hamza aliuliza haraka haraka  na Black Fog alitoa majibu ya  uelekeo na Hamza alikata simu palepale  na haraka sana alifungua mlango wa gari na kuingia ndani.

“Hey! Nini kinaendelea?”Aliuliza Regina mara baada  ya kuona sura ya Hamza ilivyokuwa siriasi ghafla tu baada ya kupokea simu.

“Kuna mtu anajaribu kumteka Irene , napaswa kuwahi kutoa msaada , Wife wewe  ita  usafiri wa Uber  kukupeleka nyumbani”Aliongea Hamza.

Regina mara baada ya kusikia kauli hio , palepale aliingia ndani ya gari   na kufunga mkanda.

“Wife , unafanya nini , naenda kumuokoa mtu!” Hamza alionekana kushangaa.

“Hata mimi pia nataka kwenda , haijalisihi ni hatari gani unaenda kukutana nayo , haijalishi ni wapi unaenda , usifikirie kuniacha nyuma”Aliongea Regina  akiwa na macho yaliojaa usiriasi  na ishara ya wasiwasi na woga,.

Hamza moyo wake ulitingishika , alijua mwanamke huyo alikuwa akihofia suala lingine la uhai na kifo kutokea , hivyo hakutaka kumuacha akienda mwenyewe.

Ingawa Hamza aliona haina haja , lakini  kuokoa muda aliishia kutingisha kichwa  na kuliwasha gari.

Alikanyaga pedeli ya spidi na kuingiza gari  ndani ya barabara na kutoka ndugki kama chui  alieachiwa kutoka katika kibanda chake na kufanya watu kushangaa na kuona labda Regina alikuwa akijutia kutoa hela nyingi na sasa ukichaa umemshika.

Tukio lilitokea  eneo la Mikocheni  kwa Warioba  kwenye barabara kuu  katikati kidogo ya bustani ya  kuuzia miti na maua nje kidogo ya Kawe , ni eneo ambalo lilikuwa na  miti mingi na hifadhi ya viwanja vya manispaa ya maendeleo ya jiji.

Mara nyingi eneo hilo lilikuwa halikosi watu ambao walikuwa wakielekea  na kutoka Mwenge , lakini kutokana na muda  pamoja na  watu kujiandaa na sikukuu eneo hilo halikuwa na watu wengi.

Muda huo ndani ya eneo hilo  kulikuwa na mapigano makali yaliokuwa yakiendelea, kulikuwa na watu kadhaa waliokuwa wakisogea kwenda mbele na kurudi nyuma kwa spidi kubwa  , huku sauti za vishjindo na milio ya visu ikisikika.

“Clang , clang!!”

Visu viwili vilionekana kuzuia  mashambulizi ya  upanga mrefu. Mwanaume aliekinga shambulizi lile alijikuta akirudi nyuma na kukwepa shambulizi lingine kutoka kwa mtu mwingine.

Mwanaume wa umri wa makamo alionekana yeye peke yake akipambana na watu wanne waliovalia Mask nyeusi na mavazi ya rangi ya  kijivu. Kwa kuangalia tu  nguvu zao zilikuwa ndogo  mmoja mmoja kulinganisha na  mtu waliekuwa wakimshambulia , lakini kwasababu walikuwa wakishambulia kwa pamoja, walionekana  kufanya  bwana yule kupata wakati mgumu.

Na kilichomuongezea ugumu zaidi ni kwamba alipaswa pia kumlinda msichana mdogo ambae  alikuwa akitetemeka pembeni yake kando ya mtaro.

Irene alikuwa katika hali ya woga kiasi kwamba  mpaka machozi yalikuywa yakimtoka , huku mikono yake akiwa amekumbatia begi  la madaftari  akiwa anatoka kujisomea.

Katika maisha yake hakuwahi kutarajia ghafla tu   akiwa katikati ya barabara atasogelewa na watu waliovalia kininja na kutaka kumteka, ilikuwa ni kama anaangalia filamu .

Ni kwa bahati nzuri tu mwanaume alievalia  mavazi meusi alijitokeza  na kumkinga kwa mbele na kumwambia asikimbie , kwani kuna uwezekano wa wengine mbele.

Muda ule  Irene akiwa hajui chakufanya   kwa kutokujua aendelee kumwamini   mtu aliemwambia  asikimbie , ghafla tu alihisi  mkono ukilishika bega lake kwa nyuma.

“Ahh!!”

Alijikuta akishituka kwa nguvu  huku akigeuka nyuma  mara mmoja.

Nyuna yake alionekana  mwanaume asiemjua , mwanaume huyo sura yake ilikuwa  imepauka sana , huku macho yake yakiwa yamesinyaa kwenda ndani. Alikuwa ni mweusi lakini mwenye nywele ndefu mno  kama za kizungu zilizofungwa  kwenda nyuma , akiwa katika mavazi ya  joho.

“Miss Irene  nifuate”Aliongea yule mwanaume kwa lugha ya kingereza, lakini sauti yake ilikuwa kali kuashiria ilikuwa kama ya mwanamke na sio ya mwanaume .

Irene alizidi kutetemeka mara baada ya kuona mtu huyo mwenye muonekano usio wa kawaida , pamoja na sauti yake isioendana na mwonekano.

“Wewe.. Wewe ni nani?”Aliuliza  

“Mimi ni Msukule wa Utumwa , sina thamani ya kujulikana kwako”Aliongea.

“Msukule wa Utumwa! Irene alijikuta  mwili ukishikwa na  baridi mara baada ya kusikia  jina  hilo.

“Msukule wa Utumwa , maana yake nini?”

“Msukule wa Utumwa ni msukule wa utumwa , hakuona maelezo mengi”Aliongea  kwa sauti ya kunong’oneza.

Irene alijikuta akichanganyikiwa zaidi na maneno yake.

“Kwanini mnataka kunikamata?”Aliuliza Irene kwa hofu.

“Msukule wa utumwa kazi yake ni kufuata maagizo ya  mtumishi wake , hatuulizi sababu”

Bazo ambae alikuwa amezingirwa na wanaume wanne wakimshambulia , mara baada ya kugeuka aliweza kumuona Msukule wa utumwa   na macho yake yalimtoka kwa  mshituko.

Palepale alijikuta akipiga sarakasi mbili matatata sana huku siraha zikipita katika uso wake na  ile anatua chini alikuwa  amepunguza ukaribu wake na Irene.

“Ms Irene sogea karibu yangu”

Irene palepale alitaka kukimbia kumsogelea 

Bazo , lakini ila anataka kufanya  hivyo yule Msukule wa utumwa , alikuwa ameshajitokeza mbele yake na kumzibia njia.

Ilikuwa ni kwa spidi sana , kiasi kwamba hata Irene mwenyewe hakujua  ni kwa namna gani  mtu huyo aliweza ghafla tu kuwa mbele yake.

Yule Msukule wa utumwa hakujali mshangao wa  Irene na  aliishia kumwangalia  Bazo kwa macho makali  yenye chuki.

Bazo palepale alikumbwa na mlipuko wa nishati za mbingu na ardhi na  kwa spidi ya hali ya juu aliruka sarakasi  , akiwa ametanguliza  kisu mbele na  kumsogelea Msukule Wa Utumwa .

Msukule  wa utumwa alisogea kama kivuli na kukwepa shambulizi la Bazo.

Lakini ni kama  Bazo alishategemea shambulizi lake  atalikwepa , vinginevyo asingeweza kujitokeza katika eneo hilo bila ya yeye kumuona. Hivyo lengo lake  ni kumfikia  Irene  na kumpatia ulinzi.

Ilionekana kundi hilo la watu , walichotaka pekee ni kumteka Irene  na sio kumuua. Hivyo  kidogo hakuwa na wasiwasi sana kuhusu usalama wake.

“Ms Irene kimbia upande  wa kushoto kwako , endelea kukimbia na usisimame”Aliongea  Bazo kwa nguvu.

Irene  haraka sana alianza kukimbia kuelekea  uelekeo alioelekezewa. Ingawa spidi yake ilikuwa ndogo sana , lakini alijitahidi kutumia  nguvu zake zote kukimbia.

Yule Mtumwa mara baada ya kuona vile , alionekana kutokuwa na  haraka na alimwangalia  Bazo kwa sura ya kikauzu.

“Unaonekana hujui  kikufaacho, nilitaka kufuata maagizo ya master na  kutokuua , lakini  ukithubutu  kuzuia  alichotaka Master . Usije kunilaumu mimi Msukule wa Utumwa kuwa mkatili”

Mara baada ya kumaliza kuongea , aliinua mkono wake juu  kwa  ishara na wale   maninja wengine wanne walimuacha  Bazo na kwenda kumzingira Irene.

Palepale yule  bwana Mtumwa  alimsogelea Bazo akiwa katika umbo  kama la nyoka. Bazo  alitaka kwenda kumsaidia Irene , lakini  kwa  uwezo alioona kutoka kwa  Mtumwa pamoja na kuzidiwa nguvu alijikuta hana jinsi.

Alijiambia mpango ni kummaliza kwanza huyo 

Msukule wa Utumwa na kisha  kwenda

kumsaidia Irene. Hivyo  aliongeza uwezo wake katika kiwango  cha juu  sana  katika kushambuliana na Msukule  wa utumwa .

Wakati kila mmoja akimsogelea mwenzake , umbo la Msukule wa utumwa lilikuwa la ajabu mno kiasi kwamba lilitengeneza hali ya kumchanganya  Bazo.

Bazo upande wake hakutaka kuingia katika mtefo wa mbinu hio na kwa kutumia kisu chake alisogea na kumltenga  Msukule  katika eneo alihisi ni shingo .Lakini katika hali ya kutotarajia , Msukule ule wa utumwa  haujukwepa kabisa shambulizi lile na badala yake  alidaka kisu kile na kilichosikiika ni sauti ya mvunujiko ilioambatana na  cheche.

Bazo mara baada ya kuangalai kwa umakini , alijikuta akiwa katika mshangao , aligundua  mkono wa Msukule wa Utumwa  ulikuwa umetengenezwa na  chuma. Mikono yake ilikuwa  ni kama  ya roboti , lakini umbo lake lilikuwa likitisha mno,  ni kama vile ni kucha za Zimwi.

Alijikuta akijiuliza huyu ni  binadamu au ni jini? Bazo  alijawa na hofu  lakini hakuacha kuendelea kushambulia. Alitumia mguu wake mmoja kurusha teke na kumlenga Msukule wa utumwa katika tumbo lake.

Msukule ule wala haukukwepa , na  teke  lile lilimpata kisawa sawa katika kiuno chake. Alionekana kupata maumivu kiasi cha  kutoa mguno  lakini haraka sana  alitumia mkono wake wa kushoto na kushika paja la Bazo.

“Siiiii!!’

Surulali yake ilichanwa na zile kucha za chuma zilitoboa ngozi yake  na kumpelekea maumivu makali.

Bazo alikuwa katika maumivu , alikuwa na bahati tu  baada ya kuona kucha zile hazikuwa na sumu, vinginevyo angeweza kufa mara moja.

Lakini mara baada ya  muda wa kupambana na huyo Msukule, Bazo aligundua , ijapokuwa  alikuwa na kasi katika kushambulia , lakini uwezo wake haukuwa mbali sana na wake , ni kama walikuwa wakilingana  ki uwezo, hivyo ingechukua muda mrefu sana mpaka mshindi kupatikana.

Ijapokuwa Bazo alitakiwa kumsaidia Irene kutoka kwa  wale  maninja wengine wanne , lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kumshinda kwanza Mskule wa utumwa.

Upande mwingine , Irene hakwenda mbali sana alikuwa ameshafikiwa na  wale  maninja wanne na kumzingira  pande zote.

Msichana huyo alijua amekwisha  kamatwa  na watu hao na hana lingine la kufanya kujisaidia, lakini ile watu wale wanataka kumkamata, ghafla tu   vivuli vya watu sita vilijitokeza kutoka pande zote  za barabara.

Watu hao sita wenyewe walikuwa na mask za vilemba usoni , walionekana  kama vile walikuwa maninja kwenye filamu  za kihistoria za kituruki.

Irene alijikuta akipiga makelele , ila wale  maninja wanne waliokuwa wakimfukuzia walishituka haraka na kuanza kushambuliana na wale watu sita  wa  mask  nyeusi za vilemba, mara baada ya kuhisi  nia yao mi kutaka kumuua Irene.

Ghafla tu pambano lilichukua sura mpya , huku  Irene akishikwa na wale  watekaji na kutupiwa pembeni  kwenye  majani kwanza kuruhusu pambano.

Bazo mara baada ya kusikia purukushani za mapigano  zikitokea upande aliokimbilia Irene, alijikuta akishikwa na hali ya kuchanganyikiwa  akijiuliza ni jambo gani lilikuwa likiendelea. Bila kujijua kitendo cha kushangaa alikuwa amempa  nafasi adui  na kumshambulia.

“Kufa!!”

Msukule wa utumwa mara baada ya kuona Bazo amefanya  kosa , palepale alichanua makucha yake ya chuma na kumlenga kifuani kama vile  ni kiumbe  cha  kishetani.

Bazo alijikuta akilaani ndani kwa ndani , lakini hata hivyo alikuwa  amechelewa sana kushitukia shambulizi  hilo, hivyo ikawa ngumu kwake kukwepa.

Ghafla  tu  kivuli cha mtu kilitokea katika maua na kumpiga kikumbo  Msukule.

Msukule  wa utumwa mara baada ya kugongwa na kitu kilichokuwa na spidi kali  mpaka kushindwa kushituka   alijikuta akifyatuliwa kama mpira   huku akitema damu nyingi.

Mara baada ya kuona  mwanaume akiwa amesimama mbele  yake, Bazo alijikuta jasho la ubaridi likimvaa  huku  ishara ya tumaini ikimrudia.

“My – Prince!”

Mtu aliemsaidia  alikuwa ni Hamza . Hamza alikuwa akiendesha  na  mara baada ya kuona amekaribia , aliona  anapaswa kwanza kuona hali ilivyo kabla ya kusogeza gari karibu , hivyo alishuka na kumuacha Regina kuendelea kuendesha.

Ijapokuwa Hamza aliharakisha kuja mahali hapo ,  lakini hakufanikiwa kufika haraka , ilikuwa ni kwa bahati tu aliweza kufika   kwa wakati na kuyaokoa maisha ya Bazo.

Hamza hakujali  makelele ya  Bazo na haraka sana aligeuka na kuangalia upande wa kushoto  kwake , pambano kali lililokuwa likiendelea  na haraka sana alikimbia upande huo.

Hamza alisogea  kwa kasi , hakujali  kabisa kundi la   maninja hao waliokuwa katika levo  ya mzunguko kamili wa mafunzo ya nishati , kwake  aliwaona kama  vifaranga na  mbwa tu.

Mara baada ya kumpaisha mmoja na  ngumi m wawili wengine aliwapiga na mateke na  kufa hapo hapo.

Irene mara baada ya kumuona Hamza ghafla tu ametokea , alijikuta  akiacha kulia  na sura yake kupoa  na kujishika magoti kwa kuhema kwa tabu.

Ilimchukua Hamza dakika moja tu kudhibiti  karibia maninja wote , watatu wakiwa wamekufa na  wengine  kupoteza fahamu.

Hamza mara baada ya kumuona msichana huyo akiwa katika hali ya woga kiasi cha kutia huruma aliishia kumshika mkono  kwa namna ya kumpoza.

“Okey! Upo salama sasa”

Irene hatimae alirudi   katika akili yake  na kujikuta akimkumbatia Hamza kwa nguvu huku akilia.

“Hamza kwanini umechelewa. Naogopa sana...” Upande wa Hamza ukweli ni kwamba hata yeye alikuwa katika hali ya kuchanganyikiwa , muda mfupi mara baada ya kuona hao  maninja waliovalia mask wakipigana  aliweza kugundua walikuwa na mafunzo yanayofanan, kama vile wametoka kambi moja.

“Hamza , hawa watu ni wakina nani , kwanini wanataka kuniteka? Kuna mtu nimemkosea au kuna mtu anataka  kunichukua  kwa nguvu kimapenzi kwasababu ya uzuri wangu?”

Hamza alishindwa kujizuia na kutabasamu , huku akjiambia kuna haja gani ya kujifikiria mzuri katika  wakati kama huu.

“Unafikiria sana , wewe sio mzuri peke yako mchi hii, mpaka  watu waagizwe kuja kukukamata”

“Oh...” Irene alijikuta akianza kufikiria kwanini  jambo hilo limemtokea  na mara  baada ya kuwaza  mtu aliemkosea jina moja tu ndio lilijitokeza kichwani mwake.

“Au ni Sister Regina amegundua  kinachoendelea kati yetu ndio maana ametuma watu kunikamata..”

“Wewe hebu acha kufikiria ujinga, najua  hawa watu wanatokea wapi , lakini sijui kwannini walitaka kukuteka na wengine walionekana kutaka kukuua”Aliongea Hamza.

Wakati Hamza akiongea aliweza kuona kulikuwa na baadhi ya  maninja waliokuwa wakijivuta vuta  kwa maumivu wakipanga kurotoka.

“Bazo!”

Aliita  Hamza na palepale  Bazo alisogea  na kuwazimisha  maninja hao   kwa mara nyingine.

“Atakaejaribu kusogea  tu , anakufa”Aliongea  Bazo  kwa tahadhari huku akichezesha kisu chake mikononi.

Hamza mara baada ya kumtuliza Irene , alimwambia akae pembeni na kisha alisogelea  wale watu  na kuwaangalia kwa namna ya kuwachunguza.

“Mmetumwa na Mathias Huge si ndio”Aliuliza  Hamza.

Swali la Hamza lilimfanya  Bazo kushangaa.

Hakutarajia maninja hao walikuwa watu kutoka Binamu na staili zao za mapigano  kuwa za watu wa Bondeni.

Maninja kadhaa ambao walikuwa na  fahamu waliishia kuziba midomo yao wakionyesha hawakuwa kabisa na  mpango wa kuongea.

“Hata kama msitake kuongea , najua mnapotokea kutokana na mbinu zenu za mapigano na nembo za mavazi yenu. Msipo nijibu moja kwa moja nitaamini mnatokea  kisiwa cha Binamu, hivyo nitamuuliza Mathias mwenyewe   anipe maelezo”Aliongea Hamza.

Muda huo , Msukule wa utumwa ambae alijeruhiwa na Hamza , alionekana kurejewa na nguvu na kusimama kusogea karibu.

“Mr Hamza , Master wangu  hakuwa na nia  ya kumdhuru  kabisa Irene . Tulitumwa hapa  kwa ajili ya kumlinda pekee  na pia kumpeleka kisiwani kama mgeni”aliongea  Msukule Mtumwa kwa sauti ya shida.

“Wewe ni towashi!?” Aliuliza Hamza akiwa amekunja sura.

Hamza alikuwa na uwezo wa  kumjua  bwana huyo  kuna kitu hakipo sawa kupitia sauti yake  na pia  msisimko wa nishati yake ya mbingu na ardhi ilikuwa sio ya binadamu wa kawaida.

“Msukule wa Utumwa  ni vijakazi  wa familia ya Master Mathias Huge , Mtumwa ni mtumwa yaani msukule”Aliongea na Hamza  macho yake yalionekana kuelewa kitu.

“Nishawahi kusikia  watu wa Binamu  wamekuwa na utaratibu wa  kuasili  wavulana Yatima kwa kuwakusanya  duniani kote  na kisha kuwakata sehemu zao za siri na ulimi , ili kuwawezesha kuvuna nishati  za mbingu na ardhi  kwa wepesi bila kuchanganywa. Sijawahi kuamini kama ni jambo la kweli, kumbe ndio nyie mnaofahamika kama Misukule ya utumwani”Aliongea Hamza.  

“Kwasababu  umesema  wewe ni kijakazi wa familia ya Huge , kwanini amekuja kunichokoza , ilihali  tayari ana madaraka yote  ndani ya  watu wa Bondeni na Binamu. Au amechaganyikiwa?” Aliongea Hamza

Msukule wa utumwa  alijua hakuwa na uwezo wa kupambana na Hamza , hivyo  aliishia kuvumilia Master wake akisimangwa.

“Mr Hamza , unapaswa kujiuliza kwanini  hao wenye Mask za vilemba ,  walikuwa wakitaka kumuua  Irene?”

Hamza mara baada ya kusikia kauli hio  alisinyaza macho na kisha aliwageukia wale maninja.

“Hata mimi nilikuwa nikijiuliza , nyie si  wote mnatokea sehemu moja, Kwanini wengine mpo hapa kwa ajili ya  kuteka na wengine mpo kwa ajili ya kuua?”

“Mr Hamza , hao unaowaona wametokea familia ya Dosala”Aliongea  Msukule wa utumwa  kwa kumaanisha.

“”Watu wa familia ya Dosala! Unamaanisha wametumwa na Mzee Dosala  na mwanae?” “Ndio , upo sahihi kabisa”Alijibu.

Hali ya wasiwasi , ilionekana katika macho ya Hamza.

Mzee Dosal aliemtaja alikuwa  ni  moja ya  familia huko bondeni ya ukoo wa Dosa.  

Dosa ni jina la ukoo  na herufi mbili za mbele zilikuwa ni uwakilishi wa mzaliwa ,Kama ilivyo kwa babu yake Regina aliefahamika kwa  jina la Dosam , sasa alikuwa na kaka yake  wa damu aliefahamika  kwa jina la Dosal licha ya mama kuwa tofauti.

Sasa ni sawa na kusema Dosal ni babu yake Regina  na inasemekana  hakuwa na uwezo wowote wa nishati za mbingu na ardhi na alitegemea nguvu ya nje , yaani konekshni  kutoka mataifa yenye nguvu kwa ajili ya kuwa na nguvu ndani ya  kitengo cha Binamu na Bondeni.

Mtoto wake Dosal , alikuwa ndio yule Mzee Suwi aliejaribu kumpokonya Regina pete , wakati wa msiba wa bibi yake, lakini Suwi yeye  alikuwa ni mtoto wa kuasiliwa , hivyo hakuwa na damu sawa na ya familia ya  Regina, hivyo ni sawa na ksuema kizazi kipya cha damu ya  Dosa kilichobakia alikuwa ni Regina peke yake.

Hayo yote Hamza aliyafahamu na alijiuliza , kama ni hivyo kwanini  Mzee huyo kutuma watu kuja kumuua Irene , kuna  uhusiano gani ama siri gani ambayo imefanya maamuzi hayo yafanyike kwa maninja kutumwa kumuua Irene?.

Hamza muda ule alijikuta akishiindwa kujizuia na  kukumbuka chuki ambayo bibi yake  Irene alionyesha mara baada ya kuonekana na yeye. Alijiuliza au  chuki ile ilikuwa na uhusiano na  suala kama hilo?.

Hamza hakuwa na majibu ya kutosha na alijiona ajipe muda kujua sakata hilo kwa undani.

“Kwanini Mzee Dosal akatuma mtu kwa ajili ya kumuua  Irene?”Aliuliza Hamza.

Irene  aliekuwa akisikiliza , alijikuta akichanganyikiwa pia , licha ya kwamba hakuwa akielewa chochote  kinachoendelea , lakini alitaka kujua kwanini watu hao walitaka kumteka na wengine walitaka kumuua.

“Mimi ni Mskule  tu  maana yake sijui  kitu”aliongea.

“Hujui au hutaki kuongea?”Aliuliza Hamza.

“Sijui. Hata kama Mr Hamza umpige huyu Msulule wa Utumwa mpaka  kifo chake , hawezi kujua kitu”

Hamza hakuwa na nia nyingine tena , alimpa ishara  Bazo  na palepale  aligeuka na kumkumbatia  Irene kwa mbele na kufanya macho yake kuwa kifuani mwake, ili asione kinachoendelea .

Irene  hakujua kwanini mwanaume huyo ghafla tu alimkumbatia kwa mbele. Lakini ndani ya sekunde  aliweza kusikia  ukulele kutoka mbele yake.

Mara baada ya muda,  Hamza alimwachia Irene  na kuondoka eneo hilo akiwa amemshika mkono .

Irene alijikuta akishindwa kujizuia na kugeuza kichwa chake kuangalia kinachoendelea na alijikuta uso wake ukifubaa mara baada ya kumuona Bazo alikuwa amemuua yule Msukule wa utumwa na wale wengine ambao walikuwa hai na sasa alikuwa akiwaondoa barabarani na kuwatupia  kwenye kiwanja kilichozungushiwa ukuta.

“Usiwe muoga , kwasababu ushapitia hili kwa mara ya kwanza , basi ni hakika utapitia tena  hali kama hii baadae..”Aliongea Hamza wakati akimwangalia msichana huyo na tabasamu.

“Ila nitakulinda  bure kabisa  bila ya kunipa hela hata kidogo.”

Irene alijikuta ujasiri ukimvaa mara baada ya kusikia maneno ya Hamza  na hatimae kutulia.Alijikuta akijibana kwenye mwili wa Hamza kimahaba  na kumnong’oneza. “Hutaki nikulipe kwasababu unajua naweza kukulipa kwa  staili nyingine”

Hamza alihisi kitu laini  na cha kuchoma choma kikigusa mkono wake , na kujiambia huyu mtoto alikuwa amefanikiwa kuwa na mtaji  mkubwa kifuani kwake.

Ile Hamza anataka kuongea  neno , ghafla tu gari lilitokea  katika makutano ya barabara ya kuingia  Kawe  na Mikochen B na  kumulikwa na tochi.

Regina akiwa kwenye gari aliweza kumuona Hamza na Irene namna walivyokuwa wameshikana na kutembea , walionekana kuwa  wapenzi kabisa.

Previoua Next