Reader Settings

Regina aliekuwa na hali ya wasiwasi , dakika kadhaa zilizopita , aijikuta akikunja ngumi kwa hasira mara baada ya kuona jambo lile. Macho yake yalikuwa yamejaa ukauzu wakati akishuka kutoka kwenye gari.

Hamza alikubwa na hofu na haraka sana alitoa mkono wake kutoka kwa Irene  na kujiweka pembeni , huku akitoa tabasamu la wasiwasi.”

“Wife nadhani   haujafikiria vibaya..”Hamza aliongea kujitetea.

Irene kwa aibu alirudi nyuma ya Hamza  huku akimwangalia  Regina kwa hofu.

“Sister Reg..”

“Mimi sio dada yako” Regina alikaripia.

“Wife nipe nafasi nijielezee”

“Nina macho , sitaki maelezo yako. Yaani nimekuchukulia poa sana , imegeuka mwalimu na  mwanafunzi mmeamua kutegana kwa  michezo ya kuongopeana kutekwa. Eti Irene anataka kutekwa ,  kumbe  kuja mpaka huku navuruga mipango yenu ya kimapenzi”

Hamza alijikuta akikosa neno , mara baada ya kuona Regina  kuelewa vibaya   na kutoona kweli kulikuwa na  shida. Ila kwa mtu yoyote angefikiria hivyo , maana hakukuwa na ishara yoyote ya watekaji ndani ya eneo hilo na  kubwa zaiudi ni kama magari yalikuwa yamezuiliwa kwa muda na sasa yalikuwa yakipita kwenye barabara hio na kufanya kila kitu kuonekana kawaida.

“Wife , sio kama unavyofikiria , ni kweli hali ilikuwa ya hatari sasa hivi . Nisikilize taratibu ni suala pia linalohusiana na wewe” Hamza aliona  anapaswa angalau kumwelezea Regina juu ya suala ambalo  Msukule wa utumwa aliongea.

Lakini Regina angewezaje kupata mudi ya kuendelea kumsikiliza.

“Hayo hayanihusu mimi , mnaweza kufanya mnavyotaka”

Mara baada ya kuongea hivyo , kwa hasira alirudi katika gari na kuligeuza na kuondoka.

Hamza aliishia tu kuganda katika eneo moja , huku akikuna kichwa chake  na kisha palepale alilazimisha tabasamu na kumwangalia Irene. “Nitakurudisha nyumbani kwanza”

“Nimemkasirisha Sister Regina sana eh ?”

“Ana hasira na mimi sio wewe , usifikirie sana”aliongea Hamza.

“Hamza , nakupenda  lakini sitaki kugombana na Da- Regina , nilidhania kwasababu una wanawake wengine hatojali ukiwa na mimi pia”Aliongea Irene.

Hamza alijua alichoongea Irene ni kweli , lakini  kuhusu Regina  hali ilikuwam imebadilika sana  tokea wafahamiane. Safari ile ya kwenda Ulaya ilikuwa  imebadilisha  sehemu kubwa ya mahusiano yao  na kuingia katika ubora mwingine kabisa.  

Zamani Regina asingejali sana kwasababu ya aina ya kukutana kwao , lakini  kipindi hicho moyo wa Regina ulikuwa umekomaa sana  kimapenzi. Lakini pia ilikuwa ngumu kwa Hamza kusema Regina hakuwa na furaha kwasababu ya wivu ,  ilikuwa ni  kuonyesha alikuwa akijali.

Lakini hata hivyo Hamza ilikuwa ngumu kwake kukata  mawasililiano mara moja na kila mwanamke , hivyo alipanga taratibu kuwasiliana na Regina mpaka amuelewe .

Alijua mchakato huo ungekuwa na  changamoto nyingi  lakini Hamza aliamini kwa namna yoyote ataweza kufanikiwa.

“Irene , usiongee chochote tena , nitakupeleka kwanza nyumbani kwenu”Aliongea Hamza na palepale alitoa simu kuita taksi , lakini Irene alimzuia  na kisha akanyoosha mkono  nyuma  kumuashiria  Bazo aliekuwa akisogea taratibu taratibu kwa umbali.

“Yule mjomba wewe ndio uliemtuma kunilinda, si ndio? Ni bora yupo hapa. Wewe nenda kamtafute Sister Regina ana hasira na haitokuwa vizuri ukinipeleka nyumbani. Utamfanya awe na hasira zaidi”

“Si muda mchache  tu mpaka kufika kwenu? Sina haja ya kujali sana nitawahi tu kurudi”Aliongea Hamza.

“Muda mchache! Wanawake wanajali huo  muda mchache kuliko mwingi utakaompa. Wewe nenda , mimi niko sawa , maana watu wabaya wenyewe washakufa”

Hamza hakutaka kuendelea kumsikiliza Irene akimbembeleza  maana hata yeye alikuwa na wasiwasi na Regina , hivyo  hakuwa na jinsi  na kumpa taarifa Bazo kumsindikiza Irene mpaka nyumbani.

Hamza  aliishia kuvuta pumzi na kuzishusha , hakutegemea Irene angeweza kumfikiria  kuhusu  hali yake. Alijiambia  kadiri msichana huyu atakavyoendelea kuwa hivi ndio  namna  itakavyokuwa ngumu kwake kumpotezea.

Kwasababu  kulikuwa na giza Hamza hakuona haja ya kuchukua taksi maana ingemchukua muda mrefu  kuzunguka , hivyo  ghafla tu alipotea.

Irene mara baada ya kuona Hamza amepotea ghafla tu katika macho yake , alijikuta akipatwa na  mshangao, huku akipepesa kope zake mara nyingi .

“Uncle huyu Hamza ni nani , kwanini ana uwezo wa ajabu hivi?”Aliuliza na  kumfanya Bazo kufikiria  kidogo kabla ya kujibu.

“Ms Irene , jukumu langu pekee ni kukulinda” “Oh! Basi sawa , nilitamani kama ungeniambia kidogo kuhusu Hamza , ila haina shida  unaweza kunisindikiza turudi , Tunapanda wote kwenye   taksi?”Aliuliza Irene akiwa  tayari alisharequest  na gari ilikuwa ikisogea ueleko wake.

“Nitakulinda kwa siri”Aliongea  na kisha palepale alirukia upande mwingine wa  fensi na kupotea.

Irene macho yake yaliishia kuchanua, alijiambia licha ya kuona mambo mengi  katika mitandao   na kucheza magemu  na kuangalia filamu , ila kuna mambo mengi ya kushangaza yaliopo katika uhalisia.

Ghafla tu  ile hofu ya kutekwa ilipotea yote na alijihisi ni kama  mwigizaji.

Wakati  Irene akipata Taksi kurudi nyumbani , upande wa Hamza alikuwa  akikata kona mitaa  kuwahi kurudi nyumbani.

Ile anafika  tu  ndio na Regina  pia alikuwa akiingiza gari  gereji  na kutoka  kuingia ndani.

Regina mara baada ya kurudi tu nyumbani alitupa mkoba wake  na  kwenda moja kwa moja mpaka chumba cha kujisomea na kujifungia.

Hamza ni kama alivyotegemea na  alipitia dirishani kwake na kurukia kwenye  balkoni ya dirisha la chumba alichokuwepo  Regina  na kusimama nje ya kioo kilichokuwa kikimuonyesha kwa ndani.

Kama kawaida aliweka muonekano wa kujitilisha huruma  huku akimwangalia Regina aliekuwa ndani  kwa hisia nyingi.

Mwanzoni Regina hakumuona Hamza , lakini mara baada ya kuvimba akiwa amekaa  kwenye  kiti , hatimae aliweza kuona kivuli cha mtu  na aligeuka ndio alipoweza kumuona Hamza alikuwa amesimama kwenye balkoni.

Hamza hakuongea chochote wala hakujitingisha , alikuwa akivuita subira Regina kumuona .

Macho yao yalikutana , Hamza alitoa tabasamu  lakini hakuongea chochote na kuishia tu kumwangalia.

Upepo wa baharini ulikuwa mwingi nje, jiapokuwa ilikuwa  ngumu kumwathiri Hamza , lakini  kwa Regina  alifikiria  ulikuwa ukimwathiri .maana katika jicho la mapenzi hakumchukulia Hamza kama sio wa kawaida.

Lakini hata hivyo Regina alikuwa amechukia  na alijifanyisha kutokujali  na alijimiminia maji kwenye glasi  na kisha alirudi kwenye kiti chake na kuendelea  kujiweka bize na kazi .

Hamza hakuongea chochote , wala hakusogea , aliishia tu kusubiri  na mwonekano wake wa ukimya.

Mara baada ya nusu saa kupita  Regina alijikuta akigeuka na kugundua Hamza bado alikuwa amesimama , ijapokuwa alikuwa amechukia lakini hakujisikia vizuri.

Alijikuta akisimama na kusogelea mlango  na kuufungua.

“Unafanya ninii  wewe? Unadhani ni sahihi kujitilisha huruma ?”

Hamza alijivunia na mbinu yake kwa kuamini Regina lazima angemwonea huruma , lakini licha ya hivyo aliendelea kuweka sura ya kizembe.

“Wife najua nimekukosea , lakini  nilijua usingeweza kunisikiliza , hivyo nikaona  nisubiri mpaka utakapo poa , kama unataka kunipiga nipo tayari , kama  unataka kunifokea nipo tayari. Siwezi kukukimbia hata siku moja”

“Hebu acha kujitilisha  huruma na nenda  kwenye chumba chako” Regina alishia kukunja ndita , mara baada ya kuona uvumilivu unamshinda , alijua kabisa  Hamza anacheza na akili yake lakini  moyo wake unajikuta tu kulainika.

“Siwezi kuondoka ,  mke wangu  kama usiponisamehe sitoondoka hapa”

“Basi endelea kusimama hapo milele na usiondoke , mimi naondoka”

Regina  mara baada ya kuongea aligeuka na kutoka nje ya chumba hicho na kushuka chini  sebuleni.

Hamza alijua  alishapewa nafasi , hivyo haraka sana aliingia ndani na kumfuata  moja kwa moja mpaka jikoni.

Muda huo Shangazi alikuwa amekwisha kulala muda mrefu tu.

Regina akiwa jikoni  alitoa baadhi ya vyakula kwenye friji , alionekana alipanga kula chakula cha usiku usiku , maana  hakuwa amekula sana wakati akiwa  kwenye mnada .

“Wife  unapaswa kunywa  na juisi , ngoja nikumiminie”aliongea Hamza akikimbilia  freezer.

“Hapana,  na  usiku wote huu unataka kunilisha vitu vya barafu. Unataka kuniona nikiganda?”

Hamza aliona alikuwa sahihi na  alihamia kwenye maji yasiokuwa na baridi sana na kutaka kumiminia lakini Regina alimzuia.

“Sitaki kunywa maji wala nini , hivyo hebu acha kuhangaika mbele yangu, nijibu swali moja tu , ni kwa umbali gani umefikia na Irene?”

Regina aliuliza huku akimwangalia  Hamza na macho kama vile anatafuta uongo  kutoka kwake.

Hamza aliishia kumeza mate  mengi  na kisha aliongea ukweli.

“Hatujafikia  ile hatua”Aliongea.

Hamza kuongea hivyo alijikuta akijisifia kwa uwezo wake wa kujizuia katika  matukio yote ambayo alikuwa amekwepa. Kwanzia kipindi ambacho hakuwa amefahamiana na Regina alisharuka zaidi ya  mitego mitatu ya Irene , baada ya kufahamiana na Regina alisharuka mitego  miwili. Kama asingekuwa  mvumilivu , ingekuwa ngumu kuongea muda huo.

“Mzee Wake anajua kuhusu kinachoendelea kati yenu?”Regina aliuliza  tena.

“Sidhani , vinginevyo  angeshaniletea matatizo muda mrefu tu”Aliongea Hamza na tabasamu la wasiwasi.

“Unajua kabisa  atakuja kukutafutia matatizo  halafu unaendelea , wewe hujui Irene ndio kwanza anapaswa kuingia chuo?”

Hamza aliishia tu kutojibu chochote , ijapokuwa aliona sio suala kubwa sana kwa  mtoto  wa umri wa  Irene kuwa na mahusiano , lakini alikuwa ni yeye  mwenye mahusiano nae na kama  Baba yake Irene akifahamu hilo  na matarajio aliokuwa nayo kwa binti yake  lazima ingekuwa habari nyingine.

“Unadhani   yule mzee na jinsi alivyoweka  nguvu zake  zote katika kumlea Irene atakubali  Au kwasababu ya cheo chako cha ufalme wa kuzimu unapanga kumlazimisha?”

“Mke wangu unafikiria mbali sana , kwanini  nifanye yote hayo ya kutaka kumlazimisha. Si itakuwa na sawa na haramia anaeteka mwanamke  kwa ajili ya kuwa  mke wake baharini. Isitoshe kwanini nifanye hayo yote wakati nina mke mzuri hivi.. hehehe”

“Hebu acha kucheka hivyo, ki ufupi., ngoja nikwambie  tu ,  bado  sijafikiria namna ya kudili  na  Eliza  na Dina lakini   ushamwingiza Irene katika orodha , mtoto ambae hata chuo hajaanza? Ni msichana ambae bado ni mjinga wa vitu vingi,    kwanini unashindwa kumzuia huyo bwana mdogo wako kisa tu anaonekana kuwa mzuri?”

Hamza alijikuta  akijiangalia hapo chini yeye mwenyewe  na kujiambia kama kweli siwezi kumzuia huyu bwana mdogo kwanini bado wewe ni bikra?.

“Wife naomba utulie , naelewa  unachomaanisha “aliongea Hamza   akiwa na tabasamu  akipanga  kwanza kutoka katika  hio dhoruba kwanza.

Muda huo huo simu ya  Hamza ilianza kuita  na mara baada ya kutoa  aliona ni Black Fog aliekuwa akipiga na alipokea haraka.

“Rhoda  vipi hali?”

“Bro! I am sorry ..”

Hamza mara baada ya kusikia sauti ya  Rhoda iliokuwa katika hali ya kitetemeshi moyo wake ulipiga kwa nguvu.

“Kuna kilichotokea tena?”

“Bazo alimsindikiza  Irene mpaka nyumbani salama lakini mara baada ya  kufika ... Bazo amefanikiwa kumuua  adui lakini kuhusu Irene

...”

“Nini kimemtokea huyo msichana?”Aliuliza Hamza  kwa sauti ya juu , macho yake  tayari yalikuwa yakitema cheche.

Hali ilimuogopesha hata Regina  na kumfanya akakamae huku akimwangalia Hamza.

Unadhani Hamza ndugu zake ni nani?,Nini kimempata Irene?

Previoua Next