Reader Settings

Worldless Book

“Nini kilichompata huyo msichana?”Lilikuwa swali la Hamza kwenda kwa Rhoda.

Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda spidi mno kwa kuhisi jambo kubwa limempata Irene.

“Amechomwa mwilini na tawi la mti. Sasa hivi Bazo amemchukua kumuwahisha  Muhasi , hospitali ya taifa”Aliongea Rhoda.

“Tawi la mti kwenye mwili wake!?” Hamza aliongea huku akihisi utosi   wa kichwa chake ukianza kumuwasha.

“Ndio , kulikuwa na  mtu aliekuwa amejificha  kwenye bustani ya nyumbani kwao , wakati anataka kuingia ndani ya geti  alimshambulia Irene kabla Bazo hajashituka”Aliongea Rhoda huku akionekana ni kama anataka kulia.

“Samahani sana Bro ..nimeshindwa kutimiza wajibu wangu”Aliongea.

“Haina haja ya kujilaumu , kama ni  mtu mwenye uwezo ambae  Bazo ameshindwa  kumtambua , basi  hakuna kitu ambacho angeweza kufanya. Naelekea huko  hospitalini sasa hivi”

Hamza hakuongea neno lingine  zaidi na palepale alikata simu  na haraka sana alikimbilia nje.

Regina pia aliweza kusikia mazunguzo ya kwenye simu na  alisita kidogo na kisha aliweka vitu alivyokuwa ameshikilia mkiononi na kumkimbilia Hamza nje.

Hamza alikuwa ndio anajiandaa kuendesha na ile anamuona Regina akiingia pia  alijikuta akimwangalia.

“Na wewe unaenda?”

“Kama isingekuwa sababu yangu ungemsindikiza Irene kwenda nyumbani  na asingepatwa na tatizo. Siwezi kukaa  na kusubiri taarifa nyumbani kwa amani”Aliongea Regina wakati akifunga mkanda.

Muda huo akili ya Hamza ilikuwa katika hali ya kuchanganyikiwa na  hakuwa na muda wa kujali ni  kipi mwanamke huyo anafikiria. Hivyo aliwasha gari na kulitoa  kwa haraka nje  ya geti.

Muhasi  ni moja ya hospitali kubwa  ya taifa ndani ya jiji la Dar es salaam. Ingawa ilikuwa  ni usiku lakini kulikuwa na madaktari bingwa wabobezi waliokuwa zamu.

Lakini hata kwa wale madaktari waliokuwa na uzoefu , walijikuta katika hali ya kiwewe mara baada ya kuona hali aliokuwa nayo Irene mara baada ya kuingizwa katika  wodi ya dharula.

Ndani ya chumba hicho cha dharula , taa zilikuwa zikiwaka lakini hali ilikuwa kinzani.

Msichana aliekuwa amelazwa  kwenye kitanda  cha wagonjwa, madaktari mbalimbali walikuwa wameitwa kuja kumwangalia , lakini karibia wote walikuwa katika hali ya kutafakari namna ya kumuokoa.

Tawi la mti wa maua  lilikuwa limemchoma Irene kuanzia tumboni  na kusababisha damu nyingi kuonekana  kupitia  mgongoni.

Irene alikuwa amepoteza fahamu na  sura yake ilikuwa imetapakaa damu.

“Mbona  wote mmesimama tu bila ya kufanya  chochote , harakisheni mumuokoe binti yangu”

Alikuwa ni  Patrin Baba yake Irene alievalia  suti  nyeusi , akiwa anaingia ndani ya eneo hilo kama vile amepandwa na ukichaa , ilionekana bado alikuwa katika majukumu yake ya kazi wakati anapokea taarifa ya kujeruhiwa kwa binti yake.

Manesi kadhaa walionekana kushindana nae nguvu  wakimwambia  asiingie ndani  na kuwapa madaktari muda wa kufikiria.

Nyuma yake alikuwepo bibi yake Irene aliekuwa amekaa kwenye  viti , akiwa amefunika uso wake na mikono huku  akionekana kulia chinichini.

Bazo alikuwa amesimama  kando ya mlango akiwa katika hali ya  majuto makubwa , kucha  ya mkono wake ilikuwa imetoboa ngozi ya mwili wake  na kufanya damu kumtoka.

Muda  mfupi alifika mwanaume mwingine kwa spidi kubwa  na kuzama ndani  na kumwangalia  msichana aliekuwa juu ya kitanda.

“Mnaota nini sasa?”Aliongea  

“Prince!”

Bazo aliishia kuita na kumwangalia Hamza kwa sekunde kadhaa kisha akashusha kichwa chake chini kwa aibu.

Regina na  Rhoda walifuatia na kumfuata Hamza ndani  na mara  baada ya kuona hali aliokuwa nayo Irene walijikuta wakikumbwa na hali ya wasiwasi.

“Hamza!” Aliita kwa jazba  Baba Irene  na kumsogelea Hamza kwa kasi.

“Wewe ndio umesababisha haya?! Umejingiza  kwenye matatizo na kumsababishia binti yangu matatizo , si ndio?”

Hamza mara baada ya kuangalia uso wa Baba Irene uliokuwa katika majonzi , alijikuta akihisi machungu katika moyo wake. Hata hivyo haukuwa muda mzuri wa kulaumiana na kuelezana  sababu ya kilichomtokea Irene, hivyo palepale alimkwida tai  na kumwangalia usoni kwa macho ya usiriasi.

“Kama unataka  binti yako kuendelea kuwa hai, unapaswa kunyamaza. Nataka kujua  sababu na  kwanini juu ya kilichomtokea kama ilivyo kwako pia”Aliongea.

Baba Irene alijikuta  akihofia muonekano wa Hamza , aliishia tu kumeza mate na kisha akapiga hatua mbili nyuma.

“Kama  binti yangu akipoteza uhai, nitakufanya ulipe na uhai wako “

Katika macho ya baba aliechanganyikiwa , ilikuwa ni wazi kabisa Hamza ndio aliemsambabishia Irene matatizo. Vinginevyo kwanini Hamza atume bodigadi wa kumlinda Irene kwa siri?.

Bibi yake Irene  aliekuwa amekaa kwenye benchi , mara baada ya kumuona Regina alionekana kuonyesha hali isiokuwa ya kawaida katika uso wake , kama vile alikuwa katika  hali ya maumivu.

Hamza alipiga hatua na kusogelea karibu na kitanda cha mgonjwa na mara baada ya kuchunguza hali yake , alionekana kushusha presha  na kuanza kufikiria cha kufanya.

“Anazidi  kupoteza damu , ondoeni kwanza huo mti”Hamza alionekana kufikia katika maamuzi.

“Wewe ni nani? Unajua  ni hatari kiasi gani  tukiuondoa huo mti sasa hivi? Tunaweza kumsababishia matatizo zaidi”

“Kwahio kama hamna mpango wa kuuondoa, mnasubiria afe  kwanza. Kama hamna njia ya kumsaidia mgonjwa mnapaswa kunisikiliza mimi kwanzia sasa”Aliongea Hamza na kisha kwa hasira aliwaangalia  madaktari hao mmoja baada ya mwingine.

“Nisikilizeni , tutachomoa  hilo tawi na kisha  tutafanya  Diagnostic peritoneal Lavage”

Madaktari wale walijikuta wakiangaliana  kwa maswali na kisha wakamwangalia wote Hamza.

“Wewe ni daktari?”Aliuliza  mmoja wao. “Mkiendelea kunichelewesha na maswali yenu , msije kunilaumu nikiwa muuaji. Nitawaua wote kujiondolea vikwazo”

Kundi  hilo la madaktari walijikuta wakitetemeka mara baada ya  kusikia maneno ya Hamza na usiriasi uliokuwa katika macho yake. Na haraka walionekana kumwangalia aliekuwa ni  kiongozi na alitoa ishara ya kutingisha kichwa na kisha kukubali kunyofoa tawi kutoka katika mwili wa  Irene.

“Tutaanza hatua za kuondoa tawi  kwenye mwili wa ngonjwa, andaeni damu kwa ajili ya kumuwekea , leta NS, sindano , na Scalpel”Aliongea Hamza.

“Damu ipo kwenye hifadhi , lakini vipi kuhusu kundi lake  la damu?”Aliuliza Daktari kiongozi.

“Hatuna taarifa zake”Alijibu moja ya mhudumu wa afya wa  masuala ya kumbukumbu za  wagonjwa.

“Binti yako ana kundi la damu lipi?”Aliuliza Hamza  akimlenga Baba Irene.

Baba Irene alionekana kushangazwa  na hali ya kitaaluma aliokuwa nayo Hamza , hakutegemea alikuwa akijua maswala ya kitabibu , ila kwa haraka haraka alijibu .

“Sijui”

“Yaani wewe ni  baba  ila hujui mtoto wako ana kundi gani la damu?”Aliongea Hamza na  Baba Irene aliishia tu kuinamisha kichwa chake  chini kwa aibu. Ilikuwa ni  moja ya ujinga uliokuwa kwa watanzania wengi kutojua  makundi ya  damu ya  watoto wao na wao wenyewe, hali ambayo  inapelekea  ucheleweshwaji wa matibabu nyakati za dharula kama hizo.

“Haraka sana  fanya  utaratibu wa kumpima”Aliongea dokta mkuu wa zamu.

“Haikuchukua muda  mtaalamu wa maabara alifika na kufanya vipimo na ndani ya dakika moja tu  vilitoa majibu , maana kila kitu kilienda kidigitali.

“Ana damu  group P na  hatuna hifadhi ya damu hio kwenye benki yetu”Aliongea mtaalamu yule wa maabara  akiwa pia katika hali ya mshangao kama vile  kipimo  kilikuwa kimekosea.

“Nini !”

Madokta wote waliokuwepo hapo , walijikuta  wakiwa katika hali ya  mshangao. Wengine walionekana hata hawakuwahi kusikia  aina hio ya group la damu na kujikuta wakiwa katika hali ya maswali mengi.

Hamza aliishia  kukunja ndita mara baada ya kusikia majibu hayo. Kundi la damu la aina ya P lilikuwa adimu sana kuonekana , ilikuwa ni sawa na kusema  kati ya  watu milioni kumi ni mmoja tu anaeweza kubahatika kuwa na kundi hilo la damu.

“Kama  hatuna aina hio ya damu  basi hatuwezi kumuongezea.Tunapaswa kufanya nini?”

“Haraka! Hebu ulizia kama katika  mtandao wa taarifa shirikishi kuna hospitali ndani ya  Dar es salaam , hata nje ya hapa kuna  hifadhi ya  damu ya kundi hilo”Aliongea dokta mkuu. Huku katika moyo wake alikuwa  akiamini  mgonjwa   matumaini ya kupona yalikuwa madogo sana. Hata kama  hospitali  nyingine  ingekuwa  na damu hio mpaka utaratibu wa kuipata na kufikishwa  hapo  wangeshachelewa.

Baba Irene aliekuwa akisikia  maelezo yote , nagoti ya miguu  yalimlegea  na alijikuta akipiga magoti chini bila ya kupenda.

“Naombeni mumuokoe  mwanangu. Msaidieni binti yangu apone”

Muda huo Baba Irene hakuwa na ule mwonekano wake wa kijasiri kama mwanausalama , alikuwa ni baba  halisia aliekuwa katika  matatizo ya kuhofia uhai wa binti yake .

Hamza alijikuta pia akishindwa kuzikabili hisia  zake, aliweza kuona   kila sekunde iliokuwa ikipotea  inapotea na uhai wa  Irene. Alijikuta akishindwa kuamini kama hana uwezo wa kumsaidia Irene. Hamza alitamani kujipiga  vibao  vingi sana ili kupata muujiza wa kubadilisha kundi hilo la damu na kuwa la   kawaida.

“Group langu la damu ni P”

Sauti kavu iliojaa ukauzu ilisikika  kutoka nyuma ya migongo ya madaktari na kufanya mwili  wa Hamza kuingiwa na ubaridi. Alijikuta akigeuka na  kuangalia upande sauti ilikosikika.

Muonekano wa Regina ulikuwa sio wa kusomeka kirahisi , alionekana ni kama vile alikuwa  katika mshangao  lakini haukuwa mshangao.

Ukweli ni kwamba mara baada ya kumuona Irene akiwa juu ya kitanda  na  sura yake ilivyokuwa katika hali ya kutia huruma  mapigo yake ya moyo yalikuwa  yakidunda kwa nguvu mno.

“Wife! Una damu Group P?!”Aliuliza Hamza akitaka kuthibitisha kwa mara nyingine.

Lakini muda huo kabla ya Regina kujibu sauti  nyingine  ya  mhudumu wa afya ilisikika.

“Kuna mtu mwenye kundi hilo la damu hapa nchini, ni taarifa kutokea  hospitali ya Mayaya. Ni mwanamke anaefahamika kwa jina la Regina Samweli Dosam. Mkazi wa Dar es salaam”

Kwa  kauli hio kila alichoongea kilitibitisha kauli ya Regina.

Kila mmoja alishikwa na butwaa , walijihisi ni kama vile Malaika alikuwa  katika eneo hilo .

Yaani wanawake wawili wenye damu

zinazofanana kimakundi  kuwepo  kimiujiza katika eneo moja?.

“Inaonekana Mungu yupo upande wa  mgonjwa”

“Imenishangaza mno!”Madaktari baadhi walioonekana  kuwa  wanafunzi walishangaa.

“Nilishapima damu yangu  muda mrefu tu na ipo  kwenye kanzidata,ni safi, mnaweza kutoa na kumsaidia mgonjwa”Aliongea Regina.

“Bosi Regina! Asante sana , asante sana , sitokuja kusahau hili maisha yangu yote”

“Baba Irene huna haja ya kunishukuru hivyo  natoa mchango wa damu  kama mtu mwingine tu. Kuokoa uhai wa mtu ni muhimu  zaidi kwa mtu yoyote”Aliongea Regina.

Haraka sana  watoa huduma walimchukua Regina na kumwandaa kwa ajili ya damu kutolewa na kuwekewa Mgonjwa.

Bibi yake Irene aliekwua ameketi kwenye kiti alionekana kuwa na hali isioelezeka katika uso wake  na alijikuta akitokwa na machozi mengi  zaidi.

Hamza mara baada ya kuona Regina kwa hiari yake kaamua kuchangia damu , alijikuta akikumbwa na  wimbi  la joto katika moyo wake.

Aliinua uso wake na kumwangalia  Bibi yake Irene  na alijikuta  akiingiwa na hali ya ufumbuzi katika akili yake.

Hatimae mara baada ya  mchakato wa  kuchangia damu kukamilika na  kuwekewa Irene . Hamza alianza mchakato wa kuondoa  tawi katika mwili wa Irene.

Sekunde  mti ule ulivyochomolewa , damu nyingi ilifyatuka kutoka kwenye jeraha.

“Anaonekana kwenda kufa , amepoteza damu nyingi sana  , hata kama huyu  dada amchangie damu  haitotosha”Aliuongea Daktari.

“Niko sawa , mnaweza kutoa damu ya kutosha”Aliongea Regina aliekuwa  amelala kitandani.

“Msije kufanya ujinga,  Siwezi kumuona mke wangu anakufa kwa ajili ya kumuokoa Irene”Alionya Hamza.

Regina alijikuta akimwangalia mwanaume huyo kwa sekunde kadhaa na kisha akaongea.

“Vipi  utafanyaje sasa?”

Hamza aligeuka na kuwaangalia madaktari  na kisha akatoa maelekezo mengine.

“Tutatumia damu yake  kupitia Renal Artery na kisha tutaipitisha kupitia Vein “

Mara baada ya kusikia maelekezo ya Hamza , madaktari wale walishindwa kumuelewa na kumfanya Hamza kutokuwa na jinsi na kuanza kuwalezea.

“Njamaanisha tutaitoa damu yake  na kuirudisha kwa wakati mmoja ili kumfanya apumue”Aliongea.

“Inawezekana! Umejifunzia wapi hii mbinu? Sijawahi kusikia inafundishwa katika chuo chochote “Aliongea Dokta mkuu ambae pia ni profesa.

“Sitaki kusikia ujinga unaongolewa darasani hapa ,  kama unataka kujifunza jifunze , tupo  kwenye dharula”Aliongea Hamza na wakati huo alikuwa akifanya kile alichokusudia.

Dakika chache mbele Hamza aliweza kufanikiwa  kutatua   tatizo la mzunguko wa damu na  upungufu wake  na  kufanikiwa hatua za kumuokoa  kwa  wakati mmoja kwa kuzuia damu isiendelee kutoka.

Dakika chache mbele mara baada ya  vipimo

(Physical sign’s) kurudi kawaida , haraka

alitolewa na kupelekwa ICU na Hamza hatimae alipumua.

Madaktari walioshuhudia kila alichokifanya Hamza , walijikuta wakimkubali mno kwa  ubingwa wake , Hata Dokta mkuu alitamani kumuona Hamza  akifanya kazi ndani ya hospitali hio na pengine kuwa profesa katika chuo  chao.

Hata hivyo Dokta huyo mara baada ya kuweka pendekezo hilo , Hamza alimgomea.

Hamza alitoka  mpaka kwenye Korido  na kuwasogelea , bibi yake Irene, baba yake ,Roda Bazo na Regina ambae  alikuwa amepumzika kwenye kiti kutokana na kutoa damu nyingi.

Mara baada ya hali ya Irene kutoka kuwa ya hatari , mambo  mengi  ambayo hayakuwa  na umuhimu kuliko uhai , yalianza kupita katika vichwa vya kila mmoja kwa mara nyingine.

Hamza alimwangalia bibi yake Irene ambae alikuwa katika hali ya mawazo na kisha aliuliza ;

“Madam kwanini usituelezee ni kipi kinachoendelea hapa?”Aliongea Hamza na kumfanya bibi yake Irene mwili wake kumtingishika.

“Wewe ! Unamaanisha nini?”

“Naweza kuelewa kwanini watu wa Bondeni  kutaka kumuua mke wangu , lakini  kwanini Dosal na mwanae wametuma watu kumuua Irene huku Mathias Huge mkuu wa kitengo cha Binamu  akitaka kumteka. Unataka kusema hujui sababu ya haya yote?”

“Unamaanisha nini!Kwamba kilichompata Irene  ni  kwasababu ya watu wa Bondeni”Aliuliza Regina aliekwua katika hali ya msahngao  mara baada ya kusikia kauli ya Hamza.

“Wife nilitaka kukuambia , lakini sikupata nafasi.. Ni kama ulivyosikia watu  waliomshambulia Irene wametumwa  na Mzee Dosal na  mwanae Suwi. Nadhani sasa unaelewa kwanini muda ule nilikwambia ni suala linalohusiana na wewe?”

Regina uso wake ulikumbwa na hali ya kutokuamini na kuchanganyikiwa kwa wakati mmoja.

“Kwanini? Si walipaswa kudili na mimi”Aliuliza Regina.

Muda ule ndio Regina alianza kukumbuka  mazungumzo yake na Hamza , pia kuhusu yeye kuwa na  group la damu sawa na Irene.

“Madam ni kipi ambacho hatujui , ni kheri ukaongea ukweli la sivyo familia yako itakuwa hatarini”Aliongea Regina akimwangalia  Bibi yake Irene.

“Unapaswa kujua nguvu ya  watu wa Binamu , wakipanga kuua mtu ni rahisi sana, kama jaribio lao la kwanza limefeli ni hakika  wakijaribu tena  lazima wafanikiwe maana watajipanga zaidi”aliongea.

“Hapana! Sio  kama najaribu kuficha, nimemuahidi Madam , siwezi kuongea chochote”

“Kila kitu kinakaribia kuwa wazi , unadhani utaweza kuficha ?”Aliongea Hamza.

“Mama wanaongea nini. Nini kinaendelea”Aliongea Baba yake Irene akionekana kuwa katika hali ya kuchanganyikiwa.

“Mwanangu! Baba yako  sio  baba yako wa damu. Kabla sijakutana na baba yako nilikuwa tayari mjamzito na baba yako ni  babu yake Regina, Mzee Dosam”

Mara  baada ya kauli hio kumtoka , mwili wa  Baba yake Irene ni kama umefunikwa na ubaridi mkali na kupelekea viungo vyake kufa ganzi.

Regina pia mara baada ya kusikia ukweli huo , alijikuta akishikwa na mshangao mkubwa kiasi cha kutoweza kuongea neno.

Hamza upande wake hakuonyesha mshangao zaidi ya kuvuta pumzi na kuzishusha.

“Kipindi cha nyuma  mimi  na Mariposa  tulikuwa vijakazi tuliotoka Bondeni  pamoja na Mzee Dosam na  Madam  lakini ndio yakutokea yakatuokea....” Alisita akionekana kushindwa kuongea.

“Baada ya kugundua ni mjamzito Madam alishindwa kunivumilia  na Mzee Dosam alinikingia  kifua lakini mwisho wa siku akaniambia niondoke. Nilikuwa mwanamke ambae sijazoea mazingira ya  ulimwengu wa kawaida yalivyo  kutokana na kukulia  Bondeni na sikuwa na elimu yoyote wala ujuzi wa kunifanya niajiriwe ,  mwisho wa siku katika  kujihangaikia ndipo nilipokuja kukutana na Shedrack , mwanzoni alikuwa akionyesha kunipenda na ujauzito wangu , lakini mara baada ya kumzaa Patrin, alitaka nimzalie  mtoto mwingine  lakini sikuwa tayari bado.Mwisho wa siku alikasirika na  kunipa talaka, baada ya muda mfupi baadae  akapoteza maisha. Ndio nilipoamua kumpatia Patrin   jina la mwisho la ukoo wangu  na maisha yakaendelea. Baada ya kumuona  Patrin  mwanangu akikua mpaka kuanzisha familia yake , nilidhani nitafurahia maisha ya amani na wajukuu, lakini  bado  watu wa  Bondeni inaonekana hawakutaka kuniacha  huru..”

Baba Irene mara baada ya kusikia hayo yote alijikuta  mshituko wake ukigeuka na kuwa huzuni na  mawazo.

“Mama! Kwanini hukuniambia hayo yote?Ulionekana kuteseka mno  , lakini mimi mwanao mpaka umri huu sijui chochote” Alijikuta akimshika mama yake mkono na  kuanza kutoa machozi ya kiume.

Regina machozi pia yalikuwa karibu , ijapokuwa   alikuwa  bibi yake  aliemfukuza , lakini alishindwa  kujizuia na kuhisi  haikuwa rahisi kwake.

Kumfukuza  mfanyakazi wa ndani  na kufanya kila liwezekanalo  kutojulikana  yeye na historia yake  na kuwaacha wajitegemee wenyewe...

Regina hakuwahi kuwaza  mambo hayo yalifanywa na bibi yake.

Hamza alijikuta akivuta pumzi na kujiambia ndio maana bibi huyo alionekana kuwa na chuki siku aliomuona na Irene , kumbe chanzo ni hayo yote.

Previoua Next