Reader Settings

Ndani ya jengo moja  lefu  lililopenezesha jiji katikati ya  Posta   , huku juu kabisa likiwa na maandishi ya JR Tower , katika Floor  namba  Ishirini na Mbili  alionekana mwanume mwenye asili ya kisomali akiwa amesimama  kwenye  dirisha ambalo lilikuwa likimpa uwezo wa kuona Madhari ya Baharini ,  bwana huyu alikuwa katika lika la Ujana , mwenye nywele zake zilizompendezesha , hakuwa mfupi sana wala hakuwa  mrefu sana , mwenye mwili wa saizi ya kati, na kwa haraka haraka ungejua bwana huyu alikuwa ni mtu wa kujipenda kutokana na mavazi ya gharama  aliovaa .

Nyuma ya  mgongo wake , kulikuwa na meza kubwa iliokuwa na tarakishi kubwa ya kampuni ya Apple  , ikiwa inatoa mwanga hafifu huku ikionekana ilikuwa ikitumiwa na bwana huyu , huku mbele ya Tarakishi hii kulikuwa na Kibao kikubwa  mfumo wa kioo kilichokuwa na  jina lililosomeka  CEO  Abubakar Hamadi, JR  Group Of Compenies.

Dakika chache za mwanaume huyu kusanifu mandhari ya nje , kama mtu ambaye alikuwa akitafuta  dosari , hatimae mlango  wa ofisi yake ulifunguliwa na alionekana kijana  mwenye nywele za Marasta akiingia na kumfanya bwana huyu atambue uwepo wa kuingia kwa mtu ofisini kwake.

“Boss nimafanikiwa kupata taarifa yake”Aliongea bwana huyu kwa heshima huku akisogelea Meza ya bei ghari iliokuwa hapo ofisni.

“Nipe ripoti”Aliongea CEO Abu huku  akikalia kiti chake na kisha alipokea bahasha iliokuwa mikononi mwa Marasta na kisha aliifungua na kuanza kupitisha macho yake huku akizidi kushangazwa na kile anachokisoma.

“Una uhakika hii ripoti  ni sahihi  , haujaichanganya na ya mtu mwingine”

“Ni sahihi kabisa  bosi , vyanzo vilivyonipatia hio taarifa ni vya kuaminika”Aliongea Marasta.

“Unaweza kwenda , lakini nataka mumfatilie huyu mtu na mnipe taarifa zote  kwa kila anachokifanya”

“Sawa bosi”Alijibu na wakati huo huo  simu ya mezani ilitoa mlio  kuonesha inaita , alinyanyua mkonga huku akimpa ishara  Marasta  kuondoka.

“Boss kuna mgeni wako”Ilikuwa ni  sauti ya  katibu  Muhtasi wake afahamikae kwa jina la Sarah.

“Sawa mruhusu”Aliongea Abu na ndani ya dakika chache mlango ulifunguliwa na mwanaume  mzee alievalia suti yake ya aina ya Navy black , akiwa anapata sapoti kwenye mkongojo  uliokuwa unang`aa  kwa  madini ya Shaba, mzee huyu licha ya kuonekana umri wake umeenda lakini Afya yake haikuwa mbaya sana.

“Mr Alex ! karibu sana”Aliongea Abuu kwa sauti ya  kiheshima huku akinyanyuka na kumkaribisha  mzee huyu  na kwenda kukaa kwenye masofa ya gharama yaliokuwa ofisini hapo.

Mzee huyu alimwangalia Abuu kwa namna flani ya kukatishwa tamaa , na kisha aliketi huku akivuta pumzi.

“Ni ujinga gani unafanya Abuu mpaka kunifanya nije mwenyewe ofisini”Aliongea mzee huyu kwa ghadhabu  huku  Abu akionekana  ni mwenye kujua kosa  lake.

“Nisamehe sana baba, najua mpango wa awali ulifeli lakini naamini mpango B utafanikiwa”.

“Swala sio mpango A wala Mpango B ninachotaka kujua ni kwanini swala la Master  linachelewa kufanikishwa, nimekupa uongozi wa kampuni yangu kwakuwa nilikuwa najua uwezo wako , kwanini swala dogo kama hili linashindikana”Abuu kimya , alionekana ni mwenye kutetemeka.

“Anza kuniambia ni kipi kilifanya mpango wako wa kwanza kushindwa na huo mpango wako B ukoje  na kama mipango yote ni ya kijinga nitakufukuza na  kumpa  mtu mwingine wa kuongoza makampuni yangu , siwezi kuvumilia ujinga katika swala hili”.

Mzee Alex ni mmiliki wa makampuni ya  JR  yote yaliokuwa yametapakaa ndani na nje ya nchi, makampuni yake  yalikuwa yakitoa huduma nyingi sana kuanzia  Maradhi , Nguo  na chakula.

Mzee Alex alikuwa ni moja ya matajiri wakubwa ndani  na nje ya taifa la Tanzania na alikuwa ndio kiongozi mkuu wa makampuni haya akihudumu kwa muda mrefu kama mkurugenzi mtendani na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi , miaka miwili nyuma alistaafu katika nafasi yake ya  ukurugenzi mtendaji na kumpa nafasi hio kijana wake aliemlea afahamikae kwa  jina la Abubakari Hamadi , moja ya sababu kubwa ya kumpatia nafasi hio kijana  huyo ni kutokana na kwamba  Mzee huyu katika uzao wake hakuwahi kubahatika  kuwa na mtoto wa kiume , kwani watoto wake wote wawili walikuwa ni wa kike  , huku Abu akiwa ni mtoto aliemlea na kumchukulia kama mwanae , ukijumlisha  uwezo mkubwa wa akili wa kijana Abuu  na ukaribu wao , aliona   anafaa kuongoza makampuni yake  na ndio hapo alipomteua kuwa mrithi wake.

*****

Alijikuta akiwa ni mwenye kukasirika mara baada ya kusikia neno ‘kahaba’ likitoka katika kinywa cha mwanaume aliekuwa mbele yake , mwanaume ambae kwa muonekano wake hakuwa kitu mbele yake , moja ya hasira  aliokuwa nayo si kutokana na yeye kuitwa kahaba na mwanaume huyu ila ni kutokna na kutokuwa kwake makini mpaka  kujikuta akitolewa usichana wake alioutunza miaka mingi  tokea ajitambue , licha ya kusumbuliwa na wanaume mbalimbali , wenye  sifa tofauti kubwa na ndogo , lakini kosa dogo alilolifanya katika maisha yake la kuamini watu , lilimpelekea kuingia katika mikono ya mwanaume aliekuwa mbele yake , ambaye  baada ya kumuangalia  kwa muda  aliona hana hadhi yoyote ya kuwa nae katika ulimwengu wa mapenzi.

“Naitwa Edna  Adebayo na sio kahaba  kama unavyonitambua”Aliongea mwanadada huyu kwa sauti yake nyororo huku akimwangalia  Roma  kwa sura iliojaa kujiamini , kama  vile hakukuwa na kitu kilichotokea kati yao.

“Kama sio kahaba  wewe ni nani , au kwasababu upo kwenye mjengo kama huu wa gharama kubwa  , kifupi wewe ni kahaba wa hadhi ya juu ambaye kapuku kama mimi nilikuotea na kukufaidi”Aliongea Roma na kuzidi kumchafua roho mwanamke  huyu na kwa Roma ni kama alikuwa amekusudia kuongea hayo maneno ili kumsoma mwanamke huyu aliokuwa mbele yake , kwani kuna kitu tokea aingie hapo ndani  na kumuona huyu mwanamke ashakigundua , hakuwa mjinga kiasi cha Rami  kuona  mwanamke anafahamika kwa jina la ‘Bossi’ kuwa kahaba kama alivyomdhania siku tatu  zilizopita.

Lakini licha ya Roma kutamka maneno hayo kwa mwanadada huyu  , alionekana ni mwenye kuzuia hasira zake zisitawale akili yake.

“Naomba uketi , nina mazungumzo na wewe”Aliongea kwa sauti ya upole  huku akitangulia kukaa yeye na  Roma alitabasamu na kisha kuketi.

“Nimeitikia wito , naomba uende moja kwa moja kwa lile uliloniitia” Aliongea Roma na kumfanya mwanadada huyu agundue mwanaume aliekuwa mbele yake ni wa namna gani , kwani  alitegemea  kuona Roma kuwa katika hali ya uoga  kama tu angegundua uwezo  wa kipesa aliokuwa nao , lakini kila kitu kilimjibu  kivingine , kwani kijana huyu alionekana kujiamini mno , jambo ambalo lilimfanya aone maamuzi alioyafanya nisahihi , alichukua glasi yake ya wine iliokuwa kwenye meza ya kioo na kisha alikunywa  mara mbili na kisha akaweka chini kwa mapozi ya kike .

“Naomba unioe”Aliongea mwanadada huyu , huku akionekana ni mwenye  kuanza kukosa ile hali ya kujiamini aliokuwa nayo mwanzo.

Kwa upande wa Roma ni kama mtu ambaye hakusikia vizuri maneno yaliomtoka mrembo huyu mwenye haiba ya upole , aliekuwa mbele yake.

“Inawezekana sijakusikia vizuri mrembo wangu my one night stand , naomba urudie kauli yako tafadhari”.

“Naomba  unioe tafadhari , ndio   jambo pekee nililokuitia mahali hapa  , nitakulipa kiasi chochote cha fedha”Aliongea mwanadada huyu huku muda huu akiweka sura  ambayo ni kama mtu aliekuwa akiongea na  mfanya biashara mwingine swala la kibiashara.

“Unaonekana kuwa mpole  , lakini pia unamuonekano wa kuwa na tabia nzuri , lakini  wito wako na  ombi lako linanifanya nikufikirie kivingine , labda unieleze vizuri ni kuelewe  vinginevyo nakataa ombi lako , kwani ndoa sio kitu cha kuombwa na mwanamke kiholela kilichotokea baina yetu ni  kosa langu na lako pia”Aliongea Roma huku akichukua Chupa ya wine na   hakujali glasi iliokuwa mbele yake , yeye aigida karibia yote na kurudisha chini.

“Nataka unioe kwa mkataba wa miezi sita , baada ya hapo tutaachana  kwa  talaka na nitakulipa kiwango kizuri cha pesa , nafanya  haya kwani kuna mwanaume ambaye baba yangu mzazi ananilazimisha kuolewa  nae , mtu ambae simpendi”.

Kwanza Roma alishangaa , lakini pia  swala hilo lilimpa ukakasi kwa wakati mmoja , aliona swala la baba yake Edna  kumlazimisha  kuolewa na mwaname mwingine ni swala ambalo linaweza  kutatuliwa kwa kumkataa huyo mwanaume na si kutaka kuoelwa na mwanaume  yoyote yule ilimradi  tu kuepuka kuolewa na mwanume asiempenda.

“Nakataa , sitaki kujua  mengi kuhusu wewe , lakini swala lako lipo nje ya uwezo wangu , siwezi kuoa mtu kwa ajili ya kujipatia pesa  huku ni sawasawa na kuuza utu wangu  dada, hili swala lako kuna njia nyingine za kulitatua”.

“Kaka  wewe kama mwanaume  unatakiwa kuwajibika kwa matendo yako , ulinitoa bar pasipo ruhusa yangu ukanipeleka mpaka geto kwako ukanitoa usichana wangu pasipo  ridhaa yangu  , lakini juu ya yote nikaacha kukufanya jambo baya  kwani ulichofanya ni kinyume  na Sheria , lakini leo hii ninakupa ofa ya kunioa tena kwa kukulipa  halafu unakataa ,nina nguvu ya kukufanya uozee jera Zaidi ya miaka therathini”Aliongea mwanadada huyu kwa sauti ya hasira.

“Nakubari kosa langu Dada na nipo tayari kwa ajili ya  adhabu nitakayopewa , lakini swala la mimi kuuza utu wangu kwako ni swala ambalo haliwezekani”Aliongea Roma kwa hasira huku akinyanyuka akitaka kuondoka .

“Ukipiga hatua mbili kutoka nje ya mlango   najitosa nje ya hili  jengo , siwezi kuishi kwa aibu ya kubakwa na mwanaume kwenye maisha yangu  na nakuapia dunia nzima itajua kuwa ulinibaka na sidhani kama utakua kuishi kwa Amani, na namna pekee ni  kukubali ombi langu”Aliongea mwanadada huyu ila Roma hakugeuka aliendelea kutembea kuelekea mlangoni , lakini ile anataka kushika kitasa , alisikia mlango wa dirisha  nyuma yake ukifunguliwa , aligeuka nyuma na kumuona Edna  akimaanisha kile ambacho anataka kufanya .

Roma alijikuta akipigwa kama na  radi kwenye kichwa chake na kuchuchumaa chini kwa maumivu ya kichwa , huku picha mbalimbali za maisha yake ya nyuma zikipita kwa kasi ,mboni za macho yake zilibadilika ghafla nakuwa za kijani  na  ndani ya sekunde kadhaa tu kwa tukio ambalo halikueleweka lilifanyika vipi alikuwa amembeba juu mrembo Edna   huku akimrudisha kwenye  sofa , kitendo hicho hata kwa mrembo huyu ambae machozi yalijaza mboni za macho yake alishangazwa na kitendo hiko.

“Sipo tayari kuona mwanamke wa pili  anapoteza uhai kwa ajili yangu”Aliongea  Roma kwa sauti nzito  baada ya kumkalisha Mrembo Edna  kwenye sofa.

“Kwa hio umekubali kunioa?”

“Sina  jinsi”Aliongea  Roma huku akifungua chupa nyingine ya Wine na kuigida kama maji.

Edna hakujali tabia ya Roma alitoa bahasha kwenye mkoba wake na kisha alichomoa karatasi  yenye mkataba wa ndoa na kisha akampatia Roma na karamu, na Roma baada ya kupokea karatasi ile ,   wala hakutaka kuangalia ni kipi kipo ndani ya hio karatasi , aliweka sahihi yake sehemu husika.

“Mbona husomi  mkataba  kwanza?

“Sina haja ya kusoma , kwani nishajua kilichopo kwenye huu mkataba”

“Kama nini”

“Kama vile  kuweka umbali katikati yetu , kutogusana na mengineo mengi”

“Ni kweli  , lakini pamoja ya hayo sheria kubwa ni juu ya ndoa yetu kuwa siri baina yetu”Aliongea Mrembo Edna.

“Nini kinafuata baada ya hapa?”

“Tutaenda Bomani kwa ajili ya kusajili ndoa yetu na kuwa mke na mume kihalali  , lakini kabla ya hayo inabidi ubadilishe mavazi  na uoge utakate”Aliongea mwanadada huyu na  kisha alitoa simu yake na kutoa maagizo na ndani ya sekunde chache tu Suzzane aliingia akiwa na  suti ,viatu  na makorokoro mengine na Roma alienda kuoga na alitumia muda mchache sana kuoga na kuvaa nguvo ambazo aliletewa  na Suzzane.

Roma alikuwa amependeza mno na suti yake ya rangi ya blue , suti ya bei ghali ambayo ilimbadilisha kwa asilimia kubwa  muonekano wake  na kuwa na muonekano wa kipedeshee.

Baada ya kutoka kwenye chumba hiki cha kubadilishia nguo , waliokuwa ndani ya chumba hiko ni kama wamemsahau kama fukara , licha ya Roma kuwa na sura ya kawaida sana  ambayo haikuwa kama ya mahadsome boy wa mjini lakini Suti aliokuwa amevaa ilimpendezesha na kumbadilisha.

Baada ya masaa  kadhaa ,Roma akiwa ameongozana na Mrembo  Edna walitoka kwenye gari ya gharama sana ana ya Mercedenz Benz  toleo jipya na kuingia ndani ya jengo la Bomani , na haikuwachukiua muda Mrefu  kila mmoja alisaini cheti cha ndoa na kisha walipiga picha ya uthibitisho na kuwa mke na mume halali.

“My wife mrembo … Mungu kweli ananipenda siamini kama nimepata mke mrembo kama wewe”Roma alianza utani wake pasipo kumzingatia Mrembo Edna  huku akijifanya kumsogelea  kwa ajili ya kumkumbatia ,   lakini aliishia kukatwa  jicho na kupigwa kikumbo na mwanadada huyu.

Waliingia kwenye gari  huku dereva akiwa  mrembo huyu na ndani ya madakika kadhaa ya barabarani gari ilikuja kusimama kwenye geti lenye ukuta mkubwa maeneo ya ushuani Osterbay  na baada ya  dakika chache geti lile lilifunguliwa na mlinzi na kisha Edna  aliingiza gari na kwenda kulipaki katika eneo husika na kisha alishuka  kwenye gari.

Lilikuwa ni jumba la kifahari mno lililokuwa mbele yao , Roma alishangazwa na mandhari mazuri ya jumba hili , na kwa harakaharaka aliona mtu anaeishi kwenye hii nyumba alikuwa mtu mwenye ukwasi mkubwa wa pesa.

“Hapa ni nyumbani kwa  baba yangu na tumekuja hapa kujitambilisha kwake , hivyo tujitahidi kuonekana kama wanandoa kweli”.

“Unaongea kama vile sisi sio wanandoa,  tunahistoria ndefu kabla hatujafanya maamuzi ya kufunga ndoa mke wangu , au  ushasahau kuwa mimi ndio niliokuingiza kwenye ulimwengu wa mapenzi, my babe Edna acha zako  bhna”Huku akimshika mkono na kumvuta kifuani , swala ambalo juu kabisa ya gorofa ya nyumba hii alionekana mzee  akishuhudia kitendo kinachofanyika , Edna   alitaka kujinasua kwenye mikono ya Roma , lakini  Roma alimpa ishara kwamba baba yake yupo juu ya ghorofa anawaangalia na yeye aliangaza macho yake juu  na kuona kivuli cha mtu kikitokomea kwenye Balcony.

“Kwenye wanaume wote ambao nishawahi kukutana nao sijawahi kuwaza nitakutana na mwanaume ambae huna aibu kama wewe”.Aliongea Edna  kwa hasira huku akitangulia kwenda mbele na kumfanya Roma atoe tabasamu la kifedhuli na kumfata.

“Baba  , nimekuja kumtambulisha  mume wangu , sitaki tena kusikia juu ya kuolewa na mwanaume mwingine . nampenda Roma na nitaishi nae mpaka kifo kitakapotutenganisha maana tunapendana “Huku akimwegamia Roma ambaye  alikuwa ni mwenye tabasamu zito huku akimwangalia mwanaume alikuwa mbele yake kwenye sebule hii kubwa iliojaa thamani za bei ghali.

“Mzee  kama alivvyosema bebi wangu hapa , mke wangu kipenzi , nyongo mkalia ini , nimekuja kujitambulisha , na naomba unisamehe kwa kuja tukiwa mke na mume , kwa majina naitwa Roma Ramoni  ni  mwenyeji wa hili jiji , kazi yangu ni kubeba mizigo  soko la Mbagala Rangi tatu”Aliongea Roma na kumfanya  mzee huyu aanze kuhema kwa taabu , huku Edna akiwa  ni mwenye kushangaa namna ambavyo Roma alikuwa akijiamini na kukosa aibu.

“Unasemaje wewe , kikaragosi .. Ednaa..!! ni laana gani unaniletea ndani ya familia yangu??”Aliongea mzee huyu huku akikaa na kuanza kuhema kwa taabu , lakini wawili hawa hawakuwa ni wenye kujali.

Previoua Next