Reader Settings

Roma aliendesha gari kama kichaa  , uzuri ni kwamba barabarani hakukuwa na magari mengi , alitumia dakika chache tu kufika ndani ya Kibaha  na kukunja kushoto  barabara ya vumbi kama vile alikuwa akielekea Bagamoyo nyuma ya kiwanda cha kuunganisha magari  na  akasonga mbele.

Alikuja kusimamisha gari yake  mita mia moja kutoka kilipokuwa kilipo kiwanda hiki cha kuunganisha magari na kisha alisimama huku akiangalia eneo ambalo watu hao walimwelekeza , bado hakuwa akiona nyumba yoyote hivyo alishindwa kusogea mbele, baada ya kusimamisha gari kwa dakika kama kumi  hivi simu yake ilianza kuita.

“Mr Ramon tumehakikisha umekuja peke yako , unaweza kusogea mbele  mita mia nne kutoka ulipo kisha kunja kulia utaona nyumba yenye geti jeusi na simamisha gari yako hapo”.

Roma  bila ya kujiuliza , aliendesha gari na baada ya kusogea umbali unaotakiwa kama alivyokuwa amepewa maagizo , aliona barabara  ya vumbi iliokuwa  ikikunja kulia , alichukua  Barbara hio na kusimamisha gari mara baada  ya kuona   ukuta mrefu  ambao ulifanya usiweze kuona ndani ya ukuta huo ndani  kuna nini , baada ya kushuka tu kwenye gari ni kama walikuwa wanamsubiri kwani kijana mmoja mwenye koti  jeusi alievalia kofia ya chepelu alimyooshea Roma bastora na kumuingiza ndani ya jumba hili.

Roma aligundua kuwa hiii sio nyumba bali ni Godauni  , kwani ndani  hapa kulikuwa na magari yale ya kuchimbia barabara yakiwa katika hali ya uchakavu na baadhi ya mavyuma mengi makachakavu.

Walimwigiza kwenye jumba lililokuwa mbele  ,upande wa kushoto huku vijana watatu wakionekana ndani ya eneo hilo wawili walikuwa na siraha za moto na mmoja aliekuwa anavuta sigara ndio hakuwa na siraha lakini alionekana kuwa ndio kiongozi , Roma alianza kuangalia mmoja mmoja kwa hasira.

“Edna yuko wapi ?”

“Tuliza wenge wewe fala”Aliongea  huku akimsukumia ndani ya chumba na hapo ndipo alipomuaona Edna akiwa amefungwa kwenye kiti , kitendo cha  Edna kumuona Roma  ni kama vile hakukitarajia, Roma alimwangalia namna mwanamke huyo alivyokuwa  ametawaliwa na machozi usoni  na kumuonea huruma, lakini baada ya Roma kugeuka upande wa  pili aliweza kumuona mtu mwingine na huyu alikuwa ni baba yake Edna wote wakiwa wamefungwa.

Mbele ya Edna kulikuwa na kijisturi ambacho kilikuwa na makaratasi na karamu , huku pembeni  kuna jambazi mmoja aliekuwa amekaa kwenye  matofari matatu  yaliokuwa yamepangwa kwa ustadi.

Roma hakuweza kutambua sura hata moja , alisukumiwa na kwenda  kufungwa karibu na baba yake Edna miguuni na mikononi kwenye kiti.

“Mnataka nini kwa Edna , nishakuja mfungueni  sasa”

“Tushakuambia tuliza wenge, wewe hata haunathamani kwetu , umeitwa hapa kwa ajili  ya kufa, na Edna ameletwa hapa kwa mpango mwingine”Roma hakuelewa kinacho endelea lakini alikuja kuelewa baada ya kuona bwana  mmoja hivi aliekuwa amekalia tofali alikuwa akimlazimisha Edna kutia saini kwenye makaratasi yaliokuwa yapo mbele yake.

“Mrembo acha kutupotezea muda tia saini umuokoe baba yako  , nitahesabu mpaka nne maana umetusumbua sana , usipo fanya kile tunachotaka  hii itamuhusu baba yako”Aliongea bwana huyu huku akionekana hana hasira hata kidogo.

Edna alimwangalia baba yake na kisha kugeuza macho kwa Roma na kisha kuziangalia karatasi zilizokuwa mbele yake , karatasi zilizokuwa zikimtaka kutia saini ili kuruhusu asilimia sitini ya hisa za kampuni yake  kwenda kwa mtu mwingine.

“Hapana sipo tayari  , nitailinda kampuni  hata kwa kifo”

“Mojaaa.. , mbilii , tatuu.. nne”.

“Paaah!!”Ulilia mlio wa risasi uliomfanya  Edna afumbe macho , kwani hakuwa tayari kushuhudia  baba yake  akipigwa risasi, jambo hili hata kwa Roma lilimshangaza sana , hakuamini kama Edna yupo tayari kumuona baba yake akifa  ili tu alinde kampuni.

“Mamaa... isiiiii... nakufaa Edna ”Ilikuwa ni sauti ya mauimivu iliomtoka mzee  Adebayo , kwani alikuwa amepigwa risasi ya  paja na damu zilikuwa zikimtiririka.

“Risasi itakayofutia itatua kwenye kichwa cha baba yako , nadhani unatuona kama tunatania , weka sahihi yako pumbavuu”

“Edna wape wanachotaka wata.. niua baba yak..o”

Edna alimwangalia baba yake kwa uchungu   huku akitoa machozi.

“Nisamehe baba sipo tayari kufanya kama wanavyotaka , watuue tu wote”Aliongea Edna na kuwafanya majambazi hawa kushangaa lakini sio majambazi tu hata Roma alikuwa akishangaa.

Roma japo yeye alionekana  kufungwa lakini ni kama amepumzika kwani hakuwa na wasiwasi kabisa.

“ Kama ndio unavyotaka basi hatuna namna tutafanya kile  ambacho unataka , na nakuambia baba yakoo atakufa lakini pia kusaini utasaini”Aliongea jambazi kiongozi na kisha alinyanyua bastora yake na kumlenga baba yake Edna , huku Edna akifumba kwa mara nyingine  macho kwani hakuwa tayari kushuhudia kifo cha baba yake.

“Nitahesabu upya mpaka tatu , kama utashindwa kutia saini hizo karatasi basi sitakuwa na jinsi kukupa kile unachotaka.. moja , mbili ….. , tatu”Edna hakutia  saini  na  jambazi liingiza kidole kwenye Triga..

“Stop nipo tayari kusaini ,.. nitasaini muacheni baba yangu”Aliongea Edna na kuwafanya majambazi hawa watabasamu na  jambazi lile kiongozi lilimpa ishara jamaa aliekuwa karibu na Edna  amsogezee karatasi.

Edna aliangalia karatasi zile huku  akitoa machozi , alichukua kalamu huku akiwa anatetemeka mno , hakuamini anakwenda  kuachia  hisa asilimia Sitini na kubakiwa na asiliamia therethini tu za umiliki ndani ya kampuni yaie kitendo ambacho kitamfanya kukosa kauli ya mwisho ndani ya kampuni.

“Hapana ngoja nimuokoe baba , pesa zinatafutwa tu na hata mama atanielewa , huyu ni baba yangu siwezi kumuangalia akifa mbele yake sitokuwa na furaha”Aliwaza Edna

“Fanya haraka”Aliongea jambazi kiongozi na Edna aliangalia  karatasi zile  na kisha kama mtu alieghaili aliweka kalamu chini na kisha akanyanyua uso  wake na kumwangalia Roma  kwa huzuni.

“Kabla sijasaini  nataka mnihakikishie jambo moja”Aliongea Edna

“Ongea”

“Mtamuachia mume wangu akiwa hai  maana hahusiki kwa chochote katika hili”Wale majambazi waliangaliana  na kisha kiongozi alitoa simu  na kusogea pembeni , alionekana hakuwa na  maamuzi ya mwisho juu  ya ombi la Edna.

Roma alishangazwa na maamuzi ya Edna    na kujikuta kuna kitu flani kipya kiliingia ndani ya moyo wake juu ya mke wake huyu wa mkataba.

“Bosi anataka  tumuahidi Roma awe huru”

“Acheni upumbavu , mdanganyeni  tu akishasaini mpigeni  Roma risasi sitaki huyo mwanaharamu aishi tumieni akili”Ilisikika sauti upande wa pili.

“Sawa bosi”

Jambazi kiongozi alirudi na kumwambia Edna kuwa wapo tayari kutii ombi lake , lakini kwa Edna hakuwa mpumbavu alikuwa anajua kabisa watu hao watamuua Roma akishafanya  kile wanachotaka.

“Kama mpo tayari nataka mumfungue yeye na baba yangu   waondoke na mimi ndipo nitasaini.. siwezi kuwaamini”Aliongea na wakaangaliana lakini awamu hii kiongozi aliona afanye maamuzi bila ya kumshirikisha bosi wake, alimpa  ishara jamaa aliekuwa ameshikilia bastora amfungue miguu Roma na baba yake Edna kisha awatoe nje.

“Wakishafika mbali na nikithibitisha wako mbali nitasaini Roma naomba umepeleke baba hospitalini  ukitoka”

“Sawa Mke wangu  nitafanya hivyo na Asante kwa kunipenda Mumeo”Huku akimkonyeza

Baada ya majambazi kukubaliana na matakwa ya Edna   jambazi  mmoja aliekuwa na bastora  alimsindikiza baba yake Edna na Roma nje , baba yake Edna   alikuwa aivuja damu japo sio sana , alikuwa akijikaza kwa maumivu.

Majambazi waliobaki baada ya kutoka walisubiria simu ya Roma  iwapigie ili kumthibitishia Edna kama ashafika mbali na yuko salama  lakini   walikuja kushituka baada ya mwili kutua ndani ya chumba hiki walichokuwepo kwa nguvu kiasi kwamba kutoa mlio , baada ya wao wote kuangalia kwa umakini ndipo walipogundua ni mwili wa mwenzao.

“Kioba!”Aliiita jambazi mkuu kwa hamaki na  ile anainua macho  alimuona Roma akiingia  , tena awamu hii alikuwa akijiamini kiasi kwamba  utadhani yeye ndio aliewaagiza hao vijana, Mwenzao alikuwa tayari ashakufa tena kifo chake kilionekana kuwa cha kikatili mno kwani shingo ilikuwa imelegea  sana.

“Katika maisha yangu nina sheriia tatu ambazo nimeziweka   kwa mtu yoyote kutozivuka , moja  sipendi kutishiwa Amani , pili  sipendi watu wanaotumia ngao watu wengine kutimiza mambo yao, tatu  kwangu neno Onyo ni mara moja ukirudia ni kifo na nyie makossa yote mnayo”Aliongea Roma  kwa sauti ya upole kabisa na hakuonekana kuwa na wasiwasi hata kidogo na isitoshe hakuwa na siraha ila  jambazi mmoja alikuwa na siraha.

“Mpige risasi unasubiri nini?”Aliongea jambazi  yule kwa pupa  na yule mwingine akainua Risasi ili kumpiga Roma , lakini kufumba macho na kufumbua , Roma tayari alikuwa ashamfikia na kilichosikika ilikuwa ni

“Crak’

“Mamaaa.. nakufaaa”

Ulikuwa mlio wa mvunjiko wa mfupa wa  mkono  uliokuwa umeshika Bastora  lakini Roma hakuishia hapo tu  alimshika shingo  na kichwa na kukizungusha na mifupa yote ya shingoni ikakatika  huku kichwa kikigeukia mgongo kitendo ambacho kilimfanya hadi Edna afumbe macho , kwani alishuhuidia Roma akiua  kikatili mno mambo ambayo hakuwahi kuwaza atayaona laivu.

Jambazi mwingine baada ya kuona  mambo sio kama alivyodhania , alikimbilia chuma na kulinyanyua huku akimtishia  nalo Roma , na kwa Roma wala hakujali kwani alizidi kumsogelea huku jambazi hili lilikianza kutetemeka , kwani hakuwahi kukutana na aina ya mtu ambaye alikuwa akiua kama anaua kuku tema kikatili kwa namna alivyoshuhudia.

“Huyu sio mtu , ni shetani  inabidi nipate upenyo wa kukimbia”Liliwwaza Jambazi hili

Jambazi alimrushia Roma lile Chuma lakini Roma alilikwepa  halafu akalidaka na kulivuta kwa nguvu kitedo ambacho Jambazi  alivutwa nalo kwani alikuwa amelishikilia kwa nguvu  na baada ya kumsogelea Roma  alipigwa teke la mguuni lililomfanya kuhisi maumivu makali mno na kutoa ukulele.

“Leo utaniambia bosi wako ni nani, aliekutuma  kumteka mke wangu”Aliongea Roma huku macho yake yakionekana sio ya kawaida hata sauti yake pia sio ile iliokuwa ikizoeleka , aliongea kama roboti.

Alimshika yule jambazi na kama vile anavunja paja la kuku alimshika mguu kwenye Goti na kulipindisha kiasi ambacho  mguu ule ulitoa sauti kubwa ya viungio kupishana  na mguu ule kugeukia mbele.

“Mamaaaa..  nakufaaa….”Ulikuwa ni ukululele wa aina yake

“Sema nani kawatuma la sivyo naendelea na mguu wa pili?”

“Nasema .. nasemaa”

“Okey !  nadhani uanze kuaongea sasa”

“Alietutuma ni Jose na Baba yake Edna”.Roma ni kama hakuwa ameelewa vizuri .

“Ongea vizuri ueleweke au unataka niendelee..”

“Huyu mzee eliekuwepo hapa na Jamaa anaefahamika kwa ina la Jose ndio alietuagiza , ila  huyo Jose anasema pia  ana bosi wake  alietoa  kazi hio”Baada   ya kuongea vile lile Jamaa ni kama Edna hakuwa akimuamini , alinyanyua karatasi zilizokuwa mbele yake na kuzisoma na alijikuta akiishiwa nguvu mara baada ya kuona  karatasi hizo zilikuwa na jina la baba yake , inamaana muda wote alitakiwa kusaini ili kuruhusu hisa ziende kwa baba yake.

Roma aliona maelezo hayo yanajitosheleza , alichukua lile chuma na bila hata ya huruma , alimchoma nalo  Shingoni kiasi cha kufanya Damu imrukie  na kumchafua kwenye nguo  mpaka usoni  Roma aligusa ile damu usoni  na kisha  kuinusa.

“Mwamba ana damu inanuka vibaya huyu” Aliwaza

Na huo ukawa ndio mwisho wa majambazi yote matatu yaliokufa kikatili mno na kwa mtu yoyote angeshuhudia maiti hizo  hakika angeishia kusema Roma ni Shetani..

Lakini wakati  anamaliza mara mlango ulisukumwa na mtu anaechehemea  huku akiwa na bastora mkononi na huyu hakuwa mwingine  bali alikuwa ni  baba yake Edna.

“Edna Saini hizo karatasi kabla sijaachia Risasi”Aliongea mzee  huyu huku akionekana ni mwenye kuvumilia maumivu kwani hadi mikono ilikuwa ikimtetemeaka.

“Baba .. siamini kama unaweza kwenda mbali kiasi hiki….”

“Kimya mpumbavu wewe mimii sio baba yako , saini karatasi hizo kabla sijakutandika risasi ya kichwa na huyu muaaji mwenzako hapa”Aliongea  huku Roma akimwangalia mzee huyu na kisha akatabasamu.

“Mzee bora ungekimbia baada ya mimi kukuacha kule nje , ila nimekupa nafasi ili hali najua ulikuwa kwenye huu mpango ila ukajileta mwenywe hivyo sina budi ya kukupeleka kuzimu”Aliongea Roma na kumfanya Edna ashangae kuona Roma alikuwa ashajua kuwa baba yake alikuwa akihusika  , alishangazwa na uwezo wa Roma na kujiuliza maswali mengi.

Baba yake Edna alimwangalia Roma  na kisha akaangalia namna Roma alivyoweka mguu wake kwenye kichwa cha jambazi linalovuja damu shingoni  na kutikisika kama kuku   bila wasiwasi kama vile kaweka mguu kwenye  tofali , mzee huyu alijikuta mwili wake ukipatwa na ubaridi  ambao hakuelewa alijiuliza huyu matu ni binadamu au mnyama.

“Baba naomba uweke hio siraha chini  nitaacha hili lipite  ,, licha ya kwamba sitokuja kusahau”

“Tulia Edna .. mmeninyanyasa sana wewe na mama yako  kiasi cha kunifanya nionekane mwanaume bwege ndani ya macho ya walimwengu , leo nalipiza maumivu mlionisababishia kwa miaka mingi”Aliongea huyu  mzee na hakuwaza tena alivuta triga yake   kwa dhumuni la kuua , lakini kabla hajatimiza azima yake alijikuta akipigwa na chuma  mikononi na Siraha ile kwenda chini.

“Kitendo cha kurudi hapa ndani  umejitafutia kifo chako”Aliongea Roma  na  kumpiga teke sehemu iliokuwa na Jeraha na kumfanya mzee huyu apige yowe , lakini Roma hakuishia hapo tu , alimkanyaga kwenye kigoti cha mguu na kusababisha mfupa wa mguu uvunjike , yote hayo  aliokuwa akiyafanya hakumuwazia Edna alikuwa kwenye hali gani.

Roma alimvunja mzee Adebayo miguu yote na hapo ndipo alipomgeukia Edna ambaye muda wote alikuwa kwenye mshituko  kiasi kwamba hakuwa hata akiongea  kwani alikua ni kama mtu aliekuwa amezimia huku anaangalia , ile Roma anamfungua Kamba Edna alizimia palepale.

Baada ya lisaa limoja Roma alifika Kigamboni na kumtoa Edna kwenye gari na kuingia  nae ndani huku Bi Wema akiwa kwenye mshangao kwani alimuona Wema akiwa na damu mwili mzima.

“Nini kimetokea Roma?”Aliuliza bibi huyu huku akionekana ni mwenye wasiwasi.

“Kuna wapuuzi wanajifanya wajanja , wamemteka mke wangu na mimi nimelipiza kwa kuwaua”Bi Wema macho yalimtoka.

“Umesema umewaua?”

“Ndio  wamekufa , mwingine ni baba yake Edna nimemvunja miguu ili   akampe taarifa anaeshirikiana nae”Huku akimpandisha Edna juu  kweye chumba chake akifuatiwa na Bi Wema .

Roma ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kuingia kwenye chumba hiki  cha  mke wake , kilikuwa ni chumba kikubwa kilichokuwa kinapendeza sana kuitwa chumba cha mwanamke CEO mkubwa ndani ya  ulimwengu wa wafanya biashara  duniani.

“Bibi atazinduka huyu baada ya muda alikuwa kwenye mshituko”

“Unajuaje Roma  wakati mtu yupo mahututi tumepeleke hospitalini”.

“Haina haja  Bi Wema, Atazinduka”Aliongea  Roma na kisha  akatoka akimuacha  bibi huyu kwenye mawazo , hakuweza kujua Roma ni mtu wa namna gani kwani alionekana kujiamini mno.

Baada ya kutoka ndani ya chumba chake aliingia bafuni na kuoga na baada ya kumaliza alichukua simu yake na kumpigia Doris na kumwambia ashamuokoa  mke  wake na yeye yuko salama  baada ya kukata simu alitafuta namba ya Rose.

****

Ilikuwa ni muda wa usiku  saa tisa kamili ndani ya chumba kikubwa anacholala mheshimiwa  Rais Senga , akiwa amepumzika na mke wake mara simu yake kubwa ya I phone ilianza kuita mfuliulizo kiasi cha kumuamsha  na  kushangaa ni nani anampigia muda huo kwani sio kawaida yake , na mara nyingi akipokea simu usiku sana  huwa ni za dharula na kuna tatizo kubwa ambalo wasaidizi wake wameshindwa kulitolea maamuzi, aliangalia jina la mpigaji na kujikuta  usingizi ukimuishia  jina kwenye kioo  lilionekana  limeandikwa Senior(Mkubwa kazini).

“Mheshimiwa kuna nini?  , maana  sio kawaida kunipigia muda huu”.

“Senga ulinihakikisha kuwa Edna atakuwa salama ndani ya taifa lako , lakini nini hiki kinaendelea ndani ya  nchi yako”

“Naomba upunguze jazba Senior nini tatizo?”

“Vijana wangu wamenitumia ripoti kwamba Edna alitekwa”

“Nini..!! , unahakika na hio taarifa Senior?”

“Nina uhakika na vijana wangu wangu Senga , nimewapa kazi hio moja tu ya kumlinda Edna  kwa siri”

“Vipi hali ya Edna kwa sasa??”.

“Ni bahati kwamba  sasa hivi ana mume , kwa hilo namsifia sana  , yule mtoto ana akili sana kachagua mume bora”

“Unamaanisha Roma ni mume bora kwa  Edna?”.

“Ndio Senga mchunge sana huyo kijana  sio mtu wa mchezo  mchezo na ni mtu katili kuwahi kutokea katika huu ulimwengu hakikisha unakuwa upande mzuri na yeye  kukusaidia kwenye mpango wako, mimi yangu ni hayo tu na nikwambie Senga haupo makini kabisa Edna anatekwa huna habari , mimi niliopo ng`ambo ya pili ya nchi yako  nimepata taarifa  kabla yako , nimekasirishwa sana na jambo hili ,Usiku mwema nadhanni tutaongea Zaidi  juu ya mipano yetu siku tukionana”Aliongea Senior na kisha kukata simu.

“Who is this Guy?”Alijiuliza mheshimiwa  Senga  huku akiwa ni mwenye kushangaa Senior anamfahamu Roma.

“ My guess  was right he is not normal , there is more hidden  info about him , I have to dive deep to  discover  more details”

Previoua Next